Kikombe Cha Fedha Ndani Ya Gunia
1Kisha Yosefu akampa yule msimamizi wa nyumbani mwake maagizo haya: “Jaza magunia ya watu hawa kiasi cha chakula ambacho wanaweza kuchukua, na uweke fedha ya kila mtu kwenye mdomo wa gunia lake. 244:2 Mwa 44:8Kisha weka kikombe changu kile cha fedha kwenye mdomo wa gunia la yule mdogo wa wote pamoja na fedha zake ambazo angenunulia nafaka yake.” Naye akafanya kama Yosefu alivyosema.
344:3 Amu 19:9Kulipopambazuka, hao watu wakaruhusiwa kuondoka pamoja na punda zao. 4Kabla hawajafika mbali kutoka mjini, Yosefu akamwambia mtumishi wake, “Wafuatilie wale watu mara moja, utakapowakuta, waambie, ‘Kwa nini mmelipiza wema kwa ubaya? 544:5 Mwa 30:27Je, kikombe hiki sicho anachonywea bwana wangu na pia hukitumia kwa kutabiri mambo yajayo? Hili ni jambo ovu mlilolitenda.’ ”
6Alipowafikia, akarudia maneno haya kwao. 744:7 Mwa 18:5Lakini wakamwambia mtumishi, “Kwa nini bwana wangu anasema maneno kama haya? Liwe mbali na watumishi wako wasije wakafanya jambo kama hilo! 844:8 Mwa 42:25Hata hivyo tulikurudishia zile fedha kutoka nchi ya Kanaani ambazo tulizikuta kwenye midomo ya magunia yetu. Hivyo kwa nini tuibe fedha au dhahabu kutoka nyumbani kwa bwana wako? 944:9 Mwa 31:32Ikiwa yeyote miongoni mwa watumishi wako atapatikana nacho, auawe, na sisi wengine tutakuwa watumwa wa bwana wangu.”
10Akajibu, “Vema sana; na iwe kama msemavyo. Yeyote atakayekutwa nacho atakuwa mtumwa wangu, lakini ninyi wengine mtakuwa hamna lawama.”
11Kila mmoja wao akafanya haraka kushusha gunia lake chini na kulifungua. 12Ndipo msimamizi akaendelea kutafuta, akianzia kwa mkubwa wa wote na akaishia kwa mdogo wa wote. Basi kikombe kikapatikana katika gunia la Benyamini. 1344:13 Mwa 37:29Kwa jambo hili, wakararua nguo zao. Ndipo wote wakapakiza mizigo yao juu ya punda zao na kurudi mjini.
1444:14 Mwa 33:3Yosefu alikuwa bado yuko nyumbani mwake wakati Yuda na kaka zake walipoingia, wote wakajitupa chini mbele yake. 1544:15 Za 26:6Yosefu akawaambia, “Ni jambo gani hili mlilolifanya? Hamjui kuwa mtu kama mimi anaweza kufahamu mambo kwa njia ya kutabiri?”
1644:16 Mwa 37:8; Za 26:6Yuda akajibu, “Tutaweza kusema nini kwa bwana wangu? Tutaweza kuzungumza nini? Tutawezaje kuthibitisha kwamba hatuna hatia? Mungu amefunua hatia ya watumishi wako. Sasa sisi tu watumwa wa bwana wangu, sisi wenyewe pamoja na yule aliyepatikana na kikombe.”
17Lakini Yosefu alisema, “Liwe mbali nami kufanya jambo kama hili! Mtu yule tu aliyekutwa na kikombe ndiye atakayekuwa mtumwa wangu. Ninyi wengine, rudini kwa baba yenu kwa amani.”
