Kumbukumbu 10 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Kumbukumbu 10:1-22

Vibao Vingine Vya Amri Kumi

(Kutoka 34:1-10)

110:1 Kut 34:2; 25:10Wakati ule Bwana aliniambia, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza uje kwangu juu mlimani. Pia utengeneze Sanduku la mbao. 210:2 Kut 25:16, 21; 2Nya 5:10; 6:11Nitaandika juu ya vibao maneno yaliyokuwa katika vile vibao vya kwanza, ambavyo ulivivunja. Kisha utaviweka ndani ya Sanduku.”

310:3 Kut 37:1-9; 34:4; 26:5Hivyo nikatengeneza Sanduku kwa mti wa mshita, nikachonga pia vibao vya mawe kama vile vya kwanza, kisha nikakwea mlimani nikiwa na vibao viwili mikononi mwangu. 410:4 Kut 24:12; 34:28; 20; 1; Kum 9:10; Yer 31:33Bwana akaandika juu ya hivi vibao kile alichokuwa amekiandika kabla, Amri Kumi alizokuwa amewatangazia juu mlimani, kutoka kwenye moto siku ile ya kusanyiko. Bwana akanikabidhi. 510:5 Kut 19:11; 25:10; 25:21; 34:29; 40:21; 1Sam 8:3; 1Fal 8:9Kisha nikashuka kutoka mlimani na kuweka vibao ndani ya Sanduku nililokuwa nimelitengeneza, kama Bwana alivyoniagiza, navyo viko huko sasa.

610:6 Hes 33:30; 27:13; 20:25-28; Kut 6:23(Waisraeli walisafiri kutoka visima vya Yaakani hadi Mosera. Huko Aroni alifariki na kuzikwa, naye Eleazari mwanawe akachukua nafasi yake kama kuhani. 710:7 Hes 33:32-34; Za 42:1; Wim 5:12; Isa 32:2Kutoka pale, walisafiri hadi Gudgoda wakaendelea mpaka Yotbatha, nchi yenye vijito vya maji. 810:8 Hes 3:6; 10:33; 16:9; Mwa 48:20; 1Nya 23:26; Kum 18:5; 21:5; Law 9:22Wakati huo Bwana aliteua kabila la Lawi kulibeba Sanduku la Agano la Bwana, kusimama mbele za Bwana ili kutoa huduma, na kutangaza baraka kwa Jina lake, kama wanavyofanya mpaka leo. 910:9 Hes 18:20; Eze 44:28Hiyo ndiyo sababu ya Walawi kutokuwa na sehemu wala urithi miongoni mwa ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama Bwana Mungu wao alivyowaambia.)

1010:10 Kut 33:17; 34:28; Kum 9:18-19; 25Basi nilikaa mlimani kwa siku arobaini usiku na mchana, kama nilivyofanya mara ya kwanza, pia Bwana alinisikiliza hata wakati huu. Haikuwa nia yake kuwaangamiza. 11Bwana akaniambia, “Nenda, ukawaongoze watu katika njia yao ili kwamba waweze kuingia na kuimiliki nchi ile niliyowaapia baba zao kuwapa.”

Mche Bwana

1210:12 Mik 6:8; Kut 20:20; 1Fal 2:3; 3:3; 4:4; Kum 5:32; 5:33; 6:13; 6:5; 11:13; 28:47; Mt 22:37; 1Tim 1:5; Za 100:2; Kum 6:5; Za 119:2; Kum 5:32Na sasa, ee Israeli, Bwana Mungu wako anataka nini kwako ila kumcha Bwana Mungu wako, kwenda katika njia zake, kumpenda na kumtumikia Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote, 1310:13 Kum 4:2; 5:33; 6:25na kuyashika maagizo ya Bwana na amri zake ninazokupa leo kwa mafanikio yako mwenyewe?

