Mwanzo 11 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Mwanzo 11:1-32

Mnara Wa Babeli

1Wakati huo dunia yote ilikuwa na lugha moja na msemo mmoja. 211:2 Mwa 10:10Watu walipoelekea upande wa mashariki, wakafika kwenye tambarare katika nchi ya Shinari11:2 Shinari ndio Babeli. nao wakaishi huko.

311:3 Kut 1:14; 5:7; Yer 43:9; Isa 9:10; Amo 5:11; Mwa 14:10Wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tufyatue matofali na tuyachome vizuri kwa moto.” Walitumia matofali badala ya mawe, na lami kwa ajili ya kushikamanishia hayo matofali. 411:4 Kum 1:28; 6:10; 9:1; Ay 20:6; Yer 51:53; 31:10; 40:15; Mwa 6:4; 9:19; Kum 30:3; 4:27; 1Fal 22:17; Es 3:8; Za 44:11; Eze 6:8; Yoe 3:2Ndipo wakasema, “Njooni, tujijengee mji wenye mnara ambao utafika hadi mbinguni, ili tujipatie jina tusije tukatawanyika usoni pa dunia yote.”

511:5 Mwa 18:21; Kut 3:6-8; 19:11, 18-20; Za 18:9; 144:5Lakini Bwana akashuka ili auone mji na mnara ambao wanadamu waliokuwa wanaujenga. 6Bwana akasema, “Ikiwa kama taifa moja wanaozungumza lugha moja wameanza kufanya hili, basi hakuna lolote watakalopanga kufanya ambalo halitawezekana kwao. 711:7 Mwa 1:26; 42:23; Kum 28:49; Isa 28:11; 33:19; Yer 5:15; 1Kor 2:11Njooni, tushuke tuvuruge lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”

811:8 Mwa 9:19; Kum 32:8; Lk 1:51Hivyo Bwana akawatawanya kutoka mahali pale kwenda katika dunia yote, nao wakaacha kuujenga huo mji. 911:9 Mwa 10:10; Za 55:9; Mdo 2:5-11; Isa 2:10, 21; 13:14; 24:1Ndiyo maana pakaitwa Babeli, kwa sababu hapo ndipo Bwana alipoivuruga lugha ya dunia nzima. Kutoka hapo Bwana akawatawanya katika uso wa dunia yote.

Shemu Hadi Abramu

(1 Nyakati 1:24-27)

1011:10 Mwa 2:4; Lk 3:36Hivi ndivyo vizazi vya Shemu.

Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi. 11Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

1211:12 Lk 3:35Wakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela. 13Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

14Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi. 15Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

16Eberi alipokuwa na miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi. 17Baada ya Eberi kumzaa Pelegi, aliishi miaka 430, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

18Pelegi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Reu. 19Baada ya Pelegi kumzaa Reu, aliishi miaka 209, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

2011:20 Lk 3:35Reu alipokuwa na miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi. 21Baada ya Reu kumzaa Serugi, aliishi miaka 207, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

2211:22 Lk 3:34Serugi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Nahori. 23Baada ya Serugi kumzaa Nahori, aliishi miaka 200, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

2411:24 Lk 3:34Nahori alipokuwa na miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera. 25Baada ya Nahori kumzaa Tera, aliishi miaka 119, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

2611:26 Lk 3:34; Yos 24:2; 2Fal 19:12; Isa 37:12; Eze 27:23Tera alipokuwa na miaka sabini, akamzaa Abramu, Nahori na Harani.

Wazao Wa Tera

2711:27 Mwa 2:4; 31:53; 12:4; 13:1-5, 8, 12; 14:12; 19:1; Lk 17:28; 2Pet 2:5-7Hawa ndio wazao wa Tera.

Tera aliwazaa Abramu, Nahori na Harani. Harani akamzaa Loti. 2811:28 Mwa 15:7; Neh 9:7; Ay 1:17; 16:11; Eze 23:23; Mdo 7:4Tera alipokuwa bado hai, Harani akafa huko Uru ya Wakaldayo, nchi alimozaliwa. 2911:29 Mwa 22:20-23; 24:10-24; 29:5; 12:5; 16:1; 17:15Abramu na Nahori walioa. Mke wa Abramu aliitwa Sarai, na mke wa Nahori aliitwa Milka; Milka na Iska walikuwa watoto wa Harani. 3011:30 Mwa 16:1; 18:11; 25:21; 29:31; 30:1, 22; Amu 13:2; 1Sam 1:5; Za 113:9Sarai alikuwa tasa, hakuwa na watoto.

3111:31 Mwa 38:11; 10:19; 12:4; 27:43; 28:5-10; 29:4; Law 18:15; 20:21; Rut 1:6, 22; 2:20; 4:15; 1Sam 4:19; 1Nya 2:4; Mik 7:6; Eze 22:11; 27:23; Mdo 7:4; 2Fal 19:12Tera akamchukua Abramu mwanawe, Loti mwana wa Harani mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka kwa pamoja katika Uru ya Wakaldayo kwenda nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani, wakaishi huko.

3211:32 Yos 24:2Tera alikufa huko Harani akiwa na miaka 205.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

创世记 11:1-32

巴别塔

1那时,天下人都用同一种语言,讲同一种话。 2人们向东迁移时,在示拿地区找到一处平原,定居下来。 3他们彼此商量说:“来呀,我们制作砖,把砖烧透吧。”他们用砖作石块,用柏油作灰泥来造塔, 4说:“来吧,让我们造一座城和一座高耸入云的塔,这样我们可以为自己扬名,不致分散在普天之下。” 5耶和华下来察看人建造的城和塔。 6耶和华说:“看啊,他们同属一个民族,都用同一种语言,现在就开始做这样的事,如果继续下去,他们会为所欲为。 7来吧,我们下去变乱他们的语言,使他们彼此言语不通。” 8于是,耶和华把他们从那里分散到普天之下,他们便停止建城了。 9因此,人称那城为巴别,因为耶和华在那里变乱了世人的语言,把他们分散到普天之下。

闪的后代

10以下是的后代。

洪水过后两年,一百岁时生亚法撒11之后又活了五百年,生儿育女。

12亚法撒三十五岁时生沙拉13之后又活了四百零三年,生儿育女。

14沙拉三十岁时生希伯15之后又活了四百零三年,生儿育女。

16希伯三十四岁时生法勒17之后又活了四百三十年,生儿育女。

18法勒三十岁时生拉吴19之后又活了二百零九年,生儿育女。

20拉吴三十二岁时生西鹿21之后又活了二百零七年,生儿育女。

22西鹿三十岁时生拿鹤23之后又活了二百年,生儿育女。

24拿鹤二十九岁时生他拉25之后又活了一百一十九年,生儿育女。

26他拉七十岁后,生了亚伯兰拿鹤哈兰

他拉的后代

27以下是他拉的后代。

他拉亚伯兰拿鹤哈兰哈兰罗得28哈兰比他父亲他拉先去世,他死在自己的家乡迦勒底吾珥29亚伯兰拿鹤都娶了妻子,亚伯兰的妻子名叫撒莱拿鹤的妻子名叫密迦,是哈兰的女儿。哈兰密迦亦迦的父亲。 30撒莱不能生育,没有孩子。

31他拉带着儿子亚伯兰、孙子——哈兰的儿子罗得、儿媳妇——亚伯兰的妻子撒莱,离开迦勒底吾珥前往迦南,他们来到哈兰,在那里定居下来。 32他拉在那里去世,享年二百零五岁11:32 “二百零五岁”有古卷作“一百四十五岁”。