Kumbukumbu 22 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Kumbukumbu 22:1-30

122:1 Kut 23:4-5; Mit 27:10; Zek 7:9Kama ukimwona ngʼombe au kondoo wa ndugu yako anapotea, usipuuze, bali uhakikishe unamrudisha kwa mwenyewe. 2Ikiwa huyo ndugu haishi karibu nawe au kama hufahamu yeye ni nani, mchukue nyumbani kwako huyo mnyama umweke mpaka mwenyewe aje kumtafuta. Ndipo umrudishie. 3Fanya vivyo hivyo ukimkuta punda wa nduguyo au joho lake au chochote alichopoteza. Usipuuze jambo hilo.

422:4 Kut 23:5; 1Kor 9:9; Rum 12:10; 2Pet 1:7; 1Yn 3:15; 4:21; Zek 7:9Kama ukimwona punda wa nduguyo au ngʼombe wake ameanguka barabarani, usipuuze jambo hilo. Msaidie asimame kwa miguu yake.

522:5 1Kor 14:40Haimpasi mwanamke kuvaa nguo za kiume wala mwanaume kuvaa nguo za kike, kwa maana Bwana Mungu wenu anachukia yeyote ambaye hufanya hivi.

622:6 Law 22:28; Neh 9:6; Za 36:6; 145:9; Mt 10:29; Lk 12:6Kama ukikuta kiota cha ndege kando ya barabara, iwe juu ya mti au chini, naye ndege amelala juu ya makinda au mayai, usimchukue huyo ndege pamoja na makinda yake. 722:7 Law 22:28; Kum 5:29; 4:20Waweza kuchukua makinda, lakini uwe na hakika ya kumwacha huyo ndege, ili upate kufanikiwa na uweze kuishi maisha marefu.

822:8 Yos 2:8; 1Sam 11:2Wakati unapojenga nyumba mpya, fanya ukuta wa kuzuia kandokando ya dari ili usijiletee hatia ya kumwaga damu juu ya nyumba yako ikiwa yeyote ataanguka kutoka humo.

922:9 Law 19:9; Mt 6:24; 9:16; 2Kor 6:14-16Usipande aina mbili za mbegu katika shamba lako la mizabibu; ikiwa utafanya hivyo, si mazao utakayopanda tu yatakuwa najisi, bali nayo matunda ya shamba la mizabibu pia.

1022:10 2Kor 6:14-16Usilime kwa maksai aliyefungwa nira pamoja na punda.

1122:11 Law 19:9; 19:19Usivae nguo za sufu na kitani zilizofumwa pamoja.

1222:12 Hes 15:37-41; Mt 23:5Fanya vishada kwenye pembe nne za joho unalovaa.

Kukiuka Taratibu Za Ndoa

1322:13 Kum 24:1; Mwa 29:21; Amu 15:1; Efe 5:28-29Ikiwa mtu atamwoa mke na, baada ya kufanya naye tendo la ndoa, akamchukia, 14akimsingizia na kumwita jina baya, akisema, “Nilimwoa mwanamke huyu, lakini nilipomkaribia sikupata uthibitisho wa ubikira wake” 1522:15 Mwa 23:10ndipo baba na mama wa msichana wataleta uthibitisho kwamba alikuwa bikira kwa wazee wa mji kwenye lango. 16Baba wa msichana atawaambia wazee, “Nilimwoza binti yangu kwa huyu mwanaume, lakini hampendi. 17Sasa amemsingizia na kusema, ‘Sikumkuta huyu binti akiwa bikira.’ Lakini hapa kuna uthibitisho wa ubikira wa binti yangu.” Kisha wazazi wake wataonyesha nguo zake kwa wazee wa mji, 1822:18 Kut 18:21; Kum 1:9-18; Rum 13:3nao wazee watamchukua huyo mwanaume na kumwadhibu. 19Watamtoza shekeli mia moja22:19 Shekeli 100 za fedha ni sawa na kilo moja. za fedha na kupewa wazazi wa msichana, kwa sababu mwanaume huyu amempa bikira wa Kiisraeli jina baya. Ataendelea kuwa mke wake; kamwe hawezi kumpa talaka siku zote za maisha yake.

2022:20 Kum 17:4Hata hivyo, kama shtaka ni la kweli na hakuna uthibitisho juu ya ubikira wa huyo msichana ulioweza kupatikana, 2122:21 Mwa 34:7; 38:24; Law 19:29; Kum 23:17-18; 1Kor 5:13; 2Sam 13:12, 13huyo msichana ataletwa kwenye mlango wa nyumba ya baba yake, na hapo watu wa mji wake watampiga kwa mawe hadi afe. Amefanya kitu cha aibu katika Israeli kwa kufanya ukahaba akiwa nyumbani kwa babaye. Lazima mwondoe uovu katikati yenu.

2222:22 2Sam 11:4; Mwa 38:24; Kut 21:12; Mt 5:27-28; Yn 8:5; 1Kor 6:9; Ebr 13:4; Law 20:10; Mit 6:22; Mal 3:5; Yn 8:5Ikiwa mwanaume atakutwa akizini na mke wa mtu mwingine, wote wawili, mwanaume na mwanamke aliyezini naye, lazima wauawe. Lazima mwondoe uovu katika Israeli.

