Taabu Ya Israeli
17:1 Yer 2:3; Hos 9:10; Wim 2:13Taabu gani hii niliyo nayo!
Nimefanana na yule akusanyaye
matunda ya kiangazi,
aokotaye masazo baada ya kuvunwa
shamba la mizabibu;
hakuna kishada chenye matunda ya kula,
hakuna hata ile tini ya mwanzoni ninayoitamani.
27:2 Za 10:8; 12:1; 57:6; Yer 2:29; 8:6; 5:26; Mit 6:17; 1Sam 24:11; Hab 1:15; Mik 3:10; Isa 3:5Wanaomcha Mungu wameondolewa kutoka nchi;
hakuna mtu mnyofu hata mmoja aliyebaki.
Watu wote wanavizia kumwaga damu,
kila mmoja anamwinda ndugu yake kwa wavu.
37:3 Mit 4:16; Kut 23:8; Hos 4:18; Isa 1:23; Eze 22:12Mikono yote miwili ni hodari katika kufanya ubaya,
mtawala anadai zawadi,
hakimu anapokea rushwa,
wenye nguvu wanaamuru wanachotaka:
wote wanafanya shauri baya pamoja.
47:4 Hes 33:55; Eze 2:6; Ay 31:14; 2Sam 23:6; Isa 22:5; Hos 9:7Aliye mwema kupita wote kati yao
ni kama mchongoma,
anayeonekana mnyofu zaidi miongoni mwao
ni mbaya kuliko uzio wa miiba.
Siku ya walinzi wako imewadia,
siku atakayokutembelea Mungu.
Sasa ni wakati wao
wa kuchanganyikiwa.
5Usimtumaini jirani;
usiweke matumaini kwa rafiki.
Hata kwa yule alalaye kifuani mwako
uwe mwangalifu kwa maneno yako.
67:6 Eze 22:7; Mwa 9:22-24; Mt 10:21, 35-36; Mk 13:12Kwa kuwa mwana humdharau baba yake,
naye binti huinuka dhidi ya mama yake,
mkwe kuwa kinyume na mama mkwe wake:
adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake hasa.
77:7 Isa 21:8; 25:9; Za 4:3; 130:5Lakini mimi, namtazama Bwana kwa matumaini,
namngoja Mungu Mwokozi wangu;
Mungu wangu atanisikia mimi.
Israeli Atainuka
87:8 Za 20:8; 22:17; 37:24; 37:5, 6; Mit 24:17; Mik 4:11; Mao 4:21; 2Sam 22:29; Isa 9:2Usifurahie msiba wangu, ee adui yangu!
Ingawa nimeanguka, nitainuka.
Japo ninaketi gizani,
Bwana atakuwa nuru yangu.
97:9 Mao 3:39-40; Za 107:10; 119:154; Isa 46:13Kwa sababu nimetenda dhambi dhidi yake,
nitabeba ghadhabu ya Bwana,
mpaka atakaponitetea shauri langu
na kuithibitisha haki yangu.
Atanileta nje kwenye mwanga,
nami nitaiona haki yake.
107:10 Za 35:26; 42:3; Isa 5:5; 51:23; Ay 40:12; Zek 10:5; 2Sam 22:43Kisha adui yangu ataliona
naye atafunikwa na aibu,
yule aliyeniambia,
“Yu wapi Bwana Mungu wako?”
Macho yangu yataona kuanguka kwake,
hata sasa atakanyagwa chini ya mguu
kama tope barabarani.
117:11 Amo 9:11; Isa 54:11Siku ya kujenga kuta zako itawadia,
siku ya kupanua mipaka yako.
127:12 Isa 19:23-25; 11:11; 60:4Siku hiyo watu watakuja kwako
kutoka Ashuru na miji ya Misri,
hata kutoka Misri hadi Frati
na kutoka bahari hadi bahari
na kutoka mlima hadi mlima.
137:13 Isa 3:10-11; Eze 12:19; 33:28-29Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake,
kwa sababu ya matunda ya matendo yao.
Sala Na Sifa
147:14 Za 23:4; 28:9; 95:7; Mik 5:4; 7:14; Hes 23:9; Kum 33:28; Wim 4:1; Isa 33:9; Yer 50:19; Eze 36:11Wachunge watu wako kwa fimbo yako,
kundi la urithi wako,
ambalo linaishi peke yake msituni,
katika nchi ya malisho yenye rutuba.
Waache walishe katika Bashani na Gileadi
kama ilivyokuwa siku za kale.
157:15 Kut 3:20; Za 78:12“Kama siku zile mlipotoka Misri,
nitawaonyesha maajabu yangu.”
167:16 Isa 26:11; Amu 18:19Mataifa yataona na kuaibika,
waliondolewa nguvu zao zote.
Wataweka mikono yao kwenye vinywa vyao
na masikio yao yatakuwa na uziwi.
177:17 Mwa 3:14; 2Sam 22:46; Isa 25:3; 59:19Wataramba mavumbi kama nyoka,
kama viumbe vitambaavyo juu ya ardhi.
Watatoka nje ya mapango yao wakitetemeka;
watamgeukia Bwana Mungu wetu kwa hofu
nao watakuogopa.
