Marko 10 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Marko 10:1-52

Mafundisho Kuhusu Talaka

(Mathayo 19:1-12; Luka 16:18)

110:1 Yn 10:40; 11:7; Mt 4:23; Mk 4:2Yesu akaondoka huko, akavuka Mto Yordani, akaenda sehemu za Uyahudi. Umati mkubwa wa watu ukaenda kwake tena, naye kama ilivyokuwa desturi yake, akawafundisha.

210:2 Mk 2:16Baadhi ya Mafarisayo wakaja ili kumjaribu kwa kumuuliza, “Je, ni halali mtu kumwacha mke wake?”

3Yesu akawajibu, “Je, Mose aliwaamuru nini?”

410:4 Kum 24:1-4; Mt 5:31Wakajibu, “Mose aliruhusu kwamba mume anaweza kumwandikia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”

510:5 Za 95:8; Ebr 3:15Yesu akawaambia, “Mose aliwaandikia sheria hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu. 610:6 Mwa 1:27; 5:2Lakini tangu mwanzo wa uumbaji, ‘Mungu aliwaumba mwanaume na mwanamke. 710:7 Mwa 2:2; 1Kor 6:16; Efe 5:31Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.’ 810:8 Mwa 2:24; 1Kor 6:16Kwa hiyo hawatakuwa wawili tena, bali mwili mmoja. 9Basi, alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”

10Walipokuwa tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamuuliza kuhusu jambo hili. 1110:11 Mt 5:32; Lk 16:8Akawajibu, “Mtu yeyote amwachaye mkewe na kuoa mke mwingine, anazini naye. 1210:12 Rum 7:3; 1Kor 7:10-11Naye mwanamke amwachaye mumewe na kuolewa na mume mwingine, anazini.”

Yesu Anawabariki Watoto Wadogo

(Mathayo 19:13-15; Luka 18:15-17)

1310:13 Mt 19:13; Lk 18:15Watu walikuwa wakimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wake wakawakemea. 1410:14 Mt 25:34Yesu alipoona yaliyokuwa yakitukia, akachukizwa. Akawaambia wanafunzi wake, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hawa. 1510:15 Mt 18:3Amin, nawaambia, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.” 1610:16 Mk 9:36Akawachukua watoto mikononi mwake, akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabariki.

Kijana Tajiri

(Mathayo 19:16-30; Luka 18:18-30)

1710:17 Mk 1:40; Lk 10:25; Mdo 20:32Yesu alipokuwa anaondoka, mtu mmoja akamkimbilia, akapiga magoti mbele yake, akamuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?”

18Yesu akamwambia, “Mbona unaniita mwema? Hakuna yeyote aliye mwema ila Mungu peke yake. 1910:19 Kut 20:12-16; Kum 5:16-20Unazijua amri: ‘Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, usidanganye, waheshimu baba yako na mama yako.’ ”

20Akamjibu, “Mwalimu, amri hizi zote nimezishika tangu nikiwa mtoto.”

2110:21 Mdo 2:45; Mt 6:20; Lk 12:33; Mt 4:19Yesu akamtazama na kumpenda, akamwambia, “Umepungukiwa na kitu kimoja. Nenda ukauze kila kitu ulicho nacho uwape maskini hizo fedha, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”

22Yule mtu aliposikia hayo, akasikitika sana. Akaondoka kwa huzuni kwa sababu alikuwa na mali nyingi.

2310:23 Za 62:10; 1Tim 6:9-17Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Itakuwa vigumu sana kwa wenye mali kuingia katika Ufalme wa Mungu!”

2410:24 Mt 7:13-14; Yn 3:5Wanafunzi wake wakashangazwa sana na maneno hayo. Lakini Yesu akawaambia tena, “Wanangu, tazama jinsi ilivyo vigumu kwa wale wanaotumainia mali kuingia katika Ufalme wa Mungu. 2510:25 Lk 12:16-20; 16:19-31Ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajiri10:25 Tajiri ina maana wale wanaotumainia mali. kuingia katika Ufalme wa Mungu.”

26Wanafunzi wake wakashangaa sana. Wakaulizana wao kwa wao, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”

2710:27 Mt 19:26Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu sivyo. Mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”

2810:28 Mt 4:18-19; Lk 18:28Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, tumeacha kila kitu na kukufuata wewe!”

29Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna mtu yeyote aliyeacha nyumba, ndugu wa kiume au wa kike, au mama au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, 3010:30 Mt 6:33; 12:32; 25:46ambaye hatalipwa mara mia katika ulimwengu huu: nyumba, ndugu wa kiume na wa kike, mama na baba na watoto, mashamba pamoja na mateso, kisha uzima wa milele katika ulimwengu ujao. 3110:31 Mt 19:30Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wa mwisho watakuwa wa kwanza.”

