Mwanzo 14 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 14:1-24

Abramu Amwokoa Loti

114:1 Mwa 10:10, 20Wakati huu Amrafeli mfalme wa Shinari, Arioko mfalme wa Elasari, Kedorlaoma mfalme wa Elamu, na Tidali mfalme wa Goimu 214:2 Mwa 10:19; 13:10kwa pamoja walikwenda kupigana vita dhidi ya Bera mfalme wa Sodoma, Birsha mfalme wa Gomora, Shinabu mfalme wa Adma, Shemeberi mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela (yaani Soari). 314:3 Hes 34:3-12; Kum 3:17; Yos 3:16; 12:3; 15:2-5; 18:19Hawa wote waliotajwa mwishoni waliunganisha majeshi yao kutoka Bonde la Sidimu (yaani Bahari ya Chumvi). 4Walikuwa wametawaliwa na Mfalme Kedorlaoma kwa miaka kumi na miwili, lakini mwaka wa kumi na tatu waliasi.

514:5 Mwa 15:20; Kum 2:10, 11, 20; 3:11-13; Yos 12:4; 13:12; 17:15; 1Nya 20:4Mnamo mwaka wa kumi na nne, Mfalme Kedorlaoma na wafalme waliojiunga naye walikwenda kupigana na kuwashinda Warefai katika Ashtaroth-Kanaimu, Wazuzi katika Hamu, Waemi katika Shawe-Kiriathaimu, 614:6 Mwa 21:21; 36:20; 32:3; 33:14-16; 36:8; Kum 2:11, 22; Yos 11:17; 24:4; 1Nya 4:42; Isa 34:5; Eze 25:8; 35:2; Amo 1:6; Hes 12:16; 10:12; 13:3, 26; Hab 3:3na Wahori katika nchi ya kilima cha Seiri, hadi El-Parani karibu na jangwa. 714:7 Mwa 16:14; 20:1; Hes 13:26; 20:1; 32:8; Kum 1:2; 25:17; 29:23; Yos 10:41; Amu 3:13; 6:3; 10:12; 12:15; 11:16; Za 29:8; 83:7; Kut 17:8; Hes 13:29; 14:25; 24:20; 1Sam 14:48; 15:2; 28:18; 2Sam 1:1; 1Nya 4:43; Hos 11:8Kisha wakarudi wakaenda En-Misfati (yaani Kadeshi), wakashinda nchi yote ya Waamaleki, pamoja na Waamori waliokuwa wakiishi Hasason-Tamari.

814:8 Mwa 13:10; 19:17-29; Hos 11:8; Kum 29:23Ndipo mfalme wa Sodoma, mfalme wa Gomora, mfalme wa Adma, mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela (yaani Soari) wakatoka kupanga majeshi yao kwenye Bonde la Sidimu 914:9 Mwa 10:22dhidi ya Kedorlaoma, mfalme wa Elamu, Tidali mfalme wa Goimu, Amrafeli mfalme wa Shinari, na Arioko mfalme wa Elasari, yaani wafalme wanne dhidi ya wafalme watano. 1014:10 Mwa 11:3; Za 11:1; Yos 2:16; 19:17, 30Basi Bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya lami, nao wafalme wa Sodoma na wa Gomora walipokimbia, baadhi ya watu walitumbukia huko na wengine wakakimbilia vilimani. 11Wale wafalme wanne wakateka mali yote ya Sodoma na Gomora pamoja na vyakula vyao vyote, kisha wakaenda zao. 1214:12 Mwa 11:27Pia walimteka Loti mwana wa ndugu yake Abramu pamoja na mali zake, kwa kuwa alikuwa akiishi Sodoma.

1314:13 Mwa 13:18; 37:28; 39:14-17; 40:15; 41:12; 43:32; Kut 3:18; 1Sam 4:6; 14:11; Hes 13:23; 32:9; Kum 1:24Mtu mmoja aliyekuwa ametoroka akaja kumpa Abramu Mwebrania taarifa. Wakati huu Abramu alikuwa anaishi karibu na mialoni ya Mamre Mwamori, aliyekuwa ndugu yake Eshkoli na Aneri, ambao wote walikuwa wameungana na Abramu. 1414:14 Kum 4:9; 34:1; Mit 22:6; Mwa 12:5; Amu 18:29; 1Fal 15:20Abramu alipopata habari kwamba jamaa yake amechukuliwa mateka, akawaita watu 318 wa nyumbani mwake waliokuwa wamefunzwa kupigana vita, wakawafuatilia hadi Dani. 1514:15 Amu 1:3-8; 7:16; 15:2; 2Sam 8:5; 1Fal 20:34; 2Fal 16:9; Isa 7:8; 8:4; 10:9; 17:1; Yer 49:23, 27; Eze 27:18Wakati wa usiku Abramu aliwagawa watu wake katika vikosi ili awashambulie, na akawafuatilia, akawafukuza hadi Hoba, kaskazini ya Dameski. 1614:16 1Sam 30:8, 18Akarudisha mali zote, na akamrudisha Loti jamaa yake na mali zake, pamoja na wanawake na watu wengine.

1714:17 2Sam 18:18Abramu aliporudi baada ya kumshinda Mfalme Kedorlaoma na wale wafalme waliojiunga naye, mfalme wa Sodoma akatoka kwenda kumlaki katika Bonde la Shawe (yaani Bonde la Mfalme).

