Mwanzo 13 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version

Mwanzo 13:1-18

Abramu Na Loti Watengana

113:1 Mwa 45:25; 12:9; 11:27Hivyo Abramu akakwea kutoka Misri kwenda Negebu, yeye na mkewe na kila kitu alichokuwa nacho, pia Loti akaenda pamoja naye. 213:2 Mwa 12:5; 26:13; 32:15; Mit 10:22; Ay 1:3; 42:12Wakati huo Abramu alikuwa tajiri sana wa mifugo, fedha na dhahabu.

313:3 Mwa 12:8-9Kutoka Negebu, akapita mahali hadi mahali, hadi akafika Betheli, mahali hapo ambapo mwanzoni alipiga hema lake kati ya Betheli na Ai 413:4 Mwa 12:7; 4:26hapo ambapo alikuwa amejenga madhabahu ya kwanza. Huko Abramu akaliitia jina la Bwana.

513:5 Mwa 11:27Basi Loti, ambaye alikuwa anafuatana na Abramu, alikuwa pia na makundi ya mbuzi, kondoo, ngʼombe na mahema. 613:6 Mwa 12:5; 33:9; 36:7Lakini nchi haikuwatosha kukaa pamoja kwa ajili ya wingi wa mali zao. 713:7 Mwa 26:20-21; 10:18; 15:20; 12:6; 34:30; Hes 20:3; Kut 3:8; Amu 1:4Ukazuka ugomvi kati ya wachunga mifugo wa Abramu na wale wa Loti. Wakati huo, Wakanaani na Waperizi ndio waliokuwa wenyeji wa nchi hiyo.

813:8 Mwa 11:27; 19:9; Mit 15:18; 20:3; Kut 2:14; Hes 16:13; Za 133:1Hivyo Abramu akamwambia Loti, “Pasiwe na ugomvi wowote kati yangu na wewe, wala kati ya wachungaji wangu na wako, kwa kuwa sisi ni ndugu. 913:9 Mwa 20:15; 34:10; 47:6; Yer 40:4Je, nchi yote haiko mbele yako? Tutengane. Kama ukielekea kushoto, nitakwenda kulia; kama ukielekea kulia, mimi nitakwenda kushoto.”

1013:10 1Fal 7:47; 2Nya 4:17; Hes 13:29; 33:48; Mwa 19:22; 2:8-10; 46:7; 14:2, 8Loti akatazama akaona lile bonde lote la Yordani kuwa lilikuwa na maji tele, kama bustani ya Bwana, kama nchi ya Misri, kuelekea Soari. (Hii ilikuwa kabla Bwana hajaharibu Sodoma na Gomora.) 11Hivyo Loti akajichagulia bonde lote la Yordani, akaelekea upande wa mashariki. Watu hao wawili wakatengana: 1213:12 Mwa 10:19; 11:27; 19:17-29; 14:12Abramu akaishi katika nchi ya Kanaani, wakati Loti aliishi miongoni mwa miji ya lile bonde na kupiga mahema yake karibu na Sodoma. 1313:13 Mwa 18:20; 19:4; 19:5; 20:6; 39:9; Isa 1:10; 3:9; Hes 32:23; 1Sam 12:23; 2Sam 12:13; Za 51:4; Eze 16:49-50; 2Pet 2:8Basi watu wa Sodoma walikuwa waovu, wakifanya sana dhambi dhidi ya Bwana.

1413:14 Mwa 28:14; 32:12; 48:16; Kum 3:27; 13:17; Isa 54:3Baada ya Loti kuondoka Bwana akamwambia Abramu, “Ukiwa hapo ulipo, inua macho yako utazame kaskazini na kusini, mashariki na magharibi. 1513:15 Mwa 12:7; Gal 3:16Nchi yote unayoiona nitakupa wewe na uzao wako hata milele. 1613:16 Mwa 12:2; 16:10; 17:20; 21:13-18; 25:16; Hes 23:10Nitaufanya uzao wako uwe mwingi kama mavumbi ya nchi, hivyo kama kuna yeyote awezaye kuhesabu mavumbi, basi uzao wako utahesabika. 1713:17 Mwa 12:7; 15:7; Hes 13:17-25Ondoka, tembea katika marefu na mapana ya nchi, kwa maana ninakupa wewe.”

1813:18 Mwa 8:20; 14:13; 18:1; 23:2, 17, 19; 25:9; 49:30; 50:13; 35:27; Hes 13:22; Yos 10:3, 36; Amu 1:10; 1Sam 30:31; 2Sam 2:1-11; 1Nya 11:1Basi Abramu akaondoa mahema yake, akaenda kuishi karibu na mialoni ya Mamre huko Hebroni, huko akamjengea Bwana madhabahu.

New Russian Translation

Бытие 13:1-18

Разделение Аврама и Лота

1Аврам с женой и всем имуществом отправился из Египта в Негев, и Лот пошел с ним. 2У Аврама теперь было много скота, серебра и золота.

3Из Негева он продолжил путь, пока не пришел в Вефиль, к тому месту, где некогда стоял его шатер, между Вефилем и Гаем, 4к тому месту, где он прежде построил жертвенник. Там Аврам призвал имя Господа.

5У Лота, который кочевал с Аврамом, тоже были стада мелкого и крупного скота и шатры, 6и земля не могла прокормить их обоих: у них было так много всего, что они не могли селиться вместе. 7Между пастухами Аврама и пастухами Лота случился раздор. Хананеи и ферезеи жили тогда в той земле.

8Тогда Аврам сказал Лоту:

— Пусть не будет раздора ни между тобой и мной, ни между твоими пастухами и моими, потому что мы родственники. 9Не вся ли земля перед тобою? Давай разделимся: если ты пойдешь налево, то я поверну направо, а если ты пойдешь направо, то я поверну налево.

10Лот посмотрел и увидел, что вся Иорданская долина до самого Цоара хорошо орошается, как сад Господа13:10 В знач.: «сад Эдем»., как земля египетская. Это было еще до того, как Господь разрушил Содом и Гоморру. 11Лот выбрал себе всю долину Иордана и отправился на восток. Они разделились: 12Аврам жил в земле Ханаанской, а Лот жил среди городов долины, поставив шатры невдалеке от Содома. 13Жители Содома были злы и тяжко грешили против Господа.

14Господь сказал Авраму после того, как Лот отделился от него:

— Оглянись вокруг с того места, где ты сейчас. Посмотри на север и на юг, на восток и на запад. 15Всю землю, которую ты видишь, Я дам тебе и твоему семени навеки. 16Я сделаю твое потомство многочисленным, как земную пыль, так что если кто сможет пересчитать пылинки, то и твое потомство будет пересчитано. 17Иди, пройди по этой земле вдоль и поперек, потому что Я дам ее тебе.

18Аврам свернул шатры и направился жить невдалеке от дубравы Мамре в Хевроне. Он построил там жертвенник Господу.