Dhambi, Toba Na Ukombozi
159:1 Hes 11:23; Isa 50:2; 30:19; 41:20; 58:9; 65:24Hakika mkono wa Bwana si mfupi hata usiweze kuokoa,
wala sikio lake si zito hata lisiweze kusikia.
259:2 Za 18:41; Yn 9:31; Yer 11:11; Isa 58:4; Eze 39:23; Yer 5:25Lakini maovu yenu yamewatenga
ninyi na Mungu wenu,
dhambi zenu zimewaficha ninyi uso wake,
ili asisikie.
359:3 2Fal 21:16; Eze 22:9; Rum 3:15; Isa 1:15; Za 7:3; Isa 3:8Kwa maana mikono yenu imetiwa mawaa kwa damu
na vidole vyenu kwa hatia.
Midomo yenu imenena uongo,
nazo ndimi zenu zimenongʼona mambo maovu.
459:4 Za 7:14; Yak 1:15; Isa 5:23; Ay 15:31; Isa 44:20; 29:20; Ay 4:8Hakuna hata mmoja anayedai kwa haki;
hakuna hata mmoja anayetetea shauri lake kwa haki.
Wanategemea mabishano matupu na kusema uongo,
huchukua mimba ya magomvi na kuzaa uovu.
559:5 Ay 8:14; Mt 3:7; Isa 11:8Huangua mayai ya nyoka wenye sumu kali
na kutanda wavu wa buibui.
Yeyote alaye mayai yao atakufa,
na wakati moja lianguliwapo, nyoka hutoka humo.
659:6 Isa 28:20; Mit 4:17; Za 55:9; Isa 58:4Utando wao wa buibui haufai kwa nguo;
hawawezi kujifunika kwa kile walichokitengeneza.
Matendo yao ni matendo maovu,
vitendo vya jeuri vipo mikononi mwao.
759:7 2Fal 21:16; Mik 3:10; Mit 6:17; Rum 3:15-17; Mk 7:21-22Miguu yao hukimbilia kwenye dhambi,
ni myepesi kumwaga damu isiyo na hatia.
Mawazo yao ni mawazo maovu;
uharibifu na maangamizi huonekana katika njia zao.
859:8 Mit 2:15; Isa 57:21; Lk 1:79; Amu 5:6; Rum 3:15-17Hawajui njia ya amani,
hakuna haki katika mapito yao.
Wameyageuza kuwa njia za upotovu,
hakuna apitaye njia hizo atakayeifahamu amani.
959:9 Yer 8:15; Ay 19:8; Za 107:14; Isa 5:30; 8:20; Lk 1:79Hivyo uadilifu uko mbali nasi,
nayo haki haitufikii.
Tunatazamia nuru, kumbe! Yote ni giza,
tunatazamia mwanga, lakini tunatembea katika giza kuu.
1059:10 Mao 4:14; Sef 1:17; Ay 3:23; Yn 11:10; Kum 28:29; Isa 6:9-10; Mao 3:6Tunapapasa ukuta kama kipofu,
tunapapasa katika njia zetu kama watu wasio na macho.
Adhuhuri tunajikwaa kama wakati wa gizagiza;
katikati ya wenye nguvu, tuko kama wafu.
1159:11 Eze 7:16Wote tunanguruma kama dubu;
tunalia kwa maombolezo kama hua.
Tunatafuta haki, kumbe hakuna kabisa;
tunatafuta wokovu, lakini uko mbali.
1259:12 Ezr 9:6; Yer 2:19; Mwa 4:7; Isa 57; 12; 3:9; Yer 51:3Kwa sababu makosa yetu ni mengi machoni pako,
na dhambi zetu zinashuhudia dhidi yetu.
Makosa yetu yako pamoja nasi daima,
nasi tunayatambua maovu yetu:
1359:13 Hes 11:20; Za 12:5; Mt 12:34; Mk 7:21-22; Mit 30; 9; Tit 1:16; Isa 48:8Uasi na udanganyifu dhidi ya Bwana,
kumgeuzia Mungu wetu kisogo,
tukichochea udhalimu na maasi,
tukinena uongo ambao mioyo yetu imeuhifadhi.
1459:14 Neh 8:1; Isa 48:1; Yer 33:16; Isa 29:21; 1:21Hivyo uadilifu umerudishwa nyuma,
nayo haki inasimama mbali,
kweli imejikwaa njiani,
uaminifu hauwezi kuingia.
1559:15 Yer 7:28; Dan 8:12; Isa 5:7Kweli haipatikani popote,
na yeyote aepukaye uovu huwa mawindo.
Bwana alitazama naye akachukizwa
kwamba hapakuwepo haki.
1659:16 Isa 41:28; 65:3; Za 98:1; Isa 53:12; 46:13Aliona kuwa hakuwepo hata mtu mmoja,
akashangaa kwamba hakuwepo hata mmoja wa kuingilia kati;
hivyo mkono wake mwenyewe
ndio uliomfanyia wokovu,
nayo haki yake mwenyewe
ndiyo iliyomtegemeza.
