Mwanzo 4 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Mwanzo 4:1-26

Kaini Na Abeli

14:1 Mwa 2:20; Ebr 11:4; 1Yn 3:12; Yud 11Adamu akakutana kimwili na mkewe Eva, naye akapata mimba, akamzaa Kaini. Eva akasema, “Kwa msaada wa Bwana nimemzaa mwanaume.” 24:2 Mt 23:35; Lk 11:51; Ebr 11:4; 12:24; Mwa 2:7Baadaye akamzaa Abeli ndugu yake.

Basi Abeli akawa mfugaji, na Kaini akawa mkulima. 34:3 Law 2:1-2; Isa 43:23; Yer 41:5; Hes 18:12Baada ya muda Kaini akaleta baadhi ya mazao ya shamba kama sadaka kwa Bwana. 44:4 Law 3:16; 2Nya 29:35; Kut 13:2, 12; Kum 15:19; Ebr 11:4Lakini Abeli akaleta fungu nono kutoka baadhi ya wazaliwa wa kwanza wa mifugo yake. Bwana akamkubali Abeli pamoja na sadaka yake, 5lakini Mungu hakumkubali Kaini pamoja na sadaka yake. Kwa hiyo Kaini akakasirika sana, uso wake ukawa na huzuni.

6Kisha Bwana akamwambia Kaini, “Kwa nini umekasirika? Kwa nini uso wako una huzuni? 74:7 Mwa 44:16; Hes 32:23; Isa 59:12; Ay 11:15; 22:27; Za 27:3; 46:2; Rum 6:16Ukifanya lililo sawa, je, hutakubalika? Lakini usipofanya lililo sawa, dhambi inakuvizia mlangoni mwako, inakutamani wewe, lakini inakupasa uishinde.”

84:8 Mt 23:35; Lk 11:51; 1Yn 3:12; Yud 11Basi Kaini akamwambia ndugu yake Abeli, “Twende shambani.” Walipokuwa shambani, Kaini akamshambulia Abeli ndugu yake, akamuua.

94:9 Mwa 3:9; Yn 8:44Kisha Bwana akamuuliza Kaini, “Ndugu yako Abeli yuko wapi?”

Akamjibu, “Sijui, je, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?”

104:10 Mwa 9:5; 37:20, 26; Kut 21:12; Hes 35:33; Kum 21:7-9; 2Sam 4:11; Ay 16:18; 24:2; 31:38; Za 9:12; 106:38; Ebr 12:24; Ufu 6:9-10Bwana akasema, “Umefanya nini? Sikiliza! Damu ya ndugu yako inanililia mimi kutoka ardhini. 114:11 Kum 11:28; 2Fal 2:24Sasa umelaaniwa na umehamishwa kutoka ardhi, ambayo imefungua kinywa chake na kupokea damu ya ndugu yako kutoka mkononi mwako. 124:12 Kum 28:15-24; Za 37:25; 59:15; 109:10Utakapoilima ardhi, haitakupa tena mazao yake. Utakuwa mtu wa kutangatanga duniani asiye na utulivu.”

13Kaini akamwambia Bwana, “Adhabu yangu ni zaidi ya niwezavyo kustahimili. 144:14 2Fal 17:18; Za 51:11; 139:7-12; Yer 7:15; 52:3; Kum 28:64-67; Mwa 9:6; Kut 21:12-14; Law 24:17; Hes 35:19-21, 27; 1Fal 2:32; 2Fal 11:16Leo unanifukuza kutoka nchi, nami nitafichwa mbali na uwepo wako. Nitakuwa mtu wa kutangatanga asiyetulia duniani na yeyote anionaye ataniua.”

154:15 Eze 9:4, 6; Kut 21:20; Law 26:21; Za 79:12Lakini Bwana akamwambia, “La sivyo, ikiwa mtu yeyote atamuua Kaini atalipizwa kisasi mara saba zaidi.” Kisha Bwana akamwekea Kaini alama ili mtu yeyote ambaye angemwona asimuue. 164:16 Yud 11; Mwa 2:8Kwa hiyo Kaini akaondoka mbele za Bwana akaenda kuishi katika nchi ya Nodi, iliyoko mashariki ya Edeni.

174:17 Za 55:9; 49:11Kaini akakutana kimwili na mkewe, naye akapata mimba na akamzaa Enoki. Wakati huo Kaini alikuwa anajenga mji, akauita Enoki jina la mtoto wake. 18Enoki akamzaa Iradi, Iradi akamzaa Mehuyaeli, Mehuyaeli akamzaa Methushaeli, na Methushaeli akamzaa Lameki.

