Mithali 3 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Mithali 3:1-35

Faida Nyingine Za Hekima

13:1 Kum 30:16; Za 44:17; Mit 4:5Mwanangu, usisahau mafundisho yangu,

bali zitunze amri zangu moyoni mwako,

23:2 Mit 9:6; 4:10kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako

na kukuletea mafanikio.

33:3 Kum 6:8; Mit 6:21; 2Kor 3:3Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe;

vifunge shingoni mwako,

viandike katika ubao wa moyo wako.

43:4 1Sam 2:26; Lk 2:52; Mdo 2:47Ndipo utapata kibali na jina zuri

mbele za Mungu na mwanadamu.

53:5 Za 4:5; Yer 9:23Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote

wala usizitegemee akili zako mwenyewe;

63:6 1Nya 28:9; Ay 33:11; Yer 42:3katika njia zako zote mkiri yeye,

naye atayanyoosha mapito yako.

73:7 Isa 5:21; Rum 12:16; Kum 4:6Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe;

mche Bwana ukajiepushe na uovu.

83:8 Za 38:3; Mit 4:22; Ay 21:24Hii itakuletea afya mwilini mwako,

na mafuta kwenye mifupa yako.

93:9 Kut 23:19; 26:1-15Mheshimu Bwana kwa mali zako na

kwa malimbuko ya mazao yako yote;

103:10 Kum 28:8; Za 144:13; Ay 22:21; Mal 3:10-12ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika,

viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.

113:11 Mit 1:8-9; Ay 5:17Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana

na usichukie kukaripiwa naye,

123:12 Mit 13:24; Ufu 3:19; Ay 3:19; 5:17; Ebr 12:5-6kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao,

kama vile baba afanyavyo

kwa mwana apendezwaye naye.

133:13 Mit 8:34, 35Heri mtu yule aonaye hekima,

mtu yule apataye ufahamu,

143:14 Ay 28:15; Mit 16:16kwa maana hekima ana faida kuliko fedha

na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.

153:15 Ay 28:17-19Hekima ana thamani kuliko marijani;

hakuna chochote unachokitamani

kinachoweza kulinganishwa naye.

163:16 1Fal 3:13-14; Mit 8:18Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume;

katika mkono wake wa kushoto

kuna utajiri na heshima.

173:17 Mit 16:7; Mt 11:28-30Njia zake zinapendeza,

mapito yake yote ni amani.

183:18 Mwa 2:9; Ufu 2:7Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia;

wale wamshikao watabarikiwa.

193:19 Ay 28:25-27; Za 104:24; Mit 8:27-29Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia,

kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;

203:20 Kum 33:28; Ay 36:28kwa maarifa yake vilindi viligawanywa,

nayo mawingu yanadondosha umande.

213:21 Mit 1:8-9; 6:20; 4:20-22Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara,

usiache vitoke machoni pako;

223:22 Kum 30:20; Mit 4:20-22ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako

na pambo la neema shingoni mwako.

23Kisha utaenda katika njia yako salama,

wala mguu wako hautajikwaa;

243:24 Law 26:6; Za 3:5; Ay 11:18; Yer 31:25ulalapo, hautaogopa;

ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.

253:25 Za 91:5; 112:7Usiogope maafa ya ghafula

au maangamizi yanayowapata waovu,

263:26 1Sam 2:9kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako

na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.

273:27 Rum 13:7; Gal 6:10Usizuie wema kwa wale wanaostahili

ikiwa katika uwezo wako kutenda.

283:28 Law 19:13; Lk 10:25-37; Kum 24:15Usimwambie jirani yako,

“Njoo baadaye, nitakupa kesho”:

wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.

293:29 Zek 8:17Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako,

ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.

303:30 Rum 12:18Usimshtaki mtu bila sababu,

wakati hajakutenda dhara lolote.

313:31 Za 37:1; Mit 24:1-2Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri

wala kuchagua njia yake iwayo yote,

323:32 Za 101:4; Ay 29:4kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu,

lakini siri yake iko kwa mwenye haki.

333:33 Ay 5:3; Mal 2:2; Zek 5:4Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu,

lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.

343:34 Za 18:25-27; Mt 23:12Huwadhihaki wale wanaodhihaki,

lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.

35Wenye hekima hurithi heshima,

bali huwaaibisha wapumbavu.