Mwanzo 48 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 48:1-22

Manase Na Efraimu

148:1 Mwa 41:52; Ebr 11:2Baada ya muda Yosefu akaambiwa kwamba, “Baba yako ni mgonjwa.” Kwa hiyo akawachukua wanawe wawili Manase na Efraimu, pamoja naye. 248:2 Mwa 48:8-9Yakobo alipoambiwa, “Mwanao Yosefu amekujia kukuona,” Israeli akakusanya nguvu zake, akaketi kitandani.

348:3 Mwa 17:1; 28:13Yakobo akamwambia Yosefu, “Mungu Mwenyezi48:3 Mungu Mwenyezi hapa ni jina la Kiebrania, El-Shaddai (yaani Mungu Mwenye utoshelevu wote). alinitokea huko Luzu katika nchi ya Kanaani, huko akanibariki, 448:4 Mwa 12:2; 15:7naye akaniambia, ‘Nitakufanya ustawi na kuongezeka hesabu yako, nitakufanya kuwa jamii ya mataifa, nami nitakupa nchi hii uimiliki milele wewe na wazao wako baada yako.’

548:5 Mwa 41:50-52; 29:32“Sasa basi, wanao wawili waliozaliwa kwako huku Misri kabla sijaja hapa kwako watahesabiwa kuwa ni wangu; Efraimu na Manase watakuwa wangu, kama vile Reubeni na Simeoni walivyo wangu. 6Lakini watoto utakaowazaa baada yao watakuwa wako. Katika nchi watakayoirithi, watatambuliwa kwa jina la ndugu zao. 748:7 Mwa 35:19; Rut 1:2Nilipokuwa ninarudi kutoka Padani, katika huzuni yangu Raheli alifariki katika nchi ya Kanaani tulipokuwa tungali tukisafiri, tukiwa karibu kufika Efrathi. Kwa hiyo nilimzika huko, kando ya njia iendayo Efrathi” (yaani Bethlehemu).

848:8 Mwa 48:2Wakati Israeli alipowaona wana wa Yosefu, akauliza, “Hawa ni nani?”

948:9 Mwa 33:5; 24:60Yosefu akamjibu baba yake, “Hawa ni wana ambao Mungu amenipa nikiwa huku.”

Ndipo Israeli akasema, “Walete kwangu ili niwabariki.”

1048:10 Mwa 27:1; 29:13Basi macho ya Israeli yalikuwa hayaoni vizuri kwa sababu ya uzee, naye aliona kwa shida. Kwa hiyo Yosefu akawaleta wanawe karibu na baba yake, Israeli akawabusu na akawakumbatia.

1148:11 Mwa 44:28; 50:23Israeli akamwambia Yosefu, “Kamwe sikutazamia kuuona uso wako tena, lakini sasa Mungu ameniruhusu kuwaona watoto wako pia.”

12Ndipo Yosefu akawaondoa wanawe magotini mwa Israeli naye akasujudu hadi nchi. 1348:13 Za 16:8; Mt 25:33Yosefu akachukua wale wana wawili, Efraimu kwenye mkono wake wa kuume akimwelekeza kwenye mkono wa kushoto wa Israeli, na Manase katika mkono wake wa kushoto akimwelekeza kwenye mkono wa kuume wa Israeli, akawaleta karibu na babu yao. 14Lakini Israeli akaupeleka mkono wake wa kuume, akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, ingawa alikuwa ndiye mdogo, na mkono wake wa kushoto akaukatisha, akauweka juu ya kichwa cha Manase, ingawa Manase alikuwa ndiye mzaliwa wa kwanza.

15Ndipo akambariki Yosefu akisema,

“Mungu ambaye baba zangu

Abrahamu na Isaki walimtii,

Mungu ambaye amekuwa mchungaji

wa maisha yangu yote mpaka leo hii,

1648:16 Yer 15:21; Ebr 11:21Malaika ambaye aliniokoa kutoka madhara yote,

yeye na awabariki vijana hawa.

Na waitwe kwa jina langu

na kwa majina ya baba zangu Abrahamu na Isaki,

wao na waongezeke kwa wingi

katika dunia.”

1748:17 Mwa 48:14Yosefu alipoona baba yake akiweka mkono wa kuume juu ya kichwa cha Efraimu, hakupendezwa, kwa hiyo akauchukua mkono wa baba yake kutoka kichwa cha Efraimu na kuuweka juu ya kichwa cha Manase. 1848:18 Mwa 48:14Yosefu akamwambia, “Hapana, baba yangu, huyu ndiye mzaliwa wa kwanza; uweke mkono wako wa kuume juu ya kichwa chake.”

