Kumbukumbu 12 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Kumbukumbu 12:1-32

Mahali Pekee Pa Kuabudia

112:1 Za 119:5; Kum 4:9-10; 6:15; 1Fal 8:40; Eze 20:19; Gal 6:9Hizi ndizo amri na sheria ambazo ni lazima mwe waangalifu kuzifuata katika nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zenu, amewapa kumiliki, kwa muda wote mtakaoishi katika nchi. 212:2 Hes 21:28; 1Fal 14:23; 2Fal 17:10; Isa 57:5; Yer 2:20; 3:6-13; Kut 34:33Haribuni kabisa kila mahali pao pa kuabudia kwenye milima mirefu, vilima na chini ya kila mti mkubwa ambamo mataifa haya mnayokwenda kuchukua ardhi yao huabudia miungu yao. 312:3 2Fal 11:8; Kut 32:20; 34:13; 1Fal 14:15; Hes 33:53; Kut 23:13; Amu 2:2; Za 16:4; Zek 13:2Bomoeni madhabahu zao, vunjeni yale mawe wanayoabudu, chomeni moto nguzo zao za Ashera; katilieni mbali sanamu za miungu yao na mfute majina yao mahali hapo.

412:4 2Fal 17:15; Yer 10:2Kamwe msimwabudu Bwana Mungu wenu kama wanavyoabudu wao. 512:5 Kut 20:24; 2Sam 7:13; Kum 14:23; 15:20; 16:2, 11; 18:6; 26:2; 1Sam 2:29; 1Fal 1:5; 5; 8:16; 9:3; 2Nya 2:4; 6:6; 7:12-16; Ezr 6:12; 7:15; Za 26:8; 78:68; Zek 2:12Bali mtatafuta mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua katika makabila yenu yote ili aliweke jina lake huko kuwa makao yake. Mahali hapo ndipo iwapasapo kwenda; 612:6 Law 27:30; Mwa 28:20; Yos 22:27; Isa 66:20; Kum 14:22hapo ndipo mtakapoleta sadaka zenu za kuteketezwa na dhabihu, zaka zenu na changizo zenu, kile ulichoweka nadhiri kutoa, sadaka zenu za hiari na malimbuko ya makundi yenu ya ngʼombe pamoja na mbuzi na kondoo. 712:7 Kut 18:12; Mhu 3:12-13; Law 23:40; Isa 62:9Hapo, katika uwepo wa Bwana Mungu wenu, ninyi pamoja na jamaa zenu, mtakula na kufurahia kila kitu ambacho mmegusa kwa mikono yenu, kwa sababu Bwana Mungu wenu amewabariki.

812:8 Amu 17:6; 21:25Msifanye kama tunavyofanya hapa leo, kila mtu anavyopenda mwenyewe, 912:9 Kut 33:14; Kum 3:20; Za 95:11; Mik 2:10; Kum 4:21kwa kuwa bado hamjafikia mahali pa mapumziko na urithi ambao Bwana Mungu wenu anawapa. 1012:10 Kum 11:31; Kut 33:14; Law 1:3; Yos 22:23Lakini mtavuka Yordani na kuishi katika nchi Bwana Mungu wenu anayowapa kama urithi, naye atawapa pumziko kutokana na adui zenu wote wanaowazunguka ili ninyi mpate kuishi kwa salama. 1112:11 Kum 14:23; 15:20; 16:2; Yos 18:1; 1Fal 8:29; Za 78:68; 87:2Kisha kuhusu mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua kuwa mahali pa makao ya Jina lake, hapo ndipo inapowapasa kuleta kila kitu ninachowaamuru: sadaka zenu za kuteketezwa na dhabihu, zaka zenu na changizo, pamoja na vitu vyote vyenye thamani ambavyo mmeweka nadhiri kumtolea Bwana. 1212:12 Kum 26:11-13; 18:20; 9:10; 10:9; 14:29Hapo furahini mbele za Bwana Mungu wenu, ninyi, wana wenu na binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, pamoja na Walawi kutoka miji yenu ambao hawana mgawo wala urithi wao wenyewe. 1312:13 Law 17:4Kuweni waangalifu, msitoe dhabihu zenu za kuteketezwa mahali popote mnapopapenda. 14Mtazitoa tu mahali pale ambapo Bwana atachagua katika mojawapo ya makabila yenu, nanyi hapo zingatieni kila jambo ninalowaamuru.

