Marko 13 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 13:1-37

Dalili Za Siku Za Mwisho

(Mathayo 24:1-2; Luka 21:5-6)

113:1 Mt 24:1; Lk 21:5Yesu alipokuwa akitoka Hekaluni, mmojawapo wa wanafunzi wake akamwambia, “Mwalimu! Tazama jinsi mawe haya yalivyo makubwa, na majengo haya yalivyo mazuri!”

213:2 Lk 19:44Ndipo Yesu akajibu akasema, “Je, unayaona majengo haya yalivyo makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali yote yatabomolewa.”

Mateso Yatabiriwa

(Mathayo 24:3-14; Luka 21:7-19)

313:3 Mt 21:1; 4:21Yesu alipokuwa ameketi kwenye Mlima wa Mizeituni mkabala na Hekalu, Petro, Yakobo, Yohana na Andrea wakamuuliza faraghani, 413:4 Mt 24:3; Lk 21:7“Tafadhali tuambie, mambo haya yatatukia lini? Nayo dalili ya kuwa hayo yote yanakaribia kutimia itakuwa gani?”

513:5 Yer 29:8; 1Tim 4:1Yesu akawaambia: “Jihadharini mtu yeyote asiwadanganye. 6Wengi watakuja kwa Jina langu wakidai, ‘Mimi ndiye,’ nao watawadanganya wengi. 7Msikiapo habari za vita na uvumi wa vita, msiwe na hofu. Mambo haya hayana budi kutukia, lakini ule mwisho bado. 813:8 Mt 24:8; Isa 19:2; 2Nya 15:6Taifa litainuka dhidi ya taifa na ufalme dhidi ya ufalme. Kutakuwa na mitetemeko sehemu mbalimbali na njaa. Haya yatakuwa ndio mwanzo wa utungu.

913:9 Mt 10:17“Lakini ninyi jihadharini. Kwa maana watawapeleka katika mabaraza yao na kupigwa mijeledi katika masinagogi. Mtashtakiwa mbele ya watawala na wafalme kwa ajili yangu, ili kuwa ushuhuda kwao. 1013:10 Mt 10:19-20Nayo habari njema lazima ihubiriwe kwanza kwa mataifa yote kabla ule mwisho haujawadia. 1113:11 Lk 12:11-12Mtakapokamatwa na kushtakiwa, msisumbuke awali kuhusu mtakalosema. Semeni tu lolote mtakalopewa wakati huo, kwa kuwa si ninyi mtakaokuwa mkinena, bali ni Roho Mtakatifu.

1213:12 Mik 7:6; Lk 12:51-53“Ndugu atamsaliti ndugu yake ili auawe, naye baba atamsaliti mtoto wake. Watoto nao wataasi dhidi ya wazazi wao na kusababisha wauawe. 1313:13 Yn 15:21; Mt 10:22Watu wote watawachukia kwa ajili ya Jina langu. Lakini yule atakayevumilia hadi mwisho ataokolewa.

Chukizo La Uharibifu

(Mathayo 24:15-28; Luka 21:20-24)

1413:14 Dan 11:31; 12:11“Mtakapoona ‘chukizo la uharibifu’ limesimama mahali pasipolipasa (asomaye na afahamu), basi wale walioko Uyahudi wakimbilie milimani. 15Yeyote aliye juu ya dari ya nyumba asishuke au kuingia ndani ili kuchukua chochote. 16Aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake. 1713:17 Lk 22:39; 21:23Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! 18Ombeni mambo haya yasitokee wakati wa baridi. 1913:19 Mk 10:6; Dan 9:26; Yoe 2:2Kwa maana siku hizo zitakuwa za dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo, hapo Mungu alipoumba ulimwengu, mpaka leo, na wala haitakuwako tena kamwe. 20Kama Bwana asingelifupisha siku hizo, kamwe asingeliokoka mtu yeyote. Lakini kwa ajili ya wateule, wale aliowachagua, amezifupisha siku hizo. 2113:21 Lk 17:23; 21:8Wakati huo mtu yeyote akiwaambia, ‘Tazama, Kristo13:21 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. huyu hapa!’ au, ‘Tazama, yuko kule,’ msisadiki. 2213:22 Mt 7:15; Yn 4:48; 2The 2:9-10Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo, nao watafanya ishara na maajabu ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale wateule. 2313:23 2Pet 3:17Hivyo jihadharini. Nimekwisha kuwaambia mambo haya yote mapema kabla hayajatukia.

Kuja Kwa Mwana Wa Adamu

(Mathayo 24:29-31; Luka 21:25-28)

2413:24 Isa 13:10“Lakini katika siku hizo, baada ya hiyo dhiki,

“ ‘jua litatiwa giza

nao mwezi hautatoa nuru yake;

2513:25 Isa 34:4; Mt 24:9nazo nyota zitaanguka kutoka angani,

na nguvu za anga zitatikisika.’

2613:26 Dan 7:13; Ufu 1:7“Ndipo watu wote watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu nyingi na utukufu. 2713:27 Zek 2:6Naye atawatuma malaika wake wawakusanye wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka miisho ya dunia hadi miisho ya mbingu.

Somo Kuhusu Mtini

(Mathayo 24:32-35; Luka 21:29-33)

2813:28 Mt 24:32; Lk 21:29“Basi jifunzeni somo hili kutokana na mtini: Matawi yake yanapoanza kuchipua na kutoa majani, mnatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia. 29Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba wakati u karibu, hata malangoni. 3013:30 Lk 17:25; Mk 9:11Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia. 3113:31 Mt 5:18Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.

