Mwanzo 29 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Mwanzo 29:1-35

Yakobo Awasili Padan-Aramu

129:1 Mwa 25:6Kisha Yakobo akaendelea na safari yake na akafika kwenye nchi za mataifa ya mashariki. 2Huko akaona kisima katika shamba, pamoja na makundi matatu ya kondoo yamelala karibu na kisima hicho kwa sababu walikuwa wanakunywa maji kutoka kwenye kisimani hicho. Jiwe lililokuwa mdomoni mwa kisima lilikuwa kubwa. 3Wakati kondoo wanapokuwa wamekusanyika hapo, wachungaji huvingirisha jiwe hilo kutoka kwenye mdomo wa kisima na kunywesha kondoo. Kisha hulirudisha jiwe mahali pake juu ya mdomo wa kisima.

429:4 Mwa 42:7; Amu 19:17Yakobo aliwauliza wachungaji, “Ndugu zangu, ninyi mmetoka wapi?”

Wakamjibu, “Tumetoka Harani.”

5Aliwaambia, “Je, mnamjua Labani, mjukuu wa Nahori?”

Wakamjibu, “Ndiyo, tunamfahamu.”

629:6 Mwa 30:22-27; Kut 2:16Kisha Yakobo akawauliza, “Je, yeye ni mzima?”

Wakasema, “Ndiyo, ni mzima, na hapa yuaja Raheli binti yake akiwa na kondoo.”

7Akasema, “Tazama, jua bado liko juu, si wakati wa kukusanya mifugo. Nywesheni kondoo na mwarudishe malishoni.”

8Walijibu, “Haiwezekani, mpaka kondoo wote wakusanyike na jiwe liwe limevingirishwa kutoka mdomo wa kisima. Ndipo tutanywesha kondoo.”

9Alipokuwa akizungumza nao, Raheli akaja pamoja na kondoo wa baba yake, kwa maana alikuwa mchunga kondoo. 10Yakobo alipomwona Raheli binti Labani, ndugu wa mama yake, pamoja na kondoo wa Labani, alikwenda na kulivingirisha jiwe kutoka mdomoni mwa kisima na kuwanywesha kondoo wa mjomba wake. 1129:11 Mwa 33:4Kisha Yakobo akambusu Raheli na akaanza kulia kwa sauti. 1229:12 Mwa 24:28; Lk 15:20Yakobo alikuwa amemwambia Raheli kuwa yeye alikuwa jamaa ya baba yake, na kwamba ni mwana wa Rebeka. Basi Raheli alikimbia na kumweleza baba yake.

1329:13 Mwa 24:29; Lk 15:20Mara Labani aliposikia habari kuhusu Yakobo, mwana wa ndugu yake, aliharakisha kwenda kumlaki. Akamkumbatia na kumbusu, halafu akamleta nyumbani kwake, kisha Yakobo akamwambia mambo yote. 1429:14 Amu 9:2; Isa 58:7Ndipo Labani akamwambia, “Wewe ni nyama yangu na damu yangu mwenyewe.”

Yakobo Awaoa Lea Na Raheli

Baada ya Yakobo kukaa kwa Labani mwezi mzima, 15Labani akamwambia, “Kwa vile wewe ni jamaa yangu, ndiyo sababu unifanyie kazi bila ujira? Niambie ujira wako utakuwa nini.”

1629:16 Mwa 30:9; Rut 4:2, 11Labani alikuwa na binti wawili, binti mkubwa aliitwa Lea na binti mdogo aliitwa Raheli. 17Lea alikuwa na macho dhaifu, lakini Raheli alikuwa na umbo la kupendeza na mzuri wa sura. 1829:18 Mwa 24:67; Hos 12:12Yakobo akampenda Raheli, akamwambia Labani, “Nitakutumikia kwa miaka saba kwa ajili ya kumpata Raheli binti yako mdogo.”

19Labani akasema, “Ni bora zaidi nikupe Raheli kuliko kumpa mtu mwingine yeyote. Kaa pamoja na mimi hapa.” 20Kwa hiyo Yakobo akatumika miaka saba ili kumpata Raheli, lakini ilionekana kwake kama siku chache tu kwa sababu ya upendo wake kwa Raheli.

2129:21 Amu 15:1Ndipo Yakobo akamwambia Labani, “Nipe mke wangu. Muda wangu umekamilika, nami nataka nikutane naye kimwili.”

2229:22 Amu 14:10; Yn 2:1-2Basi Labani akaalika watu wote wa mahali pale na akafanya karamu.

23Lakini ilipofika jioni, akamchukua Lea binti yake akampa Yakobo, naye Yakobo akakutana naye kimwili. 24Naye Labani akamtoa Zilpa, mtumishi wake wa kike, kuwa mtumishi wa Lea, binti yake.

2529:25 Mwa 12:18; 27:36Kesho yake asubuhi, Yakobo akagundua kuwa amepewa Lea! Basi Yakobo akamwambia Labani, “Ni jambo gani hili ulilonitendea? Nilikutumikia kwa ajili ya Raheli, sivyo? Kwa nini umenidanganya?”

2629:26 1Sam 14:49; 2Sam 6:23Labani akajibu, “Si desturi yetu kumwoza binti mdogo kabla ya kumwoza binti mkubwa. 27Maliza juma la arusi ya binti huyu, kisha pia nitakupa huyu binti mdogo, kwa kutumika miaka mingine saba.”

28Naye Yakobo akafanya hivyo. Akamaliza juma na Lea, kisha Labani akampa Raheli binti yake kuwa mke wake. 2929:29 1Nya 5:1; Mwa 16:1Labani akamtoa Bilha mtumishi wake wa kike kwa Raheli ili kuwa mtumishi wake. 30Pia Yakobo akakutana na Raheli kimwili, naye akampenda Raheli zaidi kuliko Lea. Yakobo akamtumikia Labani kwa miaka mingine saba.