Yesu Atabiri Mara Ya Tatu Kufa Na Kufufuka Kwake

(Mathayo 20:17-19; Luka 18:31-34)

3210:32 Mk 3:16-19Walikuwa njiani wakipanda kwenda Yerusalemu, na Yesu alikuwa ametangulia. Wanafunzi wake walishangaa, nao watu waliowafuata walijawa na hofu. Yesu akawachukua tena wale wanafunzi wake kumi na wawili kando na kuwaambia yatakayompata. 3310:33 Lk 9:51; Mt 8:20; 27:1-2Akasema, “Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atasalitiwa kwa viongozi wa makuhani na walimu wa sheria. Wao watamhukumu kifo na kumtia mikononi mwa watu wa Mataifa, 3410:34 Mdo 2:23; Mt 16:21ambao watamdhihaki na kumtemea mate, watampiga na kumuua. Siku tatu baadaye atafufuka.”

Ombi La Yakobo Na Yohana

(Mathayo 20:20-28)

3510:35 Mt 20:20; 20:20-28Kisha Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, wakaja kwake na kumwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie lolote tutakalokuomba.”

36Naye akawaambia, “Je, mwataka niwafanyie jambo gani?”

3710:37 Mt 19:28Wakamwambia, “Tupe kukaa mmoja upande wako wa kuume na mwingine upande wako wa kushoto katika utukufu wako.”

3810:38 Ay 38:2; Mt 20:22; Lk 12:50Lakini Yesu akawaambia, “Ninyi hamjui mnaloliomba. Je, mnaweza kukinywea kikombe ninyweacho mimi, au kubatizwa ubatizo nibatizwao mimi?”

3910:39 Mdo 12:22; Ufu 1:9Wakajibu, “Tunaweza.”

Kisha Yesu akawaambia, “Kikombe nikinyweacho mtakinywea na ubatizo nibatizwao mtabatizwa, 40lakini kuketi mkono wangu wa kuume au wa kushoto si juu yangu mimi kuwapa. Nafasi hizi ni kwa ajili ya wale walioandaliwa.”

4110:41 Mt 20:24Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohana. 4210:42 Lk 22:25-27Lakini Yesu akawaita wote pamoja na kuwaambia, “Mnafahamu kuwa wale wanaodhaniwa kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu, nao wenye vyeo huonyesha mamlaka yao. 4310:43 Mk 5:35Lakini isiwe hivyo kwenu. Badala yake, yeyote anayetaka kuwa mkuu miongoni mwenu hana budi kuwa mtumishi wenu, 44na yeyote anayetaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa mtumwa wa wote. 4510:45 Mt 20:28Kwa kuwa hata Mwana wa Adamu hakuja ili kutumikiwa, bali kutumika na kuutoa uhai wake uwe fidia kwa ajili ya wengi.”

Yesu Amponya Kipofu Bartimayo

(Mathayo 20:29-34; Luka 18:35-43)

4610:46 Mt 20:29; Lk 18:35-43; Mt 20:29-34; Lk 18:35-43Kisha wakafika Yeriko. Yesu alipokuwa akiondoka mjini na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mmoja, jina lake Bartimayo, mwana wa Timayo, alikuwa ameketi kando ya njia akiomba msaada. 4710:47 Mk 1:24; Mt 9:27Aliposikia kuwa ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita, akaanza kupaza sauti akisema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”

48Watu wengi wakamkemea, wakamwambia akae kimya, lakini yeye akazidi kupaza sauti, akisema, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”

49Yesu akasimama na kusema, “Mwiteni.”

Hivyo wakamwita yule mtu kipofu, wakamwambia, “Jipe moyo! Inuka, anakuita.” 50Akiwa analivua lile joho lake, alisimama na kumwendea Yesu.

5110:51 Mt 23:7Yesu akamuuliza, “Unataka nikufanyie nini?”

Yule kipofu akajibu, “Mwalimu, nataka kuona.”

5210:52 Mt 9:22; 4:19; Mk 5:34Yesu akamwambia, “Nenda zako, imani yako imekuponya.” Mara akapata kuona, akamfuata Yesu njiani.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

馬可福音 10:1-52

論婚姻

1耶穌離開那裡,來到猶太地區和約旦河東岸,人群又聚集到祂那裡。耶穌照常教導他們。 2一些法利賽人想試探耶穌,就來問祂:「男人可以休妻嗎?」 3耶穌反問道:「摩西怎麼吩咐你們的?」

4他們說:「摩西准許人寫休書休妻。」

5耶穌說:「摩西因為你們心裡剛硬,才給你們寫了這條誡命。 6太初創造時,『上帝造了男人和女人。』10·6 創世記1·27 7『因此,人要離開父母,與妻子結合, 8二人成為一體。』10·8 創世記2·24這樣,夫妻不再是兩個人,而是一體了。 9因此,上帝配合的,人不可分開。」