1512:15 Kum 14:5; 15:22; Mwa 9:3Hata hivyo, mnaweza kuwachinja wanyama wenu katika miji yenu yoyote ile na kula nyama nyingi mpendavyo kama vile mmemchinja paa au kulungu, kulingana na baraka mtakazojaliwa na Bwana Mungu wenu. Watu walio najisi au walio safi wanaweza kula. 1612:16 Mwa 9:4; Mdo 15:20; Mwa 35:14; 1Nya 11:18; Yer 7:18; Law 17:13; Kum 15:23; Yn 19:34; Law 7:26Lakini kamwe usinywe damu; imwage juu ya ardhi kama maji. 1712:17 Law 27:30; Hes 18:12-19; Kum 14:23; 15:20Hamruhusiwi kula katika miji yenu zaka yenu ya nafaka, ya divai mpya na ya mafuta, au mzaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ngʼombe na makundi yenu ya mbuzi na kondoo, wala chochote ambacho mmeweka nadhiri kukitoa, au sadaka zako za hiari, wala matoleo maalum. 1812:18 Kum 14:23; 15:20; 14:26; Neh 8:10; Mhu 3:12-13; 5:18-20Badala yake, mtakula vitu hivyo katika uwepo wa Bwana Mungu wenu mahali ambapo Bwana Mungu wenu atapachagua: wewe, wana wako na binti zako, watumishi wako wa kiume na wa kike, na Walawi kutoka miji yenu. Mnatakiwa mfurahi mbele za Bwana Mungu wenu kwa kula kitu mtakachoweka mikono yenu. 1912:19 Kum 14:27; Neh 13:10; Mal 3:8Mwe waangalifu msiwapuuze Walawi kwa muda wote mnaoishi katika nchi yenu.

2012:20 Kut 34:24; Mwa 15:8, 18; Kum 11:24; Kut 16:3Bwana Mungu wenu atakapokuwa ameongeza nchi yenu kama alivyowaahidi, nanyi mkitamani nyama na mkisema, “Ningependa nyama,” hapo unaweza kula nyingi upendavyo. 2112:21 Kum 14:24; Law 17:4Kama mahali ambapo Bwana Mungu wenu atapachagua kuweka Jina lake ni mbali sana kutoka kwenu, unaweza kuchinja wanyama kutoka makundi yenu ya ngʼombe, ya mbuzi na ya kondoo ambayo Bwana amewapa, kama nilivyokuamuru, na mkiwa katika miji yenu wenyewe mnaweza kula nyingi mtakavyo. 22Mle kama vile mngekula paa na kulungu. Wote walio najisi kiibada na walio safi mwaweza kula. 2312:23 Law 7:26; Eze 33:25; Mwa 9:4; Law 17:11, 14Lakini hakikisheni kwamba hamkunywa damu, kwa sababu damu ni uhai, kamwe msile uhai pamoja na nyama. 24Hamruhusiwi kamwe kunywa damu; imwageni juu ya ardhi kama maji. 2512:25 Kum 4:40; Kut 15:26; Kum 13:18; 1Fal 11:38; 2Fal 12:2; Isa 3:10Msinywe damu, ili mweze kufanikiwa ninyi pamoja na watoto wenu baada yenu, kwa sababu mtakuwa mkifanya lililo haki machoni pa Bwana.

2612:26 Hes 5:9-10; 18:19Lakini vichukueni vitu vyenu vilivyowekwa wakfu pamoja na vile mlivyoweka nadhiri, mwende mahali pale Bwana atakapopachagua. 2712:27 Law 1:13; 3:1-17Leteni sadaka zenu za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana Mungu wenu, vyote nyama na damu. Damu ya dhabihu zenu lazima imiminwe kando ya madhabahu ya Bwana Mungu wenu, lakini nyama mnaweza kula. 2812:28 Kum 4:40; Mhu 8:12; Za 25:12, 13; Mit 1:33; 3:1-4Mwe waangalifu kutii masharti haya yote ninayowapa, ili kwamba siku zote mweze kufanikiwa, ninyi pamoja na watoto wenu baada yenu, kwa sababu mtakuwa mkifanya lililo jema na sahihi mbele za macho ya Bwana Mungu wenu.

2912:29 Yos 23:4; Kum 6:10; Kut 23:23; Yos 23:4; Za 78:55Bwana Mungu wenu atayakatilia mbali mbele yenu mataifa ambayo punde kidogo mtayavamia na kuyaondoa. Lakini mtakapokuwa mmeyafukuza na kuishi katika nchi yao, 3012:30 Kut 10:7na baada ya kuangamizwa mbele yenu, mwe waangalifu msijiingize katika tanzi kwa kuuliza habari za miungu yao, mkisema, “Je, mataifa haya hutumikiaje miungu yao? Nasi tutafanya vivyo hivyo.” 3112:31 Law 18:25; 2Fal 3:27; Kum 9:5; Yer 32:35; 2Fal 17:15; 2Nya 33:2; 36:14Kamwe msimwabudu Bwana Mungu wenu kwa njia wanayoabudu miungu yao, kwa sababu katika kuabudu miungu yao, wanafanya aina zote za machukizo anayoyachukia Bwana. Hata huwateketeza wana wao na binti zao kwa moto kama kafara kwa miungu yao.