1410:14 Za 148:4; Isa 19:1; Hab 3:8; Neh 9:6; Ay 35:5; Za 8:3; 89:11; 104:3; Kum 33:26; Za 115:16; 1Fal 8:27; Kut 19:5; Za 24:1; Mdo 17:24Mbingu, hata mbingu za juu sana, dunia na kila kitu kilichomo ndani yake, ni mali ya Bwana Mungu wako. 1510:15 Kum 4:37; Za 105:6; 135:4; Hes 14:8; Rum 11:28; 1Pet 2:9Hata hivyo Bwana alikuwa na shauku na baba zako, akawapenda na akawachagua ninyi, wazao wao, kuliko mataifa yote, kama ilivyo leo. 1610:16 Mwa 17:11; Law 26:41; Kum 30:6; Yer 32:39; Kut 32:9; 9:13; Yer 4:4; Kum 9:6Kwa hiyo tahirini mioyo yenu, na msiwe na shingo ngumu tena. 1710:17 Yos 22:22; Za 135:9; 136:2; Dan 2:47; 11:36; Za 136:3; 1Tim 6:15; Kum 7:21; 1:17; Mal 2:9; Kut 23:8; Law 19:16; Efe 6:9Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni Mungu wa miungu na Bwana wa mabwana, Mungu mkuu, mwenye uweza na wa kutisha, ambaye hana upendeleo na hapokei rushwa. 1810:18 Kut 22:21, 22-24; 23:9; Law 19:33; Kum 27:19; Ay 29:13; Za 94:6; Isa 10:2; Yer 49:11; Hes 10:32Huwapigania yatima na wajane, humpenda mgeni, akimpa chakula na mavazi. 1910:19 Kum 7:12; Kut 22:21; Kum 24:19; Law 19:34; Eze 47:22-23Nanyi wapendeni wageni, kwa kuwa ninyi wenyewe mlikuwa wageni huko Misri. 2010:20 Mt 4:10; Kum 11:22; 13:4; 30:20; Yos 23:8; Rut 1:14; 2Fal 18:6; Za 119:31; Isa 38:3; Kut 20:7; Za 63:11Mche Bwana Mungu wako na umtumikie yeye. Shikamana naye kwa uthabiti na kuapa kwa jina lake. 2110:21 Kut 15:2; 1Sam 12:24; Za 126:2; 2Sam 7:23; Yer 17:14; Za 106:21-22Yeye ni sifa yako; yeye ni Mungu wako, ambaye alikutendea yale maajabu makubwa na ya kutisha uliyoyaona kwa macho yako mwenyewe. 2210:22 Mwa 34:30; 46:26; Mdo 7:14; Mwa 12:2; Hes 10:36Baba zako walioshuka kwenda Misri jumla yao walikuwa sabini, na sasa Bwana Mungu wako amekufanya wengi kama nyota za angani.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

申命记 10:1-22

摩西重新接受诫命

1“当时耶和华对我说,‘你要凿出两块石版,与前两块一样,也要做一个木柜,然后上山来见我。 2我要把你摔碎的那两块石版上的话重新写在你凿的石版上。你要把它们放在柜子里。’ 3于是,我用皂荚木做了一个柜子,又凿出两块石版,与前两块一样,然后带着石版上了山。 4耶和华把你们在山脚下聚会时,祂在山上的火焰中向你们颁布的十条诫命,重新刻在石版上,并把石版交给我。 5我下山后,遵照耶和华的吩咐把石版放在我做的柜子里。现在石版仍放在那里。

6“我们从亚干人的井10:6 “亚干人的井”或译“比罗比尼·亚干”或“比尼亚干井”。出发,来到摩西拉亚伦死在那里,并葬在那里,他儿子以利亚撒接替他做大祭司。 7我们从那里走到谷歌大,又走到溪流之乡约巴他8那时,耶和华把利未支派分别出来,派他们抬祂的约柜,侍立在祂面前事奉祂,奉祂的名祝福,至今未变。 9因此,利未人在众支派中没有分到土地作产业,耶和华是他们的产业,这是你们的上帝耶和华对他们的应许。

10“和前一次一样,我又在山上待了四十昼夜,耶和华又听了我的祈求,答应不毁灭你们。 11耶和华对我说,‘起来,带民众走吧,去占领我起誓要赐给他们祖先的土地。’

耶和华的要求

12以色列人啊,你们的上帝耶和华对你们有何要求?无非要你们敬畏祂,遵行祂的旨意,爱祂,全心全意地事奉祂, 13遵守祂的诫命和律例。我今天把这些诫命和律例赐给你们,是为了你们的益处。 14看啊,天和天上的天、大地和地上的万物,都属于你们的上帝耶和华。 15但耶和华只喜爱你们的祖先,从万族中拣选了他们的后裔——你们,正如今日的情形。 16所以,你们要洗心革面,不可再顽固不化。 17你们的上帝耶和华是万神之神、万主之主,是伟大、全能、可畏的上帝。祂不徇情面,不受贿赂; 18祂为孤儿寡妇主持公道,关爱寄居者,供给他们衣食。 19所以,你们要爱寄居者,因为你们也曾寄居埃及20你们要敬畏你们的上帝耶和华,事奉祂,倚靠祂,凭祂的名起誓。 21你们要赞美祂,祂是你们的上帝,你们亲眼目睹了祂为你们做的伟大而可畏的事。 22当年你们祖先下埃及时,只有七十人,现在你们的上帝耶和华使你们多如天上的星辰。