Marko 7 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Marko 7:1-37

Kilicho Safi Na Kilicho Najisi

(Mathayo 15:1-20)

17:1 Mt 15:1Mafarisayo na baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa wametoka Yerusalemu wakakusanyika mbele ya Yesu. 27:2 Mdo 11:8; Rum 14:14Wakawaona baadhi ya wanafunzi wake wakila chakula kwa mikono iliyo najisi, yaani, bila kunawa kama ilivyotakiwa na sheria ya dini ya Wayahudi. 37:3 Mk 7:5-13; Lk 11:38-39(Kwa kuwa Mafarisayo na Wayahudi wote hawali chakula pasipo kunawa kwa kufuata desturi za wazee wao. 47:4 Mt 23:25Wanapotoka sokoni hawawezi kula pasipo kunawa. Pia kuna desturi nyingine nyingi wanazofuata kama vile jinsi ya kuosha vikombe, vyungu na vyombo vya shaba.)

57:5 Gal 1:14; Kol 2:8Kwa hiyo wale Mafarisayo na walimu wa sheria wakamuuliza Yesu, “Mbona wanafunzi wako hawafuati desturi za wazee, na badala yake wanakula kwa mikono najisi?”

67:6 Isa 29:13; Mt 15:8Yesu akawajibu, “Nabii Isaya alisema ukweli alipotabiri juu yenu, ninyi wanafiki. Kama ilivyoandikwa:

“ ‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao,

lakini mioyo yao iko mbali nami.

77:7 Isa 29:13Huniabudu bure,

nayo mafundisho yao ni maagizo ya wanadamu tu.’

87:8 Mk 7:3Ninyi mmeziacha amri za Mungu na kushika desturi za watu.”

97:9 Mk 7:3Naye akawaambia, “Ninyi mnayo njia nzuri ya kukataa amri za Mungu ili mpate kuyashika mapokeo yenu! 107:10 Kut 20:21; Kum 5:16; Kut 21:17; Law 20:9Kwa mfano, Mose alisema, ‘Waheshimu baba yako na mama yako,’ na, ‘Yeyote amtukanaye baba yake au mama yake, na auawe.’ 117:11 Mt 23:16-18Lakini ninyi mwafundisha kwamba mtu akimwambia baba yake au mama yake, ‘Kile ambacho ningeweza kukusaidia ni Korbani’ (yaani kimewekwa wakfu kwa Mungu), 12basi hawajibiki tena kumsaidia baba yake au mama yake. 137:13 Ebr 4:12; Mk 7:3Kwa njia hiyo ninyi mnabatilisha neno la Mungu kwa mapokeo yenu mliyojiwekea. Nanyi mnafanya mambo mengi ya aina hiyo.”

147:14 Mt 15:10Yesu akaita tena ule umati wa watu, akawaambia, “Nisikilizeni, kila mmoja wenu na mwelewe jambo hili. 157:15 Mdo 10:14, 15Hakuna kitu kinachomwingia mtu kimtiacho unajisi, lakini kile kimtokacho ndicho kimtiacho unajisi. [ 167:16 Mt 11:15Kama mtu yeyote ana masikio ya kusikia na asikie.]”

177:17 Mk 9:28Akiisha kuuacha ule umati wa watu na kuingia ndani, wanafunzi wake wakamuuliza maana ya mfano ule. 18Akawajibu, “Je, hata nanyi hamwelewi? Je, hamfahamu kwamba kitu kimwingiacho mtu hakimtii unajisi? 197:19 Kol 2:16; 1Tim 4:3-5; Mdo 10:15Mtu akila kitu hakiingii moyoni mwake bali tumboni, na baadaye hutolewa nje ya mwili wake.” (Kwa kusema hivi, Yesu alivihalalisha vyakula vyote kuwa ni “safi.”)

20Akaendelea kusema, “Kile kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi. 217:21 Mwa 6:5; 8:21; Mt 15:21-28Kwa maana kutoka ndani ya moyo wa mtu hutoka mawazo mabaya, uasherati, wizi, uuaji, uzinzi, 227:22 Mt 20:15tamaa mbaya, uovu, udanganyifu, ufisadi, wivu, matukano, kiburi na upumbavu. 23Maovu haya yote hutoka ndani ya mtu, nayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi.”

Imani Ya Mwanamke Msirofoinike

(Mathayo 15:21-28)

247:24 Mt 21:21Ndipo Yesu akaondoka hapo akaenda sehemu za Tiro. Akaingia katika nyumba moja, naye hakutaka mtu yeyote ajue kwamba yuko humo. Lakini hakuweza kujificha. 257:25 Mt 4:24Mara mwanamke mmoja, ambaye binti yake mdogo alikuwa na pepo mchafu, akaja na kumpigia magoti miguuni pake. 26Basi huyo mwanamke alikuwa Myunani, aliyezaliwa Foinike ya Siria.7:26 Kulikuwa na Foinike ya Siria (ndio Shamu) na Foinike ya Libya. Akamsihi Yesu amtoe binti yake huyo pepo mchafu.

27Yesu akamwambia, “Waache watoto washibe kwanza, kwa maana si vyema kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.”

28Lakini yule mwanamke akamjibu, “Bwana, hata mbwa walio chini ya meza hula makombo ya chakula cha watoto.”

29Ndipo Yesu akamjibu, “Kwa sababu ya jibu lako, nenda zako nyumbani; yule pepo mchafu amemtoka binti yako.”

30Akaenda zake nyumbani akamkuta binti yake amelala kitandani, yule pepo mchafu akiwa amemtoka.

