Kumbukumbu 6 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Kumbukumbu 6:1-25

Mpende Bwana Mungu Wako

1Haya ndiyo maagizo, amri na sheria ambazo Bwana Mungu wenu aliniagiza niwafundishe ninyi ili mpate kuyashika katika nchi ambayo ninyi mnavuka Yordani kuimiliki, 26:2 Kut 20:20; 1Sam 12:24; Kum 4:9; Mwa 26:5; Kut 20:12ili kwamba ninyi, watoto wenu na watoto wao baada yao wamche Bwana Mungu wenu siku zote kwa kushika amri na maagizo yake yote ninayowapa, ili mweze kuyafurahia maisha marefu. 36:3 Mwa 15:5; Kum 5:33; 32:13-14; Kut 3:8; 13:5; 19:5Sikia, ee Israeli, nawe uwe mwangalifu kutii ili upate kufanikiwa na kuongezeka sana katika nchi itiririkayo maziwa na asali, kama Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaahidi ninyi.

46:4 Zek 14:9; Kum 4:35-39; Neh 9:6; Za 86:10; Isa 44:6; Mk 12:29; Yn 10:30; 1Kor 8:4; Efe 4:6; Yak 2:19Sikia, ee Israeli: Bwana Mungu wako, Bwana ni mmoja. 56:5 Kum 11:1, 22; Mt 22:37; Mk 12:30; Lk 10:27; 1Sam 12:24; Kum 4:29; 10:12; Yos 22:5Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote. 66:6 Kum 11:18; 30:14; 32:46; Za 26:2; 37:31; 40:8; 119:11; Mit 3:3; Isa 51:7; Yer 17:1; 31:33; Eze 40:4Amri hizi ninazokupa leo zitakuwa katika moyo wako. 76:7 Kum 4:9; 11:19; Mit 22:6; Efe 6:4Wafundishe watoto wako kwa bidii. Nena kuhusu amri hizi uketipo nyumbani na wakati utembeapo njiani, ulalapo na uamkapo. 86:8 Kut 13:9; Mt 23:5; Mit 3:3; 7:3; 6:21Zifunge kama alama juu ya mkono wako, na uzifunge juu ya paji la uso wako. 96:9 Kum 11:20; Isa 50:8; 57:8Ziandike kwenye miimo ya milango ya nyumba yako na juu ya malango yako.

106:10 Mwa 11:4; Kum 12:29; 19:1; Yos 24:13Wakati Bwana Mungu wako atakapokuleta katika nchi aliyowaapia baba zako, Abrahamu, Isaki na Yakobo, kukupa wewe, nchi kubwa, ina miji inayopendeza ambayo hukuijenga, 116:11 Yer 22:13; Law 26:5; Kum 8:10; 11:29; 31:20nyumba zilizojaa vitu vizuri vya aina nyingi ambavyo hukuvijaza, visima ambavyo hukuchimba, na mashamba ya mizabibu na mizeituni ambayo hukupanda wewe, basi, utakapokula na kushiba, 126:12 Kum 4:9, 23; 2Fal 17:38; Za 44:17; 78:7; 103:2jihadhari usije ukamwacha Bwana, aliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.

136:13 Za 33:8; 34:9; Kum 13:4; 1Sam 7:3; Yer 44:10; Mt 4:10; Lk 4:4, 8; 1Sam 20:3; Kut 20:7; Mt 5:33Utamcha Bwana Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake na kuapa kwa jina lake. 14Usifuate miungu mingine, miungu ya mataifa yanayokuzunguka; 156:15 Kum 4:24kwa kuwa Bwana Mungu wako, ambaye yuko katikati yako, ni Mungu mwenye wivu na hasira yake itawaka dhidi yako, naye atakuangamiza kutoka uso wa nchi. 166:16 Kut 17:2; Mt 4:7; Lk 4:12Usimjaribu Bwana Mungu wako kama ulivyofanya huko Masa. 176:17 Law 26:3; Kum 11:22; Za 119:4-5, 56, 100, 134, 168Utayashika maagizo ya Bwana Mungu wako kwa bidii, na masharti na amri alizokupa. 186:18 2Fal 18:6; Isa 36:7; 38:3; Kum 4:40Fanya lililo haki na jema mbele za Bwana, ili upate kufanikiwa, uweze kuingia na kuimiliki nchi nzuri ambayo Bwana aliahidi kwa kiapo kwa baba zako, 196:19 Kut 23:27; Yos 21:44; Za 78:53; 107:2; 136:24kuwafukuza kwa nguvu adui zako mbele yako kama Bwana alivyosema.

206:20 Kut 10:2; 13:14Siku zijazo, mtoto wako atakapokuuliza, “Ni nini maana ya masharti haya, amri na sheria hizi ambazo Bwana Mungu wako alikuagiza wewe?” 216:21 Kum 4:34Mwambie: “Tulikuwa watumwa wa Farao huko Misri, lakini Bwana alitutoa sisi kutoka Misri kwa mkono wenye nguvu. 22Bwana akapeleka mbele yetu ishara za miujiza na maajabu makubwa na ya kutisha mno juu ya Misri na Farao pamoja na nyumba yake yote. 23Lakini Mungu akatutoa huko, akatuleta na kutupa nchi hii ambayo aliwaahidi baba zetu kwa kiapo. 246:24 Kum 10:12; 30:6; Za 86:11; Yer 32:39; Za 27:12; 41:2; Rum 10:5Bwana akatuagiza tutii amri hizi zote na kumcha Bwana Mungu wetu, ili tupate kustawi na kuendelea kuwa hai kama ilivyo leo. 256:25 Za 103:18; 119:34, 55; Kum 24:13; Rum 9:31Kama tukizitii kwa bidii amri hizi zote mbele za Bwana Mungu wetu, kama alivyotuamuru sisi, hiyo itakuwa haki yetu.”