Maombolezo 3 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version

Maombolezo 3:1-66

3 Sura hii imetungwa kila beti likianzia, na pia kila mstari katika lile beti, na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22. 13:1 Ay 19:21; Za 88:7; Yer 15:17-18Mimi ndiye mtu aliyeona mateso

kwa fimbo ya ghadhabu yake.

23:2 Ay 19:8; Za 82:5; Yer 4:23Amenifukuzia mbali na kunifanya nitembee

gizani wala si katika nuru;

33:3 Isa 5:25; Za 38:2hakika, amegeuza mkono wake dhidi yangu

tena na tena, mchana kutwa.

43:4 Za 51:8; Isa 38:13; Yer 50:17; Ay 30:30; Mao 4:8Amefanya ngozi yangu na nyama yangu kuchakaa

na ameivunja mifupa yangu.

53:5 Yer 23:15Amenizingira na kunizunguka

kwa uchungu na taabu.

63:6 Isa 59:10; Za 143:3; 88:5-6Amenifanya niishi gizani

kama wale waliokufa.

73:7 Ay 3:23; Yer 40:4Amenizungushia ukuta ili nisiweze kutoroka,

amenifunga kwa minyororo mizito.

83:8 Kum 1:45; Ay 30:20; Za 22:2; 5:2Hata ninapoita au kulia ili kuomba msaada,

anakataa kupokea maombi yangu.

93:9 Ay 9:24; Hos 2:6; Isa 63:17Ameizuia njia yangu kwa mapande ya mawe,

amepotosha njia zangu.

103:10 Ay 10:16; Hos 13:8; Amo 5:18-19Kama dubu aviziaye,

kama simba mafichoni,

11ameniburuta kutoka njia,

akanirarua na kuniacha bila msaada.

123:12 Mao 2:4; Ay 16:12; Za 38:2; 34:2Amevuta upinde wake

na kunifanya mimi niwe lengo

kwa ajili ya mishale yake.

13Alinichoma moyo wangu kwa mishale

iliyotoka kwenye podo lake.

143:14 Mwa 38:23; Za 22:6-7; Ay 30:9; Neh 4:2-4; Mt 27:29-31; Yer 20:7Nimekuwa kichekesho kwa watu wangu wote,

wananidhihaki kwa wimbo mchana kutwa.

153:15 Yer 9:15Amenijaza kwa majani machungu

na kunishibisha kwa nyongo.

163:16 Mit 20:17Amevunja meno yangu kwa changarawe,

amenikanyagia mavumbini.

17Amani yangu imeondolewa,

nimesahau kufanikiwa ni nini.

183:18 Ay 17:15; Za 31:22Kwa hiyo nasema, “Fahari yangu imeondoka

na yale yote niliyokuwa nimetarajia kutoka kwa Bwana.”

19Nayakumbuka mateso yangu na kutangatanga kwangu,

uchungu na nyongo.

203:20 Za 42:5; 43:5Ninayakumbuka vyema,

nayo nafsi yangu imezimia ndani yangu.

21Hata hivyo najikumbusha neno hili

na kwa hiyo ninalo tumaini.

223:22 Za 130:7; Mt 3:6; Neh 9:31; Ay 34:15; Za 130:1; Hos 11:9; Za 78:38; 57:10; Mal 3:6Kwa sababu ya upendo mkuu wa Bwana, hatuangamii,

kwa kuwa huruma zake hazikomi kamwe.

233:23 Kut 34:6; Isa 33:2; Ebr 10:23Ni mpya kila asubuhi,

uaminifu wako ni mkuu.

243:24 Za 16:5Nimeiambia nafsi yangu, “Bwana ni fungu langu,

kwa hiyo nitamngojea.”

253:25 Za 33:18; Isa 25:9; 30:18; Za 130:6Bwana ni mwema kwa wale ambao tumaini lao ni kwake,

kwa yule ambaye humtafuta;

263:26 Za 37:7ni vyema kungojea kwa utulivu

kwa ajili ya wokovu wa Bwana.

273:27 Za 90:12Ni vyema mtu kuchukua nira

bado angali kijana.

