Kumbukumbu 24 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Kumbukumbu 24:1-22

Sheria Kuhusu Ndoa Na Talaka

124:1 Kum 22:13; 2Fal 17:6; Isa 50:1; Yer 3:8; Mt 1:19; 5:31; 19:7-9; Mk 10:4-5; Mal 2:16Ikiwa mtu atamwoa mke na akamchukia kwa sababu ya kukosa adabu, naye akamwandikia hati ya talaka, akampa na kumfukuza kutoka nyumbani kwake, 2ikiwa baada ya kuondoka nyumbani kwake atakuwa mke wa mtu mwingine, 3ikiwa mume wake wa pili atachukizwa naye akamwandikia hati ya talaka, akampa na kumfukuza kutoka nyumbani kwake, au kama akifa, 424:4 Yer 3:1basi yule mume wake wa kwanza, ambaye alimpa talaka, haruhusiwi kumwoa tena baada ya mwanamke huyo kuwa najisi. Hayo yatakuwa machukizo machoni pa Bwana. Usilete dhambi juu ya nchi ambayo Bwana Mungu wako anakupa kama urithi.

524:5 Kum 20:7; Mit 5:18Kama mtu ameoa karibuni, kamwe asipelekwe vitani au kupewa wajibu mwingine wowote. Kwa mwaka mmoja atakuwa huru kubaki nyumbani ili amfurahishe mke aliyemwoa.

624:6 Kut 22:22; Isa 47:2Usitoe jozi ya mawe ya kusagia, hata ikiwa lile la juu, kuweka rehani kwa ajili ya deni, kwa sababu itakuwa ni kuweka uhai wa mtu kama dhamana.

724:7 Yer 11:2; Ebr 9:15; 10:15-17; Mwa 17:9; Kut 3:1; Kum 4:2324:7 Kut 21:16; 1Kor 5:13Kama mtu akikamatwa akiiba yeyote miongoni mwa ndugu zake wa Waisraeli na kumtenda kama mtumwa au akimuuza, mwizi huyo ni lazima auawe. Nawe utaondoa uovu kutoka miongoni mwenu.

824:8 Law 13:1-46; Kum 17:9; Law 14:2; Mt 8:4; Lk 5:14; 7:14Pakitokea magonjwa ya ngozi ya kuambukiza, mwe waangalifu sana kufanya sawasawa na maagizo ya makuhani, ambao ni Walawi. Ni lazima mfuate kwa uangalifu yale niliyowaamuru. 924:9 Hes 12:10; Lk 17:32; 1Kor 10:6Kumbukeni kile Bwana Mungu wenu alichomfanyia Miriamu njiani baada ya ninyi kutoka Misri.

1024:10 Kut 22:25-27Unapomkopesha jirani yako chochote, usiingie nyumbani kwake kutwaa kile anachokitoa kama rehani. 11Ukae nje na umwache huyo mtu uliyemkopesha akuletee hiyo rehani. 1224:12 Kut 22:26Ikiwa mtu huyo ni maskini, usiende kulala ukiwa na hiyo rehani yake katika milki yako. 1324:13 Kut 22:26-27; Kum 6:25; Za 106:31; Dan 4:27; Ay 24:7, 8; 31:16-20; Eze 18:7, 12, 16; 33:15; Amo 2:8; Ay 29:11; 2Kor 9:13; 2Tim 1:18Rudisha vazi lake kabla ya machweo ya jua ili apate kulilalia. Kisha atakushukuru na kitaonekana kama kitendo cha haki mbele za Bwana Mungu wako.

1424:14 Law 19:13; 25:35-43; Kum 15:12-18; Ay 24:4; Mit 14:31; 19:17; 1Tim 5:18; Amo 4:1; Mal 3:5Usimwonee mtu maskini na mhitaji ambaye umemwajiri, akiwa ni nduguyo Mwisraeli au mgeni anayeishi katika mojawapo ya miji yenu. 1524:15 Law 25:35; 19:13; Mt 20:8; Kut 22:23; Ay 12:19; Yak 5:4; Yer 22:13Mlipe ujira wake kila siku kabla ya jua kutua, kwa sababu yeye ni maskini na anautegemea ujira huo. La sivyo, anaweza kumlilia Bwana dhidi yako, nawe ukapata hatia ya dhambi.

