Isaya 54 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Isaya 54:1-17

Utukufu Wa Baadaye Wa Sayuni

154:1 Isa 49:20; Gal 4:27; Mwa 21:6; Za 98:4; Isa 66:7; 49:20“Imba, ewe mwanamke tasa,

wewe ambaye kamwe hukuzaa mtoto;

paza sauti kwa kuimba, piga kelele kwa furaha,

wewe ambaye kamwe hukupata utungu;

kwa sababu watoto wa mwanamke aliyeachwa ukiwa ni wengi

kuliko wa mwanamke mwenye mume,”

asema Bwana.

254:2 Mwa 26:22; Isa 26:15; Kut 35:18; 39:40; Isa 49:19-20“Panua mahali pa hema lako,

tandaza mapazia ya hema lako uyaeneze mbali,

wala usiyazuie;

ongeza urefu wa kamba zako,

imarisha vigingi vyako.

354:3 Mwa 13:14; Isa 48:19; Ay 12:23; Isa 14:2; 60:4-11; 49:19Kwa maana utaenea upande wa kuume

na upande wa kushoto;

wazao wako watayamiliki mataifa

na kukaa katika miji yao iliyoachwa ukiwa.

454:4 Isa 30:10; Yoe 2:21; Isa 28:16; Mwa 30:23; Za 25:7; 119:39; Yer 22:21; Isa 47:8“Usiogope, wewe hutaaibika.

Usiogope aibu, wewe hutaaibishwa.

Wewe utasahau aibu ya ujana wako,

wala hutakumbuka tena mashutumu ya ujane wako.

554:5 Wim 3:3; Isa 41:14; 48:17; Rum 3:29; Hos 2:7-16; Za 149:2; Isa 51:13Kwa maana Muumba wako ndiye mume wako,

Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake,

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli ni Mkombozi wako,

yeye anaitwa Mungu wa dunia yote.

654:6 Isa 49:14-21; 60:15; 62:4; Yer 44:2; Hos 1:10; Kut 20:14; Mal 2:14Bwana atakuita urudi

kana kwamba ulikuwa mke aliyeachwa na kuhuzunishwa rohoni;

kama mke aliyeolewa bado angali kijana

na kukataliwa,” asema Mungu wako.

754:7 Ay 14:13; Isa 26:20; 2Kor 4:17; Isa 27:8; Za 71:11; Isa 49:18“Kwa kitambo kidogo nilikuacha,

lakini kwa huruma nyingi nitakurudisha.

854:8 Isa 9:12; Yer 31:3; Za 92:2; Isa 26:20; Za 25:6; Isa 55:3; 63:7; Hos 2:19Katika ukali wa hasira

nilikuficha uso wangu kwa kitambo,

lakini kwa fadhili za milele

nitakuwa na huruma juu yako,”

asema Bwana Mkombozi wako.

954:9 Mwa 8:21; Mik 7:18; Eze 39:29; Isa 14:24; Kum 28:20; Isa 49:18“Kwangu mimi jambo hili ni kama siku za Noa,

nilipoapa kuwa maji ya Noa kamwe hayatafunika tena dunia.

Hivyo sasa nimeapa sitawakasirikia ninyi,

kamwe sitawakemea tena.

1054:10 Za 46:2; Ebr 12:27; Mwa 9:16; Kut 34:10; Ufu 6:14; Hes 25:12; Isa 55:7Ijapotikisika milima, na vilima viondolewe,

hata hivyo upendo wangu usiokoma kwenu hautatikisika,

wala agano langu la amani halitaondolewa,”

asema Bwana, mwenye huruma juu yenu.

1154:11 Isa 14:32; 29:6; 1Nya 29:2; Ufu 21:18; 21:19-20; Isa 26:18; 28:16; Kut 24:10“Ewe mji uliyeteswa, uliyepigwa kwa dhoruba na usiyetulizwa,

nitakujenga kwa almasi, nitaweka misingi yako kwa yakuti samawi.

