Mithali 2 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Mithali 2:1-22

Faida Za Hekima

12:1 Mit 1:8Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu

na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,

22:2 Mit 22:17kutega sikio lako kwenye hekima

na kuweka moyo wako katika ufahamu,

32:3 Yak 1:5na kama ukiita busara

na kuita kwa sauti ufahamu,

42:4 Ay 3:21; Mt 13:44; 6:19-21na kama utaitafuta kama fedha

na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,

52:5 Kum 4:6ndipo utakapoelewa kumcha Bwana

na kupata maarifa ya Mungu.

62:6 Ay 12:13; Lk 21:15; Yak 1:5Kwa maana Bwana hutoa hekima,

na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.

72:7 Mwa 6:9; 15:1; Mit 30:5-6; Za 84:11Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu,

yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,

82:8 1Sam 2:9; Za 18:25kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki

na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.

92:9 Kum 1:16Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki

na sawa: yaani kila njia nzuri.

102:10 Mit 14:33Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako,

nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.

112:11 Mit 4:6Busara itakuhifadhi

na ufahamu utakulinda.

122:12 Mit 2:16; 3:13-18; 4:5Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu,

kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,

132:13 Mit 4:19; Yn 3:19; Efe 4:18wale waachao mapito yaliyonyooka

wakatembea katika njia za giza,

142:14 Mit 15:21; Yer 11:15wale wapendao kutenda mabaya

na kufurahia upotovu wa ubaya,

152:15 Za 125:5; Mit 21:8ambao mapito yao yamepotoka

na ambao ni wapotovu katika njia zao.

162:16 Mit 6:20-29; 7:5-27Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba,

kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno

ya kushawishi kutenda ubaya,

172:17 Mal 2:14; Mwa 2:24aliyemwacha mwenzi wa ujana wake

na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.

182:18 Mit 5:5; 7:27; 9:18Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo

na mapito yake kwenye roho za waliokufa.

192:19 Mit 5:8; Mhu 7:26; Ebr 13:4Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi,

au kufikia mapito ya uzima.

202:20 Ebr 6:12Hivyo utatembea katika njia za watu wema

na kushikamana na mapito ya wenye haki.

212:21 Za 37:29Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi,

nao wasio na lawama watabakia ndani yake.

222:22 Ay 18:17; Za 37:38; Kum 29:28Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi,

nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.