Marko 5 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Marko 5:1-43

Yesu Amponya Mtu Mwenye Pepo

(Mathayo 8:28-34; Luka 8:26-39)

15:1 Mt 8:28; Mk 8:26Wakafika upande wa pili wa ziwa wakaingia katika nchi ya Wagerasi. 25:2 Mk 4:1; 1:23Yesu alipotoka kwenye mashua, mara mtu mmoja mwenye pepo mchafu akatoka makaburini akakutana naye. 3Mtu huyu aliishi makaburini, wala hakuna aliyeweza kumzuia hata kwa kumfunga minyororo. 4Kwa kuwa mara kwa mara alikuwa amefungwa minyororo mikononi na miguuni, lakini akaikata hiyo minyororo na kuzivunja zile pingu miguuni mwake. Hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa na nguvu za kumzuia. 5Usiku na mchana alikuwa makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikatakata kwa mawe.

6Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akapiga magoti mbele yake. 75:7 Mt 8:29; Mdo 16:17; Ebr 7:1Akapiga kelele kwa nguvu akisema, “Una nini nami, Yesu, Mwana wa Mungu Aliye Juu Sana? Ninakusihi kwa jina la Mungu, usinitese!” 8Kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, “Mtoke mtu huyu, wewe pepo mchafu!”

9Yesu akamuuliza, “Jina lako ni nani?”

Akamjibu, “Jina langu ni Legioni,5:9 Legioni maana yake ni Jeshi. kwa kuwa tuko wengi.” 10Akamsihi Yesu sana asiwapeleke nje ya nchi ile.

11Palikuwa na kundi kubwa la nguruwe lililokuwa likilisha karibu kando ya kilima. 12Wale pepo wachafu wakamsihi Yesu wakisema, “Tuamuru twende kwenye wale nguruwe. Turuhusu tuwaingie.” 13Basi Yesu akawaruhusu, nao wale pepo wachafu wakatoka, wakawaingia hao nguruwe. Lile kundi lilikuwa na nguruwe wapatao 2,000, nao wote wakateremkia gengeni kwa kasi, nao wakatumbukia ziwani na kuzama.

14Wale watu waliokuwa wakichunga hao nguruwe wakakimbilia mjini na vijijini kueleza yaliyotukia. Watu wakatoka kwenda kuona hayo yaliyokuwa yametukia. 155:15 Mk 5:9; 5:18-19; 4:24Walipofika kwa Yesu, wakamwona yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu legioni akiwa ameketi hapo, amevaa nguo na mwenye akili timamu. Wakaogopa. 16Wale walioyaona mambo hayo wakawaeleza watu wengine yaliyomtokea yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu, na habari za lile kundi la nguruwe pia. 175:17 Mt 8:34; Mdo 16:39Basi watu wakaanza kumwomba Yesu aondoke katika nchi yao.

185:18 Lk 8:38Yesu alipokuwa anaingia kwenye mashua, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu akamsihi Yesu waende pamoja. 195:19 Mt 8:4Yesu hakumruhusu, bali alimwambia, “Nenda nyumbani kwa jamaa yako ukawaeleze mambo makuu aliyokutendea Bwana, na jinsi alivyokuhurumia.” 205:20 Mt 4:25; Mk 7:31Yule mtu akaenda zake, akaanza kutangaza katika Dekapoli mambo makuu Yesu aliyomtendea. Nao watu wote wakastaajabu.

Mwanamke Aponywa

(Mathayo 9:18-26; Luka 8:40-56)

215:21 Mt 9:1; Mk 4:1Yesu alipokwisha kuvuka tena na kufika ngʼambo, umati mkubwa wa watu ukamzunguka yeye akiwa hapo kando ya bahari. 225:22 Lk 13:14; Mdo 13:15Kisha mmoja wa viongozi wa sinagogi aliyeitwa Yairo akafika pale. Naye alipomwona Yesu, akapiga magoti miguuni pake, 235:23 Mt 19:13akamsihi akisema, “Binti yangu mdogo ni mgonjwa mahututi. Tafadhali nakusihi, njoo uweke mikono yako juu yake ili apate kupona, naye atakuwa hai.” 24Hivyo Yesu akaenda pamoja naye.

