Mhubiri 7 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Mhubiri 7:1-29

Hekima

17:1 Ufu 14:13; Wim 1:3; Mit 22:1; Ay 10:18Afadhali sifa nzuri kuliko manukato safi,

nayo siku ya kufa kuliko ya kuzaliwa.

27:2 Za 90:12; Mit 11:19; Mhu 2:14Afadhali kwenda kwenye nyumba ya msiba

kuliko kwenda kwenye nyumba ya karamu,

kwa kuwa kifo ni hatima ya kila mwanadamu,

imewapasa walio hai kuliweka hili mioyoni mwao.

37:3 2Kor 7:10; Mit 14:13Huzuni ni afadhali kuliko kicheko,

kwa sababu uso wenye huzuni wafaa kwa moyo.

47:4 Mhu 2:1; Yer 16:8Moyo wa wenye hekima uko katika nyumba ya msiba,

lakini moyo wa wapumbavu uko katika nyumba ya anasa.

57:5 Za 141:5; Mit 13:18; 15:31-32Afadhali kusikia karipio la mtu mwenye hekima,

kuliko kusikiliza wimbo wa wapumbavu.

67:6 Za 58:9; Mhu 2:2; Mit 14:13Kama ilivyo kuvunjika kwa miiba chini ya sufuria,

ndivyo kilivyo kicheko cha wapumbavu.

Hili nalo pia ni ubatili.

77:7 Kut 18:21; 23:8; Kum 16:19Dhuluma humfanya mtu mwenye hekima kuwa mpumbavu,

nayo rushwa huuharibu moyo.

87:8 Mit 14:29; Gal 5:22Mwisho wa jambo ni bora kuliko mwanzo wake,

uvumilivu ni bora kuliko kiburi.

97:9 Mit 16:32; 14:17, 29; Mt 5:22Usiwe mwepesi kukasirika rohoni mwako,

kwa kuwa hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.

10Usiseme, “Kwa nini siku za kale zilikuwa bora kuliko siku hizi?”

Kwa maana si hekima kuuliza maswali kama hayo.

117:11 Mit 8:10-11; Mhu 2:13; 11:7Hekima, kama ulivyo urithi, ni kitu chema

na huwafaidia wale walionalo jua.

12Hekima ni ulinzi kama fedha ilivyo ulinzi,

lakini faida ya maarifa ni hii:

kwamba hekima huhifadhi maisha ya aliye nayo.

137:13 Isa 14:27; Mhu 2:24; 1:15Tafakari kile Mungu alichokitenda:

Nani awezaye kunyoosha

kile ambacho yeye amekipinda?

147:14 Ay 1:21; Mhu 2:24Nyakati zikiwa nzuri, ufurahi,

lakini nyakati zikiwa mbaya, tafakari:

Mungu amefanya hiyo moja,

naam, sanjari7:14 Sanjari hapa maana yake mwandamano wa vitu, wanyama au watu. na hiyo nyingine.

Kwa hiyo, mwanadamu hawezi kugundua

kitu chochote kuhusu maisha yake ya baadaye.

157:15 Mhu 8:14; Yer 12:1; Ay 21:7; 7:7Katika maisha haya yangu ya ubatili nimeshaona haya mawili:

mtu mwadilifu akiangamia katika uadilifu wake,

naye mtu mwovu akiishi maisha marefu katika uovu wake.

16Usiwe mwenye haki kupita kiasi,

wala usiwe na hekima kupita kiasi:

kwa nini kujiangamiza mwenyewe?

177:17 Ay 15:32; Za 55:23Usiwe mwovu kupita kiasi,

wala usiwe mpumbavu:

kwa nini kufa kabla ya wakati wako?

187:18 Mhu 3:14Ni vyema kushika hilo moja

na wala usiache hilo jingine likupite.

Mtu amchaye Mungu ataepuka huko kupita kiasi.7:18 Au: atafuata hayo yote mawili.

197:19 Mhu 2:13; 9:13-18; Mit 8:14Hekima humfanya yeye aliye nayo kuwa na uwezo zaidi

kuliko watawala kumi katika mji.

207:20 1Fal 8:46; Rum 3:12, 23; Gal 3:22; Za 14:3; Mit 20:9; Ay 4:17Hakuna mtu mwenye haki duniani

ambaye hufanya mambo ya haki

na kamwe asitende dhambi.

