Kumbukumbu 8 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 8:1-20

Usimsahau Bwana

18:1 Kum 4:1; Kut 19:5; Ay 36:11; Za 16; 11; Eze 20:19Uwe mwangalifu kufuata kila agizo ninalokupa wewe leo, ili mweze kuishi, kuongezeka na mweze kuingia mkamiliki nchi ambayo Bwana aliahidi kwa kiapo kwa baba zenu. 28:2 Kum 29:5; Za 136:16; Amo 2:10; Mwa 22:1; Yos 6:17; 11:11; Kut 23:32; Amu 1:24; 2:2Kumbuka jinsi Bwana Mungu wenu alivyowaongoza katika njia yote katika jangwa kwa miaka hii arobaini, kukunyenyekeza na kukujaribu ili ajue lililoko moyoni mwako, kwamba utayashika maagizo yake au la. 38:3 Isa 2:11; Yer 44:10; Kut 16:14; 1Fal 8:36; Za 25:5; 94:12; 119:171; Mwa 3:19; Ay 23:12; Za 104:15; Mit 28:21; Isa 51:14; Yer 42:14; Ay 22:22; Za 119:13; 138:4; Kut 16:2-3; Mt 4:4; Lk 4:4Alikudhili na kukufanya uone njaa kisha akulishe kwa mana, ambayo wewe wala baba zako hamkuijua, awafundishe kuwa mwanadamu hataishi kwa mkate tu bali kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Bwana. 48:4 Kum 29:5; Neh 9:21Nguo zenu hazikuchakaa wala miguu yenu haikuvimba kwa miaka hii arobaini. 58:5 Kum 4:36; 2Sam 7:14; Ay 5:17; 33:19; Mit 3:11-12; Ebr 12:5-11; Ufu 3:19Mjue basi ndani ya mioyo yenu kama mtu anavyomwadibisha mwanawe, ndivyo Bwana Mungu wako atawaadibisha ninyi.

68:6 Kut 33:13; 1Fal 3:14; Za 81:13; 95:10; Kum 5:33Shikeni maagizo ya Bwana Mungu wenu mtembee katika njia zake na kumheshimu. 78:7 Za 106:24; Yer 3:19; Eze 20:6; Kum 11:9-12; Yer 2:7Kwa kuwa Bwana Mungu wenu anawaleta katika nchi nzuri, nchi yenye vijito na mabwawa ya maji, yenye chemchemi zinazotiririka mabondeni na katika vilima; 88:8 Kut 9:31; Mwa 49:11; Hes 13:23; 1Fal 4:25; Kum 32:13; Za 81:16nchi yenye ngano na shayiri, mizabibu na mitini, mikomamanga, mafuta ya zeituni na asali; 98:9 Amu 18:10; Ay 28:2nchi ambayo chakula hakitapungua na hamtakosa chochote; nchi ambayo miamba yake ni chuma na mnaweza kuchimba shaba kutoka kwenye vilima.

108:10 Kum 6:10-12Wakati mtakapokwisha kula na kushiba, msifuni Bwana Mungu wenu kwa ajili ya nchi nzuri aliyowapa. 118:11 Kum 4:9Jihadharini msimsahau Bwana Mungu wenu, mkashindwa kushika maagizo yake, sheria na amri zake ambazo ninawapa leo. 128:12 Mit 30:9; Hos 13:6Angalia wakati mtakapokuwa mmekula na kushiba, mkajenga nyumba nzuri na kukaa humo, 13na wakati makundi yenu ya ngʼombe na mbuzi na kondoo yatakapoongezeka na fedha na dhahabu yenu itakapoongezeka na vyote mlivyo navyo vitakapozidishwa, 148:14 Za 78:7; 106:21basi mioyo yenu isiwe na kiburi mkamsahau Bwana Mungu wenu aliyewatoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa. 158:15 Kum 1:19; 32:13; 32:10; Hes 21:6; Isa 14:29; 30:6; Kut 17:6; Ay 28:9; Za 78:15; 114:8Aliwaongoza kupitia jangwa lile kubwa na la kutisha, nchi ile ya kiu isiyo na maji, yenye nyoka wa sumu na nge. Aliwatolea maji kutoka kwenye mwamba mgumu. 168:16 Kut 16:14; 16:15; Mwa 22:1; Rum 8:28; 2Kor 4:17; Ebr 12:11; Yak 1:12; 1Pet 1:7Aliwapa mana ya kula jangwani, kitu ambacho baba zenu hawakukijua, ili kuwanyenyekesha na kuwajaribu ninyi ili mwishoni apate kuwatendea mema. 178:17 Kum 9:4, 24; 31:27; Amu 7:2; Za 44:3; Isa 10:13Mnaweza kusema, “Uwezo wangu na nguvu za mikono yangu ndizo zilizonipatia utajiri huu.” 188:18 Mwa 26:13; Kum 26:10; 28:4; 1Sam 2:7; Za 25:13; 112:3; Mit 8:18; 10:22; Mhu 9:11; Hos 2:8Lakini kumbukeni Bwana Mungu wenu, ndiye ambaye huwapa uwezo wa kupata utajiri, na hivyo kulithibitisha Agano lake, ambalo aliwaapia baba zenu, kama ilivyo leo.