Umati mkubwa wa watu ukamfuata, nao watu wakawa wanamsonga. 255:25 Law 15:25-30Hapo palikuwa na mwanamke aliyekuwa amesumbuliwa na tatizo la kutokwa damu kwa miaka kumi na miwili. 26Mwanamke huyu alikuwa ameteseka sana kwa mikono ya matabibu wengi, na kutumia kila kitu alichokuwa nacho. Lakini badala ya kupona, hali yake ilizidi kuwa mbaya. 27Alikuwa amesikia habari za Yesu, naye akaja kwa nyuma yake kwenye umati wa watu, akaligusa vazi lake, 285:28 Mt 5:20kwa maana alisema moyoni mwake, “Kama nikiweza kuligusa vazi lake tu, nitaponywa.” 295:29 Mk 5:34Mara kutoka damu kwake kukakoma, naye akajisikia mwilini mwake amepona kabisa.

305:30 Lk 5:17; 6:19Ghafula Yesu akatambua kuwa nguvu zimemtoka. Akaugeukia ule umati wa watu na kuuliza, “Ni nani aliyegusa mavazi yangu?”

31Wanafunzi wake wakamjibu, “Unaona jinsi umati wa watu unavyokusonga. Wawezaje kuuliza, ‘Ni nani aliyenigusa?’ ”

32Lakini Yesu akaangalia pande zote ili aone ni nani aliyemgusa. 33Yule mwanamke, akijua kilichomtokea, akaja, akaanguka miguuni pake akitetemeka kwa hofu, akamweleza ukweli wote. 345:34 Mt 9:22; Mdo 15:33Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako.”

Yesu Amfufua Binti Yairo

355:35 Mk 5:22Alipokuwa bado anaongea, watu wakafika kutoka nyumbani kwa Yairo. Wakamwambia, “Binti yako amekufa. Kwa nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?”

36Aliposikia hayo waliyosema, Yesu akamwambia huyo kiongozi wa sinagogi, “Usiogope. Amini tu.”

375:37 Mt 4:21Hakumruhusu mtu mwingine yeyote amfuate isipokuwa Petro, Yakobo na Yohana, nduguye Yakobo. 385:38 Mt 5:22Walipofika nyumbani kwa yule kiongozi wa sinagogi, Yesu akaona ghasia, watu wakilia na kuomboleza kwa sauti kubwa. 395:39 Mt 9:24Alipokwisha kuingia ndani, akawaambia, “Kwa nini mnafanya ghasia na kulia? Mtoto hajafa, bali amelala tu.” 405:40 Mdo 9:40Wale watu wakamcheka kwa dharau.

Lakini yeye akawatoa wote nje, akawachukua baba na mama wa yule mtoto, pamoja na wale wanafunzi aliokuwa nao. Wakaingia ndani mpaka pale alipokuwa yule mtoto. 415:41 Mk 1:31; Lk 7:14; Mdo 9:40Akamshika mtoto mkono, akamwambia, “Talitha koum!” 5:41 Talitha koum ni lugha ya Kiaramu. (maana yake ni, “Msichana, nakuambia: amka!”) 42Mara yule msichana akasimama, akaanza kutembea (alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili). Walipoona haya, wakastaajabu sana. 435:43 Mt 8:4Yesu akawaagiza kwa ukali wasimweleze mtu yeyote jambo hilo, naye akawaambia wampe yule msichana chakula.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

馬可福音 5:1-43

治好被鬼附身的人

1他們來到湖對岸的格拉森地區。 2耶穌剛下船,迎面就遇見一個被污鬼附身的人,是從墳墓裡出來的。 3那人以墳墓為家,沒有人能把他捆住,就算用鐵鏈也不行。 4因為有人多次用鐵鏈和腳鐐鎖住他,但他掙斷了鐵鏈,砸碎了腳鐐。沒有人能制伏他。 5他晝夜在墳場和山野間大喊大叫,又用石頭砍自己。