2322:23 Mt 1:18, 19Ikiwa mwanaume atakutana na bikira mjini ambaye ameposwa na mtu akazini naye, 2422:24 1Kor 5:13; Kum 21:14; Mt 1:20, 24utawachukua wote wawili kwenye lango la mji na kuwapiga kwa mawe mpaka wafe; yule msichana kwa kuwa alikuwa mjini na hakupiga kelele kuomba msaada, na yule mwanaume kwa sababu amemtenda jeuri mke wa mtu mwingine. Lazima mwondoe uovu katikati yenu.

25Lakini ikiwa itatokea mwanaume akakutana na msichana aliyeposwa huko mashambani, akambaka, mwanaume aliyefanya hivi peke yake ndiye atakayeuawa. 26Usimtendee msichana yule jambo lolote; hajafanya dhambi inayostahili kifo. Shauri hili ni kama lile la yeyote ambaye anamshambulia na kumuua kwa makusudi jirani yake, 2722:27 Mwa 39:14kwa maana mwanaume huyo alimkuta msichana huko mashambani, na ingawa msichana aliyeposwa alipiga kelele, hapakuwa na mtu wa kumwokoa.

2822:28 Kut 22:16, 17Ikiwa itatokea mwanaume akutane na bikira ambaye hajaposwa na kumbaka nao wakakutwa, 29mwanaume atamlipa baba wa msichana shekeli hamsini22:29 Shekeli 50 za fedha ni sawa na gramu 600. za fedha. Ni lazima amwoe huyo msichana, kwa maana amemfanyia jeuri. Kamwe hawezi kumpa talaka siku zote za maisha yake.

3022:30 Mwa 29:29; Law 18:8; 20:9; Kum 27:20Mwanaume asimwoe mke wa baba yake; kamwe asidhalilishe kitanda cha baba yake.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

申命記 22:1-30

其他條例

1「如果你們看見同胞的牛或羊走迷了路,不可視而不見,要把牠帶回去交給失主。 2如果失主離你們很遠,或者你們不知道失主是誰,就要把牠牽回家,等失主來找時再還給他。 3見到同胞遺失的驢、衣物或其他東西,都要這樣處理,不可視而不見。 4如果在路上看見同胞的牛或驢倒在地上,不可視而不見,要幫忙把牠扶起來。

5「女人不可穿戴男人的衣物,男人也不可穿戴女人的衣物,因為這是你們的上帝耶和華所憎惡的。

6「如果你們在路邊的樹上或地上看見鳥巢,裡面有雛鳥或蛋,並有母鳥伏在上面,不可把母鳥和雛鳥一起取走。 7你們可以取走雛鳥,但一定要放走母鳥。這樣,你們就會凡事順利,得享長壽。

8「建造新房時,要在房頂22·8 以色列人的房子都是平頂房。上安設圍欄,免得有人從房頂上掉下來,由你們家承擔流血之罪。

9「你們不可在葡萄園裡種別的作物,否則你們的收成和園中的果子都要充公。 10不可讓牛和驢同負一軛耕地。 11不可穿由羊毛和細麻合織的衣物。

12「要在外袍的四角綴上穗子。

有關女子貞操的條例

13「如果有人娶了妻子,與她同房後卻不喜歡她, 14誹謗她,說,『我娶了她,與她親近時發現她已經不是處女』, 15女方父母就要把憑據拿到城門口的長老們面前,證明女兒的貞潔。 16女方的父親要對他們說,『我把女兒嫁給這個人,現在他不喜歡我女兒, 17誹謗她,聲稱她結婚時已經不是處女,但這裡有我女兒貞潔的憑據。』女方父母要把女兒新婚之夜用過的床單在本城的長老們面前展開。 18長老們就必須抓住那人懲處他, 19罰他賠償二十兩銀子給女方的父親,因為他誹謗了一個以色列的處女。那女子仍要做他妻子,丈夫終生不可休她。

20「但如果那人的指控屬實,沒有找到那女子貞潔的憑據, 21就要把她帶到她父親的家門前,由本城的人用石頭打死她。因為她婚前淫亂,在以色列做了可恥的事。你們必須除掉你們中間的罪惡。

22「如果有人與有夫之婦通姦,必須處死姦夫和淫婦,這樣就從以色列除掉了罪惡。

23「如果有人在城中遇見已經訂婚的女子,與她行淫, 24你們必須把二人帶到城門口,用石頭打死他們。那女子該死,因為她在城中卻沒有高聲呼救;那男子該死,因為他姦污了別人的妻子。你們必須除去你們中間的罪惡。

25「如果有人在野外遇見已經訂婚的女子,強姦了她,必須處死那男子。 26但不可處死那女子,因為她沒有犯該死的罪,她像被攻擊、殺害的人一樣是無辜的。 27因為她是在野外被強姦,即使呼救也無人救她。

28「如果有人遇見未訂婚的處女,強姦了她,被發現後, 29這人要付給女方的父親十兩銀子,並娶她為妻,終生不可休她,因為他姦污了她。

30「人不可娶他父親的妻妾,因為這是對他父親的羞辱。