1948:19 Mwa 25:23; 12:2Lakini baba yake akakataa, akasema, “Ninajua, mwanangu, ninajua. Yeye pia atakuwa taifa, naye pia atakuwa mkuu. Hata hivyo, ndugu yake mdogo atakuwa mkuu kuliko yeye, nao wazao wake watakuwa kundi la mataifa.” 2048:20 Mwa 24:60Akawabarikia siku ile na kusema,

“Kwa jina lenu Israeli watatamka baraka hii:

‘Mungu na awafanye kama Efraimu na Manase.’ ”

Kwa hiyo akamtanguliza Efraimu mbele ya Manase.

2148:21 Mwa 26:3; 28:13Ndipo Israeli akamwambia Yosefu, “Mimi ninakaribia kufa, lakini Mungu atakuwa pamoja nanyi, na atawarudisha katika nchi ya baba zenu. 2248:22 Yos 24:32; Yn 4:5Kwako wewe, kama aliye juu ya ndugu zako, ninakupa sehemu moja zaidi ya ndugu zako, lile eneo nililoteka kwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”

New International Version – UK

Genesis 48:1-22

Manasseh and Ephraim

1Some time later Joseph was told, ‘Your father is ill.’ So he took his two sons Manasseh and Ephraim along with him. 2When Jacob was told, ‘Your son Joseph has come to you,’ Israel rallied his strength and sat up on the bed.

3Jacob said to Joseph, ‘God Almighty48:3 Hebrew El-Shaddai appeared to me at Luz in the land of Canaan, and there he blessed me 4and said to me, “I am going to make you fruitful and increase your numbers. I will make you a community of peoples, and I will give this land as an everlasting possession to your descendants after you.”

5‘Now then, your two sons born to you in Egypt before I came to you here will be reckoned as mine; Ephraim and Manasseh will be mine, just as Reuben and Simeon are mine. 6Any children born to you after them will be yours; in the territory they inherit they will be reckoned under the names of their brothers. 7As I was returning from Paddan,48:7 That is, North-west Mesopotamia to my sorrow Rachel died in the land of Canaan while we were still on the way, a little distance from Ephrath. So I buried her there beside the road to Ephrath’ (that is, Bethlehem).

8When Israel saw the sons of Joseph, he asked, ‘Who are these?’

9‘They are the sons God has given me here,’ Joseph said to his father.

Then Israel said, ‘Bring them to me so that I may bless them.’

10Now Israel’s eyes were failing because of old age, and he could hardly see. So Joseph brought his sons close to him, and his father kissed them and embraced them.

11Israel said to Joseph, ‘I never expected to see your face again, and now God has allowed me to see your children too.’

12Then Joseph removed them from Israel’s knees and bowed down with his face to the ground. 13And Joseph took both of them, Ephraim on his right towards Israel’s left hand and Manasseh on his left towards Israel’s right hand, and brought them close to him. 14But Israel reached out his right hand and put it on Ephraim’s head, though he was the younger, and crossing his arms, he put his left hand on Manasseh’s head, even though Manasseh was the firstborn.

15Then he blessed Joseph and said,

‘May the God before whom my fathers

Abraham and Isaac walked faithfully,

the God who has been my shepherd

all my life to this day,

16the Angel who has delivered me from all harm

– may he bless these boys.

May they be called by my name

and the names of my fathers Abraham and Isaac,

and may they increase greatly

on the earth.’

17When Joseph saw his father placing his right hand on Ephraim’s head he was displeased; so he took hold of his father’s hand to move it from Ephraim’s head to Manasseh’s head. 18Joseph said to him, ‘No, my father, this one is the firstborn; put your right hand on his head.’

19But his father refused and said, ‘I know, my son, I know. He too will become a people, and he too will become great. Nevertheless, his younger brother will be greater than he, and his descendants will become a group of nations.’ 20He blessed them that day and said,

‘In your48:20 The Hebrew is singular. name will Israel pronounce this blessing:

“May God make you like Ephraim and Manasseh.” ’

So he put Ephraim ahead of Manasseh.

21Then Israel said to Joseph, ‘I am about to die, but God will be with you48:21 The Hebrew is plural. and take you48:21 The Hebrew is plural. back to the land of your48:21 The Hebrew is plural. fathers. 22And to you I give one more ridge of land48:22 The Hebrew for ridge of land is identical with the place name Shechem. than to your brothers, the ridge I took from the Amorites with my sword and my bow.’