Waisraeli Waonewa
11:1 Mwa 46:8Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli ambao walikwenda Misri na Yakobo, kila mmoja akiwa pamoja na jamaa yake: 2Reubeni, Simeoni, Lawi na Yuda; 3Isakari, Zabuloni na Benyamini; 41:4 Mwa 35:22-26; Hes 1:20-43Dani na Naftali, Gadi na Asheri. 51:5 Mwa 46:26Wazao wote wa Yakobo walikuwa watu sabini; Yosefu alikuwa tayari yuko Misri.
61:6 Mwa 50:26; Mdo 7:15Basi Yosefu na kaka zake wote na kizazi kile chote walikufa, 71:7 Mwa 12:2; Kum 7:13; Eze 16:7lakini Waisraeli walikuwa wamezaana na kuongezeka sana, idadi yao ikawa kubwa mno, kwa hiyo wakaijaza nchi.
81:8 Yer 43:11; 46:2Kisha mfalme mpya ambaye hakufahamu habari za Yosefu akatawala Misri. 91:9 Mwa 26:16Akawaambia watu wake, “Tazameni, Waisraeli wamekuwa wengi mno kwa idadi kutuliko sisi. 101:10 Mwa 15:13; Kut 3:7; 18:11; Za 64:2; 71:10; 83:3; 105:24-25; Isa 53:3; Mdo 7:17-19Njooni, ni lazima tuwashughulikie kwa uangalifu, la sivyo watazidi kuwa wengi zaidi, na ikiwa patatokea vita, watajiunga na adui zetu kupigana dhidi yetu na kuondoka katika nchi hii.”
111:11 Kut 3:7; 5:4, 10-14; 6:6-7; 2:11; Mwa 15:13; 47:11; Yos 9:27; Isa 60:10; 1Fal 9:19, 21; 1Nya 22:2; 2Nya 8:4Basi Wamisri wakaweka wasimamizi wa kuwasimamia na kuwatesa Waisraeli kwa kazi ngumu, nao wakajenga miji ya Pithomu na Ramesesi ya kuweka akiba ya Farao. 12Lakini walivyozidi kuteswa ndivyo walivyozidi kuongezeka na kuenea katika nchi; Wamisri wakawaogopa Waisraeli, 131:13 Mwa 15:13-14; Kut 5:21; 16:3; Law 25:43-53; Kum 4:20; 26:6; 1Fal 8:15; Za 129:1; Isa 30:6; 48:10; Yer 11:4kwa hiyo wakawatumikisha kwa ukatili. 141:14 Kum 26:6; Ezr 9:9; Isa 14:3; Mwa 11:3; Kut 2:23; 3:9; Hes 20:15; Mdo 7:19; 1Sam 10:11; 2Sam 13:4Wakafanya maisha ya Waisraeli kuwa machungu kwa kufanya kazi ngumu ya kutengeneza lami na kufyatua matofali, na kazi zote za mashambani; katika kazi zao zote ngumu, Wamisri waliwatumia Waisraeli kwa ukatili.
151:15 Mwa 35:17Mfalme wa Misri akawaambia wakunga wa Kimisri waliowazalisha wanawake wa Kiebrania, ambao majina yao ni Shifra na Pua, 16“Mtakapowazalisha wanawake wa Kiebrania, chunguzeni wanapojifungua. Ikiwa ni mtoto wa kiume, muueni, lakini ikiwa ni msichana, mwacheni aishi.” 171:17 Mit 16:6; 1Sam 22:17; Dan 3:16-18; Mdo 4:18-20; 5:29Lakini hao wakunga walimcha Mungu na hawakufanya kile mfalme wa Misri alichowaambia kufanya, bali wakawaacha watoto wa kiume waishi. 18Ndipo mfalme wa Misri akawaita hao wakunga, akawauliza, “Kwa nini mmefanya hivi? Mbona mmeacha watoto wa kiume waishi?”
191:19 Law 19:11; Yos 2:4-6; 1Sam 19:14; 2Sam 17:20Wakunga wakamjibu Farao, “Wanawake wa Kiebrania ni tofauti na wanawake wa Kimisri; wao wana nguvu, nao hujifungua watoto kabla wakunga hawajafika.”
201:20 Mit 11:18; 22:8; Mhu 8:12; Isa 3:10; Ebr 6:10Kwa hiyo Mungu akawatendea mema wakunga hao. Waisraeli wakaongezeka na kuendelea kuwa wengi zaidi. 211:21 1Sam 2:35; 2Sam 7:11, 27-29; 1Fal 11:38; 14:10Kwa vile hao wakunga walimcha Mungu, Mungu akawajalia kuwa na jamaa zao wenyewe.
221:22 Mwa 41:1; Mdo 7:19Kisha Farao akatoa agizo hili kwa watu wake wote: “Kila mtoto wa kiume atakayezaliwa kwa Waebrania lazima atupwe katika Mto Naili, bali kila mtoto wa kike aachwe aishi.”
1Now these are the names of the children of Israel, which came into Egypt; every man and his household came with Jacob. 2Reuben, Simeon, Levi, and Judah, 3Issachar, Zebulun, and Benjamin, 4Dan, and Naphtali, Gad, and Asher. 5And all the souls that came out of the loins of Jacob were seventy souls: for Joseph was in Egypt already.1.5 loins: Heb. thigh 6And Joseph died, and all his brethren, and all that generation.
7¶ And the children of Israel were fruitful, and increased abundantly, and multiplied, and waxed exceeding mighty; and the land was filled with them.
8Now there arose up a new king over Egypt, which knew not Joseph. 9And he said unto his people, Behold, the people of the children of Israel are more and mightier than we: 10Come on, let us deal wisely with them; lest they multiply, and it come to pass, that, when there falleth out any war, they join also unto our enemies, and fight against us, and so get them up out of the land. 11Therefore they did set over them taskmasters to afflict them with their burdens. And they built for Pharaoh treasure cities, Pithom and Raamses. 12But the more they afflicted them, the more they multiplied and grew. And they were grieved because of the children of Israel.1.12 But…: Heb. And as they afflicted them, so they multiplied, etc 13And the Egyptians made the children of Israel to serve with rigour: 14And they made their lives bitter with hard bondage, in morter, and in brick, and in all manner of service in the field: all their service, wherein they made them serve, was with rigour.
15¶ And the king of Egypt spake to the Hebrew midwives, of which the name of the one was Shiphrah, and the name of the other Puah: 16And he said, When ye do the office of a midwife to the Hebrew women, and see them upon the stools; if it be a son, then ye shall kill him: but if it be a daughter, then she shall live. 17But the midwives feared God, and did not as the king of Egypt commanded them, but saved the men children alive. 18And the king of Egypt called for the midwives, and said unto them, Why have ye done this thing, and have saved the men children alive? 19And the midwives said unto Pharaoh, Because the Hebrew women are not as the Egyptian women; for they are lively, and are delivered ere the midwives come in unto them. 20Therefore God dealt well with the midwives: and the people multiplied, and waxed very mighty. 21And it came to pass, because the midwives feared God, that he made them houses. 22And Pharaoh charged all his people, saying, Every son that is born ye shall cast into the river, and every daughter ye shall save alive.