10回到屋裡後,門徒追問耶穌這件事。 11耶穌說:「任何人休妻另娶,就是對妻子不忠,是犯通姦罪。 12同樣,妻子若離棄丈夫另嫁,也是犯通姦罪。」

祝福孩童

13有人帶著小孩子來要讓耶穌為他們按手,門徒卻責備他們。 14耶穌看見後很生氣,對門徒說:「讓小孩子到我這裡來,不要阻止他們,因為上帝的國屬於這樣的人。 15我實在告訴你們,人若不像小孩子一樣接受上帝的國,絕不能進去。」 16於是,耶穌抱起小孩子,為他們按手祝福。

永生的代價

17耶穌正要上路,有一個人跑來跪在祂跟前,問祂:「良善的老師,我該做什麼才能承受永生?」

18耶穌說:「你為什麼稱我是良善的?只有上帝是良善的。 19你知道『不可殺人,不可通姦,不可偷盜,不可作偽證,不可欺詐,要孝敬父母』10·19 出埃及記20·12‑16申命記5·16‑20這些誡命。」

20那人說:「老師,我從小就遵行這些誡命。」

21耶穌望著他,心中愛他,便說:「你還差一件事,就是去變賣你所有的產業,送給窮人,你必有財寶存在天上,然後你還要來跟從我。」

22那人聽了,臉色驟變,便沮喪地走了,因為他有許多產業。 23耶穌環顧四周,對門徒說:「有錢人進上帝的國真難啊!」

24門徒聽了感到驚奇,耶穌便再次對他們說:「孩子們,10·24 有古卷此處有「依靠錢財的人」。進上帝的國真難啊! 25駱駝穿過針眼比有錢人進上帝的國還容易呢!」

26門徒更加驚奇,便議論說:「這樣,誰能得救呢?」

27耶穌看著他們說:「對人而言,這不可能,但對上帝而言,凡事都可能。」

28彼得說:「你看,我們已經撇下一切來跟從你了。」

29耶穌說:「我實在告訴你們,任何人為了我和福音而撇下房屋、弟兄、姊妹、父母、兒女或田地, 30今世必在房屋、弟兄、姊妹、父母、兒女或田地方面獲得百倍的回報,來世必得永生。同時他也會受到迫害。 31然而,許多為首的將要殿後,殿後的將要為首。」

耶穌第三次預言自己的受難

32在前往耶路撒冷的路上,耶穌走在眾人前面,門徒感到驚奇,其他跟隨的人也很害怕。

耶穌又把十二使徒叫到一旁,把自己將要遭遇的事告訴他們,說: 33「看啊,我們現在前往耶路撒冷,人子將被交給祭司長和律法教師,他們要判祂死刑,把祂交給外族人。 34他們會嘲弄祂,向祂吐唾沫,鞭打祂,殺害祂。但是,三天之後祂必復活!」

雅各與約翰的請求

35西庇太的兩個兒子雅各約翰上前對耶穌說:「老師,請你答應我們一個要求。」

36耶穌問:「什麼要求?」

37他們說:「在你的榮耀中,求你讓我們一個坐在你右邊,一個坐在你左邊。」

38耶穌說:「你們不知道自己在求什麼。我要喝的那杯,你們能喝嗎?我要受的洗,你們能受嗎?」

39他們說:「我們能。」

耶穌說:「我要喝的那杯,你們也要喝;我所受的洗,你們也要受。 40不過誰坐在我的左右不是我來定,而是為誰預備的,就讓誰坐。」

41其他十個門徒聽見這事,很生雅各約翰的氣。 42於是,耶穌把他們叫來,對他們說:「你們知道,外族人有君王統治他們,有大臣管理他們, 43但你們不可這樣。你們中間誰想當首領,誰就要做大家的僕人; 44誰想居首位,誰就要做大家的奴僕。 45因為就連人子也不是來受人服侍,而是來服侍人,並且犧牲性命,作許多人的贖價。」

治好瞎眼的巴底買

46耶穌和門徒來到耶利哥。當耶穌和門徒及一大群人出城的時候,有一個瞎眼的人坐在路旁乞討,他的名字叫巴底買,是底買的兒子。 47巴底買一聽說是拿撒勒人耶穌,就喊道:「大衛的後裔耶穌啊,可憐我吧!」

48許多人都責備他,叫他不要吵,但他卻更加大聲喊道:「大衛的後裔啊,可憐我吧!」

49耶穌停下腳步,說:「叫他過來吧。」

他們就對那瞎眼的說:「好了,起來吧,祂叫你呢。」

50那人丟下外衣,跳了起來,走到耶穌面前。

51耶穌問他:「你要我為你做什麼?」

他說:「老師,我想看見。」

52耶穌說:「去吧!你的信心救10·52 「救」或譯「醫治」。了你。」他立刻得見光明,在路上跟從了耶穌。