Yesu Amponya Mtu Aliyekuwa Kiziwi Na Bubu

317:31 Mt 11:21; 4:18-25; Mk 5:20Kisha Yesu akaondoka sehemu za Tiro, akapita katikati ya Sidoni, hadi Bahari ya Galilaya na kuingia eneo la Dekapoli. 327:32 Mt 9:32; Lk 11:14; Mk 5:23Huko, watu wakamletea Yesu mtu mmoja kiziwi, ambaye pia alikuwa na kigugumizi, wakamwomba aweke mkono wake juu ya huyo mtu na amponye.

337:33 Mk 8:23Baadaye Yesu akampeleka yule kiziwi kando mbali na watu, Yesu akatia vidole vyake masikioni mwa yule mtu. Kisha akatema mate na kuugusa ulimi wa yule mtu. 347:34 Mk 6:41; Yn 11:41; Mk 8:12Ndipo Yesu akatazama mbinguni, akavuta hewa ndani kwa nguvu akamwambia, “Efatha!” (yaani, “Funguka!”) 357:35 Isa 35:5-6Mara masikio yake yakafunguka na ulimi wake ukaachiliwa, akaanza kuongea sawasawa.

367:36 Mt 8:4Yesu akawaamuru wasimwambie mtu yeyote habari hizi. Lakini kadiri alivyowazuia, ndivyo walivyozidi kutangaza kwa bidii. 377:37 Isa 35:5Walistaajabu mno. Wakasema, “Amefanya mambo yote vizuri mno! Amewawezesha viziwi wasikie na bubu waseme!”

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

馬可福音 7:1-37

傳統與誡命

1有法利賽人和一些律法教師從耶路撒冷聚集到耶穌那裡。 2他們看到祂的一些門徒吃飯前沒有照禮儀洗手。 3因為法利賽人和所有的猶太人都拘守祖先的傳統,總是先照禮儀洗手之後才吃飯; 4從市場回來也要先潔淨自己,然後才吃飯。他們還拘守許多其他規矩,如洗杯、罐、銅器等。

5他們質問耶穌:「為什麼你的門徒違背祖先的傳統,竟用不潔淨的手吃飯呢?」

6耶穌回答說:「以賽亞針對你們這些偽君子說的預言一點沒錯,正如聖經上說,

「『這些人嘴上尊崇我,

心卻遠離我。

7他們的教導無非是人的規條,

他們敬拜我也是枉然。』7·7 以賽亞書29·13

8你們只知拘守人的傳統,卻無視上帝的誡命。」 9耶穌又對他們說:「你們為了拘守傳統,竟巧妙地廢除了上帝的誡命。 10摩西說,『要孝敬父母』7·10 出埃及記20·12申命記5·16,又說,『咒罵父母的,必被處死。』7·10 出埃及記21·17利未記20·9 11你們卻認為人若對父母說,『我把供養你們的錢財已經全部奉獻給上帝了』, 12他就可以不再奉養父母。 13你們就是這樣為了拘守傳統而廢除上帝的道,類似的情形還有很多。」

內心的污穢

14耶穌又召集眾人,對他們說:「你們都要聽我說,也要明白, 15從外面進去的不會使人污穢,只有從人裡面發出來的才會使人污穢。 16有耳可聽的,都應當聽!7·16 有古卷無16節。

17耶穌離開眾人,進了屋子,門徒問祂這比喻的意思。 18耶穌說:「你們也這樣糊塗嗎?豈不知從外面進去的,不會使人污穢, 19因為不能進入他的心,只能進他的腸胃,最後排進廁所。」言下之意,所有的食物都是潔淨的。

20祂接著說:「從人裡面發出來的才使人污穢, 21因為從裡面,就是從人的心裡能夠生出惡念、苟合、偷盜、謀殺、 22通姦、貪婪、邪惡、詭詐、放蕩、嫉妒、毀謗、驕傲、愚妄。 23這一切惡事都是從裡面生出來的,能使人污穢。」

外族婦人的信心

24耶穌從那裡啟程去泰爾西頓地區。祂進了一戶人家,原本不想讓人知道,卻無法避開人們的注意。 25-26當時有一個婦人的小女兒被污鬼附身,她聽見耶穌的事,就來俯伏在祂腳前,懇求祂趕出她女兒身上的鬼。這婦人是希臘人,來自敘利亞腓尼基

27耶穌對她說:「要先讓兒女們吃飽,因為把兒女的食物丟給狗吃不合適。」

28婦人說:「主啊,你說的對,但桌子下的狗也吃孩子們掉下來的碎渣呀!」

29耶穌說:「因為你這句話,你回去吧,鬼已經離開你的女兒了。」

30她回到家裡,見女兒躺在床上,鬼已經離開了。

醫治聾啞人

31耶穌離開泰爾地區,經過西頓,來到低加坡里地區的加利利湖。 32有人帶著一個又聾又啞的人來見耶穌,懇求祂把手按在這個人身上。 33耶穌就帶他離開眾人走到一邊,用指頭伸進他的耳朵,又吐唾沫抹他的舌頭, 34望天長歎,對他說:「以法大!」意思是「開了吧!」 35他的耳朵立刻開了,舌頭靈活了,說話也清楚了。 36耶穌吩咐他們不要將這事告訴別人。可是耶穌越是這樣吩咐,他們越是極力宣揚, 37聽見的人都十分驚奇,說:「祂做的一切都很好,甚至叫耳聾的聽見,啞巴說話!」