283:28 Yer 15:17Na akae peke yake awe kimya,

kwa maana Bwana ameiweka juu yake.

293:29 Yer 31:17; Ay 2:8; 42:6Na azike uso wake mavumbini

bado panawezekana kuwa na matumaini.

303:30 Ay 16:10; Isa 50:6; Mik 5:1; Mt 5:39Na atoe shavu lake kwa yule ampigaye,

na ajazwe na aibu.

313:31 Za 94:14; Isa 54:7Kwa kuwa watu hawakatiliwi mbali

na Bwana milele.

323:32 Za 106:43-45; Nah 1:12; Hos 11:8Ingawa huleta huzuni, ataonyesha huruma,

kwa kuwa upendo wake usiokoma ni mkuu.

333:33 Ay 37:23; Ebr 12:10; Yer 31:20; Eze 18:23Kwa maana hapendi kuwaletea mateso

au huzuni watoto wa wanadamu.

34Kuwaponda chini ya nyayo

wafungwa wote katika nchi,

353:35 Mwa 14:18-22Kumnyima mtu haki zake

mbele za Aliye Juu Sana,

363:36 Za 140:12; Mit 17:15; Hab 1:13; Yer 22:3kumnyima mtu haki:

Je, Bwana asione mambo kama haya?

373:37 Mit 19:21; Za 33:9-11; Mit 21:30Nani awezaye kusema nalo likatendeka

kama Bwana hajaamuru?

383:38 Ay 2:10; Isa 45:7; Yer 32:42Je, si ni kwenye kinywa cha Aliye Juu Sana

ndiko yatokako maafa na mambo mema?

393:39 Yer 30:15; Mik 7:9Mwanadamu yeyote aliye hai aweza kulalamika

wakati anapoadhibiwa kwa ajili ya dhambi zake?

403:40 2Kor 13:5; Za 119:59; 139:23-24Tuzichunguze njia zetu na kuzijaribu,

na tumrudie Bwana Mungu.

413:41 Dan 9:5; Yer 14:20; 2Fal 24:4; Yer 5:7-9; Za 86:4Tuinue mioyo yetu pamoja na mikono yetu

kwa Mungu mbinguni, na tuseme:

423:42 Dan 9:5“Tumetenda dhambi na kuasi

nawe hujasamehe.

433:43 Mao 2:2, 17, 21; Za 35:6“Umejifunika mwenyewe kwa hasira na kutufuatilia;

umetuchinja bila huruma.

443:44 Mao 2:1; Zek 7:13; Za 97:2; Isa 58:4Unajifunika mwenyewe kwa wingu,

ili pasiwe na ombi

litakaloweza kupenya.

453:45 1Kor 4:13Umetufanya takataka na uchafu

miongoni mwa mataifa.

463:46 Za 22:13; Mao 2:16“Adui zetu wote wamefumbua vinywa vyao

wazi dhidi yetu.

473:47 Yer 48:43; Isa 24:17-18; 51:19Tumeteseka kwa hofu kuu na shida ya ghafula,

uharibifu na maangamizi.”

483:48 Yer 9:1; Mao 2:18Vijito vya machozi vinatiririka kutoka machoni mwangu,

kwa sababu watu wangu wameangamizwa.

49Macho yangu yatatiririka machozi bila kukoma,

bila kupata nafuu,

503:50 Za 14:2; 80:14; Isa 63:15hadi Bwana atazame chini

kutoka mbinguni na kuona.

51Lile ninaloliona huniletea huzuni nafsini

kwa sababu ya wanawake wote wa mji wangu.

523:52 Za 35:7; 69:4Wale waliokuwa adui zangu bila sababu

wameniwinda kama ndege.

533:53 Yer 38:6; 37:16; Dan 6:17Walijaribu kukomesha maisha yangu ndani ya shimo

na kunitupia mawe;

543:54 Za 69:2; Yon 2:3-5; Eze 37:11; Za 88:5maji yalifunika juu ya kichwa changu,

nami nikafikiri nilikuwa karibu

kukatiliwa mbali.

553:55 Za 130:1; 2Nya 33:12; Yon 2:2; Za 18:5, 6Nililiitia jina lako, Ee Bwana,

kutoka vina vya shimo.