1759:17 Efe 6:14; 1The 5:8; Ay 27:6; Eze 5:13; Efe 6:17; Isa 63:3Alivaa haki kama dirii kifuani mwake,
na chapeo ya wokovu kichwani mwake,
alivaa mavazi ya kisasi
naye akajifunga wivu kama joho.
1859:18 Hes 10:35; Isa 34:8; Mt 16:27Kulingana na kile walichokuwa wametenda,
ndivyo atakavyolipa
ghadhabu kwa watesi wake
na kisasi kwa adui zake,
atavilipa visiwa sawa na wanavyostahili.
1959:19 Isa 49:12; Za 113:3; Ufu 12:15; Mt 8:11; Za 97:6Kuanzia magharibi, watu wataliogopa jina la Bwana
na kuanzia mawio ya jua, watauheshimu utukufu wake.
Wakati adui atakapokuja kama mafuriko,
Roho wa Bwana atainua kiwango dhidi yake na kumshinda.
2059:20 Yer 35:15; Mdo 2:38-39; Rum 11:26; Ay 19:25; Isa 52:8; Yoe 3:21; Yer 35:15“Mkombozi atakuja Sayuni,
kwa wale wa Yakobo
wanaozitubu dhambi zao,”
asema Bwana.
2159:21 Isa 44:3; Ebr 8:10; Eze 36:37; Mwa 9:16; Kum 29:14; Isa 42:6; Kut 4:15“Kwa habari yangu mimi, hili ndilo agano langu nao,” asema Bwana. “Roho wangu, aliye juu yenu, na maneno yangu ambayo nimeyaweka katika vinywa vyenu, havitaondoka vinywani mwenu, wala kutoka vinywani mwa watoto wenu, wala kutoka vinywani mwa wazao wao, kuanzia sasa na hata milele,” asema Bwana.
因罪與主隔絕
1看啊,耶和華的臂膀並非無力拯救,
祂的耳朵並非聾得聽不見。
2而是你們的罪過使你們與上帝隔絕,
你們的罪惡使祂轉臉不看你們,
不聽你們的祈求。
3你們的手染滿了血污,
手指沾滿了罪惡。
你們的嘴唇吐出謊言,
舌頭嘀咕惡事。
4無人按公義訴訟,
無人憑誠實申辯。
你們全憑虛言,謊話連篇,
心懷惡意,生出罪惡。
5你們孵毒蛇蛋,
人吃了這蛋必死,
蛋打破後爬出毒蛇。
你們編蜘蛛網,
6這網不能做衣服,
你們無法用所製作的遮蓋自己。
你們行為邪惡,
做事殘暴。
7你們的腳奔向邪惡,
急於濫殺無辜;
你們心懷惡念,
所到之處,大肆毀滅。
8你們不知道平安之路,
你們的行徑毫無公正;
你們走歪門邪道,
跟從你們的必不知何為平安。
9因此,正義遠離我們,
公義臨不到我們。
我們渴望光明,卻得到黑暗;
我們渴望曙光,卻仍然走在幽暗中。
10我們像盲人一樣沿牆摸索,
像無眼睛的人一樣探路。
我們在中午也跌跌撞撞,
如同走在晚上。
我們在強壯人當中如同死人。
11我們都像熊一樣咆哮,
如鴿子一般哀鳴。
我們渴望正義,卻得不到;
渴望得到拯救,卻遙不可及。
12因為我們在上帝面前過犯纍纍,
我們的罪惡向我們發出控訴。
我們被過犯纏身,自知有罪。
13我們悖逆,否認耶和華,
離棄我們的上帝,
說欺壓、叛逆的話,
吐露心中編織的謊言。
14正義被趕逐,
公義遠遠站立,
真理倒在街上,
正直被拒之門外。
15真理無處可尋,
遠離惡事的人反成了獵物。
耶和華見正義蕩然無存,感到不悅。
16祂因無人、
無一個人主持公道而驚訝,
就用自己的臂膀施行拯救,
用自己的公義維繫。
17祂以公義作鎧甲,
以救恩作頭盔,
以復仇作衣服,
以熱忱作外袍。
18祂必按各人的行為報應各人,
向祂的敵人發烈怒,
報復祂的仇敵,
向眾海島施行報應。
19這樣,日落之處的人必敬畏耶和華的名,
日出之地的人必對祂的榮耀肅然起敬。
祂必如耶和華之氣推動的急流一樣奔來。
20耶和華說:「必有一位救贖主來到錫安,
到雅各那些離棄罪惡的子孫那裡。」
21耶和華說:「這是我與他們所立的約:我賜給他們的靈和我放在他們口中的話,必不離開他們和他們的子子孫孫,從現在直到永遠。這是耶和華說的。」