1624:16 Hes 26:11; Yer 31:29-30; Eze 18:20; 2Fal 14:6Baba wasiuawe kwa ajili ya watoto wao, wala watoto wasiuawe kwa ajili ya baba zao; kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe.

1724:17 Kut 22:22; Ay 6:27; 24:9; 29:12; Za 10:17-18; 82:3; Mit 23:10; Eze 22:7; Kut 22:21; 23:2; Kum 10:18Usipotoshe hukumu ya mgeni au yatima, au kuchukua vazi la mjane kama rehani. 18Kumbukeni kwamba mlikuwa watumwa huko Misri, naye Bwana Mungu wenu akawakomboa kutoka huko. Hii ndiyo sababu ninawaamuru kutenda hili.

1924:19 Law 19:9; Kum 10:19; 27:19; Eze 47:22; Zek 7:10; Mal 3:5; Kum 14:29; Law 23:22; Mit 19:17; 28:27; Mhu 11:1Unapovuna shamba lako na ukasahau mganda, usirudi kuuchukua. Acha kwa ajili ya mgeni, yatima na mjane, ili Bwana Mungu wako aweze kukubariki wewe katika kazi zote za mikono yako. 2024:20 Law 19:10Unapovuna zeituni kutoka miti yako, usirudie matawi mara ya pili. Acha kilichobaki kwa ajili ya mgeni, yatima na mjane. 21Unapochuma zabibu katika shamba lako la mizabibu usirudie tena. Acha zinazobaki kwa ajili ya mgeni, yatima na mjane. 22Kumbuka kwamba mlikuwa watumwa katika nchi ya Misri. Ndiyo sababu ninawaamuru kufanya hili.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

申命记 24:1-22

关于婚姻的条例

1“如果有人娶妻后,发觉妻子行为不检,因而嫌弃她,他可以写休书给她,让她离开夫家。 2她离开后,可以自由再婚。 3如果她的后夫也嫌弃她,写休书给她,让她离开夫家,或者后夫死了, 4前夫不可再娶这已被玷污的女子,因为那是耶和华所憎恶的。你们不可把这种罪恶带到你们的上帝耶和华将要赐给你们的土地上。

体恤人情

5“不可叫新婚的人从军出征或办理公务。他可以留在家里一年,使新婚的妻子快乐。

6“不可拿别人的磨或磨的上盘作抵押品,因为这等于拿他们的生命作抵押。

7“如果有人绑架自己的同胞,奴役他或卖掉他,必须处死绑架者,除掉你们中间的罪恶。

8“遇到麻风病,你们要谨遵利未祭司的指示。你们要谨遵我对他们的吩咐。 9要记住你们离开埃及后,你们的上帝耶和华在米利暗身上的作为。

10“如果你们借贷给同胞,不可走进他家里索取抵押物; 11要站在外面,等他把抵押物拿出来。 12如果他是穷人,用自己的外袍作抵押,你们不可把他的外袍留到第二天, 13要在当天日落之前还给他,好让他盖着外袍睡觉。他会因此祝福你们,你们的上帝耶和华也会将此视为你们的义行。

14“不可欺压穷苦的雇工,不论他们是你们的同胞,还是住在你们城中的外族人。 15你们要在每天日落前付给他们工钱,因为他们穷苦,靠工钱维生;否则他们向耶和华控诉你们,你们就有罪了。

16“不可因孩子犯罪而处死父亲,也不可因父亲犯罪而处死孩子。各人要自负罪责。

17“你们要公正地对待寄居者和孤儿,不可拿寡妇的衣物作抵押。 18要记住,你们曾在埃及做过奴隶,你们的上帝耶和华救赎了你们。所以,我吩咐你们这样行。

19“你们在田间收割庄稼时若遗落了一捆,不可回去取,要留给孤儿寡妇和寄居者。这样,你们的上帝耶和华必使你们凡事蒙福。 20你们打橄榄时,打过一次后不可再打,要把剩下的留给孤儿寡妇和寄居者。 21你们摘葡萄时,摘过一次后不可再摘,要把剩下的留给孤儿寡妇和寄居者。 22要记住,你们曾在埃及做过奴隶。所以,我吩咐你们这样行。