1844:18 Mwa 18:30Ndipo Yuda akamwendea na kumwambia: “Tafadhali bwana wangu, mruhusu mtumishi wako aseme neno kwa bwana wangu. Usimkasirikie mtumishi wako, ingawa wewe ni sawa na Farao mwenyewe. 19Bwana wangu aliwauliza watumishi wake, ‘Mnaye baba au ndugu?’ 2044:20 Mwa 37:3; 42:13Nasi tukakujibu, ‘Tunaye baba yetu ambaye ni mzee; pia yupo mwanawe mdogo aliyezaliwa katika uzee wake. Ndugu yake amekufa, na huyu mdogo ndiye mwana pekee kwa mama yake aliyebaki, naye baba yake anampenda.’
2144:21 Mwa 42:15“Ndipo ulipowaambia watumishi wako, ‘Mleteni kwangu ili niweze kumwona kwa macho yangu mwenyewe.’ 22Nasi tukamwambia bwana wangu, ‘Kijana hawezi kumwacha baba yake; akimwacha, baba yake atakufa.’ 2344:23 Mwa 43:5Lakini ukawaambia watumishi wako, ‘Ndugu yenu mdogo asiposhuka pamoja nanyi, hamtauona uso wangu tena.’ 2444:24 Mwa 43:28Tuliporudi nyumbani kwa mtumwa wako baba yangu, tulimwambia lile bwana wangu alilokuwa amesema.
2544:25 Mwa 42:2“Ndipo baba yetu aliposema, ‘Rudini Misri mkanunue chakula kingine.’ 2644:26 Mwa 43:5Lakini tukamwambia, ‘Hatuwezi kushuka Misri mpaka ndugu yetu mdogo awe pamoja nasi ndipo tutakapokwenda. Hatutaweza kuuona uso wa yule mtu mpaka ndugu yetu mdogo awe pamoja nasi.’
2744:27 Mwa 46:19“Mtumwa wako baba yangu alituambia, ‘Mnajua mke wangu alinizalia wana wawili. 2844:28 Mwa 37:33Mmojawapo alipotea, nami nikasema, “Hakika ameraruliwa vipande vipande.” Nami sijamwona tangu wakati huo. 2944:29 Mwa 42:38Ikiwa mtaniondolea huyu tena na akapatwa na madhara, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini nikiwa mwenye huzuni.’
3044:30 1Sam 18:1“Hivyo sasa, kama kijana hatakuwa pamoja nasi nitakaporudi kwa mtumishi wako baba yangu, na kama baba yangu, ambaye maisha yake yamefungamanishwa na uhai wa kijana huyu, 31akiona kijana hayupo nasi, atakufa. Watumishi wako watashusha kichwa chenye mvi cha baba yetu kaburini kwa huzuni. 32Mtumwa wako alimhakikishia baba yangu usalama wa kijana. Nikamwambia, ‘Kama sikumrudisha kwako nitakuwa mwenye lawama mbele yako, baba yangu, maisha yangu yote!’
33“Sasa basi, tafadhali mruhusu mtumishi abaki hapa kama mtumwa wa bwana wangu badala ya kijana, naye kijana umruhusu arudi na ndugu zake. 34Ninawezaje kurudi kwa baba yangu kama kijana hatakuwa pamoja nami? La hasha! Usiniache nikaone huzuni ile itakayompata baba yangu.”
Josefs silverbägare i Benjamins säck
1Sedan befallde Josef sin närmaste man att fylla alla deras säckar med så mycket säd de kunde föra med sig och han sa till honom att lägga tillbaka vars och ens pengar överst i säckarna. 2Josef gav dessutom order om att hans egen silverbägare skulle läggas överst i Benjamins säck tillsammans med pengarna för säden. Mannen gjorde som han hade blivit tillsagd. 3Tidigt nästa morgon gav sig bröderna iväg med sina åsnor.
4När de hade kommit ett stycke från staden, sa Josef till sin närmaste man: ”Skynda dig efter dem! När du hinner upp dem, fråga varför de lönar gott med ont. 5Säg till dem: ’Är det inte den här som min herre dricker ur och som han tyder tecken med? Det var mycket illa gjort.’ ”
6När mannen hann ifatt dem, sa han till dem allt som han hade fått order om.
