Luka 3 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version

Luka 3:1-38

Yohana Mbatizaji Aanza Kuhubiri

(Mathayo 3:1-12; Marko 1:1-8; Yohana 1:19-28)

13:1 Mt 27:2Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato akiwa mtawala wa Uyahudi, Herode akiwa mfalme wa Galilaya, Filipo ndugu yake akiwa mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania akiwa mfalme wa Abilene, 23:2 Yn 18:13; Mdo 4:6; Mt 3:1nao Anasi na Kayafa wakiwa makuhani wakuu, neno la Mungu likamjia Yohana, mwana wa Zekaria huko jangwani. 33:3 Mk 3:16; Mal 1:4Akaenda katika nchi yote kandokando ya Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi. 43:4 Isa 40:3-5; Mt 3:3; Mk 1:3; Yn 1:23Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya:

“Sauti ya mtu aliaye nyikani,

‘Itengenezeni njia ya Bwana,

yanyoosheni mapito yake.

5Kila bonde litajazwa,

kila mlima na kilima vitashushwa.

Njia zilizopinda zitanyooshwa,

na zilizoparuza zitasawazishwa.

63:6 Za 98:2; Lk 2:30Nao watu wote watauona

wokovu wa Mungu.’ ”

73:7 Mt 12:34; 23:33; Rum 1:18Yohana akauambia ule umati wa watu uliokuwa unakuja ili kubatizwa naye, “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja? 83:8 Isa 51:7; Gal 3:7Basi zaeni matunda yastahiliyo toba. Wala msianze kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Kwa maana nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka mawe haya. 93:9 Mt 3:10Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti. Basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.”

103:10 Mdo 2:37; 16:30Ule umati wa watu ukamuuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?”

113:11 Isa 58:7; Eze 18:7Yohana akawaambia, “Aliye na kanzu mbili amgawie asiye nayo, naye aliye na chakula na afanye vivyo hivyo.”

123:12 Lk 7:29Watoza ushuru nao wakaja ili wabatizwe, wakamuuliza, “Bwana na sisi inatupasa tufanyeje?”

133:13 Lk 19:8Akawaambia, “Msichukue zaidi ya kiwango mlichopangiwa.”

143:14 Law 19:11Askari nao wakamuuliza, “Je, nasi inatupasa tufanye nini?”

Akawaambia, “Msimdhulumu mtu wala msimshtaki mtu kwa uongo, bali mridhike na mishahara yenu.”

153:15 Mt 3:1; Yn 1:19-20; Mdo 13:25Watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wanajiuliza mioyoni mwao iwapo Yohana angeweza kuwa ndiye Kristo.3:15 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. 163:16 Mk 1:4; Yn 1:26, 33; Mdo 11:16Yohana akawajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji.3:16 Tafsiri nyingine zinasema ndani ya maji. Lakini atakuja aliye na nguvu kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto. 173:17 Isa 30:24; Mt 13:30; 25:41Pepeto lake liko mkononi, tayari kusafisha sakafu yake ya kupuria na kuikusanya ngano ghalani, lakini makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.” 18Basi, kwa maonyo mengine mengi Yohana aliwasihi na kuwahubiria watu Habari Njema.

193:19 Mt 14:1Lakini Yohana alipomkemea Mfalme Herode kuhusu uhusiano wake na Herodia, mke wa ndugu yake, na maovu mengine aliyokuwa amefanya, 203:20 Mt 14:3-4Herode aliongezea jambo hili kwa hayo mengine yote: alimfunga Yohana gerezani.

Kubatizwa Kwa Bwana Yesu

(Mathayo 3:13-17; Marko 1:9-11)

213:21 Mt 14:23; Mk 1:35Baada ya watu wote kubatizwa, Yesu naye akabatizwa. Naye alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka. 223:22 Isa 42:1; Yn 1:32-33; Mt 3:17Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa umbo kama la hua, nayo sauti kutoka mbinguni ikasema: “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”

Ukoo Wa Bwana Yesu

(Mathayo 1:1-17)

233:23 Mt 4:17; Lk 1:27Yesu alikuwa na umri wa miaka thelathini alipoanza huduma yake. Alikuwa akidhaniwa kuwa mwana wa Yosefu,

