Kutoka 3 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Kutoka 3:1-22

Mose Na Kichaka Kinachowaka Moto

13:1 Kut 2:16, 18; 17:6; 19:1-11; 33:6; 4:27; 18:5; 24:133:1 Kum 1:2-6; 4:10, 11-15; 5:2; 1Fal 19:8; Amu 1:16; Mal 4:4Basi Mose alikuwa anachunga mifugo ya Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani. Mose akapeleka mifugo mbali nyuma ya jangwa, naye akafika Horebu, mlima wa Mungu. 23:2 Mwa 16:7; Kut 2:2-6; 19:18; 4:5; Kum 5:19; 29:1; 1Fal 19:12; Kum 33:16; Mk 12:26; Lk 20:37; Mdo 7:30Huko malaika wa Bwana akamtokea Mose katika mwali wa moto kutoka kichakani. Mose akaona kwamba ingawa kile kichaka kilikuwa kinawaka moto, kilikuwa hakiteketei. 3Ndipo Mose akawaza, “Nitageuka sasa nione kitu hiki cha ajabu, nami nione ni kwa nini kichaka hiki hakiteketei.”

43:4 Kut 19:3; 4:5; Mwa 31:11; 1Sam 3:4; Isa 6:8Bwana alipoona kuwa amegeuka ili aone, Mungu akamwita kutoka ndani ya kile kichaka, “Mose! Mose!”

Naye Mose akajibu, “Mimi hapa.”

53:5 Yer 30:21; Mwa 28:17; Mdo 7:33Mungu akamwambia, “Usikaribie zaidi. Vua viatu vyako, kwa maana mahali unaposimama ni patakatifu.” 63:6 Mwa 24:12; Kut 5:4; 24:11; 33:20; Mt 22:32; Mk 12:26; Lk 20:37; Mdo 3:13; 7:32; 1Fal 19:13; Amu 13:22; Ay 13:11; 23:16; 30:15; Isa 6:5Kisha akamwambia, “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo.” Mose aliposikia hayo, akafunika uso wake kwa sababu aliogopa kumtazama Mungu.

73:7 1Sam 1:11; 9:16; Mwa 16:11; Neh 9:9; Za 106:44; Kut 2:25; Mdo 7:34Bwana akamwambia, “Hakika nimeona mateso ya watu wangu katika Misri. Nimesikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao, nami naguswa na mateso yao. 83:8 Mwa 11:5; 12:7; 15:14; Mdo 7:34; Kut 13:5; 33:3; Law 20:24; Hes 13:27; Kum 1:25; 6:3; 8:7-9; 11:9; 26:9; 27:3; Yos 5:6; 11:3; Yer 11:5; 32:22; Eze 20:6; Amu 3:3Basi nimeshuka niwaokoe kutoka mkono wa Wamisri, niwatoe na kuwapandisha kutoka nchi hiyo, niwapeleke katika nchi nzuri na kubwa, nchi itiririkayo maziwa na asali, nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi. 93:9 Kut 1:14; Hes 10:9Sasa kilio cha Waisraeli kimenifikia, nami nimeona jinsi Wamisri wanavyowatesa. 103:10 Kut 4:12; 6:13, 26; 12:41, 51; 20:2; Yos 24:5; Mdo 7:34; 1Sam 12:6, 8; Za 105:26; Kum 4:20; 1Fal 8:16; Mik 6:4Basi, sasa nenda. Ninakutuma kwa Farao ili kuwatoa watu wangu Waisraeli kutoka Misri.”

113:11 Kut 4:10; 6:12, 30; Yer 1:6; Amu 6:15; 1Sam 9:21; 15:17; 18:18; 2Sam 7:18; 2Nya 2:6; Isa 6:5Lakini Mose akamwambia Mungu, “Mimi ni nani hata niende kwa Farao kuwatoa Waisraeli nchini Misri?”

123:12 Mwa 26:3; Kut 14:22; Rum 8:31; Hes 26:10; Yos 2:12; Amu 6:17; Za 86:17; Isa 7:14; 8:18; 20:3; Yer 44:29; Mdo 7:7Naye Mungu akasema, “Mimi nitakuwa pamoja nawe. Hii itakuwa ishara kwako kwamba ni Mimi nimekutuma: Hapo utakapokuwa umewatoa watu Misri, mtamwabudu Mungu katika mlima huu.”