3212:32 Kum 4:2; Ufu 22:18-19; Yos 1:7; Mit 30:6Angalieni kwamba mnafanya yote niliyowaamuru; msiongeze kitu wala msipunguze kitu.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

申命记 12:1-32

合宜的敬拜

1“只要你们生活在你们祖先的上帝耶和华赐给你们的土地上,就要谨遵以下律例和典章。

2“你们赶走那里的列邦后,要彻底摧毁他们在高山上、丘陵上、绿树下供奉其神明的地方。 3你们要拆毁他们的祭坛,打碎他们的神柱,焚烧他们的亚舍拉神像,砍倒他们神明的雕像,使他们的名字从那里消失。 4你们不可按照他们的方式敬拜你们的上帝耶和华。 5你们的上帝耶和华要在你们众支派中选一个地方作祂的居所,你们要去那里敬拜祂, 6把你们的燔祭及其他祭物、十一奉献、举祭、还愿祭、自愿献的祭和头生的牛羊带到那里。 7你们和家人要在那里,在你们的上帝耶和华面前吃喝;要为你们所做的一切蒙祂赐福而欢喜快乐。

8“你们不可再像今日这样各行其是, 9因为到如今你们还没有进入你们的上帝耶和华赐给你们作产业的安歇之地。 10但不久你们将渡过约旦河,定居在那片土地上。你们的上帝耶和华将使你们四境太平,安然居住, 11你们要把我吩咐你们献的燔祭、各种牲祭、十一奉献、举祭和一切还愿祭,带到你们的上帝耶和华选定的敬拜场所。 12在那里,你们和儿女、仆婢及同城中没有分到土地作产业的利未人,要一起在你们的上帝耶和华面前欢喜快乐。 13你们切不可随处向耶和华献燔祭。 14耶和华会在你们的一个支派中选定敬拜的场所,你们只可以在那里献燔祭,做我吩咐你们的一切事。

15“你们可以随意在居住的各城宰杀牲畜吃,享受你们的上帝耶和华所赐的福,像吃羚羊和鹿一样。洁净的人和不洁净的人都可以吃。 16但你们不可吃血。要把血倒在地上,像倒水一样。 17不可在你们的城里吃十一奉献的谷物、新酒和油、头生的牛羊、还愿祭、自愿献的祭和举祭; 18要在你们的上帝耶和华选定的地方,与儿女、仆婢及同城的利未人一起在你们的上帝耶和华面前吃。要为你们所做的一切,在你们的上帝耶和华面前欢喜快乐。 19切记,只要你们还住在自己的土地上,就不可忘记利未人。

20“你们的上帝耶和华按照祂的应许扩展你们的疆域后,你们若想吃肉,随时都可以吃。 21如果你们的上帝耶和华选定的敬拜场所离你们太远,你们可以在自己的城里,按照我的吩咐,随时宰杀耶和华赐给你们的牛羊吃, 22就像你们吃羚羊和鹿一样。洁净的人和不洁净的人都可以吃。 23但你们切不可吃血,因为血就是生命;你们不可把生命和肉一起吃。 24你们切不可吃血,要把血倒在地上,像倒水一样。 25你们要做耶和华视为正的事——不可吃血,以便你们及子孙凡事顺利。 26你们要把圣物和还愿祭带到耶和华选定的地方。 27你们要在你们的上帝耶和华的祭坛上献燔祭,连肉带血都要献上。要把其他祭牲的血倒在坛上,但可以吃祭肉。 28你们要认真听从我给你们的这些吩咐,做你们的上帝耶和华视为正与善的事,以便你们及子孙凡事顺利,直到永远。

29“你们的上帝耶和华将为你们铲除列国。你们要赶走他们,住在他们的土地上。 30他们从你们面前被毁灭之后,你们要谨慎,不可受诱惑去效法他们的习俗,不可打听他们神明的事,说,‘这些民族怎样供奉他们的神明呢?我也要效法。’ 31你们不可按照他们的方式敬拜你们的上帝耶和华。他们祭拜自己神明的种种行为令耶和华憎恶,他们甚至焚烧自己的儿女献给他们的神明。

32“你们要谨遵我的一切吩咐,不可增添,也不可删减。