Faida Nyingine Za Hekima
13:1 Kum 30:16; Za 44:17; Mit 4:5Mwanangu, usisahau mafundisho yangu,
bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
23:2 Mit 9:6; 4:10kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako
na kukuletea mafanikio.
33:3 Kum 6:8; Mit 6:21; 2Kor 3:3Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe;
vifunge shingoni mwako,
viandike katika ubao wa moyo wako.
43:4 1Sam 2:26; Lk 2:52; Mdo 2:47Ndipo utapata kibali na jina zuri
mbele za Mungu na mwanadamu.
53:5 Za 4:5; Yer 9:23Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote
wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
63:6 1Nya 28:9; Ay 33:11; Yer 42:3katika njia zako zote mkiri yeye,
naye atayanyoosha mapito yako.
73:7 Isa 5:21; Rum 12:16; Kum 4:6Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe;
mche Bwana ukajiepushe na uovu.
83:8 Za 38:3; Mit 4:22; Ay 21:24Hii itakuletea afya mwilini mwako,
na mafuta kwenye mifupa yako.
93:9 Kut 23:19; 26:1-15Mheshimu Bwana kwa mali zako na
kwa malimbuko ya mazao yako yote;
103:10 Kum 28:8; Za 144:13; Ay 22:21; Mal 3:10-12ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika,
viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.
113:11 Mit 1:8-9; Ay 5:17Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana
na usichukie kukaripiwa naye,
123:12 Mit 13:24; Ufu 3:19; Ay 3:19; 5:17; Ebr 12:5-6kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao,
kama vile baba afanyavyo
kwa mwana apendezwaye naye.
133:13 Mit 8:34, 35Heri mtu yule aonaye hekima,
mtu yule apataye ufahamu,
143:14 Ay 28:15; Mit 16:16kwa maana hekima ana faida kuliko fedha
na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.
153:15 Ay 28:17-19Hekima ana thamani kuliko marijani;
hakuna chochote unachokitamani
kinachoweza kulinganishwa naye.
163:16 1Fal 3:13-14; Mit 8:18Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume;
katika mkono wake wa kushoto
kuna utajiri na heshima.
173:17 Mit 16:7; Mt 11:28-30Njia zake zinapendeza,
mapito yake yote ni amani.
183:18 Mwa 2:9; Ufu 2:7Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia;
wale wamshikao watabarikiwa.
193:19 Ay 28:25-27; Za 104:24; Mit 8:27-29Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia,
kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;
203:20 Kum 33:28; Ay 36:28kwa maarifa yake vilindi viligawanywa,
nayo mawingu yanadondosha umande.
213:21 Mit 1:8-9; 6:20; 4:20-22Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara,
usiache vitoke machoni pako;
223:22 Kum 30:20; Mit 4:20-22ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako
na pambo la neema shingoni mwako.
23Kisha utaenda katika njia yako salama,
wala mguu wako hautajikwaa;
243:24 Law 26:6; Za 3:5; Ay 11:18; Yer 31:25ulalapo, hautaogopa;
ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.
253:25 Za 91:5; 112:7Usiogope maafa ya ghafula
au maangamizi yanayowapata waovu,
263:26 1Sam 2:9kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako
na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.
273:27 Rum 13:7; Gal 6:10Usizuie wema kwa wale wanaostahili
ikiwa katika uwezo wako kutenda.
283:28 Law 19:13; Lk 10:25-37; Kum 24:15Usimwambie jirani yako,
“Njoo baadaye, nitakupa kesho”:
wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.
293:29 Zek 8:17Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako,
ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.
303:30 Rum 12:18Usimshtaki mtu bila sababu,
wakati hajakutenda dhara lolote.
313:31 Za 37:1; Mit 24:1-2Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri
wala kuchagua njia yake iwayo yote,
323:32 Za 101:4; Ay 29:4kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu,
lakini siri yake iko kwa mwenye haki.
333:33 Ay 5:3; Mal 2:2; Zek 5:4Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu,
lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.
343:34 Za 18:25-27; Mt 23:12Huwadhihaki wale wanaodhihaki,
lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.
35Wenye hekima hurithi heshima,
bali huwaaibisha wapumbavu.