Mwanzo 22 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Mwanzo 22:1-24

Kujua Uthabiti Wa Abrahamu

122:1 Kut 15:25; 16:4; 20:20; Kum 8:2, 16; 13:3; Amu 2:22; 3:1; 2Nya 32:31; Za 66:10; Ebr 11:17; Yak 1:12-13; Mwa 31:11; 46:2; 1Sam 3:4-8; Isa 6:8Baadaye Mungu akamjaribu Abrahamu. Akamwambia, “Abrahamu!”

Abrahamu akajibu, “Mimi hapa.”

222:2 Yn 3:16; Ebr 11:17; 1Yn 4:9; Mwa 8:20Kisha Mungu akamwambia, “Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, Isaki umpendaye, uende katika nchi ya Moria. Mtoe huko kama sadaka ya kuteketezwa juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.”

322:3 Yos 8:10Abrahamu akaamka asubuhi na mapema siku iliyofuata, akamtayarisha punda wake. Akawachukua watumishi wake wawili pamoja na Isaki mwanawe. Baada ya kuchanja kuni za kutosha kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka kuelekea mahali Mungu alipokuwa amemwambia. 4Siku ya tatu Abrahamu akainua macho, akapaona mahali pale kwa mbali. 522:5 Kut 24:14Akawaambia watumishi wake, “Kaeni hapa pamoja na punda, wakati mimi na kijana tunakwenda kule. Tutakwenda kuabudu na kisha tutawarudia.”

622:6 Yn 19:17; Amu 19:29Abrahamu akachukua kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, akamtwika Isaki mwanawe, yeye mwenyewe akachukua moto na kisu. Walipokuwa wakienda pamoja, 722:7 Kut 29:38-42; Law 1:10; Ufu 13:8Isaki akanena akamwambia Abrahamu baba yake, “Baba yangu!”

Abrahamu akaitika, “Mimi hapa, mwanangu.”

Isaki akasema, “Moto na kuni zipo, Je, yuko wapi mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa?”

822:8 Yn 1:29Abrahamu akajibu, “Mwanangu, Mungu mwenyewe atajipatia mwana-kondoo kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa.” Nao hawa wawili wakaendelea mbele pamoja.

922:9 Mwa 4:26; 8:20; Law 1:7; 1Fal 18:33; Ebr 11:17-19; Yak 2:21Walipofika mahali pale alipokuwa ameambiwa na Mungu, Abrahamu akajenga madhabahu hapo, akaziweka kuni juu yake. Akamfunga Isaki mwanawe na akamlaza kwenye madhabahu, juu ya zile kuni. 1022:10 Mwa 18:19Kisha akanyoosha mkono wake na akachukua kisu ili amchinje mwanawe. 1122:11 Mwa 16:7; 21:17; 46:2Lakini malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akamwambia, “Abrahamu! Abrahamu!”

Akajibu, “Mimi hapa.”

1222:12 Mwa 18:19; 42:18; Kut 18:21; 1Sam 15:22; Ay 1:1; 37:24; Mit 8:13; Yak 2:21-23; Yn 3:16; 1Yn 4:9Akamwambia, “Usimdhuru kijana, wala usimtendee jambo lolote. Sasa ninajua kwamba unamcha Mungu, kwa sababu hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee.”

1322:13 Mwa 8:20; Rum 8:32Abrahamu akainua macho yake, akaona kondoo dume amenaswa pembe zake nyuma yake katika kichaka. Akaenda akamchukua huyo kondoo dume, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe. 1422:14 Kut 17:15; Amu 6:24; Isa 30:29Abrahamu akapaita mahali pale Yehova-Yire.22:14 Yehova-Yire maana yake Bwana atatupa. Mpaka siku ya leo inasemekana, “Katika mlima wa Bwana itapatikana.”

1522:15 Mwa 21:17Basi malaika wa Bwana akamwita Abrahamu kutoka mbinguni mara ya pili, 1622:16 Kut 13:11; 32:13; 33:1; Isa 45:23; 62:8; Yer 22:5; 44:26; 49:13; 51:14; Amo 6:8; Ebr 6:13; Lk 1:73akasema, “Ninaapa kwa nafsi yangu, asema Bwana, kwamba kwa sababu umefanya jambo hili na hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee, 1722:17 Mwa 12:2; 15:5; 26:24; 24:60; Ebr 6:14; Kut 32:13; Kum 7:7; 28:62; Hos 1:10; Rum 9:27; Ebr 11:12; Es 9:2hakika nitakubariki, na nitauzidisha uzao wako kama nyota za angani na kama mchanga ulioko pwani. Wazao wako watamiliki miji ya adui zao, 1822:18 Mwa 12:2-3; 17:2, 9; Mdo 3:25; Gal 3:8; Za 105:9na kupitia uzao wako mataifa yote duniani yatabarikiwa, kwa sababu umenitii.”