133:13 Mwa 32:29Mose akamwambia Mungu, “Ikiwa nitawaendea Waisraeli na kuwaambia, ‘Mungu wa baba zenu amenituma kwenu,’ nao wakiniuliza, ‘Jina lake ni nani?’ Nitawaambia nini?”

143:14 Kut 6:2-3; Yn 8:58; Ebr 13:8; Ufu 1:8; 4:8Mungu akamwambia Mose, “Mimi niko ambaye niko. Hivyo ndivyo utakavyowaambia Waisraeli: ‘Mimi niko amenituma kwenu.’ ”

153:15 Mwa 31:42; 24:12; Dan 2:23; Kut 6:3, 7; 15:3; 23:21; 34:5-7; Law 24:11; Kum 28:58; Za 30:4; 83:18; 96:2; 97:12; 135:13; 145:21; 45:17; 72:17; 102:12; Isa 42:8; Yer 16:21; 32:2; Hos 12:5Vilevile Mungu akamwambia Mose, “Waambie Waisraeli, ‘Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo amenituma kwenu.’ Hili ndilo Jina langu milele, Jina ambalo mtanikumbuka kwalo kutoka kizazi hadi kizazi.

163:16 Kut 4:29, 31; 17:5; Law 4:15; Hes 16:25; 11:16; Kum 5:23; 19:12; Amu 8:14; Rut 4:2; Mit 31:23; Eze 8:11; Mwa 24:12; 2Fal 19:16; 2Nya 6:20; Za 33:18; 66:7“Nenda, ukawakusanye wazee wa Israeli, uwaambie, ‘Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, Isaki na Yakobo, alinitokea akaniambia: Nimewatazama, nami nimeona mliyofanyiwa katika Misri. 173:17 Mwa 15:16; 46:4; Kut 6:6Nami nimeahidi kuwapandisha kutoka mateso yenu katika nchi ya Misri, niwapeleke nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi, nchi itiririkayo maziwa na asali.’

183:18 Kut 4:1, 8; 31:6; 6:12, 30; 4:23; 5:1-3; 6:11; 7:16; 9:13; 8:20, 27; 10:9, 26; Mwa 14:13; 30:26; Hes 23:4, 16“Wazee wa Israeli watakusikiliza. Kisha wewe na wazee mtakwenda kwa mfalme wa Misri na kumwambia, ‘Bwana, Mungu wa Waebrania ametutokea. Turuhusu twende safari ya siku tatu huko jangwani kutoa dhabihu kwa Bwana Mungu wetu.’ 193:19 Kut 4:21; 6:6; 7:3; 10:1; 11:9; Kum 4:34; 2Nya 6:32Lakini nafahamu kwamba mfalme wa Misri hatawaruhusu kwenda, mpaka mkono wenye nguvu umlazimishe. 203:20 Kut 6:16; 7:4-5; 9:15; 13:3-9, 14-16; 11:1; 12:31-33; 4:21; 15:11; Kum 4:34; 5:15; 7:8; 26:8; 3:24; 6:22; 2Fal 17:36; 2Nya 6:32; Za 118:15-16; 136:12; 71:19; 72:18; 77:14; 78:43; 86:10; 105:27; 106:22; Isa 41:10; 63:12; Yer 21:5; 51:25; 30:20; Mik 7:15; Mdo 7:36; Dan 9:15; Hes 14:11; Neh 9:10Kwa hiyo nitaunyoosha mkono wangu na kuwapiga Wamisri kwa maajabu yote nitakayofanya miongoni mwao. Baada ya hayo, atawaruhusu mwondoke.

213:21 Mwa 39:21; Kut 11:2; 2Nya 30:9; Neh 1:11; Za 105:37; 106:46; Yer 42:12“Nami nitawapa hawa watu upendeleo mbele ya Wamisri, kwa hiyo mtakapoondoka nchini hamtaondoka mikono mitupu. 223:22 Ay 27:16-17; Kut 11:2; 12:35; Ezr 1:4-6; 7:16; Mwa 15:14; Eze 39:10; 29:10; Za 105:37Kila mwanamke Mwisraeli atamwomba jirani yake Mmisri na mwanamke yeyote anayeishi nyumbani kwake ampe vyombo vya fedha, dhahabu na nguo, ambavyo mtawavika wana wenu na binti zenu. Hivyo mtawateka nyara Wamisri.”