1814:18 Za 7:8; 76:2; 104:15; 110:4; Ebr 7:2, 17, 21; 5:6; Mwa 3:19; Amu 9:13; 19:19; Es 1:10; Mit 31:6; Mhu 10:19; Wim 1:2; Dan 7:27Ndipo Melkizedeki mfalme wa Salemu alipoleta mkate na divai. Alikuwa kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana. 1914:19 Ebr 7:6; Mwa 1:1; 24:3; Yos 2:11; Za 148:5; Mt 11:25Naye akambariki Abramu, akisema,

“Abarikiwe Abramu na Mungu Aliye Juu Sana,

Muumba wa mbingu na nchi.

2014:20 Mwa 9:26; 24:27; 28:22; Kum 14:22; 26:12; Lk 18:12; Ebr 7:4Abarikiwe Mungu Aliye Juu Sana,

ambaye amewaweka adui zako mkononi mwako.”

Ndipo Abramu akampa Melkizedeki sehemu ya kumi ya kila kitu.

21Mfalme wa Sodoma akamwambia Abramu, “Nipe hao watu na hizo mali uchukue wewe mwenyewe.”

2214:22 Kut 6:8; Hes 14:30; Neh 9:15; Kum 32:40; Eze 20:5; Dan 12:7; Ufu 10:5-6Lakini Abramu akamwambia mfalme wa Sodoma, “Nimeinua mkono wangu kwa Bwana, Mungu Aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na dunia, na nimeapa 2314:23 1Sam 15:3, 19; 2Fal 5:16; Es 8:11; 9:10-15kwamba sitapokea kitu chochote kilicho chako, hata kama ni uzi au gidamu ya kiatu, ili kamwe usije ukasema, ‘Nimemtajirisha Abramu.’ 2414:24 Mwa 13:18Sitapokea chochote, ila kile tu watu wangu walichokula na sehemu ambayo ni fungu la watu waliokwenda pamoja nami, ambao ni Aneri, Eshkoli na Mamre. Wao na wapewe fungu lao.”

Swedish Contemporary Bible

1 Moseboken 14:1-24

Abram räddar Lot

1Vid den här tiden startade Amrafel, Shinars kung, Arjok, Ellasars kung, Kedorlaomer, Elams kung, och Tidal, Gojims kung, 2ett krig mot Bera, Sodoms kung, Birsha, Gomorras kung, Shinav, Admas kung, Shemever, Sevojims kung och kungen i Bela (som senare kallades Soar).

3Dessa kungar förenade sina arméer i Siddimdalen, dalen vid Döda havet. 4Under tolv år hade de alla varit undersåtar till kung Kedorlaomer, men på det trettonde året gjorde de uppror.

5Under det fjortonde året kom Kedorlaomer dit med sina allierade. Han segrade över refaéerna i Ashterot Karnajim, över suséerna i Ham, över eméerna i Shave Kirjatajim. 6Horéerna, som bodde på berget Seir, drev han ända till El Paran vid öknen.

7De vände sedan om till En Mishpat, som senare kallades Kadesh, och erövrade hela amalekiternas område, liksom amoréernas, som bodde i Haseson Tamar.

8Kungarna i Sodom, Gomorra, Adma, Sevojim och Bela, nuvarande Soar, drog ut och ordnade sina arméer till strid i Siddimdalen 9mot Elams kung Kedorlaomer, Gojims kung Tidal, Shinars kung Amrafel och Ellasars kung Arjok, fem kungar mot fyra. 10Dalen var full av gropar med jordbeck. När armén som tillhörde kungarna i Sodom och Gomorra flydde, föll några i groparna och resten flydde till bergen. 11Segrarna plundrade Sodom och Gomorra och tog med sig all deras egendom och mat. Sedan drog de därifrån.

12De tog också med sig Lot, Abrams brorson, som bodde i Sodom, och allt han ägde. 13En av de män som lyckats fly kom och berättade för hebrén Abram vad som hade hänt. Abram hade slagit läger bland ekarna som tillhörde amorén Mamre, bror till Eshkol och Aner, vilka alla var Abrams allierade.

14När Abram fick reda på att hans brorson Lot hade tagits till fånga, sammankallade han männen som var födda i hans hushåll, 318 män sammanlagt, och förföljde fienderna ända till Dan. 15Den natten delade han upp sina män, och de anföll dem och förföljde den flyende armén till Hova, norr om Damaskus. 16Han fick tillbaka hela bytet som de tagit, brorsonen Lot, och alla Lots ägodelar, kvinnorna och de andra. 17När Abram återvände från sitt anfall mot Kedorlaomer och de andra kungarna, kom kungen i Sodom ut för att möta honom i Shavedalen, som senare kallades Kungsdalen.

18Kungen i Salem14:18 Nuvarande Jerusalem., Melkisedek, som var präst åt Gud den Högste, kom och gav Abram bröd och vin. 19Sedan välsignade Melkisedek Abram:

”Må Gud den Högste, himlens och jordens Skapare,

välsigna Abram!

20Välsignad vare Gud den Högste,

som har överlämnat dina fiender till dig!”

Då gav Abram Melkisedek en tiondel av allting.

21Kungen i Sodom vädjade till Abram: ”Ge mig bara folket. Behåll själv hela bytet.” 22Men Abram svarade honom: ”Jag lyfter min hand och svär vid Herren Gud den Högste, himlens och jordens skapare, 23att jag inte ska ta så mycket som en enda tråd eller sandalrem från dig. Du ska inte kunna säga: ’Jag har gjort Abram rik.’ 24Jag ska ingenting ha. Det räcker med det som mina unga män har ätit av din mat. Men ge en del av bytet till mina stridskamrater Aner, Eshkol och Mamre.”