187:18 Kut 10:8; 1Sam 2:2; Isa 43:25; 54:9; 57:16; Zek 3:4; Yer 31:20; 50:20; Kut 15:11; 34:6, 7, 9; Za 89:6-8; 103:9; 2Nya 6:21; 30:9; Za 103:8-13; Yoe 2:32; Amo 5:15; Mik 2:12Ni nani Mungu kama wewe,
ambaye anaachilia dhambi
na kusamehe makosa
ya mabaki ya urithi wake?
Wewe huwi na hasira milele,
bali unafurahia kuonyesha rehema.
197:19 Isa 43:25; Rum 6:6; Yer 31:34Utatuhurumia tena,
utazikanyaga dhambi zetu
chini ya nyayo zako,
na kutupa maovu yetu yote
katika vilindi vya bahari.
207:20 Gal 3:16; Kum 11:29; 7:8; Lk 1:72; Za 108:4Utakuwa wa kweli kwa Yakobo,
nawe utamwonyesha Abrahamu rehema,
kama ulivyowaahidi kwa kiapo baba zetu
siku za kale.
فساد اخلاقی اسرائيل
1چه مصيبتی! من مانند شخص گرسنهای هستم كه روی درختان ميوهای نمیيابد و بر تاكها انگوری پيدا نمیكند. هيچ انگور و انجيری بر درختان باقی نمانده است. 2هيچ آدم خوب و پرهیزگاری روی زمين يافت نمیشود. همه قاتلند و برای برادران خود نقشهٔ قتل میكشند. 3دستهايشان برای ارتكاب گناه مهارت دارند. حاكم و قاضی هر دو رشوه میخواهند. آدمهای پولدار به آنها رشوه میدهند و میگويند چه میخواهند و آنها نيز برای انجام خواستههای ايشان نقشه میكشند. 4حتی بهترين ايشان مثل خار میباشد؛ ولی روز مجازات آنها فرا رسيده است و همه آشفته خواهند شد.
5به هيچكس اعتماد نكن، نه به بهترين دوستت و نه حتی به همسرت! 6زيرا در اين روزگار پسر به پدر اهانت میكند، دختر با مادرش مخالفت میورزد و عروس با مادر شوهرش دشمنی میكند. آری، اهل خانهٔ شخص، دشمنان او میباشند.
7و اما من منتظر ياری خداوند هستم. صبر میكنم تا خدا مرا نجات دهد. او دعای مرا مستجاب خواهد فرمود.
نجات قوم اسرائيل
8ای دشمنان به ما نخنديد، زيرا اگرچه به زمين بيفتيم، باز برخواهيم خاست! اگرچه در تاريكی باشيم، خود خداوند روشنايی ما خواهد بود! 9وقتی خداوند ما را تنبيه كند، تحمل خواهيم كرد، زيرا نسبت به او گناه كردهايم. سرانجام او در برابر دشمنانمان از ما حمايت كرده، ايشان را به سبب تمام بديهايی كه به ما روا داشتهاند، مجازات خواهد كرد. خداوند ما را از تاريكی بيرون آورده، در روشنايی قرار خواهد داد و ما شاهد عمل نجاتبخش او خواهيم بود. 10آنگاه دشمنانمان خواهند ديد كه خداوند پشتيبان ماست و از اين كه به ما طعنه زده میگفتند: «خدای شما كجاست؟» شرمنده خواهند شد. آنگاه با چشمان خود خواهيم ديد كه ايشان مثل گل كوچهها پايمال میشوند.
11ای اسرائيل، شهرهايت بزرگتر و بهتر از قبل بازسازی خواهند شد، 12و قوم تو از آشور و مصر، از ناحيهٔ رود فرات، و از درياها و كوهستانهای دور دست نزد تو باز خواهند گشت. 13اما سرزمينهای ديگر به سبب گناهان مردمشان ويران خواهند گرديد.
رحمت خداوند بر اسرائيل
14ای خداوند، بيا و بر قوم خود شبانی كن؛ گلهٔ خود را رهبری فرما و گوسفندانت را كه در جنگل تنها ماندهاند، مانند گذشته به چراگاههای سرسبز و حاصلخيز باشان و جلعاد هدايت كن.
15خداوند در پاسخ میفرمايد: «بلی، مثل زمانی كه شما را از اسارت مصر بيرون آوردم، معجزههای بزرگی برای شما خواهم كرد.»
16مردم جهان كارهای او را خواهند ديد و از قدرت ناچيزشان شرمنده خواهند شد. از ترس دست بر دهان خواهند گذاشت و گوشهايشان كر خواهد شد. 17مثل مار از سوراخهای خود بيرون خزيده، با ترس و لرز در حضور خداوند، خدای ما خواهند ايستاد.
18خداوندا، خدايی مثل تو نيست كه گناه را ببخشد. تو گناهان بازماندگان قوم خود را میآمرزی و تا ابد خشمگين نمیمانی، چون دوست داری رحم كنی. 19بلی، بار ديگر بر ما ترحم خواهی فرمود. گناهان ما را زير پاهای خود لگدمال خواهی كرد و آنها را به اعماق دريا خواهی افكند! 20چنانكه قرنها پيش به يعقوب وعده فرمودی ما را بركت خواهی داد و همانطور كه با پدر ما ابراهيم عهد بستی، بر ما رحم خواهی فرمود.