Mathayo 12 – NEN & SZ-PL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 12:1-50

Bwana Wa Sabato

(Marko 2:23-28; Luka 6:1-5)

112:1 Kum 23:25Wakati huo Yesu alipitia kwenye mashamba ya nafaka siku ya Sabato. Wanafunzi wake walikuwa na njaa, nao wakaanza kuvunja masuke ya nafaka na kuyala. 212:2 Kut 20:10; Yn 9:6Lakini Mafarisayo walipoona jambo hili, wakamwambia, “Tazama! Wanafunzi wako wanafanya jambo lisilo halali kufanywa siku ya Sabato.”

312:3 1Sam 21:1-6Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma alichofanya Daudi na wenzake walipokuwa na njaa? 412:4 Law 24:5-9Aliingia katika nyumba ya Mungu, akala mikate iliyowekwa wakfu, yeye na wenzake, jambo ambalo halikuwa halali kwao kufanya, isipokuwa makuhani peke yao. 512:5 Hes 28:9-10; Yn 7:22-23Au hamjasoma katika Sheria kwamba siku ya Sabato makuhani huvunja sheria ya Sabato Hekaluni lakini hawahesabiwi kuwa na hatia? 612:6 Mt 12:41-42Nawaambia wazi kwamba, yeye aliye mkuu kuliko Hekalu yupo hapa. 712:7 Hos 6:6; Mt 9:13Kama mngekuwa mmejua maana ya maneno haya, ‘Nataka rehema, wala si dhabihu,’ msingewalaumu watu wasio na hatia, 812:8 Mt 8:20kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”

Yesu Anamponya Mtu Aliyepooza Mkono

(Marko 3:1-6; Luka 6:6-11)

912:9 Mk 3:1; Lk 6:6Yesu akaondoka mahali hapo, akaingia ndani ya sinagogi lao, 1012:10 Lk 14:3; Yn 9:6na huko alikuwepo mtu aliyepooza mkono. Wakitafuta sababu ya kumshtaki Yesu, wakamuuliza, “Je, ni halali kuponya siku ya Sabato?”

1112:11 Lk 15:5Yesu akawaambia, “Ni nani miongoni mwenu, mwenye kondoo wake ambaye huyo kondoo akitumbukia shimoni siku ya Sabato hatamtoa? 1212:12 Mt 6:26; 10:31Mtu ana thamani kubwa kuliko kondoo. Kwa hiyo ni halali kutenda mema siku ya Sabato.”

13Ndipo akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa ukawa mzima kama ule mwingine. 1412:14 Mwa 37:18; Yn 11:53Lakini Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri baya juu ya Yesu jinsi watakavyoweza kumuua.

Mtumishi Aliyechaguliwa Na Mungu

1512:15 Mt 4:23Lakini Yesu alipoyatambua mawazo yao, akaondoka mahali hapo. Watu wengi wakamfuata, naye akawaponya wagonjwa wao wote, 1612:16 Mt 8:4akiwakataza wasiseme yeye ni nani. 1712:17 Isa 42:1-4; 41:9Hii ilikuwa ili litimie lile neno lililonenwa kwa kinywa cha nabii Isaya kusema:

1812:18 Mt 3:7; Isa 42:1-4; 41:9“Tazama mtumishi wangu niliyemchagua,

mpendwa wangu, ninayependezwa naye.

Nitaweka Roho wangu juu yake,

naye atatangaza haki kwa mataifa.

19Hatagombana wala hatapiga kelele,

wala hakuna atakayesikia sauti yake njiani.

20Mwanzi uliopondeka hatauvunja,

na utambi unaofuka moshi hatauzima,

mpaka atakapoifanya haki ishinde.

2112:21 Isa 42:1-4Katika Jina lake mataifa

wataweka tumaini lao.”

Yesu Na Beelzebuli

(Marko 3:20-30; Luka 11:14-23)

2212:22 Mt 4:24; 9:32-33Kisha wakamletea mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, na alikuwa kipofu na bubu. Yesu akamponya, hata akaweza kusema na kuona. 2312:23 Mt 9:27Watu wote wakashangaa na kusema, “Je, yawezekana huyu ndiye Mwana wa Daudi?”

2412:24 Mk 3:22; Mt 9:34Lakini Mafarisayo waliposikia jambo hili wakasema, “Mtu huyu anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa Beelzebuli,12:24 Beelzebuli au Beelzebubu; pia 12:27. mkuu wa pepo wachafu.”

