Mwanzo 36 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version

Mwanzo 36:1-43

Wazao Wa Esau

(1 Nyakati 1:34-42)

136:1 Mwa 2:4; 25:30Hivi ndivyo vizazi vya Esau (yaani Edomu).

236:2 Mwa 26:34; 28:8-9Esau akaoa wake kutoka miongoni mwa wanawake wa Kanaani: Ada binti wa Eloni Mhiti, Oholibama binti wa Ana, mjukuu wa kike wa Sibeoni Mhivi, 3pia akaoa Basemathi binti wa Ishmaeli, dada yake Nebayothi.

436:4 1Nya 1:35Ada akamzalia Esau Elifazi, Basemathi akamzaa Reueli, 536:5 1Nya 1:35Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wana wa Esau waliozaliwa kwake huko Kanaani.

636:6 Mwa 12:5; 1Nya 1:35Esau akawachukua wake zake, watoto wake wa kiume na wa kike na wote wa nyumbani mwake, mifugo yake pamoja na wanyama wake wengine wote na mali yake yote ambayo alikuwa ameipata akiwa Kanaani, akahamia katika nchi iliyo mbali na Yakobo ndugu yake. 736:7 Mwa 13:6; 27:39Mali zao zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba haikuwa rahisi wao kuishi pamoja, nchi waliyokuwa wakiishi isingewatosha wote kwa ajili ya mifugo yao. 836:8 Kum 2:4Kwa hiyo Esau (ambaye ni Edomu) aliishi katika nchi ya kilima huko Seiri.

936:9 Mwa 2:4Hawa ndio wazao wa Esau, baba wa Waedomu, katika nchi ya kilima cha Seiri.

1036:10 Mwa 36:3Haya ndiyo majina ya wana wa Esau:

Elifazi, mwana wa Esau ambaye mkewe Ada alimzalia; na Reueli, mwana wa Esau ambaye mkewe Basemathi alimzalia.

1136:11 1Nya 1:45Wana wa Elifazi ni:

Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi.

1236:12 Kut 17:8, 16; 1Sam 15:2Elifazi mwana wa Esau alikuwa pia na suria aliyeitwa Timna, ambaye alimzalia Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Ada mke wa Esau.

1336:13 Mwa 36:3Wana wa Reueli ni:

Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Basemathi mkewe Esau.

1436:14 Mwa 36:2Wana wa Oholibama binti Ana, mkewe Esau, aliyekuwa mjukuu wa Sibeoni, aliomzalia Esau ni:

Yeushi, Yalamu na Kora.

1536:15 Mwa 36:19-40; Kut 15:15Hawa ndio waliokuwa wakuu miongoni mwa wazao wa Esau:

Wakuu wa wana wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau ni:

Temani, Omari, Sefo, Kenazi, 1636:16 Mwa 32:3Kora, Gatamu na Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wakuu waliotoka kwa Elifazi huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Ada.

1736:17 1Nya 1:37Wakuu wa wana wa Reueli, mwana wa Esau ni:

Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa Reueli huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Basemathi mkewe Esau.

1836:18 Mwa 36:2Wakuu wa wana wa Esau ambao mkewe Oholibama alimzalia ni:

Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa mke wa Esau, Oholibama binti Ana.

1936:19 1Nya 1:35Hawa ndio waliokuwa wana wa Esau (ndiye Edomu), na hawa ndio waliokuwa wakuu wao.

2036:20 Mwa 14:6Hawa ndio walikuwa wana wa Seiri, Mhori, waliokuwa wakiishi katika nchi ile:

Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana, 2136:21 Mwa 36:30Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio wana wa Seiri huko Edomu waliokuwa wakuu kwa Wahori.

22Wana wa Lotani walikuwa:

Hori na Homamu. Timna alikuwa dada yake Lotani.

23Wana wa Shobali walikuwa:

Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo na Onamu.

2436:24 Mwa 36:2Wana wa Sibeoni walikuwa:

Aiya na Ana. Huyu Ana ndiye aligundua chemchemi ya maji moto jangwani alipokuwa akichunga punda za Sibeoni baba yake.

