Maombolezo 1 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Maombolezo 1:1-22

1 Sura hii imetungwa kila beti likianzia, na pia kila mstari katika lile beti, na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22. 11:1 Isa 47:7-8; Ezr 4:20; Eze 5:5; Isa 3:26; Yer 42:2; Law 26:43; Mao 1:9Tazama jinsi mji ulivyoachwa ukiwa,

mji ambao zamani ulikuwa umejaa watu!

Jinsi ambavyo umekuwa kama mama mjane,

ambaye wakati fulani alikuwa maarufu miongoni mwa mataifa!

Yule ambaye alikuwa malkia miongoni mwa majimbo

sasa amekuwa mtumwa.

21:2 Za 6:6; Yer 4:30; Mik 7:5; Yer 30:14; 13:17; Mao 1:16; Ay 7:3Kwa uchungu, hulia sana usiku,

machozi yapo kwenye mashavu yake.

Miongoni mwa wapenzi wake wote

hakuna yeyote wa kumfariji.

Rafiki zake wote wamemsaliti,

wamekuwa adui zake.

31:3 Yer 13:19; Kum 28:64-65; Kut 15:9; Law 26:14, 32, 33Baada ya mateso na kufanyishwa kazi kikatili,

Yuda amekwenda uhamishoni.

Anakaa miongoni mwa mataifa,

hapati mahali pa kupumzika.

Wote ambao wanamsaka wamemkamata

katikati ya dhiki yake.

41:4 Isa 27:10; Yer 9:11; Yoe 1:8-13Barabara zielekeazo Sayuni zaomboleza,

kwa kuwa hakuna yeyote anayekuja

kwenye sikukuu zake zilizoamriwa.

Malango yake yote yamekuwa ukiwa,

makuhani wake wanalia kwa uchungu,

wanawali wake wanahuzunika,

naye yuko katika uchungu wa maumivu makuu.

51:5 Isa 22:5; Yer 10:20; 39:9; 30:14; Mao 3:39; Yer 30:15; 52:28-30; Za 5:10; Mao 2:17Adui zake wamekuwa mabwana zake,

watesi wake wana raha.

Bwana amemletea huzuni

kwa sababu ya dhambi zake nyingi.

Watoto wake wamekwenda uhamishoni,

mateka mbele ya adui.

61:6 Yer 13:18; Za 9:14; Law 26:36Fahari yote imeondoka

kutoka kwa Binti Sayuni.

Wakuu wake wako kama ayala

ambaye hapati malisho,

katika udhaifu wamekimbia

mbele ya anayewasaka.

71:7 2Fal 14:26; Yer 37:7; Mik 4:11; Mao 4:17; Yer 2:26Katika siku za mateso yake na kutangatanga,

Yerusalemu hukumbuka hazina zote

ambazo zilikuwa zake siku za kale.

Wakati watu wake walipoanguka katika mikono ya adui,

hapakuwepo na yeyote wa kumsaidia.

Watesi wake walimtazama

na kumcheka katika maangamizi yake.

81:8 Isa 59:2-13; Za 38:8; Yer 13:22-26; 2:22Yerusalemu ametenda dhambi sana

kwa hiyo amekuwa najisi.

Wote waliomheshimu wanamdharau,

kwa maana wameuona uchi wake.

Yeye mwenyewe anapiga kite

na kugeukia mbali.

91:9 Isa 47:7; Eze 24:13; Yer 13:18; Mhu 4:1; Yer 16:7; Za 25:18; Kum 32:29Uchafu wake umegandamana na nguo zake;

hakuwaza juu ya maisha yake ya baadaye.

Anguko lake lilikuwa la kushangaza,

hapakuwepo na yeyote wa kumfariji.

“Tazama, Ee Bwana, teso langu,

kwa maana adui ameshinda.”

101:10 Neh 13:1; Kum 23:3; Yer 51:51; Isa 64:11; Za 74:7-8Adui ametia mikono

juu ya hazina zake zote,

aliona mataifa ya kipagani

wakiingia mahali patakatifu pake,

wale uliowakataza kuingia

kwenye kusanyiko lako.

111:11 Za 38:8; Yer 38:9; 37:21; 52:6Watu wake wote wanalia kwa uchungu

watafutapo chakula;

wanabadilisha hazina zao kwa chakula

ili waweze kuendelea kuishi.

“Tazama, Ee Bwana, ufikiri,

kwa maana nimedharauliwa.”

121:12 Yer 18:16; Isa 10:4; Yer 30:24; Dan 9:12; Isa 13:13; Mit 24:21; Lk 21:22“Je, si kitu kwenu, ninyi nyote mpitao kando?

