Mhubiri 6 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Mhubiri 6:1-12

1Nimeona ubaya mwingine chini ya jua, nao unalemea sana wanadamu: 26:2 Kum 8:7-10; Za 17:14; Amu 18:10; Mhu 5:13-19Mungu humpa mwanadamu utajiri, mali na heshima, hivyo hakukosa chochote moyo wake unachokitamani. Lakini Mungu hamwezeshi kuvifurahia, badala yake mgeni ndiye anayevifurahia. Hili ni ubatili, ni ubaya unaosikitisha.

36:3 Ay 3:3, 16; Es 7:10; Mhu 4:3Mtu anaweza kuwa na watoto mia moja naye akaishi miaka mingi, lakini haidhuru kuwa ataishi muda mrefu kiasi gani, kama hawezi kufurahia mafanikio yake na kwamba hapati mazishi ya heshima, ninasema afadhali mtoto aliyezaliwa akiwa amekufa kuliko yeye. 4Kuzaliwa kwake hakuna maana, huondokea gizani na gizani jina lake hufunikwa. 5Ingawa hakuwahi kuliona jua wala kujua kitu chochote, yeye ana pumziko zaidi kuliko mtu huyo, 66:6 Mhu 2:16Hata kama huyo mtu ataishi miaka elfu mara mbili na zaidi, lakini akashindwa kufurahia mafanikio yake, je, wote hawaendi sehemu moja?

76:7 Mit 16:26; 27:20; 1Tim 6:6-8Juhudi zote za binadamu ni kwa ajili ya kinywa chake,

hata hivyo hamu yake kamwe haitoshelezwi.

86:8 Mhu 2:15Mtu mwenye hekima ana faida gani

zaidi ya mpumbavu?

Mtu maskini anapata faida gani

kwa kujua jinsi ya kujistahi

mbele ya watu wengine?

9Ni bora kile ambacho jicho linakiona

kuliko hamu isiyotoshelezwa.

Hili nalo ni ubatili,

ni kukimbiza upepo.

106:10 Ay 9:32; Isa 45:9; Mhu 3:15Lolote lililopo limekwisha kupewa jina,

naye mwanadamu alivyo ameshajulikana;

hakuna mtu awezaye kushindana

na mwenye nguvu kuliko yeye.

11Maneno yanavyokuwa mengi,

ndivyo yanavyokosa maana,

Je, hilo linamfaidia vipi yeyote?

126:12 Yak 4:14; Ay 10:20; 20:8; 14:2; 1Nya 29:15; Za 39:6Kwa maana ni nani anayejua lililo jema kwa ajili ya maisha ya mwanadamu, katika siku chache na za ubatili anazopita kama kivuli? Ni nani awezaye kumwambia yatakayotokea chini ya jua baada ya yeye kuondoka?

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

傳道書 6:1-12

1我看見日光之下有一件可悲的事,重重地壓在人身上: 2上帝賜給人財富、產業和尊榮,叫他擁有所渴望的一切,卻使他無法享用,倒讓別人享用。這是虛空,是極大的悲哀。 3人若有一百個兒子,並且長壽,但心中卻從未因福樂而滿足,死後又不得安葬,我看這樣的人還不如流產的胎兒。 4這胎兒在虛空中來,在黑暗中去,名字隱沒在黑暗中, 5沒有見過天日,一無所知,然而這胎兒比那人更享安息。 6就算那人活了千年,又活千年,卻不能享受福樂,又如何呢?世人最終豈不都同歸一處嗎? 7人人為口腹勞碌,卻永不滿足。 8那麼,智者比愚人有什麼優勢呢?貧窮人即使懂得如何處世,又有什麼益處呢? 9滿足於眼前所有的,勝過心中貪想的。這也是虛空,如同捕風。 10一切存在的事物都已命名,人的本質也被識透;人無法與比他更強的較量。 11其實話越多,越虛空,這對人又有什麼益處? 12人生短暫虛空,如影飛逝,有誰知道什麼對人有益?誰能告訴人死後日光之下會發生什麼事?