Kumbukumbu 11 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

Kumbukumbu 11:1-32

Mpende Na Umtii Bwana

111:1 Kum 6:5; Law 8:35; Zek 3:7Mpende Bwana Mungu wako na kushika masharti yake, amri zake, sheria zake na maagizo yake siku zote. 211:2 Kum 31:13; Za 78:6; 136:12; Kum 3:24; 5:24; 8:5; Za 11:3; Kut 7:8-21Kumbuka hivi leo kwamba sio watoto wako walioona na kujua adhabu ya Bwana Mungu wako: utukufu wake, mkono wake wenye nguvu, mkono wake ulionyooshwa; 3ishara alizozifanya na mambo aliyoyafanya katikati ya Misri, kwa Farao mfalme wa Misri na kwa nchi yake yote; 411:4 Kut 15:1; 14:27; Hes 21:4lile alilolifanyia jeshi la Wamisri, farasi na magari yake, jinsi alivyowafurikisha na maji ya Bahari ya Shamu walipokuwa wakiwafuatilia ninyi, na jinsi Bwana alivyowaletea angamizo la kudumu juu yao. 5Sio watoto wenu walioyaona yale Mungu aliyowafanyia huko jangwani mpaka mkafika mahali hapa, 611:6 Hes 16:1-35; Za 106:16-18; Isa 24:19wala lile Mungu alilowafanyia Dathani na Abiramu, wana wa Eliabu wa kabila la Reubeni, wakati ardhi ilipofungua kinywa chake katikati ya Israeli yote, ikawameza pamoja na walio nyumbani mwao, hema zao na kila kitu kilichokuwa hai ambacho kilikuwa mali yao. 711:7 Kum 5:3Bali ilikuwa ni macho yenu wenyewe ambayo yaliyaona mambo haya yote makuu Bwana aliyoyatenda.

811:8 Ezr 9:10; Kum 31:6-7, 23; Yos 1:7Kwa hiyo fuateni maagizo yote ninayowapa leo, ili mpate kuwa na nguvu za kuingia na kuiteka nchi ile ambayo mnavuka Yordani kuimiliki, 911:9 Kum 5:16; 9:5; Kut 3:8; Mit 10:27; Kum 4:40; Mit 3:1, 26ili mpate kuishi siku nyingi katika nchi ile ambayo Bwana aliapa kuwapa baba zenu na wazao wao, nchi itiririkayo maziwa na asali. 1011:10 Isa 11:15; 37:25; Zek 8:7Nchi mnayoiingia kuimiliki haifanani na nchi ya Misri mlikotoka ambako mlipanda mbegu yenu na kuinywesha, kama bustani ya mboga. 1111:11 Eze 36:4; Kum 8:7; Neh 9:25Lakini nchi mnayovuka Yordani kuimiliki ni nchi ya milima na mabonde inywayo mvua kutoka mbinguni. 1211:12 1Fal 8:29; 9:3Ni nchi ambayo Bwana Mungu wenu anaitunza; macho ya Bwana Mungu wenu yanaitazama daima kutoka mwanzo wa mwaka hadi mwisho wa mwaka.

1311:13 Kum 6:17; 10:12; 4:29; Yer 17:24; 2The 3:5Hivyo kama mkiyatii maagizo yangu ninayowapa leo kwa uaminifu, yaani kwa kumpenda Bwana Mungu wenu, na kumtumikia kwa moyo wako wote na kwa roho yenu yote, 1411:14 Law 26:4; Mdo 14:17; Za 147:8; Yer 3:3; Yoe 2:23; Yak 5:7; Yer 5:24ndipo atawanyweshea mvua katika nchi yenu kwa majira yake, mvua ya masika na ya vuli, ili mpate kuvuna nafaka zenu, divai mpya na mafuta. 1511:15 Za 104:14; Law 26:5; Kum 6:11; Za 104:14; Yoe 2:19Nitawapa majani kwa ajili ya ngʼombe wenu, nanyi mtakula na kushiba.

