Marko 14 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 14:1-72

Shauri La Kumuua Yesu

(Mathayo 26:1-5; Luka 22:1-2; Yohana 11:45-53)

114:1 Yn 11:55; 13:1; Mt 12:14; 26:1-5; Lk 22:1-2Zilikuwa zimebaki siku mbili tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka, na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwa wakitafuta njia ya kumkamata Yesu kwa hila na kumuua. 214:2 Mt 26:1-5; Lk 22:1-2Lakini walisema, “Tusilifanye jambo hili wakati wa Sikukuu, maana watu wanaweza wakafanya ghasia.”

Yesu Kupakwa Mafuta Huko Bethania

(Mathayo 26:6-13; Yohana 12:1-8)

314:3 Mt 21:17; Lk 7:37-39Yesu alikuwa Bethania nyumbani kwa Simoni aliyekuwa na ukoma. Wakati alipokuwa ameketi mezani akila chakula cha jioni, mwanamke mmoja aliingia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya nardo14:3 Nardo ni aina ya manukato yaliyotengenezwa kutokana na mimea yenye mizizi inayotoa harufu nzuri. safi ya thamani kubwa. Akaivunja hiyo chupa, akamiminia hayo manukato kichwani mwa Yesu.

4Baadhi ya watu waliokuwepo pale walikuwa wakisemezana wao kwa wao, “Upotevu huu wote ni wa nini? 5Mafuta haya yangeweza kuuzwa kwa zaidi ya dinari14:5 Dinari 300 ni sawa na mshahara wa kibarua wa siku 300. 300, na fedha hizo wakapewa maskini.” Wakamkemea vikali huyo mwanamke.

6Lakini Yesu akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Mwacheni! Yeye amenitendea jambo zuri sana. 714:7 Kum 15:11Maskini mtakuwa nao siku zote na mnaweza kuwasaidia wakati wowote mnaotaka. Lakini mimi hamtakuwa nami siku zote. 814:8 Yn 19:40Huyu mwanamke amenitendea lile aliloweza. Ameumiminia mwili wangu manukato ili kuniandaa kwa maziko yangu. 914:9 Mt 24:14; Mk 16:15Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”

Yuda Akubali Kumsaliti Yesu

(Mathayo 26:14-16; Luka 22:3-6)

1014:10 Mk 3:16-19; Mt 10:4; 26:14-16; Lk 23:3-6Kisha Yuda Iskariote, mmoja wa wale wanafunzi kumi na wawili, akaenda kwa viongozi wa makuhani ili kumsaliti Yesu kwao. 1114:11 Mt 26:14-16; Lk 22:3-6Walifurahi sana kusikia jambo hili na wakaahidi kumpa fedha. Hivyo yeye akawa anatafuta wakati uliofaa wa kumsaliti.

Yesu Ala Pasaka Na Wanafunzi Wake

(Mathayo 26:17-25; Luka 22:7-14, 21-23; Yohana 13:21-30)

1214:12 Kum 16:1-4; 1Kor 5:714:12 Mt 26:17-19; 22:7-13Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo kwa desturi mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa, wanafunzi wa Yesu wakamuuliza, “Unataka twende wapi ili tukuandalie mahali pa kula Pasaka?”

1314:13 Mt 26:17-19; 22:7-13Basi akawatuma wawili miongoni mwa wanafunzi wake, akawaambia, “Nendeni mjini. Huko mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni. 1414:14 Mt 26:17-19; 22:7-13Mwambieni mwenye nyumba ile atakayoingia, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba changu cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’ 1514:15 Mdo 1:13; Mt 26:17-19; 22:7-19Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani, kilichopambwa tena kilicho tayari. Tuandalieni humo.”

1614:16 Mt 26:17-19; 22:7-19Wale wanafunzi wakaondoka na kwenda mjini, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.

1714:17 Mt 26:20Ilipofika jioni, Yesu akaja pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili. 1814:18 Za 41:10Walipoketi mezani wakila, Yesu akawaambia, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti, mmoja anayekula pamoja nami.”