2536:25 Mwa 36:2Watoto wa Ana walikuwa:

Dishoni na Oholibama binti wa Ana.

26Wana wa Dishoni walikuwa:

Hemdani, Eshbani, Ithrani na Kerani.

27Wana wa Eseri walikuwa:

Bilhani, Zaavani na Akani.

28Wana wa Dishani walikuwa:

Usi na Arani.

2936:29 Mwa 36:20Hawa ndio waliokuwa wakuu wa Wahori:

Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana, 3036:30 Mwa 36:21Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Wahori, kufuatana na makundi yao, katika nchi ya Seiri.

Watawala Wa Edomu

(1 Nyakati 1:43-54)

3136:31 Mwa 17:6Wafuatao ni wafalme waliotawala Edomu kabla ya mfalme yeyote wa Israeli kutawala:

32Bela mwana wa Beori alikuwa mfalme wa Edomu. Mji wake uliitwa Dinhaba.

3336:33 Isa 34:6Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akawa mfalme baada yake.

3436:34 Yer 49:7Yobabu alipofariki, Hushamu kutoka nchi ya Watemani akawa mfalme baada yake.

3536:35 Rut 1:1, 6; Mwa 19:37Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi, aliyeshinda Midiani katika nchi ya Moabu, akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Avithi.

36Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka akawa mfalme baada yake.

3736:37 Mwa 26:22Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi ngʼambo ya Mto Frati akawa mfalme baada yake.

38Shauli alipofariki, Baal-Hanani mwana wa Akbori akawa mfalme baada yake.

39Baal-Hanani mwana wa Akbori alipofariki, Hadadi akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Pau, na mkewe aliitwa Mehetabeli binti Matredi, binti Me-Zahabu.

4036:40 Mwa 36:15Hawa ndio wakuu waliotokana na Esau, kwa majina, kufuatana na koo zao na nchi zao:

Timna, Alva, Yethethi, 41Oholibama, Ela, Pinoni, 42Kenazi, Temani, Mibsari, 4336:43 Mwa 36:9Magdieli na Iramu. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Edomu, kufuatana na makazi yao katika nchi waliyoimiliki.

Huyu ndiye alikuwa Esau, baba wa Waedomu.

Nueva Versión Internacional

Génesis 36:1-43

Descendientes de Esaú

36:10-141Cr 1:35-37

36:20-281Cr 1:38-42

1Esta es la historia de Esaú, es decir, Edom.

2Esaú se casó con mujeres cananeas: con Ada, hija de Elón, el hitita; con Aholibama, hija de Aná y nieta de Zibeón, el heveo; 3y con Basemat, hija de Ismael y hermana de Nebayot.

4Esaú tuvo estos hijos: con Ada tuvo a Elifaz; con Basemat, a Reuel; 5con Aholibama, a Jeús, Jalán y Coré. Estos fueron los hijos que tuvo Esaú mientras vivía en la tierra de Canaán.

6Después Esaú tomó a sus esposas, hijos, hijas y a todas las personas que lo acompañaban, junto con su ganado y todos sus animales, todos los bienes que había adquirido en la tierra de Canaán y se trasladó a otra región para alejarse de su hermano Jacob. 7Los dos habían acumulado tantos bienes que no podían estar juntos; la tierra donde vivían no bastaba para alimentar al ganado de ambos. 8Fue así como Esaú, o sea, Edom, se asentó en la región montañosa de Seír.

9Esta es la historia de Esaú, padre de los edomitas, que habitaron en la región montañosa de Seír.

10Los nombres de sus hijos son estos:

Elifaz, hijo de Ada, esposa de Esaú; y Reuel, hijo de Basemat, esposa de Esaú.

11Los hijos de Elifaz fueron:

Temán, Omar, Zefo, Gatán y Quenaz. 12Elifaz tuvo un hijo con una concubina36:12 Véase nota en Gn 22:24. suya, llamada Timná, al que llamó Amalec. Todos estos fueron nietos de Ada, esposa de Esaú.