194:19 Mwa 2:9; 29:28; Kum 21:15; Rut 4:11; 1Sam 1:2Lameki alioa wanawake wawili, mmoja aliitwa Ada, na mwingine Sila. 20Ada akamzaa Yabali ambaye ni baba wa wale walioishi katika mahema na kufuga wanyama. 214:21 Mwa 31:27; Kut 15:20; 1Sam 16:16; 1Nya 25:3; Za 33:2; 43:4; 150:4; Isa 16:11; Dan 3:5; Ay 21:12; 30:31Kaka yake aliitwa Yubali, aliyekuwa baba wa wote wapigao zeze na filimbi. 224:22 Kut 35:35; 1Sam 13:19; 2Fal 24:14Pia Sila alikuwa na mtoto wa kiume aliyeitwa Tubali-Kaini ambaye alifua vifaa vya aina mbalimbali vya shaba na chuma. Naama alikuwa dada wa Tubali-Kaini.

234:23 Mwa 9:6-9; Kut 20:13; 21:12; 23:7; Law 19:18; 24:17; Kum 27:24Lameki akawaambia wake zake,

“Ada na Sila nisikilizeni mimi;

wake wa Lameki sikieni maneno yangu.

Nimemuua mtu kwa kunijeruhi,

kijana mdogo kwa kuniumiza.

244:24 Kum 32:35; 2Fal 9:7; Za 18:47; Isa 35:4; Yer 51:56; Mt 18:22; Nah 1:2Kama Kaini atalipizwa kisasi mara saba,

basi Lameki itakuwa mara sabini na saba.”

254:25 Mwa 5:3; 1Nya 1:1Adamu akakutana kimwili na mke wake tena, akamzaa mwana, akamwita Sethi, akisema, “Mungu amenijalia mwana mwingine badala ya Abeli, kwa kuwa Kaini alimuua.” 264:26 Mwa 5:3; 12:8; 13:4; 21:33; 22:9; 26:25; 33:20; Lk 3:38; Kut 17:15; Sef 3:9; 1Fal 18:24; Za 116:17; Yoe 2:32; Mdo 2:21Naye Sethi akamzaa mwana, akamwita Enoshi.

Wakati huo watu wakaanza kuliitia jina la Bwana.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

創世記 4:1-26

該隱和亞伯

1亞當和他妻子夏娃同房,夏娃便懷孕,生了該隱。她說:「耶和華讓我得了一個男孩。」 2後來,夏娃又生了該隱的弟弟亞伯亞伯做了牧羊人,該隱做了農夫。

3過了些日子,該隱把地裡的出產當祭物獻給耶和華, 4亞伯也把羊群中頭生的羊及其最肥美的部分獻給耶和華。耶和華悅納亞伯和他的祭物, 5卻不悅納該隱和他的祭物。該隱便非常惱火,面色陰沉。 6耶和華問該隱:「你為什麼惱火?為什麼面色陰沉? 7如果你做得對,難道不會蒙悅納嗎?如果你做得不對,罪就蹲伏在你的門口,要控制你,但你必須制伏罪。」

8該隱對弟弟亞伯說:「我們去田間吧!」4·8 「我們去田間吧!」參照《七十士譯本》,希伯來文無此句。他們在田間的時候,該隱動手打亞伯,把他殺了。

9後來,耶和華問該隱:「你弟弟亞伯在哪裡?」他說:「我不知道!難道我是我弟弟的看護人嗎?」 10耶和華說:「你做了什麼事?你弟弟的血從地裡向我哭訴。 11地張開口從你手上接受了你弟弟的血,現在你在地上必受咒詛。 12你種地,地卻不會再為你效力,你必在地上四處漂泊。」 13該隱對耶和華說:「這懲罰太重!我承受不了。 14今天你把我從此地趕出去,使我不能再見你的面。我在地上四處漂泊,見到我的人都會殺我。」 15耶和華對他說:「不會的,因為凡殺你的,必遭受七倍的報應。」於是,耶和華在該隱身上留下一個記號,免得見到他的人殺他。 16該隱離開耶和華,來到伊甸東邊的挪得住下來。

該隱的後代

17該隱和妻子同房,他的妻子就懷孕,生了以諾該隱建了一座城,用他兒子的名字給這城取名叫以諾18以諾以拿以拿米戶雅利米戶雅利瑪土撒利瑪土撒利拉麥19拉麥娶了兩個妻子,一個叫亞大,另一個叫洗拉20亞大生了雅八雅八是遊牧民族的祖先, 21雅八的弟弟叫猶八,他是彈琴吹笛之人的鼻祖。 22洗拉生了土八·該隱,他是打造各種銅鐵器具的匠人4·22 「他是打造各種銅鐵器具的匠人」或譯「他是銅匠、鐵匠的祖先」。,他的妹妹叫拿瑪

23拉麥對他的兩個妻子說:

亞大洗拉,你們聽我的聲音;

拉麥的妻子啊,側耳聽我的話,

有人傷我,我殺了他,

青年打我,我宰了他。

24該隱的遭受七倍的報應,

拉麥的遭受七十七倍的報應。」

塞特和以挪士

25亞當又與妻子夏娃同房,夏娃生了一個兒子,取名叫塞特,因為她說:「上帝賜我另一個兒子來代替亞伯,因為該隱殺了他。」 26塞特生了一個兒子,給他取名叫以挪士。那時候,人開始求告耶和華的名。