563:56 Rum 8:26; Za 116:1-2; 6:8Ulisikia ombi langu: “Usikizibie masikio yako

kilio changu nikuombapo msaada.”

573:57 Isa 41:10; Yak 4:8; Za 46:1; 69:18; Isa 58:9Ulikuja karibu nilipokuita,

nawe ukasema, “Usiogope.”

583:58 Yer 51:36; Za 34:22; Yer 50:34; 1Sam 25:39Ee Bwana, ulichukua shauri langu,

ukaukomboa uhai wangu.

593:59 Yer 18:19; Za 35:23Umeona, Ee Bwana, ubaya niliotendewa.

Tetea shauri langu!

603:60 Yer 11:20; 18:18Umeona kina cha kisasi chao,

mashauri yao yote mabaya dhidi yangu.

61Ee Bwana, umesikia matukano yao,

mashauri yao yote mabaya dhidi yangu:

623:62 Eze 36:3kile adui zangu wanachonongʼona na kunungʼunikia

dhidi yangu mchana kutwa.

633:63 Ay 30:9; Za 139:2Watazame! Wakiwa wameketi au wamesimama,

wananidhihaki katika nyimbo zao.

643:64 Za 28:4; Yer 51:6; 2Tim 4:14; Yer 11:20; Ufu 6:10Uwalipe kile wanachostahili, Ee Bwana,

kwa yale ambayo mikono yao imetenda.

653:65 Kut 14:8; Kum 2:30; Isa 6:10; Za 8:3Weka pazia juu ya mioyo yao,

laana yako na iwe juu yao!

66Wafuatilie katika hasira na uwaangamize

kutoka chini ya mbingu za Bwana.

New Arabic Version

مراثي إرميا 3:1-66

1أَنَا هُوَ الرَّجُلُ الَّذِي شَهِدَ الْبَلِيَّةَ الَّتِي أَنْزَلَهَا قَضِيبُ سُخْطِهِ. 2قَادَنِي وَسَيَّرَنِي فِي الظُّلْمَةِ مِنْ غَيْرِ نُورٍ. 3حَقّاً إِنَّهُ يَمُدُّ يَدَهُ عَلَيَّ مَرَّةً تِلْوَ الْمَرَّةِ طُولَ النَّهَارِ. 4أَبْلَى لَحْمِي وَجِلْدِي. هَشَّمَ عِظَامِي. 5حَاصَرَنِي وَأَحَاطَنِي بِالْعَلْقَمِ وَالْمَشَقَّةِ. 6أَسْكَنَنِي فِي الظُّلْمَةِ كَمَوْتَى الْحِقَبِ الْغَابِرَةِ. 7سَيَّجَ حَوْلِي حَتَّى لَا أُفْلِتَ. أَثْقَلَ عَلَيَّ قُيُودِي. 8حَتَّى حِينَ أَصْرُخُ وَأَسْتَغِيثُ يَصُدُّ صَلاتِي. 9قَدْ أَغْلَقَ عَلَيَّ طُرُقِي بِحِجَارَةٍ مَنْحُوتَةٍ، وَجَعَلَ مَسَالِكِي مُلْتَوِيَةً. 10هُوَ لِي كَدُبٍّ مُتَرَبِّصٍ، وَكَأَسَدٍ مُتَرَصِّدٍ فِي مَكْمَنِهِ. 11أَضَلَّ طُرُقِي وَمَزَّقَنِي إِرْباً. دَمَّرَنِي. 12وَتَّرَ قَوْسَهُ وَنَصَبَنِي هَدَفاً لِسَهْمِهِ. 13اخْتَرَقَ كُلْيَتَيَّ بِنِبَالِ جُعْبَتِهِ. 14صِرْتُ مَثَارَ هُزْءٍ لِشَعْبِي وَأُهْجِيَةً لَهُمُ الْيَوْمَ كُلَّهُ. 15أَشْبَعَنِي مَرَارَةً، وَأَرْوَانِي أَفْسَنْتِيناً. 16هَشَّمَ أَسْنَانِي بِالْحَصَى، وَطَمَرَنِي بِالرَّمَادِ. 17فَتَنَاءَتْ نَفْسِي عَنِ السَّلامِ، وَنَسِيتُ طَعْمَ الْخَيْرَاتِ. 18فَقُلْتُ: «تَلاشَتْ قُوَّتِي، وَكُلُّ مَا كُنْتُ أَرْجُوهُ مِنَ الرَّبِّ».

