Kumbukumbu 22 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Kumbukumbu 22:1-30

122:1 Kut 23:4-5; Mit 27:10; Zek 7:9Kama ukimwona ngʼombe au kondoo wa ndugu yako anapotea, usipuuze, bali uhakikishe unamrudisha kwa mwenyewe. 2Ikiwa huyo ndugu haishi karibu nawe au kama hufahamu yeye ni nani, mchukue nyumbani kwako huyo mnyama umweke mpaka mwenyewe aje kumtafuta. Ndipo umrudishie. 3Fanya vivyo hivyo ukimkuta punda wa nduguyo au joho lake au chochote alichopoteza. Usipuuze jambo hilo.

422:4 Kut 23:5; 1Kor 9:9; Rum 12:10; 2Pet 1:7; 1Yn 3:15; 4:21; Zek 7:9Kama ukimwona punda wa nduguyo au ngʼombe wake ameanguka barabarani, usipuuze jambo hilo. Msaidie asimame kwa miguu yake.

522:5 1Kor 14:40Haimpasi mwanamke kuvaa nguo za kiume wala mwanaume kuvaa nguo za kike, kwa maana Bwana Mungu wenu anachukia yeyote ambaye hufanya hivi.

622:6 Law 22:28; Neh 9:6; Za 36:6; 145:9; Mt 10:29; Lk 12:6Kama ukikuta kiota cha ndege kando ya barabara, iwe juu ya mti au chini, naye ndege amelala juu ya makinda au mayai, usimchukue huyo ndege pamoja na makinda yake. 722:7 Law 22:28; Kum 5:29; 4:20Waweza kuchukua makinda, lakini uwe na hakika ya kumwacha huyo ndege, ili upate kufanikiwa na uweze kuishi maisha marefu.

822:8 Yos 2:8; 1Sam 11:2Wakati unapojenga nyumba mpya, fanya ukuta wa kuzuia kandokando ya dari ili usijiletee hatia ya kumwaga damu juu ya nyumba yako ikiwa yeyote ataanguka kutoka humo.

922:9 Law 19:9; Mt 6:24; 9:16; 2Kor 6:14-16Usipande aina mbili za mbegu katika shamba lako la mizabibu; ikiwa utafanya hivyo, si mazao utakayopanda tu yatakuwa najisi, bali nayo matunda ya shamba la mizabibu pia.

1022:10 2Kor 6:14-16Usilime kwa maksai aliyefungwa nira pamoja na punda.

1122:11 Law 19:9; 19:19Usivae nguo za sufu na kitani zilizofumwa pamoja.

1222:12 Hes 15:37-41; Mt 23:5Fanya vishada kwenye pembe nne za joho unalovaa.

Kukiuka Taratibu Za Ndoa

1322:13 Kum 24:1; Mwa 29:21; Amu 15:1; Efe 5:28-29Ikiwa mtu atamwoa mke na, baada ya kufanya naye tendo la ndoa, akamchukia, 14akimsingizia na kumwita jina baya, akisema, “Nilimwoa mwanamke huyu, lakini nilipomkaribia sikupata uthibitisho wa ubikira wake” 1522:15 Mwa 23:10ndipo baba na mama wa msichana wataleta uthibitisho kwamba alikuwa bikira kwa wazee wa mji kwenye lango. 16Baba wa msichana atawaambia wazee, “Nilimwoza binti yangu kwa huyu mwanaume, lakini hampendi. 17Sasa amemsingizia na kusema, ‘Sikumkuta huyu binti akiwa bikira.’ Lakini hapa kuna uthibitisho wa ubikira wa binti yangu.” Kisha wazazi wake wataonyesha nguo zake kwa wazee wa mji, 1822:18 Kut 18:21; Kum 1:9-18; Rum 13:3nao wazee watamchukua huyo mwanaume na kumwadhibu. 19Watamtoza shekeli mia moja22:19 Shekeli 100 za fedha ni sawa na kilo moja. za fedha na kupewa wazazi wa msichana, kwa sababu mwanaume huyu amempa bikira wa Kiisraeli jina baya. Ataendelea kuwa mke wake; kamwe hawezi kumpa talaka siku zote za maisha yake.

2022:20 Kum 17:4Hata hivyo, kama shtaka ni la kweli na hakuna uthibitisho juu ya ubikira wa huyo msichana ulioweza kupatikana, 2122:21 Mwa 34:7; 38:24; Law 19:29; Kum 23:17-18; 1Kor 5:13; 2Sam 13:12, 13huyo msichana ataletwa kwenye mlango wa nyumba ya baba yake, na hapo watu wa mji wake watampiga kwa mawe hadi afe. Amefanya kitu cha aibu katika Israeli kwa kufanya ukahaba akiwa nyumbani kwa babaye. Lazima mwondoe uovu katikati yenu.

2222:22 2Sam 11:4; Mwa 38:24; Kut 21:12; Mt 5:27-28; Yn 8:5; 1Kor 6:9; Ebr 13:4; Law 20:10; Mit 6:22; Mal 3:5; Yn 8:5Ikiwa mwanaume atakutwa akizini na mke wa mtu mwingine, wote wawili, mwanaume na mwanamke aliyezini naye, lazima wauawe. Lazima mwondoe uovu katika Israeli.

