Anguko La Babeli
147:1 Mao 2:10; Isa 21:9; 23:12; Yer 51:33; Zek 2:7; Ay 2:13; Isa 29:4“Shuka uketi mavumbini,
ee Bikira Binti Babeli;
keti chini pasipo na kiti cha enzi,
ee binti wa Wakaldayo.
Hutaitwa tena mwororo wala wa kupendeza.
247:2 Mt 24:41; Kut 11:5; Amu 16:21; Mwa 24:65; Isa 32:11Chukua mawe ya kusagia, usage unga,
vua shela yako.
Pandisha mavazi yako, ondoa viatu vyako,
vuka vijito kwa shida.
347:3 Mwa 2:25; Rum 12:19; Neh 3:5; Isa 13:18-19; 20:4; 34:8; Eze 16:37Uchi wako utafunuliwa
na aibu yako itaonekana.
Nitalipa kisasi;
sitamhurumia hata mmoja.”
447:4 Yer 50:34; Amo 4:13; Isa 48:2, 17; Ay 19:25Mkombozi wetu: Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake;
ndiye yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
547:5 Dan 2:37; Isa 13:10, 19; 9:2; 21:9; Ufu 17:18; Ay 2:13; Ufu 18:7“Keti kimya, ingia gizani,
Binti wa Wakaldayo,
hutaitwa tena malkia wa falme.
647:6 2Nya 28:9; Isa 10:13; Zek 1:15; Kum 13:15; Yer 50:11; Isa 14:6; 42:24Niliwakasirikia watu wangu
na kuaibisha urithi wangu;
niliwatia mikononi mwako,
nawe hukuwaonea huruma.
Hata juu ya wazee
uliweka nira nzito sana.
747:7 Ufu 18:7; Kum 32:29; Isa 10:13; Dan 4:30; Isa 42:23-25Ukasema, ‘Nitaendelea
kuwa malkia milele!’
Lakini hukutafakari mambo haya
wala hukuwaza juu ya kile kingeweza kutokea.
847:8 Isa 32:9; 45:6; 49:21; 54:4; Sef 2:15; Ufu 18:7“Sasa basi, sikiliza, ewe kiumbe mpenda anasa,
ukaaye mahali pako pa salama,
na kujiambia mwenyewe,
‘Mimi ndiye, wala hakuna mwingine zaidi yangu.
Kamwe sitakuwa mjane,
wala sitafiwa na watoto.’
947:9 1The 5:3; Isa 13:8; Nah 3:4; Za 55:15; Mal 3:5; Kum 18:10-11; Ufu 9:21; 18:8-10Haya mawili yatakupata, kufumba na kufumbua,
katika siku moja:
kufiwa na watoto, na ujane.
Yote yatakupata kwa kipimo kikamilifu,
ijapokuwa uchawi wako ni mwingi,
na uaguzi wako ni mwingi.
1047:10 Ay 15:31; 2Fal 21:16; Isa 5:21; 29:15; Za 52:7; 62:10Umeutegemea uovu wako,
nawe umesema, ‘Hakuna yeyote anionaye.’
Hekima yako na maarifa yako vinakupoteza
unapojiambia mwenyewe,
‘Mimi ndiye, wala hakuna mwingine zaidi yangu.’
1147:11 Dan 5:30; Za 55:15; 1The 5:3; Isa 10:3; 14:15; 21:9; Lk 17:27; Isa 17:14Maafa yatakujia,
nawe hutaweza kuyaondoa kwa uaguzi.
Janga litakuangukia,
wala hutaweza kulikinga kwa fidia;
msiba mkuu usioweza kuutabiri
utakujia ghafula.
1247:12 Kut 7:11“Endelea basi na uaguzi wako,
na wingi wa uchawi wako,
ambao umeutumikia tangu utoto wako.
Labda utafanikiwa,
labda unaweza ukasababisha hofu kuu.
1347:13 Yer 51:58; Hab 2:13; Isa 19:3; 5:29; 43:13; 57:10; 46:7; Dan 2:2Ushauri wote uliopokea umekuchosha bure!
Wanajimu wako na waje mbele,
wale watazama nyota watabiriao mwezi baada ya mwezi,
wao na wawaokoe na lile linalokuja juu yenu.
1447:14 Isa 5:24; Nah 1:10; Yer 50:30-32; Isa 30:30; 10:17Hakika wako kama mabua makavu;
moto utawateketeza.
Hawawezi hata kujiokoa wao wenyewe
kutokana na nguvu za mwali wa moto.
Hapa hakuna makaa ya kumtia mtu yeyote joto;
hapa hakuna moto wa kuota.
1547:15 Ufu 18:11; Isa 44:17Hayo ndiyo yote wanayoweza kuwatendea ninyi,
hawa ambao umetaabika nao
na kufanya nao biashara tangu utoto.
Kila mmoja atatoroka;
hakuna yeyote awezaye kukuokoa.
The Fall of Babylon
1“Go down, sit in the dust,
Virgin Daughter Babylon;
sit on the ground without a throne,
queen city of the Babylonians.47:1 Or Chaldeans; also in verse 5
No more will you be called
tender or delicate.
2Take millstones and grind flour;
take off your veil.
Lift up your skirts, bare your legs,
and wade through the streams.
3Your nakedness will be exposed
and your shame uncovered.
I will take vengeance;
I will spare no one.”
4Our Redeemer—the Lord Almighty is his name—
is the Holy One of Israel.
5“Sit in silence, go into darkness,
queen city of the Babylonians;
no more will you be called
queen of kingdoms.
6I was angry with my people
and desecrated my inheritance;
I gave them into your hand,
and you showed them no mercy.
Even on the aged
you laid a very heavy yoke.
7You said, ‘I am forever—
the eternal queen!’
But you did not consider these things
or reflect on what might happen.
8“Now then, listen, you lover of pleasure,
lounging in your security
and saying to yourself,
‘I am, and there is none besides me.
I will never be a widow
or suffer the loss of children.’
9Both of these will overtake you
in a moment, on a single day:
loss of children and widowhood.
They will come upon you in full measure,
in spite of your many sorceries
and all your potent spells.
10You have trusted in your wickedness
and have said, ‘No one sees me.’
Your wisdom and knowledge mislead you
when you say to yourself,
‘I am, and there is none besides me.’
11Disaster will come upon you,
and you will not know how to conjure it away.
A calamity will fall upon you
that you cannot ward off with a ransom;
a catastrophe you cannot foresee
will suddenly come upon you.
12“Keep on, then, with your magic spells
and with your many sorceries,
which you have labored at since childhood.
Perhaps you will succeed,
perhaps you will cause terror.
13All the counsel you have received has only worn you out!
Let your astrologers come forward,
those stargazers who make predictions month by month,
let them save you from what is coming upon you.
14Surely they are like stubble;
the fire will burn them up.
They cannot even save themselves
from the power of the flame.
These are not coals for warmth;
this is not a fire to sit by.
15That is all they are to you—
these you have dealt with
and labored with since childhood.
All of them go on in their error;
there is not one that can save you.