Mithali 17 – NEN & HTB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 17:1-28

117:1 Mit 15:16, 17; 16:8Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu

kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.

217:2 Mit 10:5; 19:26Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye,

naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.

317:3 Mit 27:21; Yer 17:10; 1Pet 1:7; Za 26:2Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu,

bali Bwana huujaribu moyo.

4Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya;

mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.

517:5 Mit 14:31; Ay 31:39; Eze 25:3; Oba 1:12Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake;

yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.

617:6 Za 125:5; Mit 13:22Wana wa wana ni taji la wazee,

nao wazazi ni fahari ya watoto wao.

717:7 Mit 16:10Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu:

je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!

817:8 Mwa 39:21; Dan 6:3Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho;

kokote kigeukiapo, hufanikiwa.

917:9 Mit 10:12; 16:28Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo,

bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.

10Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua

kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.

11Mtu mbaya hupenda kuasi tu;

mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.

1217:12 1Sam 25:25Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake,

kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.

1317:13 Yer 18:20; 1Sam 19:4; Rum 12:17; Za 109:4-5Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema,

kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.

1417:14 Mit 20:3; Mt 5:25-26; Mdo 6:1Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji;

kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.

1517:15 Za 94:21; Kut 23:6-7; Mit 18:5; Mao 3:34-36; Isa 5:23Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki,

naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki:

Bwana huwachukia sana wote wawili.

1617:16 Mit 23:23Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu,

wakati yeye hana haja ya kupata hekima?

1717:17 2Sam 15:21; Mit 27:10Rafiki hupenda wakati wote

naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.

1817:18 Mit 6:1-5; 11:5Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani,

naye huweka dhamana kwa jirani yake.

19Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi;

naye ainuaye sana lango lake17:19 Kuinua lango maana yake ni kusema kwa majivuno. hutafuta uharibifu.

20Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa;

naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.

2117:21 Mit 10:1Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni;

hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.

2217:22 Kut 12:46; Za 22:15Moyo wenye furaha ni dawa nzuri,

bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.

2317:23 Kut 18:21; 1Sam 8:3Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri

ili kupotosha njia ya haki.

2417:24 Ay 31:1; Mhu 2:14Mtu wa ufahamu huitazama hekima,

lakini macho ya mpumbavu huhangaika

hadi kwenye miisho ya dunia.

2517:25 Mit 10:1Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake

na uchungu kwa yeye aliyemzaa.

2617:26 Za 94:21; Mit 18:5Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia,

au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.

2717:27 Ay 6:24; Mit 14:29Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia,

naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.

2817:28 Ay 2:13; Mit 10:19Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza,

na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.

Het Boek

Spreuken 17:1-28

1Beter een droog stuk brood met vrede erbij, Dan een huis vol feestmaaltijden en twist. 2Een verstandige knecht heeft meer te zeggen dan een ontaarde zoon, En deelt met diens broeders de erfenis. 3De smeltkroes voor het zilver, de oven voor het goud; Maar de harten toetst Jahweh! 4De boosdoener luistert naar zondige taal, De valsaard heeft oor voor heilloze woorden. 5Wie een arme bespot, smaadt zijn Schepper; Wie leedvermaak heeft, blijft niet ongestraft. 6Kleinkinderen zijn de kroon der grijsaards, Vaders de trots van hun kinderen. 7Als oprechte taal een dwaas niet staat, Past een edelman zeker geen leugentaal. 8Het geschenk is een toversteen voor wie het geeft; Waarheen hij zich wendt, hij heeft succes. 9Wie een misdaad bemantelt, zoekt de vrede te bewaren; Wie de zaak weer ophaalt, brengt onenigheid tussen vrienden. 10Op een verstandig mens maakt één vermaning meer indruk, Dan honderd slagen op een dwaas. 11Een boze zoekt enkel verzet; Daarom stuurt men een wreden bode op hem af. 12Beter een berin te ontmoeten, van haar jongen beroofd, Dan een dwaas in zijn dwaasheid. 13Als iemand goed met kwaad vergeldt, Zal van zijn huis het kwaad niet wijken. 14Als ruzie ontstaat, is het hek van de dam; Bind dus in, voor de twist losbarst. 15Wie een boosdoener vrijspreekt en een onschuldige veroordeelt, Zijn beiden een even grote gruwel voor Jahweh. 16Waartoe dient geld in de hand van een dwaas, Om wijsheid te kopen, als hij toch geen verstand heeft? 17Een vriend laat altijd zijn genegenheid blijken, In tijd van nood toont hij zich als een broeder. 18Hoe kortzichtig de mens, die handslag geeft, En zich borg stelt voor zijn naaste. 19Wie op ruzie gesteld is, is op zonde gesteld; Wie hooghartig spreekt, zoekt zijn eigen val. 20Een vals karakter zal geen zegen ondervinden; Wie zijn woorden verdraait, zal in het ongeluk storten. 21Wie een domoor verwekt heeft, heeft zich hartzeer bezorgd; De vader van een zot kent geen vreugde. 22Een blij hart doet het lichaam goed, Neerslachtigheid verdort het gebeente. 23De boze neemt een geschenk uit de buidel aan, Om de wegen van het recht te verdraaien. 24De verstandige houdt de wijsheid voor ogen, De ogen van een domoor dwalen af naar de uithoeken der aarde. 25Een dom kind is een ergernis voor zijn vader, Een verdriet voor haar, die het baarde. 26Onschuldigen beboeten is al niet goed; Maar edele mensen slaan, gaat alle perken te buiten! 27Wie verstandig is, is spaarzaam met zijn woorden; Een man van ervaring is koelbloedig. 28Als hij zwijgt, geldt zelfs een dwaze voor wijs; Als hij zijn mond maar houdt, voor verstandig.