19Wakaanza kuhuzunika na kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”

2014:20 Yn 13:18-27Akawajibu, “Ni mmoja miongoni mwenu ninyi kumi na wawili, yule anayechovya mkate kwenye bakuli pamoja nami. 2114:21 Mt 8:20Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa.”

Kuanzishwa Kwa Meza Ya Bwana

(Mathayo 26:26-30; Luka 22:14-20; 1 Wakorintho 11:23-25)

2214:22 Mt 14:22Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni mle; huu ndio mwili wangu.”

2314:23 1Kor 10:16Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, nao wote wakanywa kutoka humo.

2414:24 Mt 26:28Akawaambia, “Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi. 2514:25 Mt 3:2Amin, nawaambia, sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya katika Ufalme wa Mungu.”

2614:26 Mt 21:1Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.

Yesu Atabiri Kuwa Petro Atamkana

(Mathayo 26:31-35; Luka 22:31-34; Yohana 13:36-38)

2714:27 Zek 13:7Yesu akawaambia, “Ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa:

“ ‘Nitampiga mchungaji,

nao kondoo watatawanyika.’

2814:28 Mk 16:7Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”

2914:29 Mt 26:33-34; Lk 22:33, 34; Yn 13:37, 38Petro akasema, “Hata kama wengine wote watakuacha, mimi sitakuacha.”

3014:30 Lk 22:34; Yn 13:38Yesu akamwambia, “Amin, nakuambia; leo, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, wewe mwenyewe utanikana mara tatu.”

3114:31 Lk 22:33; Yn 13:37Lakini Petro akasisitiza zaidi, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.

Yesu Aomba Katika Bustani Ya Gethsemane

(Mathayo 26:36-46; Luka 22:39-46)

3214:32 Mt 26:36; Lk 22:29; Yn 13:37Wakaenda mahali paitwapo Gethsemane. Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa, nami niende nikaombe.” 33Kisha akawachukua pamoja naye Petro, Yakobo na Yohana. Akaanza kuhuzunika sana na kutaabika. 3414:34 Yn 12:27Akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe.”

3514:35 Mk 14:41; Mt 26:18Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba kwamba kama ingewezekana saa hiyo ya mateso imwondokee. 3614:36 Rum 8:15; Gal 4:6; Mt 20:22; 26:39Akasema, “Abba,14:36 Abba ni neno la Kiaramu ambalo maana yake ni Baba; ni mtoto wa kuzaa tu angeweza kulitumia kwa baba yake. Baba, mambo yote yawezekana kwako. Niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali vile upendavyo wewe.”

37Akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, “Simoni, umelala? Je, hukuweza kukesha hata kwa saa moja? 3814:38 Mt 6:13; Rum 7:22-23Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”

39Akaenda tena kuomba, akisema maneno yale yale. 40Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito. Nao hawakujua la kumwambia.

4114:41 Mt 26:18Akaja mara ya tatu, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Imetosha! Saa imewadia. Tazameni, Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi. 4214:42 Mt 26:46; Yn 18:1, 2Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”

Yesu Akamatwa

(Mathayo 26:47-56; Luka 22:47-53; Yohana 18:3-12)

4314:43 Mt 10:4Yesu alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale wanafunzi Kumi na Wawili, akatokea. Alikuwa amefuatana na umati wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani, walimu wa sheria, na wazee.

44Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni, mkamchukue chini ya ulinzi.” 4514:45 Mt 23:7Mara Yuda akamjia Yesu na kusema, “Rabi.”14:45 Rabi ni neno la Kiebrania ambalo maana yake ni daktari, mwalimu au bwana. Walikuwa na madaraja matatu: La chini kabisa Rab (bwana), la pili Rabi (bwana wangu), na la juu kabisa Raboni (mkuu wangu, bwana wangu mkuu). Akambusu. 46Wale watu wakamkamata Yesu, wakamweka chini ya ulinzi. 47Ndipo mmoja wa wale waliokuwa wamesimama karibu aliuchomoa upanga wake na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.

4814:48 Mt 26:55; Lk 22:52Kisha Yesu akawaambia, “Mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi? 4914:49 Mt 26:55; Isa 53:7-12Siku kwa siku nilikuwa pamoja nanyi nikifundisha Hekaluni, wala hamkunikamata. Lakini Maandiko sharti yatimie.” 5014:50 Za 88:8; Mk 14:27Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha, wakakimbia.

