Mika 7 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Mika 7:1-20

Taabu Ya Israeli

17:1 Yer 2:3; Hos 9:10; Wim 2:13Taabu gani hii niliyo nayo!

Nimefanana na yule akusanyaye

matunda ya kiangazi,

aokotaye masazo baada ya kuvunwa

shamba la mizabibu;

hakuna kishada chenye matunda ya kula,

hakuna hata ile tini ya mwanzoni ninayoitamani.

27:2 Za 10:8; 12:1; 57:6; Yer 2:29; 8:6; 5:26; Mit 6:17; 1Sam 24:11; Hab 1:15; Mik 3:10; Isa 3:5Wanaomcha Mungu wameondolewa kutoka nchi;

hakuna mtu mnyofu hata mmoja aliyebaki.

Watu wote wanavizia kumwaga damu,

kila mmoja anamwinda ndugu yake kwa wavu.

37:3 Mit 4:16; Kut 23:8; Hos 4:18; Isa 1:23; Eze 22:12Mikono yote miwili ni hodari katika kufanya ubaya,

mtawala anadai zawadi,

hakimu anapokea rushwa,

wenye nguvu wanaamuru wanachotaka:

wote wanafanya shauri baya pamoja.

47:4 Hes 33:55; Eze 2:6; Ay 31:14; 2Sam 23:6; Isa 22:5; Hos 9:7Aliye mwema kupita wote kati yao

ni kama mchongoma,

anayeonekana mnyofu zaidi miongoni mwao

ni mbaya kuliko uzio wa miiba.

Siku ya walinzi wako imewadia,

siku atakayokutembelea Mungu.

Sasa ni wakati wao

wa kuchanganyikiwa.

5Usimtumaini jirani;

usiweke matumaini kwa rafiki.

Hata kwa yule alalaye kifuani mwako

uwe mwangalifu kwa maneno yako.

67:6 Eze 22:7; Mwa 9:22-24; Mt 10:21, 35-36; Mk 13:12Kwa kuwa mwana humdharau baba yake,

naye binti huinuka dhidi ya mama yake,

mkwe kuwa kinyume na mama mkwe wake:

adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake hasa.

77:7 Isa 21:8; 25:9; Za 4:3; 130:5Lakini mimi, namtazama Bwana kwa matumaini,

namngoja Mungu Mwokozi wangu;

Mungu wangu atanisikia mimi.

Israeli Atainuka

87:8 Za 20:8; 22:17; 37:24; 37:5, 6; Mit 24:17; Mik 4:11; Mao 4:21; 2Sam 22:29; Isa 9:2Usifurahie msiba wangu, ee adui yangu!

Ingawa nimeanguka, nitainuka.

Japo ninaketi gizani,

Bwana atakuwa nuru yangu.

97:9 Mao 3:39-40; Za 107:10; 119:154; Isa 46:13Kwa sababu nimetenda dhambi dhidi yake,

nitabeba ghadhabu ya Bwana,

mpaka atakaponitetea shauri langu

na kuithibitisha haki yangu.

Atanileta nje kwenye mwanga,

nami nitaiona haki yake.

107:10 Za 35:26; 42:3; Isa 5:5; 51:23; Ay 40:12; Zek 10:5; 2Sam 22:43Kisha adui yangu ataliona

naye atafunikwa na aibu,

yule aliyeniambia,

“Yu wapi Bwana Mungu wako?”

Macho yangu yataona kuanguka kwake,

hata sasa atakanyagwa chini ya mguu

kama tope barabarani.

117:11 Amo 9:11; Isa 54:11Siku ya kujenga kuta zako itawadia,

siku ya kupanua mipaka yako.

127:12 Isa 19:23-25; 11:11; 60:4Siku hiyo watu watakuja kwako

kutoka Ashuru na miji ya Misri,

hata kutoka Misri hadi Frati

na kutoka bahari hadi bahari

na kutoka mlima hadi mlima.

137:13 Isa 3:10-11; Eze 12:19; 33:28-29Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake,

kwa sababu ya matunda ya matendo yao.

Sala Na Sifa

147:14 Za 23:4; 28:9; 95:7; Mik 5:4; 7:14; Hes 23:9; Kum 33:28; Wim 4:1; Isa 33:9; Yer 50:19; Eze 36:11Wachunge watu wako kwa fimbo yako,

kundi la urithi wako,

ambalo linaishi peke yake msituni,

katika nchi ya malisho yenye rutuba.

Waache walishe katika Bashani na Gileadi

kama ilivyokuwa siku za kale.

157:15 Kut 3:20; Za 78:12“Kama siku zile mlipotoka Misri,

nitawaonyesha maajabu yangu.”

167:16 Isa 26:11; Amu 18:19Mataifa yataona na kuaibika,

waliondolewa nguvu zao zote.

Wataweka mikono yao kwenye vinywa vyao

na masikio yao yatakuwa na uziwi.

177:17 Mwa 3:14; 2Sam 22:46; Isa 25:3; 59:19Wataramba mavumbi kama nyoka,

kama viumbe vitambaavyo juu ya ardhi.

Watatoka nje ya mapango yao wakitetemeka;

watamgeukia Bwana Mungu wetu kwa hofu

nao watakuogopa.

187:18 Kut 10:8; 1Sam 2:2; Isa 43:25; 54:9; 57:16; Zek 3:4; Yer 31:20; 50:20; Kut 15:11; 34:6, 7, 9; Za 89:6-8; 103:9; 2Nya 6:21; 30:9; Za 103:8-13; Yoe 2:32; Amo 5:15; Mik 2:12Ni nani Mungu kama wewe,

ambaye anaachilia dhambi

na kusamehe makosa

ya mabaki ya urithi wake?

Wewe huwi na hasira milele,

bali unafurahia kuonyesha rehema.

197:19 Isa 43:25; Rum 6:6; Yer 31:34Utatuhurumia tena,

utazikanyaga dhambi zetu

chini ya nyayo zako,

na kutupa maovu yetu yote

katika vilindi vya bahari.

207:20 Gal 3:16; Kum 11:29; 7:8; Lk 1:72; Za 108:4Utakuwa wa kweli kwa Yakobo,

nawe utamwonyesha Abrahamu rehema,

kama ulivyowaahidi kwa kiapo baba zetu

siku za kale.