Mwanzo 42 – NEN & CARST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 42:1-38

Ndugu Za Yosefu Waenda Misri

142:1 Mdo 7:12Wakati Yakobo alipofahamu kuwa kuna nafaka huko Misri, akawaambia wanawe, “Mbona mnakaa tu hapa mnatazamana?” 242:2 Mwa 43:8Akaendelea kuwaambia, “Nimesikia kuwa huko Misri kuna nafaka. Telemkeni huko mkanunue chakula kwa ajili yetu, ili tuweze kuishi wala tusife.”

3Ndipo wale ndugu kumi wa Yosefu, wakateremka huko Misri kununua nafaka. 442:4 Mwa 42:38Lakini Yakobo hakumtuma Benyamini, ndugu yake Yosefu, pamoja na wengine, kwa sababu aliogopa asije akapatwa na madhara. 542:5 Mdo 7:11Hivyo wana wa Israeli walikuwa miongoni mwa wale waliokwenda Misri kununua nafaka, kwani njaa ilikuwa katika nchi ya Kanaani pia.

642:6 Mwa 41:41Wakati huo Yosefu alikuwa mtawala wa nchi ya Misri, naye alikuwa ndiye aliwauzia watu wote nafaka. Kwa hiyo wakati ndugu zake Yosefu walipofika, wakamsujudia hadi nyuso zao zikagusa ardhi. 7Mara Yosefu alipowaona ndugu zake, akawatambua, lakini akajifanya mgeni na kuzungumza nao kwa ukali, akiwauliza, “Ninyi mnatoka wapi?”

Wakamjibu, “Tumetoka katika nchi ya Kanaani kuja kununua chakula.”

8Ingawa Yosefu aliwatambua ndugu zake, wao hawakumtambua. 942:9 Mwa 37:7Ndipo Yosefu alipokumbuka ndoto zake kuwahusu wao, akawaambia, “Ninyi ni wapelelezi! Mmekuja kuangalia mahali ambapo nchi yetu haina ulinzi.”

10Wakamjibu, “Sivyo bwana wangu. Watumishi wako wamekuja kununua chakula. 11Sisi sote ni wana wa baba mmoja. Watumishi wako ni watu waaminifu, wala sio wapelelezi.”

12Akawaambia, “La hasha! Mmekuja kuangalia mahali ambapo nchi yetu haina ulinzi.”

1342:13 Mwa 37:33Lakini wakamjibu, “Watumishi wako walikuwa kumi na wawili, wana wa mtu mmoja ambaye anaishi katika nchi ya Kanaani. Sasa mdogo wetu wa mwisho yupo na baba yetu na mwingine alikufa.”

14Yosefu akawaambia, “Ni sawa kabisa kama nilivyowaambia: Ninyi ni wapelelezi! 1542:15 1Sam 17:55Na hivi ndivyo mtakavyojaribiwa: Hakika kama Farao aishivyo, hamtaondoka mahali hapa mpaka ndugu yenu mdogo aje hapa. 1642:16 Mwa 42:11Tumeni mmoja wenu akamlete huyo ndugu yenu, wengine mtawekwa gerezani, ili maneno yenu yajaribiwe kuona kama mnasema kweli. La sivyo, hakika kama Farao aishivyo ninyi ni wapelelezi!” 1742:17 Mwa 40:4Akawaweka wote chini ya ulinzi kwa siku tatu.

1842:18 Law 25:43Siku ya tatu Yosefu akawaambia, “Fanyeni hili nanyi mtaishi, kwa maana namwogopa Mungu: 19Ikiwa ninyi ni watu waaminifu, mmoja wa ndugu zenu na abaki kifungoni, nanyi wengine pelekeni nafaka kwa jamaa yenu wanaoteseka kwa njaa. 20Lakini ni lazima mniletee ndugu yenu mdogo hapa, ili maneno yenu yathibitike na kwamba msife.” Wakakubali kufanya hivyo.

2142:21 Mwa 45:5Wakaambiana wao kwa wao, “Hakika tunaadhibiwa kwa sababu ya ndugu yetu. Tuliona jinsi alivyohuzunika alipokuwa anatusihi kuponya maisha yake, lakini hatukumsikiliza, hiyo ndiyo sababu dhiki hii imetupata.”

2242:22 Mwa 9:5Reubeni akawajibu, “Sikuwaambieni msitende dhambi dhidi ya kijana? Lakini hamkunisikiliza! Sasa ni lazima tuadhibiwe kwa ajili ya damu yake.” 2342:23 Mwa 11:7Hawakujua kuwa Yosefu angewaelewa, kwa sababu alitumia mkalimani.

