Mathayo 28 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Mathayo 28:1-20

Yesu Afufuka

(Marko 16:1-10; Luka 24:1-12; Yohana 20:1-10)

128:1 Mt 27:56Baada ya Sabato, alfajiri mapema siku ya kwanza ya juma, Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikwenda kulitazama kaburi.

228:2 Mt 27:51; Yn 20:12; Mdo 5:9Ghafula, pakawa na tetemeko kubwa la ardhi, kwa sababu malaika wa Bwana alishuka kutoka mbinguni, akaenda penye kaburi, akalivingirisha lile jiwe na kulikalia. 328:3 Dan 7:9; Yn 20:12Sura ya huyo malaika ilikuwa kama umeme, na mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji. 4Wale walinzi wa kaburi walimwogopa sana, wakatetemeka hata wakawa kama wafu.

528:5 Mt 14:27Yule malaika akawaambia wale wanawake, “Msiogope, kwa maana ninajua kuwa mnamtafuta Yesu aliyesulubiwa. 628:6 Mt 16:21Hayupo hapa, kwa kuwa amefufuka, kama vile alivyosema. Njooni mpatazame mahali alipokuwa amelazwa. 728:7 Mt 26:32Kisha nendeni upesi mkawaambie wanafunzi wake kwamba, ‘Amefufuka kutoka kwa wafu, naye awatangulia kwenda Galilaya. Huko ndiko mtamwona. Sasa nimekwisha kuwaambia.’ ”

8Hivyo wale wanawake wakaondoka pale kaburini wakiwa wamejawa na hofu, bali wakiwa na furaha nyingi. Wakaenda mbio kuwaeleza wanafunzi wake habari hizo. 928:9 Yn 20:14-18Ghafula, Yesu akakutana nao, akasema, “Salamu!” Wale wanawake wakamkaribia, wakaishika miguu yake, wakamwabudu. 1028:10 Rum 8:29; Ebr 2:11-17Ndipo Yesu akawaambia, “Msiogope. Nendeni mkawaambie ndugu zangu waende Galilaya, ndiko watakakoniona.”

Taarifa Ya Walinzi

1128:11 Mt 27:65-66Wakati wale wanawake walikuwa njiani wakienda, baadhi ya wale askari waliokuwa wakilinda kaburi walienda mjini na kuwaeleza viongozi wa makuhani kila kitu kilichokuwa kimetukia. 12Baada ya viongozi wa makuhani kukutana na wazee na kutunga hila, waliwapa wale askari kiasi kikubwa cha fedha 1328:13 Mt 27:64wakiwaambia, “Inawapasa mseme, ‘Wanafunzi wake walikuja wakati wa usiku na kumwiba sisi tulipokuwa tumelala.’ 1428:14 Mt 27:2Kama habari hizi zikimfikia mtawala, sisi tutamwondolea mashaka nanyi hamtapata tatizo lolote.” 15Kwa hiyo wale askari wakazipokea hizo fedha nao wakafanya kama walivyoelekezwa. Habari hii imeenea miongoni mwa Wayahudi mpaka leo.

Yesu Awatuma Wanafunzi Wake

(Marko 16:14-18; Luka 24:36-49; Yohana 20:19-23; Matendo 1:6-8)

1628:16 Mt 26:32Basi wale wanafunzi kumi na mmoja wakaenda hadi Galilaya kwenye ule mlima ambao Yesu alikuwa amewaagiza. 17Walipomwona, wakamwabudu; lakini baadhi yao wakaona shaka. 1828:18 Dan 7:13, 14; Efe 1:20-22Yesu akawajia na kusema, “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. 1928:19 Isa 49:6; Mdo 14:21Kwa sababu hii, enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, 2028:20 Mt 18:20; Yn 14:23nanyi wafundisheni kuyashika mambo yote niliyowaamuru ninyi. Hakika mimi niko pamoja nanyi siku zote, hadi mwisho wa nyakati.”

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

馬太福音 28:1-20

耶穌復活

1安息日剛過,週日黎明時分,抹大拉瑪麗亞和另一位瑪麗亞一同到墳墓去察看。

2突然,大地劇烈地震動,主的天使從天而降,把墓口的石頭滾開,坐在上面。 3他的容貌如閃電,衣裳潔白如雪。 4看守墓穴的衛兵嚇得渾身發抖,像死人一樣。

5天使對那兩個女人說:「不要怕,我知道你們是在找那位被釘十字架的耶穌。 6祂不在這裡,正如祂所說的,祂已經復活了。你們來看,這是安放祂的地方。 7現在你們快去告訴祂的門徒,祂已經從死裡復活,要先你們一步去加利利,你們將在那裡見到祂。記住,我已經告訴你們了。」

8她們聽了又害怕又欣喜,連忙離開墳墓,跑去告訴門徒。 9忽然,耶穌迎面而來,對她們說:「願你們平安!」她們就上前抱住祂的腳敬拜祂。

10耶穌對她們說:「不要害怕。你們去告訴我的弟兄,叫他們到加利利去,他們將在那裡見到我。」

行賄造謠

11她們還在趕路的時候,有些守墓的衛兵已經進城把整件事告訴祭司長。 12祭司長和長老聚集商議,決定用重金買通守墓的衛兵, 13又吩咐他們:「你們就說,『夜裡我們熟睡的時候,耶穌的門徒來把祂的屍體偷走了。』 14如果這件事傳到總督那裡,我們會跟他解釋,保你們無事。」 15守衛收下錢,便依照吩咐去做。於是,這說法在猶太人中一直流傳到今天。

大使命

16十一個門徒趕到加利利,到了耶穌和他們約定的山上, 17看到耶穌就敬拜祂,但有些人仍然心存疑惑。 18耶穌上前對門徒說:

「天上地下所有的權柄都交給我了。 19所以,你們要去使萬民作我的門徒,奉父、子、聖靈的名給他們施洗, 20教導他們遵守我吩咐你們的一切。記住,我必常與你們同在,一直到世界的末了。」