Hakuna Ajuaye Siku Wala Saa

(Mathayo 24:36-44)

3213:32 Mdo 1:7; 1The 5:1-2“Kwa habari ya siku ile na saa hakuna yeyote ajuaye, hata malaika walio mbinguni wala Mwana, ila Baba peke yake. 33Jihadharini! Kesheni! Kwa maana hamjui wakati ule utakapowadia. 3413:34 Mt 25:14Ni kama mtu anayesafiri. Anaiacha nyumba yake na kuwaachia watumishi wake kuiangalia, kila mtu na kazi yake, kisha akamwamuru yule bawabu aliye mlangoni akeshe.

3513:35 Mt 24:42, 44“Basi kesheni kwa sababu hamjui ni lini mwenye nyumba atakaporudi: iwapo ni jioni, au ni usiku wa manane, au alfajiri awikapo jogoo, au mapambazuko. 36Kama akija ghafula, asije akawakuta mmelala. 3713:37 Lk 12:35-40Lile ninalowaambia ninyi, nawaambia watu wote: ‘Kesheni!’ ”

Nueva Versión Internacional

Marcos 13:1-37

Las señales del fin del mundo

1Cuando Jesús salía del Templo, uno de sus discípulos le dijo:

―¡Mira, Maestro! ¡Qué piedras! ¡Qué edificios!

2―¿Ves todos estos grandiosos edificios? —contestó Jesús—. No quedará piedra sobre piedra, pues todo será derribado.

3Más tarde, Jesús estaba sentado en el monte de los Olivos, frente al Templo. Y Pedro, Santiago, Juan y Andrés le preguntaron en privado:

4―Dinos, ¿cuándo sucederá eso, y cuál será la señal de que todo está a punto de cumplirse?

5―Tengan cuidado de que nadie los engañe —comenzó Jesús a decirles—. 6Vendrán muchos que, usando mi nombre, dirán: “Yo soy el Cristo”. Así engañarán a muchos. 7Cuando sepan de guerras y de rumores de guerras, no se alarmen. Es necesario que eso suceda, pero no será todavía el fin. 8Se levantará nación contra nación, y reino contra reino. Habrá terremotos en diferentes lugares; también habrá hambre. Esto será apenas el comienzo de los dolores.

9»Pero ustedes cuídense. Los entregarán a los tribunales y los azotarán en las sinagogas. Por mi causa comparecerán ante gobernadores y reyes para dar testimonio ante ellos. 10Pero primero tendrá que predicarse la buena noticia a todas las naciones. 11Y, cuando los arresten, no se preocupen de antemano por lo que van a decir. Solo declaren lo que se les dé a decir en ese momento. No serán ustedes los que hablen, sino el Espíritu Santo.

12»El hermano entregará a la muerte al hermano, y el padre, al hijo. Los hijos se rebelarán contra sus padres y harán que los maten. 13Por causa de mi nombre todo el mundo los odiará, pero el que se mantenga firme hasta el fin será salvo.

14»Ahora bien, cuando vean “el horrible sacrilegio” donde no debe estar (el que lee, que lo entienda), entonces los que estén en Judea huyan a las montañas. 15El que esté en el techo no baje ni entre en casa para llevarse nada. 16Y el que esté en el campo no regrese a buscar su capa. 17¡Ay de las que estén embarazadas o amamantando en aquellos días! 18Oren para que esto no suceda en invierno. 19Porque serán días de gran sufrimiento, como no lo ha habido desde el principio, cuando Dios creó el mundo, ni lo habrá jamás. 20Si el Señor no hubiera acortado esos días, nadie sobreviviría; pero, por causa de los que él ha elegido, los ha acortado. 21Entonces, si alguien les dice a ustedes: “¡Miren, aquí está el Cristo!” o “¡Miren, allí está!”, no lo crean, 22porque surgirán falsos Cristos y falsos profetas. Y harán maravillas y milagros para engañar, de ser posible, aun a los elegidos. 23Así que tengan cuidado; se lo he dicho a ustedes de antemano.

24»Pero en aquellos días, después de ese tiempo de sufrimiento,

»“se oscurecerá el sol

y no brillará más la luna.

25Las estrellas caerán del cielo

y los cuerpos celestes serán sacudidos”.

26»Verán entonces al Hijo del hombre venir sobre las nubes con gran poder y gloria. 27Y él enviará a sus ángeles para reunir a sus seguidores de los cuatro puntos cardinales, desde el último rincón de la tierra hasta lo último del cielo.

28»Aprendan de la higuera esta lección: Tan pronto como se ponen tiernas sus ramas y brotan sus hojas, ustedes saben que el verano está cerca. 29Igualmente, cuando vean que suceden estas cosas, sepan que el tiempo está cerca, a las puertas. 30Les aseguro que todas estas cosas sucederán antes de que muera la gente de este tiempo. 31El cielo y la tierra pasarán, pero mis palabras jamás pasarán.

Estar preparados

32»Pero, en cuanto al día y la hora, nadie lo sabe, ni siquiera los ángeles en el cielo, ni el Hijo, sino solo el Padre. 33¡Estén alerta! Manténganse despiertos porque ustedes no saben cuándo llegará ese tiempo. 34Es como cuando un hombre sale de viaje y deja su casa al cuidado de sus siervos, cada uno con su tarea, y le manda al portero que vigile.

35»Por lo tanto, manténganse despiertos, porque no saben cuándo volverá el dueño de la casa. No saben si será al atardecer, o a la medianoche, o al canto del gallo, o al amanecer. 36No permitan que los encuentre dormidos, aunque venga de repente. 37Lo que les digo a ustedes, se lo digo a todos: ¡Manténganse despiertos!».