1922:19 Mwa 21:14; 26:23; 28:10Ndipo Abrahamu akawarudia watumishi wake, wakaondoka wakaenda wote pamoja mpaka Beer-Sheba. Abrahamu akaishi huko Beer-Sheba.

Wana Wa Nahori

2022:20 Mwa 11:29Baada ya muda, Abrahamu akaambiwa, “Milka pia amepata watoto, amemzalia ndugu yako Nahori wana: 2122:21 Mwa 10:23; Ay 32:2; Yer 25:23Usi mzaliwa wake wa kwanza, Buzi nduguye, Kemueli (baba wa Aramu), 2222:22 Mwa 24:15, 47; 25:20Kesedi, Hazo, Pildashi, Yidlafu na Bethueli.” 2322:23 Mwa 24:15; 11:29Bethueli akamzaa Rebeka. Milka alimzalia Nahori nduguye Abrahamu hao wana wanane. 2422:24 Mwa 25:6; 35:22; 36:12; Amu 8:31; 2Sam 3:7; 1Fal 2:22; 11:3; 1Nya 1:32; Wim 6:8Suria wake Nahori aliyeitwa Reuma pia alikuwa na wana: Teba, Gahamu, Tahashi na Maaka.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

創世記 22:1-24

上帝考驗亞伯拉罕

1這些事以後,上帝要考驗亞伯拉罕,就呼喚他:「亞伯拉罕!」他回答說:「我在這裡。」 2上帝說:「帶著你的兒子,你的獨生子,你疼愛的以撒前往摩利亞,在我指示你的山上把他獻為燔祭。」 3亞伯拉罕清早起來,準備好驢,劈好獻燔祭用的柴,帶著兩個僕人和兒子以撒動身前往上帝指示他的地方。 4到了第三天,亞伯拉罕抬頭遠遠看見那地方, 5就對僕人說:「你們和驢在這裡等著,我和孩子到那邊敬拜上帝,然後便回來。」

6亞伯拉罕把獻燔祭用的柴放在兒子以撒肩上,自己手裡拿著火種和刀。父子二人一同向前走。 7以撒說:「父親。」亞伯拉罕說:「兒子,什麼事?」以撒說:「你看,火種和柴都有了,但獻燔祭用的羊羔在哪裡呢?」 8亞伯拉罕說:「兒子,上帝會親自預備獻燔祭的羊羔。」二人就一同向前走。

9他們到了上帝指示的地方,亞伯拉罕就築起祭壇,把柴擺在上面,然後把以撒捆起來放在祭壇上面的柴上。 10亞伯拉罕伸手拿起刀來,要殺他的兒子。 11耶和華的天使從天上呼喚他說:「亞伯拉罕亞伯拉罕!」他回答說:「我在這裡。」 12天使說:「不可動孩子,不可傷害他!現在我知道你敬畏上帝,因為你不惜把你的兒子,你的獨生子獻給我。」 13這時亞伯拉罕抬頭一看,見有一隻公綿羊兩角卡在稠密的樹叢中,於是把羊取來代替他的兒子獻為燔祭。 14亞伯拉罕稱那地方為「耶和華以勒22·14 「耶和華以勒」或譯「耶和華必預備」。。直到今天人們還說:「在耶和華的山上必有預備。」

15耶和華的天使再次從天上呼喚亞伯拉罕16對他說:「耶和華說,『你既然不惜獻上你的兒子,你的獨生子,我憑自己起誓, 17我必賜福給你,使你的後裔多如天上的星和海邊的沙。你的後裔必奪取仇敵的城池, 18天下萬國必因你的後裔而蒙福,因為你聽從了我的話。』」 19於是,亞伯拉罕回到僕人那裡,他們一同返回亞伯拉罕居住的別示巴

拿鶴的後代

20過了些日子,有人告訴亞伯拉罕:「密迦為你兄弟拿鶴生了幾個兒子, 21長子烏斯烏斯的弟弟布斯亞蘭的父親基姆利22基薛哈瑣必達益拉彼土利。」 23彼土利利百加的父親。密迦亞伯拉罕的兄弟拿鶴生了這八個兒子。 24拿鶴的妾流瑪生了提八迦含他轄瑪迦