Yosefu alikuwa mwana wa Eli,

24Eli alikuwa mwana wa Mathati,

Mathati alikuwa mwana wa Lawi,

Lawi alikuwa mwana wa Melki,

Melki alikuwa mwana wa Yanai,

Yanai alikuwa mwana wa Yosefu,

25Yosefu alikuwa mwana wa Matathia,

Matathia alikuwa mwana wa Amosi,

Amosi alikuwa mwana wa Nahumu,

Nahumu alikuwa mwana wa Esli,

Esli alikuwa mwana wa Nagai,

26Nagai alikuwa mwana wa Maathi,

Maathi alikuwa mwana wa Matathia,

Matathia alikuwa mwana wa Semeini,

Semeini alikuwa mwana wa Yoseki,

Yoseki alikuwa mwana wa Yoda,

273:27 Mt 1:12; 1Nya 3:17Yoda alikuwa mwana wa Yoanani,

Yoanani alikuwa mwana wa Resa,

Resa alikuwa mwana wa Zerubabeli,

Zerubabeli alikuwa mwana wa Shealtieli,

Shealtieli alikuwa mwana wa Neri,

28Neri alikuwa mwana wa Melki,

Melki alikuwa mwana wa Adi,

Adi alikuwa mwana wa Kosamu,

Kosamu alikuwa mwana wa Elmadamu,

Elmadamu alikuwa mwana wa Eri,

29Eri alikuwa mwana wa Yoshua,

Yoshua alikuwa mwana wa Eliezeri,

Eliezeri alikuwa mwana wa Yorimu,

Yorimu alikuwa mwana wa Mathati,

Mathati alikuwa mwana wa Lawi,

30Lawi alikuwa mwana wa Simeoni,

Simeoni alikuwa mwana wa Yuda,

Yuda alikuwa mwana wa Yosefu,

Yosefu alikuwa mwana wa Yonamu,

Yonamu alikuwa mwana wa Eliakimu,

Eliakimu alikuwa mwana wa Melea,

313:31 2Sam 5:14; 1Nya 3:5Melea alikuwa mwana wa Mena,

Mena alikuwa mwana wa Matatha,

Matatha alikuwa mwana wa Nathani,

Nathani alikuwa mwana wa Daudi,

323:32 Rut 4:22; 1Nya 2:10Daudi alikuwa mwana wa Yese,

Yese alikuwa mwana wa Obedi,

Obedi alikuwa mwana wa Boazi,

Boazi alikuwa mwana wa Salmoni,

Salmoni alikuwa mwana wa Nashoni,

333:33 Rut 4:18-22; 1Nya 2:10Nashoni alikuwa mwana wa Aminadabu,

Aminadabu alikuwa mwana wa Aramu,

Aramu alikuwa mwana wa Hesroni,

Hesroni alikuwa mwana wa Peresi,

Peresi alikuwa mwana wa Yuda,

343:34 Mwa 11:24-26Yuda alikuwa mwana wa Yakobo,

Yakobo alikuwa mwana wa Isaki,

Isaki alikuwa mwana wa Abrahamu,

Abrahamu alikuwa mwana wa Tera,

Tera alikuwa mwana wa Nahori,

35Nahori alikuwa mwana wa Serugi,

Serugi alikuwa mwana wa Reu,

Reu alikuwa mwana wa Pelegi,

Pelegi alikuwa mwana wa Eberi,

Eberi alikuwa mwana wa Sala,

363:36 Mwa 5:28-32; 11:12Sala alikuwa mwana wa Kenani,

Kenani alikuwa mwana wa Arfaksadi,

Arfaksadi alikuwa mwana wa Shemu,

Shemu alikuwa mwana wa Noa,

Noa alikuwa mwana wa Lameki,

373:37 Mwa 5:12-25Lameki alikuwa mwana wa Methusela,

Methusela alikuwa mwana wa Enoki,

Enoki alikuwa mwana wa Yaredi,

Yaredi alikuwa mwana wa Mahalaleli,

Mahalaleli alikuwa mwana wa Kenani,

383:38 Mwa 5:19Kenani alikuwa mwana wa Enoshi,

Enoshi alikuwa mwana wa Sethi,

Sethi alikuwa mwana wa Adamu,

Adamu alikuwa mwana wa Mungu.

