Kuzaliwa Kwa Isaki
121:1 Mwa 17:20; 1Sam 2:21; Mwa 8:1; 17:6; 18:14; 4:23; Ebr 11:11Wakati huu Bwana akamrehemu Sara kama alivyokuwa amesema, naye Bwana akamtendea Sara kile alichokuwa ameahidi. 221:2 Mwa 17:19; 30:6; 18:10; Gal 4:22; Ebr 11:11Sara akapata mimba, akamzalia Abrahamu mwana katika uzee wake, majira yale ya Mungu aliomwahidi. 321:3 Mwa 16:11; Yos 24:3Abrahamu akamwita Isaki yule mwana ambaye Sara alimzalia. 421:4 Mwa 17:10-12; Mdo 7:8Isaki alipokuwa na umri wa siku nane, Abrahamu akamtahiri, kama Mungu alivyomwamuru. 521:5 Mwa 12:4; Ebr 6:15Abrahamu alikuwa na miaka 100 wakati Isaki mwanawe alipozaliwa.
621:6 Mwa 17:17; Ay 8:21; Za 126:2; Isa 12:6; 35:2; 44:23; 52:9; 54:1Sara akasema, “Mungu ameniletea kicheko, kila mmoja atakayesikia jambo hili atacheka pamoja nami.” 721:7 Mwa 17:17Akaongeza kusema, “Nani angemwambia Abrahamu kuwa Sara angenyonyesha watoto? Tena nimemzalia mwana katika uzee wake.”
Hagari Na Ishmaeli Wafukuzwa
821:8 1Sam 1:23Mtoto akakua, akaachishwa kunyonya. Siku hiyo Isaki alipoachishwa kunyonya, Abrahamu alifanya sherehe kubwa. 921:9 Mwa 16:15; 39:14; Gal 4:29Lakini Sara aliona kuwa mwana ambaye Hagari, Mmisri, aliyemzalia Abrahamu alikuwa anadhihaki, 1021:10 Mwa 39:17; 25:6; Gal 4:30Sara akamwambia Abrahamu, “Mwondoe mwanamke huyo mtumwa pamoja na mwanawe, kwa kuwa mwana wa mwanamke mtumwa kamwe hatarithi pamoja na mwanangu Isaki.”
1121:11 Mwa 17:18Jambo hili lilimhuzunisha sana Abrahamu kwa sababu lilimhusu mwanawe. 1221:12 Mt 1:2; Rum 9:7; Ebr 11:18Lakini Mungu akamwambia, “Usihuzunike hivyo kwa sababu ya kijana na mtumishi wako wa kike. Sikiliza lolote Sara analokuambia, kwa sababu uzao wako utahesabiwa kupitia kwake Isaki. 1321:13 Mwa 13:16Nitamfanya huyu mwana wa mtumishi wako wa kike kuwa taifa pia, kwa sababu naye ni uzao wako.”
1421:14 Mwa 16:1; 22:19; 26:33; 28:10; 46:1-5; Yos 15:28; 19:2; Amu 20:1; 1Sam 3:20; 1Nya 4:28; Neh 11:27Kesho yake asubuhi na mapema, Abrahamu akachukua chakula na kiriba cha maji, akampa Hagari. Akaviweka mabegani mwa Hagari, akamwondoa pamoja na kijana. Hagari akashika njia, akatangatanga katika jangwa la Beer-Sheba.
15Maji yalipokwisha kwenye kiriba, akamwacha kijana chini ya mojawapo ya vichaka. 1621:16 Yer 6:26; Amo 8:10; Zek 12:10Kisha akajiendea zake akaketi karibu, umbali wa kutupa mshale, akawaza, “Siwezi kumwangalia kijana akifa.” Ikawa alipokuwa ameketi pale karibu, akaanza kulia kwa huzuni.
1721:17 Kut 3:7; Hes 20:16; Za 6:8; Kum 26:7; Mwa 16:7; 22:11, 15; 15:1; 17:20Mungu akamsikia kijana akilia, malaika wa Mungu akamwita Hagari kutoka mbinguni na kumwambia, “Kuna nini Hagari? Usiogope, Mungu amesikia kijana analia akiwa amelala pale. 18Mwinue kijana na umshike mkono, kwa maana nitamfanya kuwa taifa kubwa.”