2322:23 Mt 1:18, 19Ikiwa mwanaume atakutana na bikira mjini ambaye ameposwa na mtu akazini naye, 2422:24 1Kor 5:13; Kum 21:14; Mt 1:20, 24utawachukua wote wawili kwenye lango la mji na kuwapiga kwa mawe mpaka wafe; yule msichana kwa kuwa alikuwa mjini na hakupiga kelele kuomba msaada, na yule mwanaume kwa sababu amemtenda jeuri mke wa mtu mwingine. Lazima mwondoe uovu katikati yenu.

25Lakini ikiwa itatokea mwanaume akakutana na msichana aliyeposwa huko mashambani, akambaka, mwanaume aliyefanya hivi peke yake ndiye atakayeuawa. 26Usimtendee msichana yule jambo lolote; hajafanya dhambi inayostahili kifo. Shauri hili ni kama lile la yeyote ambaye anamshambulia na kumuua kwa makusudi jirani yake, 2722:27 Mwa 39:14kwa maana mwanaume huyo alimkuta msichana huko mashambani, na ingawa msichana aliyeposwa alipiga kelele, hapakuwa na mtu wa kumwokoa.

2822:28 Kut 22:16, 17Ikiwa itatokea mwanaume akutane na bikira ambaye hajaposwa na kumbaka nao wakakutwa, 29mwanaume atamlipa baba wa msichana shekeli hamsini22:29 Shekeli 50 za fedha ni sawa na gramu 600. za fedha. Ni lazima amwoe huyo msichana, kwa maana amemfanyia jeuri. Kamwe hawezi kumpa talaka siku zote za maisha yake.

3022:30 Mwa 29:29; Law 18:8; 20:9; Kum 27:20Mwanaume asimwoe mke wa baba yake; kamwe asidhalilishe kitanda cha baba yake.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

申命记 22:1-30

其他条例

1“如果你们看见同胞的牛或羊走迷了路,不可视而不见,要把它带回去交给失主。 2如果失主离你们很远,或者你们不知道失主是谁,就要把它牵回家,等失主来找时再还给他。 3见到同胞遗失的驴、衣物或其他东西,都要这样处理,不可视而不见。 4如果在路上看见同胞的牛或驴倒在地上,不可视而不见,要帮忙把它扶起来。

5“女人不可穿戴男人的衣物,男人也不可穿戴女人的衣物,因为这是你们的上帝耶和华所憎恶的。

6“如果你们在路边的树上或地上看见鸟巢,里面有雏鸟或蛋,并有母鸟伏在上面,不可把母鸟和雏鸟一起取走。 7你们可以取走雏鸟,但一定要放走母鸟。这样,你们就会凡事顺利,得享长寿。

8“建造新房时,要在房顶22:8 以色列人的房子都是平顶房。上安设围栏,免得有人从房顶上掉下来,由你们家承担流血之罪。

9“你们不可在葡萄园里种别的作物,否则你们的收成和园中的果子都要充公。 10不可让牛和驴同负一轭耕地。 11不可穿由羊毛和细麻合织的衣物。

12“要在外袍的四角缀上穗子。

有关女子贞操的条例

13“如果有人娶了妻子,与她同房后却不喜欢她, 14诽谤她,说,‘我娶了她,与她亲近时发现她已经不是处女’, 15女方父母就要把凭据拿到城门口的长老们面前,证明女儿的贞洁。 16女方的父亲要对他们说,‘我把女儿嫁给这个人,现在他不喜欢我女儿, 17诽谤她,声称她结婚时已经不是处女,但这里有我女儿贞洁的凭据。’女方父母要把女儿新婚之夜用过的床单在本城的长老们面前展开。 18长老们就必须抓住那人惩处他, 19罚他赔偿二十两银子给女方的父亲,因为他诽谤了一个以色列的处女。那女子仍要做他妻子,丈夫终生不可休她。

20“但如果那人的指控属实,没有找到那女子贞洁的凭据, 21就要把她带到她父亲的家门前,由本城的人用石头打死她。因为她婚前淫乱,在以色列做了可耻的事。你们必须除掉你们中间的罪恶。

22“如果有人与有夫之妇通奸,必须处死奸夫和淫妇,这样就从以色列除掉了罪恶。

23“如果有人在城中遇见已经订婚的女子,与她行淫, 24你们必须把二人带到城门口,用石头打死他们。那女子该死,因为她在城中却没有高声呼救;那男子该死,因为他奸污了别人的妻子。你们必须除去你们中间的罪恶。

25“如果有人在野外遇见已经订婚的女子,强奸了她,必须处死那男子。 26但不可处死那女子,因为她没有犯该死的罪,她像被攻击、杀害的人一样是无辜的。 27因为她是在野外被强奸,即使呼救也无人救她。

28“如果有人遇见未订婚的处女,强奸了她,被发现后, 29这人要付给女方的父亲十两银子,并娶她为妻,终生不可休她,因为他奸污了她。

30“人不可娶他父亲的妻妾,因为这是对他父亲的羞辱。