2512:25 Mt 9:4Yesu alijua walichokuwa wakiwaza, hivyo akawaambia, “Kila ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe huangamia. Hali kadhalika kila mji au watu wa nyumba moja waliogawanyika dhidi yao wenyewe hawawezi kusimama. 2612:26 Mt 4:10Kama Shetani akimtoa Shetani, atakuwa amegawanyika yeye mwenyewe. Basi ufalme wake utawezaje kusimama? 2712:27 Mdo 19:13Nami kama natoa pepo wachafu kwa nguvu za Beelzebuli, watu wenu je, wao hutoa pepo wachafu kwa uwezo wa nani? Hivyo basi, wao ndio watakaowahukumu. 2812:28 1Yn 3:8; Mt 3:2Lakini kama mimi ninatoa pepo wachafu kwa Roho wa Mungu, basi Ufalme wa Mungu umekuja juu yenu.

2912:29 Isa 49:24-25; Lk 11:21-22“Au tena, mtu awezaje kuingia katika nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Akishamfunga, ndipo hakika anaweza kuteka nyara mali zake.

3012:30 Mk 9:40; Yn 11:52; Lk 11:23“Mtu asiyekuwa pamoja nami yu kinyume nami, na mtu ambaye hakusanyi pamoja nami, hutawanya. 3112:31 Mk 3:28-29; Lk 12:10Kwa hiyo nawaambia, kila dhambi na kufuru watu watasamehewa, lakini mtu atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa. 3212:32 Tit 2:12; Efe 1:21; Ebr 6:5Mtu yeyote atakayesema neno dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote anenaye neno dhidi ya Roho Mtakatifu hatasamehewa, iwe katika ulimwengu huu au katika ulimwengu ujao.

Mti Na Matunda Yake

(Luka 6:43-45)

3312:33 Mt 7:16-17; Lk 6:43-44“Ufanye mti kuwa mzuri, nayo matunda yake yatakuwa mazuri. Au ufanye mti kuwa mbaya, na matunda yake yatakuwa mabaya. Kwa maana mti hutambulika kwa matunda yake. 3412:34 Mt 3:7; 23:33; 15:18; Yn 8:43Enyi uzao wa nyoka! Mnawezaje kunena mambo mema, wakati ninyi ni waovu? Kwa maana kinywa cha mtu huyanena yale yaliyoujaza moyo wake. 3512:35 Lk 6:45Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka hazina ya mambo mema yaliyohifadhiwa ndani yake, naye mtu mwovu hutoa yaliyo maovu kutoka hazina ya mambo maovu yaliyohifadhiwa ndani yake. 36Lakini nawaambia, katika siku ya hukumu watu watatoa hesabu kuhusu kila neno lisilo maana walilonena. 37Kwa maana kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.”

Ishara Ya Yona

(Marko 8:11-12; Luka 11:29-32)

3812:38 Yn 6:30; 1Kor 1:22Kisha baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamwambia, “Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako.”

3912:39 Yn 1:7; Mt 8:20; 16:21Lakini yeye akawajibu, “Kizazi kiovu na cha uzinzi kinaomba ishara! Lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ile ishara ya nabii Yona. 4012:40 Yn 2:1, 2; 1:17; Mt 8:20; 16:21Kwa maana kama vile Yona alivyokuwa ndani ya tumbo la nyangumi12:40 Nyangumi ni samaki mkubwa sana. kwa siku tatu, usiku na mchana, vivyo hivyo Mwana wa Adamu atakuwa katika moyo wa nchi siku tatu, usiku na mchana. 4112:41 Yn 1:2; 3:15Siku ya hukumu watu wa Ninawi watasimama pamoja na kizazi hiki na kukihukumu; kwa maana wao walitubu waliposikia mahubiri ya Yona. Na tazama, hapa yupo yeye aliye mkuu kuliko Yona. 4212:42 1Fal 10:2; 2Nya 9:1Malkia wa Kusini atasimama wakati wa hukumu na kukihukumu kizazi hiki. Kwa kuwa yeye alikuja kutoka miisho ya dunia ili kuisikiliza hekima ya Solomoni. Na hapa yupo aliye mkuu kuliko Solomoni.”