1921:19 Hes 22:31; Mwa 16:7Ndipo Mungu akamfumbua Hagari macho yake naye akaona kisima cha maji. Hivyo akaenda akajaza kiriba maji na kumpa kijana anywe.
2021:20 Mwa 26:3, 24; 28:15; 39:2; Lk 1:66Mungu akawa pamoja na huyu kijana alipokuwa akiendelea kukua. Aliishi jangwani na akawa mpiga upinde. 2121:21 Mwa 14:6; 24:4, 38; 28:2; 34:4-8; Amu 14:2Alipokuwa akiishi katika Jangwa la Parani, mama yake akampatia mke kutoka Misri.
Mapatano Katika Beer-Sheba
2221:22 Mwa 20:2; 26:26-28; 28:15; 31:3-5, 42; 39:2-3; Za 46:7; 1Sam 3:19; 16:18; Isa 7:14; 8:8-10; 41:10; 43:5Wakati huo Abimeleki na Fikoli mkuu wa majeshi yake wakamwambia Abrahamu, “Mungu yu pamoja nawe katika kila kitu unachofanya. 2321:23 Mwa 25:33; 26:31; 31:53; Yos 2:12; 1Fal 2:8; 1Sam 24:21Sasa niapie hapa mbele za Mungu kwamba hutanitenda hila mimi, watoto wangu wala wazao wangu. Nitendee mimi na nchi ambayo unaishi kama mgeni wema ule ule ambao nimekutendea.”
24Abrahamu akasema, “Ninaapa hivyo.”
2521:25 Mwa 26:15-22Ndipo Abrahamu akalalamika kwa Abimeleki kuhusu kisima cha maji ambacho watumishi wa Abimeleki walikuwa wamekinyangʼanya. 26Lakini Abimeleki akasema, “Sijui ni nani ambaye amefanya hili. Hukuniambia, leo tu ndipo ninasikia habari zake.”
2721:27 Mwa 26:28-31; 31:44, 53Hivyo Abrahamu akaleta kondoo na ngʼombe, akampa Abimeleki, nao watu hawa wawili wakafanya mapatano. 28Abrahamu akatenga kondoo wa kike saba kutoka kwenye kundi, 29Abimeleki akamuuliza Abrahamu, “Ni nini maana ya hawa kondoo wa kike saba uliowatenga peke yao?”
3021:30 Mwa 31:44-52; Isa 19:20; Yos 22:27-34; 24:27; Mal 2:14Abrahamu akamjibu, “Upokee hawa kondoo wa kike saba kutoka mkononi mwangu kama ushahidi kuwa nilichimba kisima hiki.”
31Hivyo mahali pale pakaitwa Beer-Sheba, kwa sababu watu wawili waliapiana hapo.
3221:32 Mwa 10:14; 26:33Baada ya mapatano kufanyika huko Beer-Sheba, Abimeleki na Fikoli mkuu wa majeshi yake wakarudi katika nchi ya Wafilisti. 3321:33 1Sam 22:6; 31:13; Mwa 4:26; Kut 15:18; Kum 32:40; 33:27; Ay 36:26; Za 10:16; 45:6; 90:2; 93:2; 102:24; 103:19; 146:10; Isa 40:28; Yer 10:10; Hab 1:12; 3:6; Ebr 13:8Abrahamu akapanda mti wa mkwaju huko Beer-Sheba, na hapo akaliitia jina la Bwana, Mungu wa milele. 3421:34 Mwa 10:14Naye Abrahamu akakaa katika nchi ya Wafilisti kwa muda mrefu.
Saraʼs zoon Isaak
1Toen deed de Here wat Hij had beloofd: 2Sara raakte in verwachting. Zo schonk ze Abraham op zijn hoge leeftijd nog een zoon en precies op de tijd die de Here had genoemd. 3Abraham noemde de zoon die Sara hem geschonken had, Isaak (dat ‘Gelach’ betekent) 4en acht dagen later besneed hij hem, zoals God had bepaald. 5Abraham was toen honderd jaar oud.