19اُذْكُرْ بَلِيَّتِي وَتَيَهَانِي وَالأَفْسَنْتِينَ وَالْمَرَارَةَ. 20مَا بَرِحَتْ نَفْسِي تَذْكُرُهَا وَهِيَ مُنْحَنِيَةٌ فِي دَاخِلِي.

21وَلَكِنْ هَذَا مَا أُنَاجِي بِهِ نَفْسِي، لِذَلِكَ يَغْمُرُنِي الرَّجَاءُ: 22مِنْ إِحْسَانَاتِ الرَّبِّ أَنَّنَا لَمْ نَفْنَ، لأَنَّ مَرَاحِمَهُ لَا تَزُولُ. 23تَتَجَدَّدُ فِي كُلِّ صَبَاحٍ. فَائِقَةٌ أَمَانَتُكَ. 24تَقُولُ نَفْسِي: «الرَّبُّ هُوَ نَصِيبِي فَلِذَلِكَ أَرْجُوهُ». 25الرَّبُّ صَالِحٌ لِمَنْ يَرْجُونَهُ وَلِلنَّفْسِ الَّتِي تَلْتَمِسُهُ. 26خَيْرٌ لِلْمَرْءِ أَنْ يَنْتَظِرَ بِصَمْتٍ خَلاصَ الرَّبِّ. 27خَيْرٌ لِلْمَرْءِ أَنْ يَحْمِلَ النِّيرَ فِي حَدَاثَتِهِ. 28لِيَعْتَكِفْ وَحِيداً فِي صَمْتٍ لأَنَّ الرَّبَّ قَدْ وَضَعَ النِّيرَ عَلَيْهِ. 29لِيُوَارِ وَجْهَهُ فِي التُّرَابِ تَذَلُّلاً، عَسَى أَنْ يَكُونَ هُنَاكَ رَجَاءٌ. 30لِيَبْذُلْ خَدَّهُ لِلاطِمِ، وَيَشْبَعْ تَعْيِيراً. 31لأَنَّ الرَّبَّ لَا يَنْبِذُ إِلَى الأَبَدِ. 32فَإِنَّهُ وَلَوْ أَحْزَنَ يَرْأَفُ بِمُقْتَضَى رَحْمَتِهِ الْفَائِقَةِ. 33لأَنَّهُ لَا يَتَعَمَّدُ أَنْ يَبْتَلِيَ أَبْنَاءَ الْبَشَرِ بِالْبُؤْسِ وَالأَسَى، 34وَلا أَنْ يَسْحَقَ أَسْرَى الأَرْضِ تَحْتَ الأَقْدَامِ، 35وَلا أَنْ يَجُورَ أَحَدٌ عَلَى حُقُوقِ الإِنْسَانِ، أَمَامَ عَيْنَيِ الرَّبِّ الْعَلِيِّ 36أَوْ أَنْ لَا يُنْصَفَ الإِنْسَانُ فِي دَعْوَاهُ. أَلا يَرَى الرَّبُّ هَذِهِ الأُمُورَ؟ 37مَنْ ذَا الَّذِي يَقْضِي بِأَمْرٍ فَيَتَحَقَّقَ إِنْ لَمْ يَكُنِ الرَّبُّ قَدْ أَمَرَ بِهِ؟ 38أَلَيْسَ مِنْ فَمِ الْعَلِيِّ يَصْدُرُ الضُّرُّ وَالْخَيْرُ؟