51Kijana mmoja, ambaye hakuwa amevaa kitu isipokuwa alijitanda nguo ya kitani, alikuwa akimfuata Yesu. Walipomkamata, 52alikimbia uchi, akaliacha vazi lake.

Yesu Mbele Ya Baraza La Wayahudi

(Mathayo 26:57-68; Luka 22:54-71; Yohana 18:13-24)

5314:53 Mt 26:57; Yn 18:13Wakampeleka Yesu kwa kuhani mkuu, nao viongozi wa makuhani wote, na wazee na walimu wa sheria wote wakakusanyika pamoja. 5414:54 Mt 26:3; Yn 18:18Petro akamfuata kwa mbali, hadi uani kwa kuhani mkuu. Huko akaketi pamoja na walinzi, akiota moto.

5514:55 Mt 5:22Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi14:55 Baraza la Wayahudi hapa ina maana ya Sanhedrin ambalo lilikuwa ndilo baraza la juu kabisa la utawala wa Kiyahudi, lililoundwa na wazee 70 pamoja na kuhani mkuu. lote wakatafuta ushahidi dhidi ya Yesu ili wapate kumuua. Lakini hawakupata jambo lolote. 56Wengi walitoa ushahidi wa uongo dhidi yake, lakini maelezo yao hayakukubaliana.

57Ndipo wengine wakasimama wakatoa ushahidi wa uongo dhidi yake, wakisema: 5814:58 Mk 15:29; Yn 2:19“Sisi tulimsikia akisema, ‘Mimi nitalibomoa Hekalu hili lililojengwa na wanadamu, na katika siku tatu nitajenga jingine ambalo halikujengwa na wanadamu.’ ” 59Lakini hata hivyo, ushahidi wao haukukubaliana.

6014:60 Mt 26:62Basi kuhani mkuu akasimama mbele yao, akamuuliza Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?” 6114:61 Isa 54:7; Lk 23:9; Mt 16:16; Yn 4:25-26Lakini Yesu akakaa kimya, hakusema neno lolote.

Kuhani mkuu akamuuliza tena, “Je, wewe ndiwe Kristo,14:61 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. Mwana wa Mungu Aliyebarikiwa?”

6214:62 Ufu 1:7; Dan 7:13Yesu akajibu, “Mimi ndimi. Nanyi mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”

6314:63 Hes 14:6; Mdo 14:14Kuhani mkuu akararua mavazi yake, akasema, “Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi? 6414:64 Law 24:16Ninyi mmesikia hayo makufuru. Uamuzi wenu ni gani?”

Wote wakamhukumu kwamba anastahili kifo. 6514:65 Mt 16:21Kisha baadhi ya watu wakaanza kumtemea mate; wakamfunga kitambaa machoni, wakampiga kwa ngumi na kumwambia, “Tabiri!” Walinzi wakamchukua na kumpiga makofi.

Petro Amkana Yesu

(Mathayo 26:69-75; Luka 22:56-62; Yohana 18:15-18, 25-27)

6614:66 Lk 22:55; Yn 18:16Petro alipokuwa bado yuko chini kwenye ua wa jumba la kifalme, tazama akaja mmoja wa watumishi wa kike wa kuhani mkuu. 6714:67 Mk 14:54; 1:24Alipomwona Petro akiota moto, akamtazama sana, akamwambia,

“Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”

6814:68 Mk 14:30, 72Lakini Petro akakana, akasema, “Sijui wala sielewi unalosema.” Naye akaondoka kuelekea kwenye njia ya kuingilia.

6914:69 Mt 26:71; Lk 22:58; Yn 18:25Yule mtumishi wa kike alipomwona mahali pale, akawaambia tena wale waliokuwa wamesimama hapo, “Huyu mtu ni mmoja wao.” 7014:70 Mdo 2:7Lakini Petro akakana tena.

Baada ya muda kidogo wale waliokuwa wamesimama hapo karibu na Petro wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana wewe pia ni Mgalilaya!” 7114:71 Mk 14:30, 72Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui huyu mtu mnayesema habari zake!”