13Los hijos de Reuel fueron:

Najat, Zera, Sama y Mizá. Estos fueron los nietos de Basemat, esposa de Esaú.

14Los hijos de la otra esposa de Esaú, Aholibama, que era hija de Aná y nieta de Zibeón:

Jeús, Jalán y Coré.

15Estos fueron los líderes de los descendientes de Esaú:

De los hijos de Elifaz, primogénito de Esaú, los jefes fueron:

Temán, Omar, Zefo, Quenaz, 16Coré, Gatán y Amalec. Estos fueron los jefes de los descendientes de Elifaz en la tierra de Edom; todos ellos fueron nietos de Ada.

17De los hijos de Reuel, hijo de Esaú, los jefes fueron:

Najat, Zera, Sama y Mizá. Estos fueron los jefes de los descendientes de Reuel en la tierra de Edom; todos ellos, nietos de Basemat, esposa de Esaú.

18De los hijos de Aholibama, hija de Aná y esposa de Esaú, los jefes fueron:

Jeús, Jalán y Coré.

19Estos fueron descendientes de Esaú, también llamado Edom, y a su vez jefes de sus respectivas tribus.

20Estos fueron los descendientes de Seír, el horeo, que habitaban en aquella región:

Lotán, Sobal, Zibeón, Aná, 21Disón, Ezer y Disán. Estos descendientes de Seír fueron los jefes de los horeos en la tierra de Edom.

22Hijos de Lotán:

Horí y Homán. Lotán tenía una hermana llamada Timná.

23Hijos de Sobal:

Alván, Manajat, Ebal, Sefó y Onam.

24Hijos de Zibeón:

Ayá y Aná. Este último es el mismo que encontró las aguas termales en el desierto mientras cuidaba los asnos de su padre Zibeón.

25Hijos de Aná:

Disón y Aholibama, hija de Aná.

26Hijos de Disán:

Hemdán, Esbán, Itrán y Querán.

27Hijos de Ezer:

Bilán, Zaván y Acán.

28Hijos de Disán:

Uz y Arán.

29Los jefes de los horeos fueron:

Lotán, Sobal, Zibeón, Aná, 30Disón, Ezer y Disán.

Cada uno de ellos fue jefe de su tribu en la región de Seír.

Los reyes de Edom

36:31-431Cr 1:43-54

31Los reyes que a continuación se mencionan reinaron en la tierra de Edom antes de que los israelitas tuvieran rey:

32Bela, hijo de Beor, que reinó en Edom. El nombre de su ciudad era Dinaba.

33Cuando murió Bela, reinó en su lugar Jobab, hijo de Zera, que provenía de Bosra.

34Cuando murió Jobab, reinó en su lugar Jusán, que provenía de la región de Temán.

35Cuando murió Jusán, reinó en su lugar Hadad, hijo de Bedad. Este derrotó a Madián en el campo de Moab. El nombre de su ciudad era Avit.

36Cuando murió Hadad, reinó en su lugar Samla, que provenía de Masreca.

37Cuando murió Samla, reinó en su lugar Saúl, que provenía de Rejobot, que está junto al río Éufrates.

38Cuando murió Saúl, reinó en su lugar Baal Janán, hijo de Acbor.

39Cuando murió Baal Janán, hijo de Acbor, reinó en su lugar Hadad.36:39 Hadad (mss. hebreos, Pentateuco Samaritano y Siríaca; véase 1Cr 1:50); Hadar (TM). Su ciudad se llamaba Pau y su esposa fue Mehetabel, hija de Matred y nieta de Mezab.

40Estos son los nombres de los jefes que descendieron de Esaú, cada uno según su clan y región:

Timná, Alvá, Jetet,

41Aholibama, Elá, Pinón,

42Quenaz, Temán, Mibzar,

43Magdiel e Iram.

Estos fueron los jefes de Edom, según los lugares que habitaron.

Este fue Esaú, padre de los edomitas.