39فَلِمَاذَا يَشْتَكِي الإِنْسَانُ الْحَيُّ حِينَ يُعَاقَبُ عَلَى خَطَايَاهُ؟

40لِنَفْحَصْ طُرُقَنَا وَنَخْتَبِرْهَا وَنَرْجِعْ إِلَى الرَّبِّ. 41لِنَرْفَعْ قُلُوبَنَا وَأَيْدِيَنَا إِلَى اللهِ فِي السَّمَاوَاتِ. 42قَدْ تَعَدَّيْنَا وَتَمَرَّدْنَا، وَأَنْتَ لَمْ تَغْفِرْ. 43لَفَّعْتَ نَفْسَكَ بِالْغَضَبِ وَتَعَقَّبْتَنَا. قَتَلْتَ مِنْ غَيْرِ رَحْمَةٍ. 44تَلَفَّعْتَ بِالسَّحَابِ حَتَّى لَا تَبْلُغَ إِلَيْكَ صَلاةٌ. 45قَدْ جَعَلْتَنَا أَوْسَاخاً وَأَقْذَاراً بَيْنَ الشُّعُوبِ. 46فَتَحَ عَلَيْنَا جَمِيعُ أَعْدَائِنَا أفْوَاهَهُمْ، 47وَحَلَّ بِنَا الرُّعْبُ وَالْهَلاكُ وَالدَّمَارُ وَالسَّحْقُ. 48تَفِيضُ عَيْنَايَ بِأَنْهَارِ مِيَاهٍ عَلَى دَمَارِ ابْنَةِ شَعْبِي. 49لَنْ تَكُفَّ عَيْنَايَ عَنِ الْبُكَاءِ أَبداً، 50حَتَّى يُشْرِفَ الرَّبُّ مِنَ السَّمَاءِ وَيُبْصِرَ. 51تَتْلَفُ عَيْنَايَ عَلَى مَصِيرِ كُلِّ بَنَاتِ مَدِينَتِي. 52قَدِ اصْطَادَنِي، كَعُصْفُورٍ، أَعْدَائِي الَّذِينَ لَمْ أُسِئْ إِلَيْهِمْ، 53طَرَحُونِي حَيًّا فِي الْجُبِّ وَرَجَمُونِي بِالْحِجَارَةِ. 54طَغَتِ الْمِيَاهُ فَوْقَ رَأْسِي، فَقُلْتُ: «قَدْ هَلَكْتُ».

55اسْتَغَثْتُ بِاسْمِكَ يَا رَبُّ مِنْ أَعْمَاقِ الْجُبِّ، 56فَسَمِعْتَ صَوْتِي. لَا تَصُمَّ أُذُنَيْكَ عَنْ صُرَاخِ اسْتِغَاثَتِي. 57اقْتَرَبْتَ حِينَ دَعَوْتُكَ إِذْ قُلْتَ: «لا تَخَفْ». 58قَدْ دَافَعْتَ عَنْ دَعْوَايَ يَا رَبُّ، وَافْتَدَيْتَ حَيَاتِي. 59أَنْتَ شَهِدْتَ مَا أَسَاءُوا بِهِ إِلَيَّ يَا رَبُّ، فَاقْضِ فِي دَعْوَايَ. 60قَدْ رَأَيْتَ انْتِقَامَهُمْ كُلَّهُ وَسَائِرَ مُؤَامَرَاتِهِمْ عَلَيَّ. 61سَمِعْتَ تَعْيِيرَهُمْ يَا رَبُّ، وَجَمِيعَ مُؤَامَرَاتِهِمْ عَلَيَّ. 62وَسَمِعْتَ كَلامَ أَعْدَائِي وَتَدْبِيرَاتِهِمْ ضِدِّي الْيَوْمَ كُلَّهُ. 63رَاقِبْ جُلُوسَهُمْ وَقِيَامَهُمْ، فَقَدْ أَصْبَحْتُ أُهْجِيَةً لَهُمْ.

64جَازِهِمْ يَا رَبُّ بِمُقْتَضَى مَا جَنَتْهُ أَيْدِيهِمْ. 65اجْعَلْ عَلَى قُلُوبِهِمْ غَشَاوَةً، وَلْتَكُنْ لَعْنَتُكَ عَلَيْهِمْ. 66تَعَقَّبْهُمْ بِسُخْطٍ وَأَهْلِكْهُمْ مِنْ تَحْتِ سَمَاوَاتِكَ يَا رَبُّ.