1611:16 Kum 4:19; 8:19; 29:18; Ay 31:9; 27Jihadharini, la sivyo mtashawishika kugeuka na kuabudu miungu mingine na kuisujudia. 1711:17 Kum 6:15; 9:19; 1Fal 17:1; 2Nya 6:26; 7:13; Law 26:20; Kum 4:26; 28:12, 24Ndipo hasira ya Bwana itawaka dhidi yenu, naye atafunga mbingu ili mvua isinyeshe nayo ardhi haitatoa mazao, nanyi mtaangamia mara katika nchi nzuri ambayo Bwana anawapa. 1811:18 Kut 13:9; Kum 6:6-8Yawekeni haya maneno yangu katika mioyo yenu na akili zenu, yafungeni kama alama juu ya mikono yenu na kwenye paji za nyuso zenu. 1911:19 Kut 12:26; Kum 6:7; Za 145:4; Isa 38:19; Yer 32:39; Kum 4:9-10Wafundisheni watoto wenu, yazungumzeni wakati mketipo nyumbani na wakati mtembeapo njiani, wakati mlalapo na wakati mwamkapo. 2011:20 Kum 6:9; Hab 2:2Yaandikeni juu ya miimo ya nyumba zenu na juu ya malango yenu, 2111:21 Ay 5:26; Mit 3:2; 4:10; 9:11; Za 72:5ili kwamba siku zenu na siku za watoto wenu zipate kuwa nyingi katika nchi ile Bwana aliyoapa kuwapa baba zenu, kama zilivyo nyingi siku za mbingu juu ya nchi.

2211:22 Kum 6:17; 6:5; 10:20Kama mkishika kwa makini maagizo haya yote ninayowapa kuyafuata, ya kumpenda Bwana Mungu wenu, kuenenda katika njia zake zote na kushikamana naye kwa uthabiti, 2311:23 Kum 9:5; 4:38; Kut 23:28; Kum 9:1ndipo Bwana atawafukuza mataifa haya yote mbele yako, nawe utawafukuza mataifa yaliyo makubwa na yenye nguvu kukuliko wewe. 2411:24 Mwa 15:18; Kum 1:36; 12:20; 19:8; Yos 1:3; 14:9; Mwa 2:14Kila mahali mtakapoweka mguu wenu patakuwa penu: Nchi yenu itaenea kutoka jangwa la Lebanoni, na kutoka mto wa Frati hadi bahari ya magharibi11:24 Yaani Bahari ya Mediterania. 2511:25 Kum 2:25; Kut 23:27; Kum 7:24Hapatakuwa na mtu atakayeweza kusimama dhidi yenu. Bwana Mungu wenu, kama alivyoahidi, ataweka juu ya nchi yote utisho na hofu kwa ajili yenu popote mwendako.

2611:26 Za 24:5; Law 26:14-17; Kum 27:13-26; 30:1, 15, 19; Mao 2:17; Dan 9:11; Mal 3:9; 4:6Tazama, leo ninaweka mbele yenu baraka na laana: 2711:27 Kum 28:1-14; Za 24:5baraka kama mtatii maagizo ya Bwana Mungu wenu, ambayo ninawapa leo; 2811:28 2Nya 24:20; Yer 42:13; 44:16; Kum 4:28; 13:6-13; 29:26; 1Sam 26:19laana kama hamtatii maagizo ya Bwana Mungu wenu na kuacha njia ambayo ninawaamuru leo kwa kufuata miungu mingine, ambayo hamkuijua. 2911:29 Mwa 9:7; Kum 27:4; Yos 8:30; Kum 27:12-13; Yos 8:33; Yn 4:20Wakati Bwana Mungu wenu atakapokuwa amewaleta katika nchi mnayoiingia kuimiliki, mtatangaza baraka kutoka Mlima Gerizimu, na kutangaza laana kutoka Mlima Ebali. 3011:30 Mwa 12:6; Yos 4:19; 5:9; 9:6; 10:6; 14:6; 15:7; Amu 2:1; 2Fal 2:1; Mik 6:5; Hes 33:53; Kum 12:10; Yos 1:11; 11:23Kama mnavyofahamu, milima hii ipo ngʼambo ya Yordani, magharibi ya barabara, kuelekea machweo ya jua, karibu na miti mikubwa ya More, katika nchi ya wale Wakanaani wanaoishi Araba, jirani na Gilgali. 3111:31 Kum 28:1-14; Za 24:5Karibu mvuke ngʼambo ya Yordani kuingia na kuimiliki nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa. Wakati mtakapokuwa mmeichukua na mnaishi humo, 32hakikisheni kwamba mnatii amri na sheria zote ninazoziweka mbele yenu leo.