Mafundisho Kuhusu Pepo Mchafu

(Luka 11:24-26)

43“Pepo mchafu amtokapo mtu, hutangatanga katika sehemu zisizo na maji akitafuta mahali pa kupumzika, lakini hapati. 44Ndipo husema, ‘Nitarudi kwenye nyumba yangu nilikotoka.’ Naye arudipo huikuta ile nyumba ikiwa tupu, imefagiliwa na kupangwa vizuri. 4512:45 2Pet 2:20Kisha huenda na kuwaleta pepo wachafu wengine saba wabaya kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo. Nayo hali ya mwisho ya yule mtu huwa ni mbaya kuliko ile ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kiovu.”

Mama Na Ndugu Zake Yesu

(Marko 3:31-35; Luka 8:19-21)

4612:46 Lk 11:24; Ay 1:7; 1Pet 5:8Wakati alikuwa angali anazungumza na makutano, mama yake na ndugu zake wakasimama nje wakitaka kuongea naye. 47Ndipo mtu mmoja akamwambia, “Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kuongea na wewe.”

4812:48 Lk 2:49Lakini yeye akamjibu na kumwambia yule mtu, “Mama yangu ni nani, nao ndugu zangu ni nani?” 49Akawanyooshea mkono wanafunzi wake, akasema, “Hawa hapa ndio mama yangu na ndugu zangu! 5012:50 Mt 6:10; Yn 15:14Kwa maana yeyote afanyaye mapenzi ya Baba yangu wa mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”

Słowo Życia

Mateusza 12:1-50

Pan szabatu

1Pewnego razu, w szabat, Jezus szedł przez pole. Idący z Nim uczniowie poczuli głód. Zaczęli więc zrywać kłosy i jeść ziarno. 2Zauważyli to oczywiście faryzeusze i oburzyli się:

—Twoi uczniowie robią rzeczy niedozwolone w szabat!

3—Czy nie czytaliście, co zrobił król Dawid, gdy wraz z towarzyszami podróży poczuł głód?—odpowiedział im Jezus. 4—Wszedł do świątyni i wziął dla siebie oraz swoich towarzyszy poświęcony chleb, który wolno było jeść tylko kapłanom. 5Czy nie czytaliście w Prawie Mojżesza, że kapłani, pracujący w szabat w świątyni, łamią nakaz odpoczynku, a mimo to są niewinni? 6Mówię wam: Macie tu do czynienia z czymś ważniejszym niż świątynia! 7Gdybyście wiedzieli, co znaczą słowa: „Pragnę waszej miłości, a nie ofiar”, wówczas nie potępialibyście niewinnych. 8Ja, Syn Człowieczy, mam władzę nad szabatem.

9Następnie udał się stamtąd do synagogi. 10Znajdował się tam człowiek ze sparaliżowaną ręką, faryzeusze zapytali więc Jezusa:

—Czy taką pracę, jak uzdrawianie, również można wykonywać w szabat?—szukali bowiem pretekstu do oskarżenia Go.

11—Czy jeśli któraś z waszych owiec wpadłaby w szabat do dołu, to nie wyciągnęlibyście jej?—zapytał Jezus. 12—O ile bardziej cenny jest człowiek! Oczywiście, że w szabat wolno czynić dobro.

13—Wyciągnij rękę!—zwrócił się do chorego.

Ten posłuchał i natychmiast jego ręka stała się równie zdrowa jak druga.

Wybrany sługa Boga

14Wtedy faryzeusze odeszli i zaczęli się naradzać, jak Go zabić. 15On jednak poznał ich plany i opuścił synagogę. Tłum podążył za Nim i wszyscy chorzy zostali uzdrowieni. 16Zabronił im jednak opowiadać o tym innym. 17W ten sposób spełniło się proroctwo Izajasza:

18„To jest mój Sługa, którego wybrałem,

mój ukochany, w którym mam upodobanie!

Dam Mu swojego Ducha, by sądził narody.

19Nie będzie się sprzeczał ani krzyczał,

nikt nie usłyszy Jego podniesionego głosu.

20On nie dołamie nawet nadłamanej trzciny

ani nie zgasi wątłego płomyka.

Zwycięsko przeprowadzi swój sąd,

21a Jego imię będzie źródłem nadziei dla narodów”.

Jezus i Belzebub

22Przyprowadzono wtedy do Jezusa człowieka niemego i ślepego—zniewolonego przez demona. Jezus uzdrowił go, przywracając mu wzrok i mowę, 23a cały tłum wpadł w podziw, mówiąc:

—Czyż On nie jest Mesjaszem, potomkiem króla Dawida?