7”Hur kan du anklaga oss för något sådant, herre?” frågade de. ”Vi skulle aldrig få för oss att göra något sådant. 8Vi tog ju med oss tillbaka de pengar som vi hittade i våra säckar. Varför skulle vi då stjäla silver eller guld från din husbondes hus? 9Om du hittar bägaren hos någon av oss, dina tjänare, så ska han dö, och alla vi övriga ska bli slavar åt dig, herre.” 10”Bra, det får bli som ni säger. Den som man finner bägaren hos blir min slav”, svarade mannen. ”Ni andra får gå fria.”
11De tog snabbt ned sina säckar från åsneryggarna och öppnade dem. 12Mannen började leta i den äldste broderns säck och slutade hos den yngste. Han hittade slutligen bägaren i Benjamins säck. 13Då slet de sönder sina kläder i förtvivlan, lastade åsnorna igen och återvände till staden. 14Josef var fortfarande hemma när Juda och hans bröder kom, och de föll ned på marken inför honom.
15”Vad är det ni har gjort?” frågade Josef. ”Förstår ni inte att en man som jag kan tyda tecken?” 16Juda svarade: ”Vad ska vi säga, herre? Hur ska vi kunna förklara oss? Hur kan vi bevisa att vi är oskyldiga? Gud har dragit upp dina tjänares skuld. Vi är nu dina slavar, herre, både vi andra och han i vars säck bägaren återfanns.”
17”Aldrig”, sa Josef. ”Bara den som bägaren återfanns hos ska bli min slav. Resten av er kan återvända hem till er far utan att oroa er.”
18Då steg Juda fram och sa: ”Låt mig bara få säga en sak, herre! Ha tålamod med mig bara ett ögonblick, och bli inte vred på din tjänare, fastän du är som farao själv. 19Du frågade oss, herre, om vår far och om vi hade ytterligare någon bror, 20och vi svarade, herre: ’Ja, vår gamle far lever. Han har en son, en yngling, som han fått på gamla dagar. Dennes bror är död, och han är den ende som är kvar av sin mors barn. Hans far älskar honom mycket.’ 21Då sa du till oss, dina tjänare: ’Ta med honom hit, så att jag kan få se honom.’ 22Men vi sa: ’Herre, pojken kan inte lämna sin far, för då kommer hans far att dö.’ 23Men du sa till oss: ’Kom inte tillbaka hit, om ni inte har er yngste bror med er.’ 24Därför återvände vi till vår far, din tjänare, och berättade för honom vad du, herre, hade sagt. 25När han sedan sa: ’Gå tillbaka och köp oss lite mat’, 26svarade vi: ’Vi kan inte resa utan att ta vår yngste bror med oss. Vi får inte visa oss för mannen utan att vår yngste bror är med.’
27Då sa min far, din tjänare, till oss: ’Ni vet att min hustru fick två söner, och att 28en av dem gick bort för att aldrig återvända, förmodligen söndersliten av vilda djur, för jag har aldrig sett honom sedan dess. 29Om ni tar hans bror ifrån mig och något ont drabbar honom också, driver ni er gråhårige far med sorg ner i dödsriket.’ 30Herre, om jag nu går tillbaka till min far och pojken inte är med oss – så fäst som han är vid pojken – 31kommer han att dö när han ser att pojken inte är med oss. Vi, dina tjänare, driver då vår gråhårige far med sorg ner i dödsriket. 32Herre, jag – din tjänare – lovade min far att jag skulle ta ansvaret för pojken. Jag sa till honom, att om jag inte hade honom med mig tillbaka, så skulle jag bära skulden inför honom för alltid. 33Herre, låt mig stanna som slav i stället för pojken, och låt honom få återvända hem med sina bröder. 34Hur skulle jag kunna återvända hem till min far utan honom? Skona mig från att behöva se min fars förtvivlan.”