120:1 Law 10:9; Hab 2:5; 1Sam 25:36; 1Fal 20:16; Mit 31:4Mvinyo ni mdhihaki na kileo ni mgomvi;
yeyote apotoshwaye navyo hana hekima.
220:2 Mit 8:36; 19:12; Es 7:7Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba;
yeye amkasirishaye hupoteza uhai wake.
320:3 Mwa 13:8; Mit 17:14Ni kwa heshima ya mtu kujitenga ugomvi,
bali kila mpumbavu ni mwepesi kugombana.
420:4 Mit 6:6; Mhu 10:18Mvivu halimi kwa majira;
kwa hiyo wakati wa mavuno hutazama
lakini hapati chochote.
520:5 Za 18:16Makusudi ya moyo wa mwanadamu ni maji yenye kina,
lakini mtu mwenye ufahamu huyachota.
620:6 Za 12:1; Mt 6:2; Mhu 7:28; Lk 18:8Watu wengi hujidai kuwa na upendo usiokoma,
bali mtu mwaminifu ni nani awezaye kumpata?
720:7 Za 26:1; 37:25-26; 112:2Mtu mwenye haki huishi maisha yasiyo na lawama,
wamebarikiwa watoto wake baada yake.
820:8 1Fal 7:7; Mit 25:4-5Wakati mfalme aketipo katika kiti chake cha enzi kuhukumu,
hupepeta ubaya wote kwa macho yake.
920:9 Mhu 7:20; 1Fal 8:46; 1Yn 1:8Ni nani awezaye kusema, “Nimeuweka moyo wangu safi;
mimi ni safi na sina dhambi?”
1020:10 Mit 20:23; 11:1Mawe ya kupimia yaliyo tofauti na vipimo tofauti,
Bwana huchukia vyote viwili.
1120:11 Za 39:1; Mt 7:16Hata mtoto hujulikana kwa matendo yake,
kama tabia yake ni safi na adili.
1220:12 Kut 4:11; Rum 11:26; Za 94:9Masikio yasikiayo na macho yaonayo,
Bwana ndiye alivifanya vyote viwili.
1320:13 Mit 6:11; 19:15; Rum 12:11Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini,
uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.
14“Haifai, haifai!” asema mnunuzi,
kisha huondoka akijisifia ununuzi wake.
1520:15 Ay 28:12, 16, 17, 18, 19Dhahabu kunayo, na marijani kwa wingi,
lakini midomo inenayo maarifa
ni kito cha thamani kilicho adimu.
1620:16 Kut 22:26; Mit 27:13Chukua vazi la yule awekaye dhamana
kwa ajili ya mgeni;
lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo
kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
17Chakula kilichopatikana kwa hila ni kitamu kwa mwanadamu,
bali huishia na kinywa kilichojaa changarawe.
1820:18 Mit 11:14; 24:6Fanya mipango kwa kutafuta mashauri,
ukipigana vita, tafuta maelekezo.
1920:19 Mit 11:13Maneno ya kusengenya husababisha kutokuaminika,
kwa hiyo mwepuke mtu anayezungumza kupita kiasi.
2020:20 Kut 21:17; Mit 30:11; Ay 18:5; Law 20:9Ikiwa mtu atamlaani baba yake au mama yake,
taa yake itazimwa katika giza nene.
2120:21 Mit 28:8; Hab 2:6Urithi upatikanao haraka mwanzoni,
hautabarikiwa mwishoni.
2220:22 Mit 24:29; Yer 42:11; Kum 32:35; Rum 12:17-19Usiseme, “Nitakulipiza kwa ajili ya kosa hili!”
Mngojee Bwana, naye atakuokoa.
2320:23 Kum 25:13Bwana anachukia sana mawe ya kupimia ya udanganyifu,
nazo mizani zisizo halali hazimpendezi.
2420:24 Mit 19:21; Yer 10:23; Rum 8:26Hatua za mtu huongozwa na Bwana.
Anawezaje basi mtu yeyote kuelewa njia yake mwenyewe?
2520:25 Mhu 5:2-5; Yer 44:25Ni mtego kwa mtu kuweka wakfu kitu kwa haraka
na baada ya kitambo kidogo kufikiria tena nadhiri zake.
2620:26 Mit 20:8Mfalme mwenye hekima hupepeta waovu,
hulipitisha gurudumu la kupuria juu yao.
2720:27 Za 119:105; Mit 16:2Taa ya Bwana huchunguza roho ya mwanadamu,
huchunguza utu wake wa ndani.
2820:28 Mit 29:14; Isa 16:5Upendo na uaminifu humweka mfalme salama,
kwa njia ya upendo, kiti chake cha enzi huwa salama.
2920:29 Mit 16:31Utukufu wa vijana ni nguvu zao,
mvi ni fahari ya uzee.
3020:30 Za 51:2; Mit 22:15Mapigo na majeraha huusafisha ubaya,
nayo michapo hutakasa utu wa ndani.