24Gdy faryzeusze dowiedzieli się o tym cudzie, stwierdzili:

—Wypędza demony, bo Belzebub, władca demonów, mu w tym pomaga.

25—Każde królestwo, które jest wewnętrznie skłócone, upadnie—odparł Jezus, znając ich myśli. —I żadne miasto ani dom nie przetrwają, jeśli panuje w nich niezgoda. 26Jeśli szatan wypędza szatana, to zwalcza siebie samego. Jak więc jego królestwo może przetrwać? 27Skoro ja wypędzam demony mocą Belzebuba, to dzięki komu robią to wasi synowie? To oni was osądzą! 28Lecz jeśli wypędzam demony mocą Ducha Bożego, znaczy to, że przyszło do was królestwo Boże. 29Jak można wejść do domu siłacza i okraść go, jeśli się go najpierw nie obezwładni? Dopiero wtedy można zabrać jego rzeczy. 30Kto nie jest po mojej stronie, jest przeciwko Mnie. A kto ze Mną nie zbiera, ten rozprasza. 31Dlatego ostrzegam: Każdy grzech i bluźnierstwo mogą być przebaczone, lecz bluźnierstwo przeciwko Duchowi Świętemu nie będzie przebaczone! 32Jeśli ktoś powiedziałby coś przeciwko Mnie, Synowi Człowieczemu, może otrzymać przebaczenie. Ale jeśli ktoś powiedziałby coś przeciwko Duchowi Świętemu, nie otrzyma przebaczenia ani w tym, ani w przyszłym życiu. 33Albo uznajcie, że drzewo jest dobre—i wtedy daje dobry owoc, albo uznajcie, że jest złe—a wtedy i jego owoc jest zły. Drzewo rozpoznaje się przecież po owocach. 34Jesteście podli! Zresztą jak wy, źli ludzie, możecie mówić coś dobrego? Przecież usta, gdy mówią, czerpią z serca. 35Człowiek dobry wyciąga ze swojego skarbca dobre rzeczy, a człowiek zły—złe rzeczy. 36Ostrzegam was: W dniu sądu ludzie zdadzą sprawę z każdego niepotrzebnego słowa, które wypowiedzieli. 37Na podstawie twoich własnych słów zostaniesz uniewinniony albo skazany!

Znak Jonasza

38Pewnego dnia kilku przywódców religijnych z ugrupowania faryzeuszy powiedziało do Jezusa:

—Nauczycielu! Chcemy, abyś dokonał jakiegoś szczególnego cudu.

39—To złe i niewierne Bogu pokolenie domaga się cudu!—odpowiedział Jezus. —Ale nie zobaczy go, z wyjątkiem znaku proroka Jonasza. 40Tak jak Jonasz przebywał w brzuchu wielkiej ryby trzy dni i trzy noce, tak też Ja, Syn Człowieczy, pozostanę w ziemi trzy dni i trzy noce. 41Mieszkańcy Niniwy podczas sądu wystąpią z oskarżeniem przeciw temu pokoleniu. Bo oni opamiętali się, słuchając Jonasza, a do was mówi ktoś o wiele większy niż on. 42Również królowa Południa powstanie na sądzie i oskarży to pokolenie. Ona przybyła z końca świata, by słuchać mądrości Salomona. Wy zaś macie przed sobą kogoś większego niż on.

43Jezus kontynuował:

—Gdy demon wyjdzie z człowieka, błąka się po pustkowiach, szukając wytchnienia, ale go tam nie znajduje. 44Wówczas mówi sobie: „Wrócę do mojego domu, z którego wyszedłem”. Przychodzi więc i widzi, że dom nie jest zajęty, że jest wysprzątany i ozdobiony. 45Przyprowadza więc ze sobą siedem innych, gorszych od siebie demonów i razem zamieszkują. A wtedy stan takiego człowieka jest o wiele gorszy niż na początku. Podobnie będzie i z tym złym pokoleniem.

Matka i bracia Jezusa

46Podczas gdy Jezus przemawiał do tłumu, na zewnątrz domu czekała Jego matka i bracia. Chcieli z Nim porozmawiać. 47Ktoś powiadomił więc Jezusa:

—Twoja matka i bracia czekają na zewnątrz i chcą z Tobą porozmawiać.

48—Kto jest moją matką i moimi braćmi?—zapytał Jezus. 49I wskazując na uczniów, rzekł:

—Oto moja matka i moi bracia! 50Moim bratem i siostrą, i matką jest każdy, kto wypełnia wolę mojego Ojca w niebie.