2442:24 Mwa 43:14, 23Yosefu akajitenga nao akaanza kulia, kisha akawarudia na kuzungumza nao tena. Akataka Simeoni akamatwe na kufungwa mbele yao.

2542:25 Yer 40:5Yosefu akatoa amri ya kujaza magunia yao nafaka na kuweka fedha ya kila mmoja ndani ya gunia lake, kisha wapewe mahitaji ya njiani. Baada ya kufanyiwa hayo yote, 26wakapakiza nafaka juu ya punda zao, wakaondoka.

2742:27 Isa 1:3Walipofika mahali pa kulala huko njiani mmoja wao akafungua gunia lake ili amlishe punda wake, akakuta fedha yake kwenye mdomo wa gunia lake. 2842:28 Mk 5:3Akawaambia ndugu zake, “Fedha yangu imerudishwa. Iko ndani ya gunia langu.”

Mioyo yao ikazimia, na kila mmoja akamgeukia mwenzake wakitetemeka, wakaulizana, “Ni nini hiki Mungu alichotufanyia?”

2942:29 Mwa 44:24Walipofika kwa Yakobo baba yao katika nchi ya Kanaani, wakamweleza mambo yote yaliyowapata. Wakasema, 3042:30 Mwa 42:7“Huyo mtu ambaye ndiye bwana katika nchi hiyo alisema nasi kwa ukali, akatutendea kana kwamba sisi tulikuwa tunaipeleleza nchi. 31Lakini tulimwambia, ‘Sisi ni watu waaminifu, sio wapelelezi. 32Tulizaliwa ndugu kumi na wawili, wana wa baba mmoja. Mmoja alikufa, na mdogo wetu wa mwisho yupo na baba yetu huko Kanaani.’

33“Ndipo huyo mtu aliye bwana katika nchi hiyo alipotuambia, ‘Hivi ndivyo nitafahamu kuwa ninyi ni watu waaminifu: Mwacheni mmoja wa ndugu zenu pamoja nami hapa, kisha nendeni mpeleke chakula kwa ajili ya jamaa yenu inayoteseka kwa njaa. 3442:34 Mwa 34:10Lakini mleteni huyo ndugu yenu mdogo kwangu, ndipo nitajua kuwa ninyi sio wapelelezi, ila ni watu waaminifu. Kisha nitamrudisha ndugu yenu, nanyi mtaweza kufanya biashara katika nchi hii.’ ”

35Walipokuwa wanamimina nafaka kutoka kwenye magunia yao, ndani ya gunia la kila mtu kulikuwa na mfuko wa fedha! Wakati wao na baba yao walipoona mifuko ya fedha, wakaogopa. 3642:36 Mwa 42:24Yakobo baba yao akawaambia, “Ninyi mmenipokonya watoto wangu. Yosefu hayupo na Simeoni hayupo tena na sasa mnataka kumchukua Benyamini. Kila kitu ni kinyume nami!”

37Ndipo Reubeni akamwambia baba yake, “Waweza kuwaua wanangu wote wawili, ikiwa sitamrudisha Benyamini kwako. Mkabidhi Benyamini katika uangalizi wangu, nami nitamrudisha.”

3842:38 Mwa 37:33Lakini Yakobo akasema, “Mwanangu hatashuka huko pamoja nanyi; ndugu yake amekufa naye ndiye peke yake aliyebaki. Ikiwa atapatwa na madhara katika safari mnayoiendea, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini kwa masikitiko.”

Священное Писание (Восточный перевод), версия для Таджикистана

Начало 42:1-38

Первое прибытие братьев Юсуфа в Египет

1Когда Якуб узнал, что в Египте есть зерно, он сказал сыновьям:

– Что вы смотрите друг на друга?

2И продолжил:

– Я слышал, что в Египте есть зерно. Идите и купите его там для нас, чтобы мы выжили и не погибли.

3Десять братьев Юсуфа отправились в Египет, чтобы купить зерна, 4но Вениамина, брата Юсуфа, Якуб не отпустил с остальными, потому что боялся, как бы с ним не случилось беды.

5Так среди многих других и сыновья Исроила пришли покупать зерно, потому что в земле Ханона был голод.

6Юсуф правил всей страной; он и продавал зерно народу по всему Египту, и когда братья Юсуфа пришли, они поклонились ему лицом до земли. 7Как только Юсуф увидел братьев, он сразу узнал их, но притворился незнакомцем и заговорил с ними сурово.