7214:72 Mk 14:30, 68; Mt 26:75; Mk 14:50Papo hapo jogoo akawika mara ya pili. Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alikuwa amemwambia: “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.” Akavunjika moyo, akalia sana.

New International Reader’s Version

Mark 14:1-72

A Woman Pours Perfume on Jesus at Bethany

1The Passover and the Feast of Unleavened Bread were only two days away. The chief priests and the teachers of the law were plotting to arrest Jesus secretly. They wanted to kill him. 2“But not during the feast,” they said. “The people may stir up trouble.”

3Jesus was in Bethany. He was at the table in the home of Simon, who had a skin disease. A woman came with a special sealed jar. It contained very expensive perfume made out of pure nard. She broke the jar open and poured the perfume on Jesus’ head.

4Some of the people there became angry. They said to one another, “Why waste this perfume? 5It could have been sold for more than a year’s pay. The money could have been given to poor people.” So they found fault with the woman.

6“Leave her alone,” Jesus said. “Why are you bothering her? She has done a beautiful thing to me. 7You will always have poor people with you. You can help them any time you want to. But you will not always have me. 8She did what she could. She poured perfume on my body to prepare me to be buried. 9What I’m about to tell you is true. What she has done will be told anywhere the good news is preached all over the world. It will be told in memory of her.”

10Judas Iscariot was one of the 12 disciples. He went to the chief priests to hand Jesus over to them. 11They were delighted to hear that he would do this. They promised to give Judas money. So he watched for the right time to hand Jesus over to them.

The Last Supper

12It was the first day of the Feast of Unleavened Bread. That was the time to sacrifice the Passover lamb. Jesus’ disciples asked him, “Where do you want us to go and prepare for you to eat the Passover meal?”

13So he sent out two of his disciples. He told them, “Go into the city. A man carrying a jar of water will meet you. Follow him. 14He will enter a house. Say to its owner, ‘The Teacher asks, “Where is my guest room? Where can I eat the Passover meal with my disciples?” ’ 15He will show you a large upstairs room. It will have furniture and will be ready. Prepare for us to eat there.”

16The disciples left and went into the city. They found things just as Jesus had told them. So they prepared the Passover meal.

17When evening came, Jesus arrived with the 12 disciples. 18While they were at the table eating, Jesus said, “What I’m about to tell you is true. One of you who is eating with me will hand me over to my enemies.”

19The disciples became sad. One by one they said to him, “Surely you don’t mean me?”

20“It is one of you,” Jesus replied. “It is the one who dips bread into the bowl with me. 21The Son of Man will go just as it is written about him. But how terrible it will be for the one who hands over the Son of Man! It would be better for him if he had not been born.”

22While they were eating, Jesus took bread. He gave thanks and broke it. He handed it to his disciples and said, “Take it. This is my body.”

23Then he took a cup. He gave thanks and handed it to them. All of them drank from it.

24“This is my blood of the covenant,” he said to them. “It is poured out for many. 25What I’m about to tell you is true. I won’t drink wine with you again until the day I drink it in God’s kingdom.”

26Then they sang a hymn and went out to the Mount of Olives.

Jesus Says That the Disciples Will Turn Away

27“You will all turn away,” Jesus told the disciples. “It is written,

“ ‘I will strike the shepherd down.

Then the sheep will be scattered.’ (Zechariah 13:7)

28But after I rise from the dead, I will go ahead of you into Galilee.”

29Peter said, “All the others may turn away. But I will not.”

30“What I’m about to tell you is true,” Jesus answered. “It will happen today, in fact tonight. Before the rooster crows twice, you yourself will say three times that you don’t know me.”

31But Peter would not give in. He said, “I may have to die with you. But I will never say I don’t know you.” And all the others said the same thing.

Jesus Prays in Gethsemane

32Jesus and his disciples went to a place called Gethsemane. Jesus said to them, “Sit here while I pray.” 33He took Peter, James and John along with him. He began to be very upset and troubled. 34“My soul is very sad. I feel close to death,” he said to them. “Stay here. Keep watch.”

