Mithali 26 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Mithali 26:1-28

126:1 Isa 32:6; 1Sam 12:17; Mit 19:10Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno,

ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.

226:2 Hes 23:8; Kum 23:5Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake

au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi,

ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.

326:3 Za 32:9; Mit 10:13Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda,

nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!

426:4 Isa 36:21Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake,

ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.

526:5 Mt 16:14; 21:24-27; Mit 3:7Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake,

ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.

626:6 Mit 10:26Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara,

ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.

726:7 Mit 26:9Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia

ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.

826:8 Mit 26:1Kama kufunga jiwe kwenye kombeo,

ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.

926:9 Mit 26:7Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi

ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.

10Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo,

ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.

1126:11 Kut 8:15; Za 85:8; 2Pet 2:22Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake,

ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.

1226:12 Ufu 3:17; Mit 29:20Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima

machoni pake mwenyewe?

Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.

1326:13 Mit 6:6-11; 24:30-34; 22:13Mvivu husema, “Yuko simba barabarani,

simba mkali anazunguka mitaa!”

1426:14 Mit 6:9Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake,

ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.

1526:15 Mit 19:24Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani,

naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.

16Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe,

kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.

17Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio,

ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.

18Kama mtu mwendawazimu

atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,

1926:19 Efe 5:4ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema,

“Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”

2026:20 Mit 22:10Bila kuni moto huzimika;

pasipo uchongezi ugomvi humalizika.

2126:21 Mit 14:17Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto,

ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.

2226:22 Mit 18:8; Eze 22:9Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu;

huingia sehemu za ndani sana za mtu.

2326:23 Lk 22:48Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo

ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.

2426:24 Za 31:18; 41:6; Mit 10:18; Za 31:18; 41:6Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake,

lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.

2526:25 Za 28:3; Yer 9:4-8Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini,

kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.

26Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu,

lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.

2726:27 Za 7:15-16; 35:8; Mhu 10:8; Mit 28:10; Es 6:13; 7:9Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake,

kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.

2826:28 Mit 13:6; 29:5; Za 12:3Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza,

nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.