217:21 Mit 30:10Usitie maanani kila neno linalosemwa na watu,

la sivyo, waweza kumsikia

mtumishi wako akikulaani:

22kwa kuwa unafahamu moyoni mwako

kwamba wewe mwenyewe mara nyingi

umewalaani wengine.

237:23 Mhu 1:17; Rum 1:22Yote haya niliyajaribu kwa hekima, nikasema,

“Nimeamua kuwa na hekima”:

lakini hii ilikuwa nje ya uwezo wangu.

247:24 Ay 28:12; 11:12; Isa 55:8-9Vyovyote hekima ilivyo,

hekima iko mbali sana na imejificha,

ni nani awezaye kuigundua?

257:25 Ay 28:3; Mhu 1:17Nikageuza fikira zangu ili kuelewa,

kuchunguza na kuitafuta hekima

na kusudi la mambo,

na ili kuelewa ujinga wa uovu,

na wazimu wa upumbavu.

267:26 Kut 10:7; Amu 14:15; Mit 7:23; 22:14; 2:16-19; 5:3-5Nimeona jambo lililo chungu kuliko mauti,

mwanamke ambaye ni mtego,

ambaye moyo wake ni wavu wa kutegea

na mikono yake ni minyororo.

Mtu ampendezaye Mungu atamkwepa,

bali mwenye dhambi atanaswa naye.

27Mhubiri anasema, “Tazama, hili ndilo nililogundua:

“Nimegundua kitu kimoja baada ya kingine nilipokuwa katika kusudi la mambo:

287:28 1Fal 11:3ningali natafiti

lakini sipati:

nilimpata mwanaume mmoja mnyofu miongoni mwa elfu,

lakini hakuna mwanamke mmoja mnyofu miongoni mwao.

29Hili ndilo peke yake nililolipata:

Mungu amemuumba mwanadamu mnyofu,

lakini mwanadamu amebuni mambo mengi.”

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

傳道書 7:1-29

1美好的名聲勝過珍貴的膏油,

人死之日勝過出生之時。

2探望喪家勝過參加宴席,

因為死亡是每個人的結局,

活著的人要把這事銘記在心。

3哀傷勝過歡笑,

因為哀傷磨煉心靈。

4智者的心思考死亡,

愚人的心只顧作樂。

5聽智者的責備,

勝過聽愚人的頌歌。

6愚人的笑聲像鍋底下燒荊棘的噼啪聲。

這也是虛空。

7欺壓使智者變愚昧,

賄賂敗壞人心。

8事情的結局勝過事情的開端;

恆久忍耐勝過心驕氣傲。

9不要輕易發怒,

因為愚人心懷怒氣。

10不要問為什麼過去比現在好,

因為這樣問不明智。

11智慧如同產業一樣美好,

有益於得見日光的世人。

12智慧提供保障,

如同金錢一樣。

智慧能保全智者的生命。

這就是知識的好處。

13你要思想上帝的作為,

因為上帝弄彎的,

誰能使它變直呢?

14順境時要快樂,

逆境時要思想:

兩者都是上帝的安排,

好叫人不能預知將來。

15在我虛空的一生中,我見過義人行義,反而滅亡;惡人行惡,卻享長壽。 16為人不要過分正直,也不要過於聰明,何必自取毀滅呢? 17不要過分邪惡,也不要做愚人,何必時候未到就死呢? 18最好是持守這個教訓也不放鬆那個教訓,因為敬畏上帝的人必避免兩個極端。 19智慧使一個智者比城裡十個官長更有能力。 20誠然,在地上無法找到一個一生行善、從未犯罪的義人。 21你不要斤斤計較別人所說的每一句話,免得聽見你的僕人咒詛你, 22因為你心裡知道自己也曾多次咒詛別人。 23我用智慧試驗過這一切。我說:「我要做智者」,誰知智慧卻離我甚遠。 24智慧如此遙不可及、深不可測,誰能找得到呢?

25我用心去認識、探究、追尋智慧和事物的原委,並去認識邪惡帶來的愚昧和無知帶來的狂妄。 26我發現有的婦人比死亡更苦毒,她是個陷阱,心如網羅,手像鎖鏈。討上帝喜悅的人避開她,罪人卻被她俘虜。 27-28傳道者說:「看啊,我事事反復探索,要查明萬事之理,卻沒有尋獲。但我發現在一千個男子中還可以找到一位正直人,在眾女子中卻未找到一位。 29我只發現一件事,上帝造的人本來正直,人卻找出各種詭計。」