Angalieni kote mwone.

Je, kuna maumivu kama maumivu yangu

yale yaliyotiwa juu yangu,

yale Bwana aliyoyaleta juu yangu

katika siku ya hasira yake kali?

131:13 Ay 30:30; Za 102:3; Hab 3:16; Yer 44:6; Eze 12:13; Ay 18:8; Za 66:11; Hos 7:12“Kutoka juu alipeleka moto,

akaushusha katika mifupa yangu.

Aliitandia wavu miguu yangu

na akanirudisha nyuma.

Akanifanya mkiwa,

na mdhaifu mchana kutwa.

141:14 Isa 47:6; Yer 15:12; 32:5“Dhambi zangu zimefungwa kwenye nira,

kwa mikono yake zilifumwa pamoja.

Zimefika shingoni mwangu

na Bwana ameziondoa nguvu zangu.

Amenitia mikononi mwa wale

ambao siwezi kushindana nao.

151:15 Yer 37:10; Isa 41:2; 28:1; Yer 18:21; Ufu 14:19; Yer 14:17; Amu 6:11; Isa 63:3“Bwana amewakataa wapiganaji wa vita

wote walio kati yangu,

ameagiza jeshi dhidi yangu

kuwaponda vijana wangu wa kiume.

Katika shinikizo lake la divai Bwana amemkanyaga

Bikira Binti Yuda.

161:16 Za 119:136; Ay 7:3; Yer 16:7; 13:17; 14:17; Isa 22:4; Mao 3:48-49“Hii ndiyo sababu ninalia

na macho yangu yanafurika machozi.

Hakuna yeyote aliye karibu kunifariji,

hakuna yeyote wa kuhuisha roho yangu.

Watoto wangu ni wakiwa

kwa sababu adui ameshinda.”

171:17 Yer 4:31; Kut 23:21; Law 18:25-28Sayuni ananyoosha mikono yake,

lakini hakuna yeyote wa kumfariji.

Bwana ametoa amri kwa ajili ya Yakobo

kwamba majirani zake wawe adui zake;

Yerusalemu umekuwa

kitu najisi miongoni mwao.

181:18 1Sam 12:14; Kum 28:32; Neh 9:33; Ezr 9:15; Kut 9:27; Dan 9:7Bwana ni mwenye haki,

hata hivyo niliasi dhidi ya amri yake.

Sikilizeni, enyi mataifa yote,

tazameni maumivu yangu.

Wavulana wangu na wasichana wangu

wamekwenda uhamishoni.

191:19 Mao 2:20; Yer 14:15; 22:20“Niliita washirika wangu

lakini walinisaliti.

Makuhani wangu na wazee wangu

waliangamia mjini

walipokuwa wakitafuta chakula

ili waweze kuishi.

201:20 Yer 4:19; Kum 32:25; Eze 7:15; Ay 20:2; Mao 2:11; Isa 16:11; Hos 11:8“Angalia, Ee Bwana, jinsi nilivyo katika dhiki!

Nina maumivu makali ndani yangu,

nami ninahangaika moyoni mwangu,

kwa kuwa nimekuwa mwasi sana.

Huko nje, upanga unaua watu,

ndani, kipo kifo tu.

211:21 Za 38:8; Mao 2:15; Yer 30:16; Isa 47:11; Za 6:6“Watu wamesikia ninavyolia kwa uchungu,

lakini hakuna yeyote wa kunifariji.

Adui zangu wote wamesikia juu ya dhiki yangu,

wanafurahia lile ulilolitenda.

Naomba uilete siku uliyoitangaza

ili wawe kama mimi.

221:22 Neh 4:5; Za 6:6“Uovu wao wote na uje mbele zako;

uwashughulikie wao

kama vile ulivyonishughulikia mimi

kwa sababu ya dhambi zangu zote.

Kulia kwangu kwa uchungu ni kwingi

na moyo wangu umedhoofika.”