Wana Wa Yakobo

3129:31 Kum 21:15-17; Za 127:3Bwana alipoona kwamba Lea hapendwi, akampa watoto, lakini Raheli alikuwa tasa. 3229:32 Mwa 30:23; Hes 1:5Lea akapata mimba akazaa mwana. Akamwita Reubeni,29:32 Reubeni maana yake Ona mwana, yaani Yehova ameangalia taabu yangu. kwa maana alisema, “Ni kwa sababu Bwana ameona huzuni yangu. Hakika mume wangu sasa atanipenda.”

3329:33 Kut 6:15; 1Nya 4:24Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Kwa sababu Bwana alisikia kwamba sipendwi, amenipa tena huyu mwana.” Kwa hiyo akamwita Simeoni.29:33 Simeoni maana yake Anasikia, yaani sasa ataungana nami kama Raheli.

34Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Sasa afadhali mume wangu ataambatana na mimi, kwa sababu nimemzalia wana watatu.” Kwa hiyo akamwita Lawi.29:34 Lawi maana yake Nimeunganishwa, yaani na mume wangu.

3529:35 Mwa 49:8; Mt 1:2-3Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Wakati huu nitamsifu Bwana.” Kwa hiyo akamwita Yuda.29:35 Yuda maana yake Sifa, yaani Nitamsifu Yehova. Kisha akaacha kuzaa watoto.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

创世记 29:1-35

雅各到达舅父家

1雅各继续前行,来到东方人住的地方, 2看见田间有一口井,有三群羊卧在井边,因为当地人用那口井的水饮羊。井口封着一块大石头。 3羊群聚集在井旁的时候,牧人就把井口的石头滚开饮羊,随后再把石头放回原处。

4雅各问牧人:“弟兄们,你们是从哪里来的?”他们说:“我们是从哈兰来的。” 5雅各问道:“你们认识拿鹤的孙子拉班吗?”他们说:“我们认识。” 6雅各又问:“他好吗?”他们回答说:“很好。你看,他的女儿拉结带着羊群来了。” 7雅各对他们说:“太阳还高,不到把羊关起来的时候,你们饮了羊,再放它们去吃草吧!” 8他们说:“不行,要等所有的羊群到齐,把井口的石头滚开后,才能饮羊。”

9雅各还在跟他们说话的时候,拉结就带着她父亲的羊群来到井边,她是个牧羊女。 10雅各看见表妹拉结和舅父拉班的羊群来了,就上前把井口的石头滚开,饮他舅父的羊。 11他亲吻拉结,并放声大哭。 12雅各告诉拉结自己是她父亲的外甥,是利百加的儿子。拉结便跑去告诉她父亲。

13拉班听见外甥雅各来了,就跑去迎接他,拥抱他,亲吻他,然后把他接到自己家里。雅各把事情的经过告诉他。 14拉班说:“你真是我的骨肉至亲啊!”雅各拉班家里住了一个月。

雅各娶妻

15一天,拉班对他说:“虽然我们是亲戚,也不能让你白白地替我工作。告诉我,你希望得到什么报酬?” 16拉班有两个女儿,大的叫利亚,小的叫拉结17利亚两眼无神29:17 “两眼无神”或译“两眼很美丽”。,而拉结长得美丽多姿。 18雅各爱上了拉结,于是对拉班说:“我愿意为你工作七年,请把你小女儿拉结许配给我。” 19拉班说:“把她嫁给你比嫁给外人好,你就留下来吧!” 20雅各为了拉结拉班工作了七年。因为他深爱拉结,所以这七年在他眼中就像短短的几天。

21一天,雅各拉班说:“期限已经满了,现在请把我妻子给我,我好和她同房。” 22于是,拉班就摆设宴席款待当地的人。 23到了晚上,拉班却把女儿利亚交给雅各雅各和她同房。 24拉班又把自己的婢女悉帕送给女儿利亚做婢女。

25早上,雅各才发现娶的是利亚,就对拉班说:“你对我做的是什么事啊!我服侍你不就是为了拉结吗?你为什么骗我?” 26拉班说:“依照本地的习俗,妹妹不能比姐姐先出嫁。 27等这女儿七天的婚期过了,我就把那个女儿也许配给你,你再替我工作七年。”

28雅各同意了。过了七天,拉班把女儿拉结嫁给雅各29又把自己的婢女辟拉送给拉结30雅各也和拉结同房,他深爱拉结胜过爱利亚。他又替拉班工作了七年。

雅各的儿女

31耶和华看见利亚失宠,就使利亚生育,但拉结却不生育。 32利亚怀孕生了一个儿子,给孩子取名叫吕便29:32 “吕便”意思是“看,一个儿子”,此词发音像希伯来文“他看见了我的痛苦”一词的发音。。她说:“耶和华看见了我的痛苦,现在我丈夫一定会爱我。” 33她又怀孕生了一个儿子,就说:“耶和华听见我失宠,所以又给我这个儿子。”于是,她给孩子取名叫西缅29:33 “西缅”意思是“听见”。34她又再度怀孕,生了一个儿子,就说:“这次我丈夫一定会依恋我,因为我给他生了三个儿子。”于是,他给孩子取名叫利未29:34 “利未”意思是“联合”。35后来,利亚再次怀孕,生了一个儿子,她说:“这次我要赞美耶和华!”于是,她给孩子取名叫犹大29:35 “犹大”意思是“赞美”。。之后,利亚停止了生育。