Mwanzo 7 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version

Mwanzo 7:1-24

17:1 Mwa 6:18; 9:6; Mt 24:38; Ebr 11:7; Lk 17:26-27; 1Pet 3:20; 2Pet 2:5; Eze 14:14Ndipo Bwana akamwambia Noa, “Ingia katika safina wewe na jamaa yako yote, kwa sababu katika kizazi hiki nimeona ya kuwa wewe ni mwenye haki. 27:2 Mwa 8:20; Law 10:10; 11:1-47; Kum 14:3-20; Eze 44:23; Hag 2:12; Mdo 10:14-15Uchukue wanyama saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, na wanyama wawili wawili wa kila aina walio najisi wa kiume na wa kike. 37:3 Mwa 6:20Pia uchukue ndege saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, ili kuhifadhi aina zao mbalimbali katika dunia yote. 47:4 Mwa 2:8; 6:7, 13; 1Fal 13:34; Yer 28:16; Hes 13:25; 1Sam 17:16; 1Fal 19:8; Kut 24:18; 32:1; 34:28; Kum 9:9, 11, 18, 25; 10:10; Ay 37:6; Mt 4:2Siku saba kuanzia sasa nitaleta mvua juu ya nchi kwa siku arobaini usiku na mchana, nami nitafutilia mbali kutoka uso wa nchi kila kiumbe hai nilichokiumba.”

57:5 Mwa 6:22Noa akafanya yote kama Bwana alivyomwamuru.

67:6 Mwa 5:32Noa alikuwa na miaka 600 gharika ilipokuja juu ya dunia. 77:7 Mwa 6:18Noa na mkewe na wanawe na wake zao wakaingia katika safina ili waepuke ile gharika. 8Jozi ya wanyama walio safi na walio najisi, ndege na viumbe vitambaavyo, 97:9 Mwa 6:22wa kiume na wa kike, walikuja kwa Noa wakaingia katika safina kama Mungu alivyomwamuru Noa. 10Baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya dunia.

117:11 Mwa 5:32; 8:2, 4, 14; Ay 28:11; Za 36:6; 42:7; 78:23; Mit 8:24; Isa 24:18; 51:10; Eze 26:19; 2; 2Fal 7:2; Mal 3:10Katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili mwaka wa 600 wa kuishi kwake Noa, siku hiyo ndipo chemchemi zote hata zilizo chini sana ya ardhi zilibubujika kwa nguvu, na malango ya mafuriko ya mbinguni yakafunguliwa. 127:12 1Sam 12:17; Ay 28:26Mvua ikanyesha juu ya nchi siku arobaini usiku na mchana.

137:13 Mwa 8:16; 6:18; 1Pet 3:20; 2Pet 2:5Siku hiyo Noa, na mkewe, na wanawe Shemu, Hamu na Yafethi pamoja na wake zao wakaingia katika ile safina. 147:14 Mwa 1:11Nao walikuwa pamoja na kila mnyama wa mwituni kufuatana na aina yake, wanyama wote wafugwao kufuatana na aina zao, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi kwa aina yake, na kila ndege kufuatana na aina yake, naam kila kiumbe chenye mabawa. 157:15 Mwa 6:19Viumbe vyote vyenye pumzi ya uhai ndani yake vikaja kwa Noa viwili viwili, vikaingia katika safina. 167:16 Mwa 6:22Wanyama walioingia katika safina walikuwa wa kiume na wa kike, wa kila kiumbe chenye uhai kama Mungu alivyomwamuru Noa, ndipo Bwana akamfungia ndani.