198:19 Kum 6:14; 4:26; 30:18; Za 16:4; Yer 7:6; 13:10; 25:6Ikiwa mtamsahau Bwana Mungu wenu, mkaifuata miungu mingine, mkaiabudu na kuisujudia, ninashuhudia dhidi yenu leo kwamba hakika mtaangamizwa. 208:20 2Fal 21:2; Za 10:16; Eze 5:5-17; Mao 1:1-22; 2:17; Dan 9:12; Zek 1:6Kama mataifa Bwana aliyoyaangamiza mbele yenu, ndivyo ninyi mtakavyoangamizwa kwa kutokumtii Bwana Mungu wenu.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

申命記 8:1-20

不可忘記耶和華

1「你們要謹遵我今日吩咐你們的一切誡命,以便能夠存活,生養眾多,並且得到耶和華起誓要賜給你們祖先的土地。 2要記住這四十年來你們的上帝耶和華怎樣在曠野引領你們,祂磨煉你們、考驗你們,好知道你們的心意如何、肯不肯遵守祂的誡命。 3祂讓你們忍饑挨餓,然後賜給你們祖祖輩輩從未見過的嗎哪吃,為了使你們明白人活著不是單靠食物,乃是靠祂口中的每一句話。 4這四十年來,你們的衣服沒有穿破,雙腳也沒有走腫。 5你們心裡要明白,你們的上帝耶和華管教你們,如同父親管教兒子。

6「所以,你們要遵守你們的上帝耶和華的誡命,行祂的道,敬畏祂, 7因為祂要帶你們到一個佳美之地。那裡的谷中和山間流淌著條條溪流、股股清泉; 8那裡盛產大麥、小麥、葡萄、無花果、石榴、橄欖油和蜂蜜; 9那裡食物充足,一無所缺;那裡礦產資源豐富,石頭就是鐵,山中可以採銅。 10你們吃飽喝足後,要讚美你們的上帝耶和華,因為祂賜給你們那佳美之地。

11「你們要謹慎,免得忘記你們的上帝耶和華,不遵守我今天吩咐你們的誡命、典章和律例。 12當你們豐衣足食、居室華美、 13牛羊眾多、金銀日增的時候, 14切勿心驕氣傲,忘記你們的上帝耶和華。祂把你們從受奴役之地——埃及救出來, 15帶領你們走過乾旱、可怕、毒蛇和蠍子出沒的大曠野。祂使堅硬的磐石流出水來給你們喝, 16在曠野中把你們祖先從未見過的嗎哪賜給你們吃,為要磨煉你們、考驗你們,使你們最終得到益處。 17你們切勿以為是憑自己的雙手和能力致富的。 18要記住,是你們的上帝耶和華賜給你們致富的能力,為要堅立祂給你們祖先的誓約,正如今日的情形。

19「我今天警告你們,如果你們忘記你們的上帝耶和華,去追隨、供奉、祭拜其他神明,你們必滅亡。 20如果你們不聽從你們的上帝耶和華,你們必滅亡,正如祂使列國在你們面前滅亡一樣。