New Russian Translation

От Луки 3:1-38

Иоанн Креститель готовит путь для Иисуса

(Мат. 3:1–12; Мк. 1:2–8; Ин. 1:19–28)

1В пятнадцатый год правления кесаря Тиберия, когда Иудеей управлял Понтий Пилат, Ирод был правителем Галилеи, его брат Филипп — правителем Итуреи и Трахонитской области3:1 Итурея, Трахонитская область и Авилинея— это современная территория Ливана и Сирии., Лисаний — правителем Авилинеи, 2а первосвященниками были Анна и Кайафа,3:1–2 Тиберий был императором Рима в 14–37 гг. Понтий Пилат был римским наместником в Иудее в 26–36 гг. Ирод Антипа, Филипп (сын Ирода Великого и Клеопатры) и Лисаний были правителями перечисленных выше областей. Анна был первосвященником в 6–15 гг. и не утратил своего влияния и после этого. А его зять Кайафа занимал этот пост в 18–36 гг. слово Бога было к Иоанну, сыну Захарии, в пустыне. 3После этого Иоанн пошел по всем областям, прилегающим к Иордану, и проповедовал крещение в знак покаяния для прощения грехов. 4Как написано в книге пророка Исаии:

«Голос раздается в пустыне:

„Приготовьте путь Господу,

сделайте прямыми дороги Его!

5Всякий овраг пусть будет засыпан,

а всякая гора и холм — опустятся;

извилистые пути пусть станут прямыми,

и неровные — пусть станут ровными,

6чтобы всё человечество увидело Божье спасение“»3:4–6 Ис. 40:3–5..

7Иоанн говорил толпам, которые приходили принять крещение от него:

— Вы, змеиное отродье! Кто предупредил вас, чтобы вы бежали от грядущего гнева? 8Делами докажите искренность вашего покаяния. Не думайте говорить в себе: «Наш отец Авраам!» Говорю вам, что Бог может и из этих камней сотворить детей Аврааму. 9Уже и топор лежит у корня деревьев, и всякое дерево, не приносящее хорошего плода, будет срублено и брошено в огонь.

10— Что же нам делать? — спрашивал народ.

11Иоанн отвечал:

— Тот, у кого две рубахи, пусть даст одну тому, у кого ее нет вообще, и тот, у кого есть еда, пусть сделает то же самое.

12Сборщики налогов тоже приходили принять крещение.

— Учитель, — спрашивали они, — что нам делать?

13— Не требуйте с людей больше, чем положено, — говорил он им.

14Спрашивали его и солдаты:

— А что делать нам?

Иоанн ответил:

— Не вымогайте у людей денег силой и угрозами, никого ложно не обвиняйте и довольствуйтесь своим жалованьем.

15Народ был в напряженном ожидании, и всех интересовало, не Христос ли Иоанн. 16На это Иоанн отвечал им всем:

— Я крещу вас водой, но придет Тот, Кто могущественнее меня, я даже недостоин развязать ремни Его сандалий. Он будет крестить вас Святым Духом и огнем. 17У Него в руках лопата, чтобы провеять зерно на току; пшеницу Он соберет в Свое хранилище, а мякину сожжет в неугасимом огне.

18И много другого говорил Иоанн, убеждая народ и возвещая ему Радостную Весть.

19Когда же он стал упрекать четвертовластника Ирода за женитьбу на Иродиаде, жене его брата, и за всё другое зло, которое тот совершил, 20Ирод ко всему злу добавил еще одно, заключив Иоанна в темницу.

Иоанн крестит Иисуса

(Мат. 3:13–17; Мк. 1:9–11; Ин. 1:32–34)

21Когда весь народ крестился, был крещен и Иисус, и когда после крещения Он молился, раскрылись небеса, 22и на Него спустился Святой Дух в телесном виде, в образе голубя. И с небес прозвучал голос:

— Ты Сын Мой, любимый Мною! В Тебе Моя радость!

Родословие Иисуса

(Мат. 1:1–17)

23Иисусу было около тридцати лет, когда Он начал Свое служение. Он был, как все думали, сыном Иосифа, сына Илия, 24чьими предками были:

Матфат, Левий, Мелхий,

Ианнай, Иосиф, 25Маттафия,

Амос, Наум, Еслий,

Наггей, 26Мааф, Маттафия,

Шимьи, Иосих, Иодай,

27Иоханан, Рисай, Зоровавель,

Шеалтиил, Нирий, 28Мелхий,

Аддий, Косам, Элмадам,

Ир, 29Иосий3:29 Или: Иисус., Элиезер,

Иорим, Матфат, Левий,

30Симеон, Иуда, Иосиф,

Ионам, Элиаким, 31Мелеай,

Маинай, Маттафай, Нафан,

Давид, 32Иессей, Овид,

Боаз, Салмон, Нахшон,

33Аминадав, Админ, Арний,

Хецрон, Парец, Иуда,

34Иаков, Исаак, Авраам,

Терах, Нахор, 35Серуг,

Реу, Пелег, Евер,

Шелах, 36Каинан, Арпахшад,

Сим, Ной, Ламех,

37Мафусал, Енох, Иаред,

Малелеил, Каинан, 38Енос,

Сиф, Адам,

Бог.