– Откуда вы пришли? – спросил он.

– Из земли Ханона, чтобы купить еды, – ответили они.

8Юсуф узнал своих братьев, но они не узнали его. 9Он вспомнил свои сны про них и сказал:

– Вы шпионы! Вы пришли высмотреть уязвимые места в нашей земле.

10– Что ты, господин, – ответили они, – твои рабы пришли купить еды. 11Мы все сыновья одного отца. Твои рабы честные люди, не шпионы.

12Он сказал им:

– Нет, вы пришли высмотреть, где в нашей земле уязвимые места.

13Но они ответили:

– Рабов твоих было двенадцать братьев, сыновей одного отца, который живёт в земле Ханона. Младший и сейчас с отцом, а одного больше нет.

14Юсуф сказал им:

– Я же сказал, что вы – шпионы! 15И вот как я вас проверю: верно, как и то, что жив фараон, вы не уйдёте отсюда, пока не придёт сюда ваш младший брат. 16Пошлите одного из вас за братом, а остальные будут сидеть в темнице. Так я проверю ваши слова – правду ли вы мне говорите. Если нет, то верно, как и то, что жив фараон, – вы шпионы!

17И он отдал их всех под стражу на три дня.

18На третий день Юсуф сказал им:

– Сделайте, что я скажу, и будете жить, потому что я боюсь Всевышнего. 19Если вы честные люди, пусть один из вас останется здесь в темнице, а остальные пойдут и отнесут зерно вашим голодающим семьям. 20Но вы должны привести ко мне вашего младшего брата, чтобы ваши слова подтвердились и вы остались в живых.

Так они и сделали.

21Они сказали друг другу:

– Ясно, что мы терпим наказание за нашего брата. Мы видели его отчаяние, когда он умолял нас, но мы не стали слушать, и вот нас постигла эта беда.

22Рувим ответил:

– Я же говорил вам – не грешите против мальчика, но вы не послушали! Теперь наступает расплата за его кровь.

23Они и не думали, что Юсуф понимает их, потому что он говорил с ними через переводчика. 24Он отвернулся от них и заплакал, потом снова повернулся и заговорил с ними. Он взял от них Шимона и связал его у них на глазах.

Возвращение в Ханон

25Юсуф приказал наполнить их сумки зерном, положить серебро каждого из них обратно ему в мешок и дать им запасов на дорогу; так и было исполнено. 26Они погрузили зерно на ослов и отправились в путь.

27Когда они остановились на ночлег, один из них развязал мешок, чтобы взять корм для осла, и увидел в отверстии мешка своё серебро.

28– Моё серебро вернулось! – сказал он братьям. – Вот оно, в моём мешке.

Сердце у них замерло; они в страхе повернулись друг к другу и сказали:

– Что это сделал с нами Всевышний?

29Придя к своему отцу Якубу в землю Ханона, они рассказали ему обо всём, что с ними случилось. Они сказали:

30– Человек, который правит той землёй, говорил с нами сурово и принял нас за шпионов. 31Но мы сказали ему: «Мы честные люди, не шпионы. 32Нас было двенадцать братьев, сыновей одного отца. Одного больше нет, а младший сейчас с отцом в Ханоне».

33Тогда человек, который правит той землёй, сказал нам: «Вот как я узнаю, честные вы люди или нет: оставьте одного брата здесь со мной, возьмите еды для ваших голодающих семей и идите своей дорогой; 34но приведите ко мне вашего младшего брата – так я узнаю, что вы не шпионы, а честные люди. Тогда я отдам вам вашего брата и позволю торговать42:34 Или: «свободно передвигаться». в этой земле».

35Разбирая мешки, каждый обнаружил там свой узелок с серебром. Увидев серебро, и они, и их отец испугались.

36Якуб сказал им:

– Вы лишили меня детей. Юсуфа больше нет, и Шимона больше нет, а теперь вы хотите взять Вениамина. Всё обернулось против меня!

37Рувим сказал отцу:

– Предай смерти обоих моих сыновей, если я не приведу его назад к тебе. Поручи его моей заботе, и я приведу его обратно.

38Но Якуб ответил:

– Мой сын не пойдёт туда с тобой; его родной брат мёртв, из детей Рахили он остался один. Если в пути с ним случится беда, то этой скорбью вы сведёте мою седую голову в могилу42:38 Букв.: «в Шеол». Шеол – место, где пребывают души умерших. То же в 44:29, 31..