Kutoka 2 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Kutoka 2:1-25

Kuzaliwa Kwa Mose

12:1 Mwa 29:34; Kut 6:20; Hes 26:29Basi mtu mmoja wa nyumba ya Lawi akaoa mwanamke Mlawi, 22:2 Mwa 39:6; Ebr 11:23naye mwanamke huyo akapata mimba, akazaa mtoto wa kiume. Alipoona mtoto huyo ni mzuri, akamficha kwa miezi mitatu. 32:3 Isa 18:2; Mwa 6:14; 41:2; Ay 8:11; Mdo 7:21Lakini alipoona hawezi kumficha zaidi, akamtengenezea kisafina cha mafunjo, akakipaka lami. Kisha akamweka huyo mtoto ndani yake, akakificha katikati ya matete kando ya ukingo wa Mto Naili. 42:4 Kut 15:20Dada ya huyo mtoto akasimama mbali ili kuona kitakachompata mtoto.

52:5 Kut 7:15; 8:20Ndipo binti Farao akateremka mtoni Naili kuoga, nao wahudumu wake wakawa wanatembea ukingoni mwa mto. Binti mfalme akaona kisafina katikati ya manyasi, akamtuma mmoja wa watumwa wake wa kike kukichukua. 6Alifungua kisafina akaona mtoto ndani yake. Mtoto alikuwa akilia, akamhurumia. Akasema, “Huyu ni mmoja wa watoto wa Kiebrania.”

7Ndipo dada wa huyo mtoto akamuuliza binti Farao, “Je, niende nikakutafutie mmoja wa wanawake wa Kiebrania akulelee huyu mtoto?”

8Binti Farao akamjibu, “Ndiyo, nenda.” Yule msichana akaenda akamleta mama wa mtoto. 9Binti Farao akamwambia, “Mchukue huyu mtoto unisaidie kumlea, nami nitakulipa.” Basi yule mwanamke akamchukua mtoto na kumlea. 102:10 1Sam 1:20; 2Sam 22:17Mtoto alipokua, akampeleka kwa binti Farao, naye akawa mwanawe. Akamwita jina lake Mose akisema, “Nilimtoa kwenye maji.”

Mose Akimbilia Midiani

112:11 Mdo 7:23; Ebr 11:24-26; Kut 1:11Siku moja, baada ya Mose kukua, akaondoka kwenda walikokuwa watu wake, na akachunguza jinsi walivyokuwa wakifanya kazi ngumu. Akamwona Mmisri akimpiga Mwebrania, mmojawapo wa watu wake. 12Mose akatazama huku na huko asione mtu yeyote, akamuua yule Mmisri, akamficha mchangani. 132:13 Mdo 7:26Kesho yake akatoka, akaona Waebrania wawili wakipigana. Akamuuliza yule aliyekosa, “Mbona unampiga Mwebrania mwenzako?”

142:14 Mwa 13:8; Mdo 7:27Yule mtu akamjibu, “Ni nani aliyekufanya mtawala na mwamuzi juu yetu? Je, unataka kuniua kama ulivyomuua yule Mmisri?” Ndipo Mose akaogopa na kuwaza, “Jambo lile nililofanya lazima limefahamika.”

152:15 Kut 4:19; Ebr 11:27; Mwa 31:21Farao aliposikia jambo hili, alijaribu kumuua Mose, lakini Mose akamkimbia Farao na kwenda kuishi katika nchi ya Midiani, akaketi kando ya kisima. 162:16 Kut 3:1; 18:1; Mwa 24:11Kuhani wa Midiani alikuwa na binti saba, nao wakaja kisimani ili kuchota maji na kujaza hori kwa ajili ya kunyweshea mifugo ya baba yao. 172:17 1Sam 30:8; Za 31:2; Mwa 29:10Baadhi ya wachungaji wakaja wakawafukuza hao wasichana. Ndipo Mose akainuka, akawasaidia na kunywesha mifugo yao.

182:18 Kut 3:1; 4:18; 18:5-12; Hes 10:29Hao wasichana waliporudi nyumbani kwa Reueli baba yao, akawauliza, “Imekuwaje leo mmerudi mapema hivyo?”

19Wakamjibu, “Mmisri mmoja alituokoa kutoka mikononi mwa wachungaji. Pia mtu huyo alituchotea maji na kunywesha mifugo.”

202:20 Mwa 18:2-5Akawauliza binti zake, “Yuko wapi? Mbona mmemwacha? Mkaribisheni ale chakula.”