Japanese Contemporary Bible

哀歌 1:1-22

1

エルサレムの荒廃と悲しみ

1かつて人々でにぎわっていたエルサレムの通りが、

今はひっそり静まり返っています。

諸国の女王だった町は今では奴隷のようで、

悲しみに沈む未亡人のように座り込んで嘆いています。

2夜通し泣いて、涙が彼女の頬を伝います。

恋人たち(エジプトや他の同盟国)は、

誰ひとり声をかけてもくれません。

今ではみな、敵となっているからです。

3ユダは労役で苦しんだ果てに、

捕囚となって遠い国へ引いて行かれたのです。

今は征服者の手に落ち、

外国で不安な毎日を過ごしています。

4シオン(エルサレム)への道は、

神殿で例祭を祝うにぎやかな参拝客の列も途絶え、

すっかりさびれて、憂いに沈んでいます。

都の城門はさびつき、祭司たちはうめき、

おとめたちは悲しみに打ちひしがれています。

シオンは泣き伏しています。

5敵がわがもの顔に振る舞っています。

エルサレムの多くの罪のために、

主が罰を加えたからです。

幼い子どもたちは捕らえられ、

奴隷として遠くへ連れ去られました。

6シオンの美しさも威厳も、すっかりなくなりました。

指導者たちは、

あてもなく牧草地をさまよう飢えた鹿のようで、

敵に出会っても逃げる力さえありません。

7エルサレムは悲しみのどん底で、

過ぎ去った楽しい日々を思い浮かべます。

今はもう、

援助の手を伸ばしてくれる者もなく、

屈した敵の前で、あざけりの的となっています。

8エルサレムは罪に罪を重ねたので、

汚いぼろきれのように捨てられました。

丸裸にされ、人前にさらされ、

かつては尊敬の眼で見た人たちも、

今では軽蔑のまなざしを向けるだけです。

彼女はあまりの恥ずかしさにうめき、顔を隠します。

9この都は不品行の罪にうつつを抜かし、

確実に罰が下るという事実に

顔を背けていました。

落ちぶれてしまった今、

だれも助けてくれないので、彼女は叫びます。

「ああ主よ、私の不幸に目を留めてください。

敵はあんなに勝ち誇っています。」

10敵は貴重品をすべて取り上げ、

彼女を無一物にしました。

そればかりか、神聖な神殿を荒らし回りました。

そこに入ることさえ神が禁じた外国人によって。

11民はうめき、必死にパンを探し求めます。

持ち物を全部売り払い、少しでも体力を回復しようと、

食べ物をあさります。

「主よ、ごらんください。

私がどんなにさげすまれているかを

知ってください」とエルサレムは祈ります。

12道行く人よ、何とも思わないのですか。

主が燃える怒りの日に、

こんなにも私を悩ませたのです。

これ以上の悲しみを見たことがあるでしょうか。

13主が天から送った火は、

私の骨の中で燃え続けています。

主は行く道に落とし穴を置き、私を追い返しました。

私を病気にしたまま置き去りにし、

つらい思いをさせました。

14主は私の罪を編んで綱とし、

それで私を引いて、奴隷のくびきに結びつけました。

私を骨抜きにして、敵の手に渡しました。

私は敵のなすがままになっています。

15主は味方の勇士をみな踏みつけました。

主の命令によって強力な軍隊が押し寄せて来て、

すぐれた若者たちを倒しました。

主は愛する都を、

酒ぶねのぶどうのように踏みつぶしました。

16このことで、私は泣いています。

私を助けられるのは主だけだというのに、

主は私を慰めもせず、遠く離れて立っています。

子どもたちに未来はありません。

私たちは征服された民です。

17エルサレムは助けを求めて哀願しますが、

だれも慰めてくれません。

主がこう語ったからです。

「隣人が敵となれ。

この都は悪臭を放つぼろきれのように、

投げ捨てられてしまうがいい。」

18主がこう言うのも、もっともなことです。

私たちは神に反逆したからです。

しかし、すべての国々の民よ、

私の苦悩と絶望に目を留めてください。

息子も、娘も、

奴隷として遠い国へ引いて行かれました。

19私は同盟国の助けを求めましたが、

彼らは少しも役に立たず、がっかりするばかりでした。

祭司も、長老も、同じことでした。

彼らは、残飯をあさってうろつきながら、

道ばたで飢え死にしたのです。

20主よ、私の苦しみに目を留めてください。

私の心は傷つき、たましいは絶望にあえいでいます。

私がひどく背いたからです。

外に出ると、剣が待ち伏せし、

家にいても、病気と死が私を捕らえて放しません。

21私のうめきを聞いてください。

助けてくれる者はどこにもいません。

敵は私が苦しんでいるのを聞きました。

彼らは、主が私に罰を加えたと知って、

喜んでいます。

しかし主よ。お約束どおり、

彼らも私と同じ目に会う時が来るはずです。

22主よ、彼らの罪にも目を留め、

あなたが私に下したのと同じ罰を

彼らにも下してください。

私はため息をくり返し、

私の心はしおれきっているのです。