35He went a little farther. Then he fell to the ground. He prayed that, if possible, the hour might pass by him. 36Abba, Father,” he said, “everything is possible for you. Take this cup of suffering away from me. But let what you want be done, not what I want.”

37Then he returned to his disciples and found them sleeping. “Simon,” he said to Peter, “are you asleep? Couldn’t you keep watch for one hour? 38Watch and pray. Then you won’t fall into sin when you are tempted. The spirit is willing, but the body is weak.”

39Once more Jesus went away and prayed the same thing. 40Then he came back. Again he found them sleeping. They couldn’t keep their eyes open. They did not know what to say to him.

41Jesus returned the third time. He said to them, “Are you still sleeping and resting? Enough! The hour has come. Look! The Son of Man is about to be handed over to sinners. 42Get up! Let us go! Here comes the one who is handing me over to them!”

Jesus Is Arrested

43Just as Jesus was speaking, Judas appeared. He was one of the 12 disciples. A crowd was with him. They were carrying swords and clubs. The chief priests, the teachers of the law, and the elders had sent them.

44Judas, who was going to hand Jesus over, had arranged a signal with them. “The one I kiss is the man,” he said. “Arrest him and have the guards lead him away.” 45So Judas went to Jesus at once. Judas said, “Rabbi!” And he kissed Jesus. 46The men grabbed Jesus and arrested him. 47Then one of those standing nearby pulled his sword out. He struck the servant of the high priest and cut off his ear.

48“Am I leading a band of armed men against you?” asked Jesus. “Do you have to come out with swords and clubs to capture me? 49Every day I was with you. I taught in the temple courtyard, and you didn’t arrest me. But the Scriptures must come true.” 50Then everyone left him and ran away.

51A young man was following Jesus. The man was wearing nothing but a piece of linen cloth. When the crowd grabbed him, 52he ran away naked. He left his clothing behind.

Jesus Is Taken to the Sanhedrin

53The crowd took Jesus to the high priest. All the chief priests, the elders, and the teachers of the law came together. 54Not too far away, Peter followed Jesus. He went right into the courtyard of the high priest. There he sat with the guards. He warmed himself at the fire.

55The chief priests and the whole Sanhedrin were looking for something to use against Jesus. They wanted to put him to death. But they did not find any proof. 56Many witnesses lied about him. But their stories did not agree.

57Then some of them stood up. Here is what those false witnesses said about him. 58“We heard him say, ‘I will destroy this temple made by human hands. In three days I will build another temple, not made by human hands.’ ” 59But what they said did not agree.

60Then the high priest stood up in front of them. He asked Jesus, “Aren’t you going to answer? What are these charges these men are bringing against you?” 61But Jesus remained silent. He gave no answer.

Again the high priest asked him, “Are you the Messiah? Are you the Son of the Blessed One?”

62“I am,” said Jesus. “And you will see the Son of Man sitting at the right hand of the Mighty One. You will see the Son of Man coming on the clouds of heaven.”

63The high priest tore his clothes. “Why do we need any more witnesses?” he asked. 64“You have heard him say a very evil thing against God. What do you think?”

They all found him guilty and said he must die. 65Then some began to spit at him. They blindfolded him. They hit him with their fists. They said, “Prophesy!” And the guards took him and beat him.

Peter Says He Does Not Know Jesus

66Peter was below in the courtyard. One of the high priest’s female servants came by. 67When she saw Peter warming himself, she looked closely at him.

“You also were with Jesus, that Nazarene,” she said.

68But Peter said he had not been with him. “I don’t know or understand what you’re talking about,” he said. He went out to the entrance to the courtyard.

69The servant saw him there. She said again to those standing around, “This fellow is one of them.” 70Again he said he was not.

After a little while, those standing nearby said to Peter, “You must be one of them. You are from Galilee.”

71Then Peter began to curse. He said to them, “I don’t know this man you’re talking about!”

72Right away the rooster crowed the second time. Then Peter remembered what Jesus had spoken to him. “The rooster will crow twice,” he had said. “Before it does, you will say three times that you don’t know me.” Peter broke down and cried.