1254:12 Ufu 21:21Nitafanya minara yako ya akiki,

malango yako kwa vito vingʼaavyo,

nazo kuta zako zote za vito vya thamani.

1354:13 Mik 4:2; Ebr 8:11; Law 26:6; Isa 11:9; 28:9; 48:18; Yn 6:45Watoto wako wote watafundishwa na Bwana,

nayo amani ya watoto wako itakuwa kuu.

1454:14 2Sam 7:10; Isa 9:4; 17:14; 26:2; Yer 30:20; Sef 3:17; Zek 9:8Kwa haki utathibitika:

Kuonewa kutakuwa mbali nawe;

hutaogopa chochote.

Hofu itakuwa mbali nawe;

haitakukaribia wewe.

1554:15 Isa 41:11-16Kama mtu yeyote akikushambulia,

haitakuwa kwa ruhusa yangu;

yeyote akushambuliaye

atajisalimisha kwako.

1654:16 Isa 44:12; 10:5; 13:5“Tazama, ni mimi niliyemuumba mhunzi,

yeye afukutaye makaa kuwa moto,

na kutengeneza silaha inayofaa kwa kazi yake.

Tena ni mimi niliyemwambia mharabu

kufanya uharibifu mwingi.

1754:17 Isa 29:8; Mdo 6:10; Isa 45:24-25; 41:11; 56:6-8; Zek 1:20-21; Isa 65:8-9Hakuna silaha itakayofanyizwa dhidi yako

itakayofanikiwa,

nawe utauthibitisha kuwa mwongo

kila ulimi utakaokushtaki.

Huu ndio urithi wa watumishi wa Bwana

na hii ndiyo haki yao itokayo kwangu,”

asema Bwana.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

以賽亞書 54:1-17

主愛不移

1耶和華說:「不生育、未生養的婦人啊,要歡唱;

未曾生產的女子啊,

要歡呼高歌;

因為沒有丈夫的比有丈夫的兒女更多。

2要擴大你支帳篷的地方,

儘量鋪開帳篷的幔子,

放長繩子,釘牢橛子。

3因為你要向左右擴展,

你的後裔要佔據列國,

使荒涼的城邑重新有人居住。

4「不要害怕,因為你不會再受羞辱;

不要恐懼,因為你不會再受凌辱。

你必忘記年輕時的羞辱,

不再想起寡居時的恥辱。

5因為造你的是你的丈夫,

祂名叫萬軍之耶和華;

你的救贖主是以色列的聖者,

祂被稱為普天下的上帝。

6耶和華要召你回來,

如同召一個遭遺棄、

心中憂傷的少妻。

這是你的上帝說的。

7我丟棄了你片刻,

但我要懷著極大的憐憫接你回來。

8我盛怒之下暫時掩面不理你,

但我要以永遠不變的慈愛憐憫你。

這是你的救贖主耶和華說的。

9「這對我而言就像挪亞的時代,

我怎樣起誓不再讓挪亞時代的洪水淹沒大地,

我也照樣起誓不再向你發怒,

也不再斥責你。

10大山可以挪開,

小山可以遷移,

但我的慈愛必不離開你,

我平安的約也不會更改。

這是憐憫你的耶和華說的。

11「困苦不堪、飽經風雨、

得不著安慰的城啊,

我要以彩石作你的地基,

用藍寶石建造你的根基,

12用紅寶石建你的城樓、

水晶造你的城門、

寶石建你的城牆。

13你的兒女都必受耶和華的訓誨,

安享太平。

14你必因公義而堅立,

再不會受欺壓,

也不會擔驚受怕,

因為恐懼不會臨近你。

15倘若有人來攻打你,

那必不是我的旨意。

攻打你的必然失敗。

16看啊,是我造了煽旺炭火、

鑄造合用兵器的鐵匠,

是我造了毀滅者。

17為攻擊你而造的兵器必不能奏效,

你必駁倒所有控告你的人。

這是耶和華眾僕人的產業,

是我給他們的勝利54·17 「勝利」或譯「公義」。

這是耶和華說的。」