212:21 Kut 4:25; 18:2; Hes 12:1Mose akakubali kukaa kwa huyo mtu, ambaye alimpa Mose binti yake aliyeitwa Sipora amwoe. 222:22 Amu 18:30; Mwa 23:4; Ebr 11:13Sipora alizaa mtoto wa kiume, naye Mose akamwita Gershomu, akisema, “Nimekuwa mgeni katika nchi ya kigeni.”

232:23 Mdo 7:30; Kut 4:19; 1:14; 3:7-9; 6:5; Hes 20:15-16; Kum 26:7; Yak 5:4; Amu 2:18; 1Sam 12:8; Za 5:2; 18:6; 39:12; 81:7Baada ya muda mrefu, mfalme wa Misri akafa. Waisraeli wakalia kwa huzuni katika utumwa wao, walilia na kilio chao cha kutaka msaada kwa ajili ya utumwa kikamfikia Mungu. 242:24 Mwa 8:1; 9:15; 15:15; 17:4; 22:16-18; 26:3; 28:13-15; Kut 32:13; 2Fal 13:23; Za 105:10, 42; Yer 14:21Mungu akasikia kilio chao cha huzuni, akakumbuka Agano alilofanya na Abrahamu pamoja na Isaki na Yakobo. 252:25 Kut 3:7; 4:31; Lk 1:25Kwa hiyo Mungu akawaangalia Waisraeli na kuwahurumia.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

出埃及记 2:1-25

摩西出生

1有一个利未族的人跟他同族的女子结婚。 2那女子怀孕,生了一个男婴。她看见孩子可爱,就把他藏了三个月。 3后来无法再藏下去,她就拿来一个蒲草篮子,外面涂上防水的沥青和柏油,然后把婴儿放在里面,又把篮子放在尼罗河边的芦苇丛中。 4婴儿的姐姐远远地站着,要看看她的弟弟究竟会怎样。

5这时,法老的女儿来到河边沐浴,宫女们在河边行走。公主发现了芦苇丛中的篮子,便吩咐一个婢女去把它取来。 6公主打开一看,原来是一个男婴。公主看见孩子在哭,就可怜他,说:“他是希伯来人的孩子。” 7婴儿的姐姐对公主说:“我去找一个希伯来妇女当奶妈,为你哺养他好吗?” 8公主回答说:“好!”那女孩就跑去把婴孩的母亲带来。 9公主对那妇女说:“你把孩子抱去,替我哺养他,我会给你工钱。”她便把孩子抱去哺养。 10孩子渐渐长大,她便把他带到公主那里,孩子就做了公主的儿子。公主给孩子取名叫摩西,意思是“我把他从水中拉了上来”。

11后来,摩西长大了,他去看望做苦工的希伯来同胞,看见一个埃及人在殴打他的一个希伯来同胞。 12他左右观望,见四下无人,便下手杀了那埃及人,把尸体埋藏在沙地里。 13第二天,他又出去,看见两个希伯来人在打架,便过去对理亏的人说:“你为什么打自己的同胞呢?” 14那人说:“谁立你做我们的首领和审判官?难道你要杀我,像杀那个埃及人一样吗?”摩西听了,害怕起来,心想:“我做的事一定被人知道了。” 15法老听说这件事后,便想杀死摩西摩西为了躲避法老,就逃到米甸居住。一天他坐在一口井旁, 16米甸祭司的七个女儿来打水,要把水倒进槽里饮她们父亲的羊。 17这时,来了另外一群牧人要把她们赶走。摩西便起来帮助她们,打水饮她们的羊群。 18她们回到父亲流珥2:18 “流珥”又名“叶特罗”。那里,父亲问道:“你们今天怎么这么快就回来了?” 19她们答道:“有一个埃及人救我们免遭牧人的欺负,还帮我们打水饮羊群。” 20他又问女儿们:“现在那人在哪里?你们怎么可以丢下他不管呢?去请他来吃点东西。” 21后来,摩西同意住在那人家里。那人把女儿西坡拉许配给他。 22后来,西坡拉生了一个儿子,摩西给他取名叫革舜,意思是“我成了在异乡寄居的人”。

23过了多年,埃及王死了。以色列人受尽奴役,就哀叹呼求,声音传到上帝那里。 24上帝听见他们的哀声,顾念从前跟亚伯拉罕以撒雅各所立的约, 25就垂顾他们,体恤他们。