Isaya 58 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Isaya 58:1-14

Mfungo Wa Kweli

158:1 Isa 24:20; 40:6; 48:8; Eze 3:17; Isa 57:12“Piga kelele, usizuie.

Paza sauti yako kama tarumbeta.

Watangazieni watu wangu uasi wao,

na kwa nyumba ya Yakobo dhambi zao.

258:2 Isa 29:13; Yak 4:8Kwa maana kila siku hunitafuta,

wanaonekana kutaka kujua njia zangu,

kana kwamba walikuwa taifa linalotenda lililo sawa,

na ambalo halijaziacha amri za Mungu wake.

Hutaka kwangu maamuzi ya haki,

nao hutamani Mungu awakaribie.

358:3 Law 16:29; Mal 3:14; Zek 7:5-6; Kut 10:3; 2Nya 6:37; Yer 44:10; Isa 22:13Wao husema, ‘Mbona tumefunga, nawe hujaona?

Mbona tumejinyenyekeza, nawe huangalii?’

“Lakini katika siku ya kufunga kwenu, mnafanya mnavyotaka

na kuwadhulumu wafanyakazi wenu wote.

458:4 Mal 2:16; Mao 3:44; Mik 3:4; 1Fal 21:9-13; Isa 59:6; Eze 7:11; 8:18; 1Sam 8:18Kufunga kwenu huishia kwenye magomvi na mapigano,

na kupigana ninyi kwa ninyi kwa ngumi za uovu.

Hamwezi kufunga kama mnavyofanya leo

na kutazamia sauti zenu kusikiwa huko juu.

558:5 Zek 7:5; 1Fal 21:27; Mt 6:16; Ay 2:8; Isa 36:6Je, hii ndiyo aina ya mfungo niliouchagua,

siku moja tu ya mtu kujinyenyekeza?

Je, ni kwa kuinamisha kichwa chini kama tete,

na kwa kujilaza juu ya nguo ya gunia na majivu?

Je, huo ndio mnaouita mfungo,

siku iliyokubalika kwa Bwana?

658:6 Neh 5:10-11; Kum 14:29; Lk 4:19; Yoe 2:12-13; Yer 34:9; Amo 4:1; Isa 9:4“Je, hii si ndiyo aina ya mfungo niliyoichagua:

kufungua minyororo ya udhalimu,

na kufungua kamba za nira,

kuwaweka huru walioonewa,

na kuvunja kila nira?

758:7 Ay 22:7; Dan 4:27; Ebr 13:12; Ay 31:19-20; Mwa 29:14; Mt 25:36; Eze 18:16Je, sio kushirikiana chakula chako na wenye njaa

na kuwapatia maskini wasiokuwa na makao hifadhi,

unapomwona aliye uchi, umvike,

wala si kumkimbia mtu wa nyama na damu yako mwenyewe?

858:8 Isa 9:2; 30:26; Kut 14:19; Ay 11:17; Isa 26:2Ndipo nuru yako itajitokeza kama mapambazuko

na uponyaji wako utatokea upesi;

ndipo haki yako itakapokutangulia mbele yako,

na utukufu wa Bwana utakuwa mlinzi nyuma yako.

958:9 Mit 6:13; Za 50:12; 12:2; Isa 59:13; Ay 8:6; Dan 9:20; Zek 10:6Ndipo utaita, naye Bwana atajibu,

utalia kuomba msaada,

naye atasema: Mimi hapa.

“Kama ukiiondoa nira ya udhalimu,

na kunyoosha kidole na kuzungumza maovu,

1058:10 Kum 15:7-8; Ay 11:17; Isa 42:16nanyi kama mkimkunjulia mtu mwenye njaa nafsi zenu

na kutosheleza mahitaji ya walioonewa,

ndipo nuru yenu itakapongʼaa gizani,

nao usiku wenu utakuwa kama adhuhuri.

1158:11 Za 104:28; Wim 4:15; Yn 4:14; Za 48:14; Isa 42:16; 48:7; Za 68:1; 72:6Bwana atakuongoza siku zote,

atayatosheleza mahitaji yako katika nchi kame,

naye ataitia nguvu mifupa yako.

Utakuwa kama bustani iliyonyweshwa vizuri,

kama chemchemi ambayo maji yake hayakauki kamwe.

12Watu wako watajenga tena magofu ya zamani

na kuinua misingi ya kale;

utaitwa Mwenye Kukarabati Kuta Zilizobomoka,

Mwenye Kurejeza Barabara za Makao.

1358:13 Law 19:20; Kut 20:8; Za 37:4; Isa 56:2“Kama ukitunza miguu yako isivunje Sabato,

na kutokufanya kama vile upendavyo katika siku yangu takatifu,

kama ukiita Sabato siku ya furaha

na siku takatifu ya Bwana ya kuheshimiwa,

kama utaiheshimu kwa kutoenenda

katika njia zako mwenyewe,

na kutokufanya yakupendezayo

au kusema maneno ya upuzi,

1458:14 Ay 22:26; Kum 32:13; Isa 1:20; Za 105:10-11ndipo utakapojipatia furaha yako katika Bwana,

nami nitakufanya upande juu ya miinuko ya nchi

na kusherehekea urithi wa Yakobo baba yako.”

Kinywa cha Bwana kimenena haya.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

以賽亞書 58:1-14

真正的虔誠

1「你要高聲呼喊,不要停止;

要放聲高呼,像響亮的號角。

要向我的子民宣告他們的過犯,

雅各家宣告他們的罪惡。

2他們天天尋求我,

樂於認識我的道,

像沒有丟棄他們上帝法令的正義之邦。

他們向我求公義的判決,

似乎樂於到我面前。

3他們說,『我們禁食,你為什麼不看呢?

我們刻苦己身,你為什麼不理睬呢?』

我說,『看啊,禁食之日你們仍然隨心所欲,

壓榨你們的工人。

4你們一面禁食,一面爭鬧打鬥,惡拳相向。

今天這種禁食不能使你們的禱告在高天蒙垂聽。

5難道這是我要的讓人刻苦己身的禁食日嗎?

難道像蘆葦一樣垂著頭、

躺在麻布和爐灰上就是禁食嗎?

這就是你們所謂的禁食,

所謂的蒙耶和華悅納的日子嗎?

6「『我要的禁食豈不是,

除去邪惡的鎖鏈,

解開軛上的繩索,

折斷一切的軛,

使受欺壓的人得到自由嗎?

7豈不是把你們的食物分給饑餓的人,

接待無家可歸的窮人,

送衣服給赤身露體的人,

不躲避求助的親人嗎?

8如果你們這樣做,你們的光必如晨光照耀,

你們的創傷必迅速痊癒,

你們的公義必在前引路,

耶和華的榮耀必在後面保護你們。

9你們求告,耶和華必應允;

你們呼求,耶和華必回應。

如果你們不再欺壓、指責和譭謗,

10如果你們給饑餓的人食物,

使困苦的人得飽足,

你們的光必照亮黑暗,

你們的黑夜必變成正午。

11耶和華必不斷地引導你們,

使你們在乾旱之地得到飽足,筋骨強健。

你們必像灌溉充足的園子,

又像湧流不息的泉源。

12你們必重修古老的荒場,

重建遠古的根基。

你們必被稱為修補斷垣、

重建居民街道的人。

13「『如果你們遵守安息日,

在我的聖日不做私事,

以安息日為樂,

尊崇耶和華的聖日,

不隨意行事,

不妄自說話,

14就必以耶和華為樂,

耶和華必使你們在地上受尊崇,

並享用你們先祖雅各的產業。』」

這是耶和華親口說的。