New International Version

Deuteronomy 11:1-32

Love and Obey the Lord

1Love the Lord your God and keep his requirements, his decrees, his laws and his commands always. 2Remember today that your children were not the ones who saw and experienced the discipline of the Lord your God: his majesty, his mighty hand, his outstretched arm; 3the signs he performed and the things he did in the heart of Egypt, both to Pharaoh king of Egypt and to his whole country; 4what he did to the Egyptian army, to its horses and chariots, how he overwhelmed them with the waters of the Red Sea11:4 Or the Sea of Reeds as they were pursuing you, and how the Lord brought lasting ruin on them. 5It was not your children who saw what he did for you in the wilderness until you arrived at this place, 6and what he did to Dathan and Abiram, sons of Eliab the Reubenite, when the earth opened its mouth right in the middle of all Israel and swallowed them up with their households, their tents and every living thing that belonged to them. 7But it was your own eyes that saw all these great things the Lord has done.

8Observe therefore all the commands I am giving you today, so that you may have the strength to go in and take over the land that you are crossing the Jordan to possess, 9and so that you may live long in the land the Lord swore to your ancestors to give to them and their descendants, a land flowing with milk and honey. 10The land you are entering to take over is not like the land of Egypt, from which you have come, where you planted your seed and irrigated it by foot as in a vegetable garden. 11But the land you are crossing the Jordan to take possession of is a land of mountains and valleys that drinks rain from heaven. 12It is a land the Lord your God cares for; the eyes of the Lord your God are continually on it from the beginning of the year to its end.

13So if you faithfully obey the commands I am giving you today—to love the Lord your God and to serve him with all your heart and with all your soul— 14then I will send rain on your land in its season, both autumn and spring rains, so that you may gather in your grain, new wine and olive oil. 15I will provide grass in the fields for your cattle, and you will eat and be satisfied.

16Be careful, or you will be enticed to turn away and worship other gods and bow down to them. 17Then the Lord’s anger will burn against you, and he will shut up the heavens so that it will not rain and the ground will yield no produce, and you will soon perish from the good land the Lord is giving you. 18Fix these words of mine in your hearts and minds; tie them as symbols on your hands and bind them on your foreheads. 19Teach them to your children, talking about them when you sit at home and when you walk along the road, when you lie down and when you get up. 20Write them on the doorframes of your houses and on your gates, 21so that your days and the days of your children may be many in the land the Lord swore to give your ancestors, as many as the days that the heavens are above the earth.

22If you carefully observe all these commands I am giving you to follow—to love the Lord your God, to walk in obedience to him and to hold fast to him— 23then the Lord will drive out all these nations before you, and you will dispossess nations larger and stronger than you. 24Every place where you set your foot will be yours: Your territory will extend from the desert to Lebanon, and from the Euphrates River to the Mediterranean Sea. 25No one will be able to stand against you. The Lord your God, as he promised you, will put the terror and fear of you on the whole land, wherever you go.

26See, I am setting before you today a blessing and a curse— 27the blessing if you obey the commands of the Lord your God that I am giving you today; 28the curse if you disobey the commands of the Lord your God and turn from the way that I command you today by following other gods, which you have not known. 29When the Lord your God has brought you into the land you are entering to possess, you are to proclaim on Mount Gerizim the blessings, and on Mount Ebal the curses. 30As you know, these mountains are across the Jordan, westward, toward the setting sun, near the great trees of Moreh, in the territory of those Canaanites living in the Arabah in the vicinity of Gilgal. 31You are about to cross the Jordan to enter and take possession of the land the Lord your God is giving you. When you have taken it over and are living there, 32be sure that you obey all the decrees and laws I am setting before you today.