17Kwa siku arobaini mafuriko yaliendelea kujaa duniani na maji yalivyozidi kuongezeka, yaliinua safina juu sana kutoka kwenye uso wa nchi. 18Maji yakajaa na kuongezeka sana juu ya nchi, na safina ikaelea juu ya uso wa maji. 197:19 Za 104:6Maji yakazidi kujaa juu ya nchi, yakaifunika milima yote mirefu chini ya mbingu yote. 207:20 Mwa 8:4-5; 2Pet 3:6Maji yakaendelea kujaa yakaifunika milima kwa kina cha zaidi ya dhiraa kumi na tano.7:20 Dhiraa 15 ni sawa na mita 7. 217:21 Mwa 6:7, 13; 2Pet 3:6Kila kiumbe hai kitambaacho juu ya nchi kikaangamia: Ndege, wanyama wa kufugwa, wanyama pori, viumbe vyote juu ya nchi na wanadamu wote. 227:22 Mwa 1:30Kila kiumbe juu ya nchi kavu chenye pumzi ya uhai kikafa. 237:23 Ay 14:19; 21:18; 22:11, 16; Lk 17:27; Za 90:5; Isa 28:2; Mt 24:39; Ebr 11:7; 1Pet 3:20; 2Pet 2:5Kila kitu chenye uhai juu ya uso wa nchi kilifutiliwa mbali, watu, wanyama, viumbe vitambaavyo na ndege warukao angani wakafutiliwa mbali toka duniani. Waliobaki ni Noa peke yake na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya safina.

247:24 Mwa 8:3; Ay 12:15Maji yakaifunika dunia kwa siku 150.

Nueva Versión Internacional

Génesis 7:1-24

1El Señor dijo a Noé: «Entra en el arca con toda tu familia porque tú eres el único hombre justo que he encontrado de esta generación. 2De todos los animales puros, lleva siete machos y siete hembras; pero de los impuros, solo un macho y una hembra. 3Lleva también siete machos y siete hembras de las aves del cielo, para conservar su especie sobre la tierra. 4Porque dentro de siete días haré que llueva sobre la tierra durante cuarenta días y cuarenta noches, y así borraré de la superficie de la tierra a todo ser viviente que hice».

5Noé hizo todo de acuerdo con lo que el Señor había mandado.

6Tenía Noé seiscientos años cuando las aguas del diluvio inundaron la tierra. 7Entonces, para salvarse de las aguas del diluvio, entró en el arca junto con sus hijos, su esposa y sus nueras. 8De los animales puros e impuros, de las aves y de todos los seres que se arrastran por el suelo, 9entraron con Noé por parejas, el macho y su hembra, tal como Dios se lo había mandado. 10Al cabo de los siete días, las aguas del diluvio comenzaron a caer sobre la tierra.

11Cuando Noé tenía seiscientos años, precisamente en el día diecisiete del mes segundo, se reventaron las fuentes del mar profundo y se abrieron las compuertas del cielo. 12Cuarenta días y cuarenta noches llovió sobre la tierra.

13Ese mismo día entraron en el arca Noé, sus hijos Sem, Cam y Jafet, su esposa y sus tres nueras. 14Junto con ellos entró toda clase de animales salvajes y domésticos, de animales que se arrastran por el suelo y de aves. 15Así entraron en el arca con Noé parejas de todos los seres vivientes; 16entraron un macho y una hembra de cada especie, tal como Dios se lo había mandado a Noé. Luego el Señor cerró la puerta del arca.

17El diluvio cayó sobre la tierra durante cuarenta días. Cuando crecieron las aguas, elevaron el arca por encima de la tierra. 18Las aguas crecían y aumentaban cada vez más, pero el arca se mantenía a flote sobre ellas. 19Tanto crecieron las aguas, que cubrieron las montañas más altas que hay debajo de los cielos. 20El nivel del agua subió más de quince codos7:20 Es decir, aprox. 7 m. por encima de las montañas. 21Así murió todo ser viviente que se movía sobre la tierra: las aves, los animales salvajes y domésticos, todo tipo de animal que se arrastraba por el suelo y todo ser humano. 22Pereció todo ser que habitaba la tierra seca y tenía aliento de vida. 23Dios borró de la faz de la tierra a todo ser viviente, desde los seres humanos hasta los ganados, los reptiles y las aves del cielo. Todos fueron borrados de la faz de la tierra. Solo quedaron Noé y los que estaban con él en el arca.

24Y la tierra quedó inundada ciento cincuenta días.