6Sara was trots en blij. ‘God heeft mij vreugde gebracht,’ zei zij. ‘Allen die ervan horen, zullen net zo blij zijn als ik. 7Wie had kunnen dromen dat ik nog een baby zou krijgen? En toch heeft Abraham op zijn oude dag nog een zoon van mij gekregen.’ 8Het kind groeide op en de dag kwam dat hij geen borstvoeding meer nodig had. Bij die gelegenheid hield Abraham een groot feestmaal. 9Sara zag dat Ismaël, de zoon van Hagar, lachte. 10Ze ging naar Abraham en zei: ‘Stuur die slavin en haar zoon weg, want ik wil niet dat mijn zoon Isaak de erfenis deelt met de zoon van een slavin.’ 11Deze eis bracht Abraham in moeilijkheden, want Ismaël was tenslotte zijn zoon.
12Maar God zei tegen hem: ‘U hoeft u geen zorgen te maken over die twee. Doe wat Sara heeft gezegd, want alleen Isaaks kinderen zullen uw nakomelingen genoemd worden. 13Maar ook Hagars zoon zal Ik stamvader van een volk maken, omdat hij ook een zoon van u is.’
14Abraham stond de volgende morgen vroeg op, maakte eten klaar voor onderweg en bond een waterzak op Hagars rug. Zo stuurde hij hen beiden weg. Hagar zwierf door de woestijn van Berseba en wist niet waar zij heen moest. 15Toen het water op was, legde zij het kind onder een struik en ging zelf een eind verderop zitten. 16‘Ik kan niet aanzien hoe hij sterft,’ klaagde zij en barstte in huilen uit.
17God hoorde de jongen schreeuwen en de Engel van God riep Hagar vanuit de hemel toe: ‘Hagar, wat is er aan de hand? U moet niet bang zijn! God heeft het huilen van het kind gehoord. 18Ga naar de jongen toe en troost hem, want Ik zal zijn nakomelingen tot een machtig volk maken.’ 19Toen opende God haar ogen en zij zag een bron. Ze vulde haar waterzak en gaf het kind te drinken. 20-21 God zegende de jongen, die in de woestijn van Paran opgroeide en een uitstekende boogschutter werd. Zijn moeder regelde later voor hem een huwelijk met een Egyptisch meisje.
22In diezelfde tijd brachten koning Abimelech en zijn opperbevelhebber Pichol Abraham een bezoek. De koning zei: ‘Het is duidelijk dat God u overal mee helpt, 23beloof mij daarom dat u mij en mijn opvolgers nooit zult bedriegen, maar altijd op goede voet zult blijven met mijn land. Ik heb u immers ook goed behandeld. Kunt u mij dat bij de naam van God zweren?’ 24Abraham antwoordde: ‘Goed, ik zweer het.’ 25Daarop beklaagde hij zich bij Abimelech over een bron die de dienaren van de koning zich hadden toegeëigend. 26‘U hebt me dat nooit verteld,’ zei de koning. ‘Ik hoor het vandaag voor het eerst. Ik weet niet wie dat gedaan heeft.’ 27Toen schonk Abraham de koning schapen en ossen en zij sloten een verbond.
28-30Abraham hield echter zeven lammeren apart. ‘Waarom doet u dat?’ vroeg de koning verwonderd. ‘Deze lammeren zijn ook voor u,’ zei Abraham, ‘en zij zijn het teken dat ik de put gegraven heb.’ 31Vanaf dat moment werd de plaats Berseba (Put van de Eed) genoemd, want daar sloten Abraham en Abimelech hun verbond. 32Na de plechtigheid keerden Abimelech en Pichol terug naar hun woonplaats. 33Abraham plantte een tamarisk bij de put en aanbad daar de Here, de eeuwige God. 34Abraham bleef nog lange tijd in het land van de Filistijnen wonen.