6他遠遠看見耶穌,就跑過去跪下來拜祂,高聲喊道: 7「至高上帝的兒子耶穌啊,我和你有什麼關係?看在上帝的份上,求你不要折磨我!」 8原來,耶穌已經對他身上的鬼說:「污鬼,從這人身上出來!」

9耶穌問:「你叫什麼名字?」

他說:「我的名字叫『群』,因為我們是一大群。」

10接著污鬼再三哀求耶穌,不要把牠們趕出那個地區。 11當時有一大群豬在附近山坡上吃食。 12污鬼就央求耶穌說:「讓我們到豬群裡去,附在牠們身上吧!」

13耶穌允許了,污鬼就離開那人,進入豬群。那群豬就一路奔下陡坡,衝進湖裡淹死了,約有兩千頭。

14放豬的人逃走了,把這事傳遍了城裡鄉間,人們都跑來看個究竟。 15他們到了耶穌那裡,看見那曾被群鬼附身的人神智清醒、衣著整齊地坐在那裡,都很害怕。 16目擊者把被鬼附身的人和豬群的事告訴了他們, 17他們就請求耶穌離開他們那裡。

18耶穌上船的時候,那曾被鬼附身的人懇求耶穌讓他隨行。 19耶穌沒有答應,而是對他說:「回去見你的家人,把主為你所行的奇事和祂憐憫你的經過都告訴他們吧!」

20這人就回到低加坡里一帶傳揚耶穌為他所行的奇事,人們都很驚奇。

耶穌醫治有信心的人

21耶穌再坐船回到對岸,有一大群人在岸邊圍著祂。 22這時來了一個名叫雅魯的會堂主管,他一見到耶穌便俯伏在祂腳前, 23迫切懇求說:「我小女兒快要死了,求你去把手按在她身上,醫治她,救她一命。」

24耶穌和他同去,一大群人跟著祂,擁擠著祂。

25有一個婦人患血漏病已經十二年, 26經過許多醫生的診治,受盡痛苦,耗盡錢財,病情仍沒有好轉,反而更加嚴重。 27她聽見耶穌的事,就夾在人群中從耶穌背後摸祂的衣服, 28心想:「我只要摸到祂的衣服,就會痊癒。」

29她的血漏立刻止住了,她感到自己痊癒了。 30耶穌馬上知道有能力從自己身上發出,便在人群中轉過身來問:「誰摸了我的衣服?」

31門徒對祂說:「你看,這麼多人在你周圍擠來擠去,你怎麼問誰摸你呢?」

32耶穌環視四周,要找出摸祂的人。 33那婦人害怕得發抖,知道在自己身上發生了什麼,就上前俯伏在耶穌腳前,將實情說了出來。

34耶穌說:「女兒,你的信心救了你。安心去吧!你的病好了。」

35耶穌還在說話的時候,有人從雅魯家趕來,對雅魯說:「你的女兒已經死了,何必再麻煩老師呢?」

36耶穌聽了,就對雅魯說:「不要怕,只要信。」 37於是,祂帶著彼得雅各雅各的弟弟約翰雅魯家,不准其他人跟著。 38他們到了會堂主管家,耶穌看見在場的人嚎啕大哭,場面混亂。 39耶穌進去問道:「你們為什麼亂哄哄地哭叫呢?這孩子沒有死,只是睡著了。」

40眾人都譏笑祂。耶穌讓他們全部出去,然後帶著女孩的父母和三個門徒進了孩子的房間。 41祂拉著女孩的手說:「大利大,古米!」意思是:「小女孩,我吩咐你起來!」

42女孩應聲而起,開始走動。當時她十二歲。在場的人都驚奇不已。 43耶穌鄭重叮囑他們不要把這事張揚出去,又吩咐他們給女孩東西吃。