117:1 Mit 15:16, 17; 16:8Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu
kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
217:2 Mit 10:5; 19:26Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye,
naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
317:3 Mit 27:21; Yer 17:10; 1Pet 1:7; Za 26:2Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu,
bali Bwana huujaribu moyo.
4Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya;
mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
517:5 Mit 14:31; Ay 31:39; Eze 25:3; Oba 1:12Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake;
yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
617:6 Za 125:5; Mit 13:22Wana wa wana ni taji la wazee,
nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
717:7 Mit 16:10Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu:
je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
817:8 Mwa 39:21; Dan 6:3Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho;
kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
917:9 Mit 10:12; 16:28Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo,
bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
10Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua
kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
11Mtu mbaya hupenda kuasi tu;
mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
1217:12 1Sam 25:25Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake,
kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
1317:13 Yer 18:20; 1Sam 19:4; Rum 12:17; Za 109:4-5Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema,
kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
1417:14 Mit 20:3; Mt 5:25-26; Mdo 6:1Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji;
kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
1517:15 Za 94:21; Kut 23:6-7; Mit 18:5; Mao 3:34-36; Isa 5:23Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki,
naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki:
Bwana huwachukia sana wote wawili.
1617:16 Mit 23:23Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu,
wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
1717:17 2Sam 15:21; Mit 27:10Rafiki hupenda wakati wote
naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
1817:18 Mit 6:1-5; 11:5Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani,
naye huweka dhamana kwa jirani yake.
19Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi;
naye ainuaye sana lango lake17:19 Kuinua lango maana yake ni kusema kwa majivuno. hutafuta uharibifu.
20Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa;
naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
2117:21 Mit 10:1Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni;
hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
2217:22 Kut 12:46; Za 22:15Moyo wenye furaha ni dawa nzuri,
bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
2317:23 Kut 18:21; 1Sam 8:3Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri
ili kupotosha njia ya haki.
2417:24 Ay 31:1; Mhu 2:14Mtu wa ufahamu huitazama hekima,
lakini macho ya mpumbavu huhangaika
hadi kwenye miisho ya dunia.
2517:25 Mit 10:1Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake
na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
2617:26 Za 94:21; Mit 18:5Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia,
au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
2717:27 Ay 6:24; Mit 14:29Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia,
naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
2817:28 Ay 2:13; Mit 10:19Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza,
na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.
1Лучше сухая корка с покоем и миром,
чем дом, полный заколотого скота, а в нем — вражда.
2Мудрый слуга будет править беспутным сыном
и получит долю наследства среди братьев.
3Тигель17:3 Сосуд из огнеупорного материала для плавки или прокаливания чего-либо на сильном огне. — для серебра, и для золота — горн плавильный,
а Господь испытывает сердца.
4Нечестивый слушает уста злодея;
лгун внимает пагубному языку.
5Издевающийся над нищим оскорбляет его Создателя,
радующийся несчастью не останется безнаказанным.
6Внуки — венец старикам,
а отцы — гордость своих сыновей.
7Не пристала глупцу высокая речь,
а тем более благородному — лживое слово!
8Взятка — как волшебный камень в глазах дающего ее:
куда он ни повернется, преуспеет.
9Прощающий оскорбление ищет любви,
а напоминающий о нем отталкивает близкого друга.
10Упрек сильнее воздействует на разумного,
чем сто ударов на глупца.
11Только смуты ищет злодей,
и вестник17:11 Или: ангел. безжалостный будет послан против него.
12Лучше встретить медведицу, лишенную медвежат,
чем глупца с его глупостью.
13Если человек воздает за добро злом,
зло не покинет его дома.
14Ссору начать — что плотину пробить;
остановись, прежде чем она вспыхнет.
15Оправдывающий виноватого и обвиняющий невиновного17:15 Или: праведника. —
Господь гнушается их обоих.
16Зачем глупцу на премудрость деньги,
если учиться он не желает?
17Друг любит во всякое время,
и брат рожден разделить беду.
18Лишь неразумный человек дает залог,
чтобы ручаться за другого.
19Кто любит ссоры, тот любит грех;17:19 Или: «Любящий грех, любит ссоры…»
тот, кто бахвалится,17:19 Букв.: кто высоко строит свои ворота. ищет падения.
20Развращенный сердцем не преуспеет;
лживый язык попадет в беду.
21Горе тому, кто родил глупца;
нет радости отцу дурня.
22Веселое сердце исцеляет, как лекарство,
а подавленный дух иссушает кости.
23Нечестивый тайно берет взятку,
чтобы извратить пути правосудия.
24Разумный держит на мудрости взгляд,
а глаза глупца блуждают на краях земли.
25Глупый сын — горе для отца
и горечь для матери.
26Нехорошо и наказывать невиновного,
и знатных бичевать за правду.
27Человек знания осторожен в словах,
и рассудительный — хладнокровен.
28Даже глупца, когда он молчит, сочтут мудрым,
и когда он удерживает язык, — рассудительным.