Isaya 43 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version

Isaya 43:1-28

Mwokozi Pekee Wa Israeli

143:1 Mwa 2:7; 32:28; Isa 45:3-4; Kut 6:6; Isa 42:6; 27:11; Ay 19:25Lakini sasa hili ndilo asemalo Bwana,

yeye aliyekuumba, ee Yakobo,

yeye aliyekuhuluku, ee Israeli:

“Usiogope kwa maana nimekukomboa,

nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu.

243:2 Mwa 26:3; Kum 31:6-8; Isa 30:27; 8:7; Dan 3:25-27; Kut 14:22; Isa 29:6Unapopita kwenye maji makuu,

nitakuwa pamoja nawe,

unapopita katika mito ya maji,

hayatakugharikisha.

Utakapopita katika moto,

hutaungua,

miali ya moto haitakuunguza.

343:3 Mit 21:18; Kut 30:2; Isa 20:3; Mwa 10:7; Eze 29:20; Za 68:31; Amu 2:18; Kut 14:30Kwa kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wako,

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako.

Ninaitoa Misri kuwa fidia yako,

Kushi na Seba badala yako.

443:4 Isa 63:9; Ufu 3:9; Kut 19:5-6; Isa 49:5Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu,

nami kwa kuwa ninakupenda,

nitatoa watu badala yako

na mataifa badala ya maisha yako.

543:5 Isa 44:2; Mwa 21:22; Kut 14:22; Mdo 18:10; Yer 30:10-11; Mt 8:11; Zek 8:7; Isa 24:14Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe,

nitawaleta watoto wako kutoka mashariki,

na kukukusanya kutoka magharibi.

643:6 Eze 16:61; 2Kor 6:18; Eze 36:24; Yer 23:8; Kum 30:4; Isa 60:4; 11:12Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’

nayo kusini, ‘Usiwazuie.’

Walete wana wangu kutoka mbali,

na binti zangu kutoka miisho ya dunia:

743:7 Yak 2:7; Isa 29:23; Yer 15:16; Efe 2:10; Isa 56:5; 62:2; 63:19; Za 89:9kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu,

niliyemuumba kwa utukufu wangu,

niliyemhuluku na kumfanya.”

843:8 Isa 6:9-10; 42:20; Eze 12:2Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni,

wenye masikio lakini hawasikii.

943:9 Isa 45:20; 48:14; 41:26Mataifa yote yanakutanika pamoja,

na makabila yanakusanyika.

Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya,

na kututangazia mambo yaliyopita?

Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi,

ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.”

1043:10 Isa 41:8-9; 19:21; Za 86:10; Yer 14:22; Yos 24:22; Kum 4:35; Isa 45:5-6, 14“Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana,

“na mtumishi wangu niliyemchagua,

ili mpate kunijua na kuniamini,

na kutambua kwamba Mimi ndiye.

Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa,

wala hatakuwepo mwingine baada yangu.

1143:11 Isa 42:8; Za 18:31; Isa 25:9; 63:4; Kut 6:2Mimi, naam mimi, ndimi Bwana,

zaidi yangu hakuna mwokozi.

1243:12 Kum 32:16; Za 81:9; Isa 44:8Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza:

Mimi, wala si mungu mgeni katikati yenu.

Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana,

“kwamba Mimi ndimi Mungu.

1343:13 Hes 23:8; Ay 9:12; Za 90:2; Mit 8:23; Kum 32:39; Isa 48:12Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye.

Hakuna hata mmoja awezaye kuokoa

kutoka mkononi wangu.

Mimi ninapotenda,

ni nani awezaye kutangua?”

Huruma Za Mungu, Na Kukosa Uaminifu Kwa Israeli

1443:14 Isa 13:14-15; 23:13; Kut 15:13; Ay 19:25; Isa 41:20Hili ndilo Bwana asemalo,

Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli:

“Kwa ajili yenu nitatumana Babeli

na kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi,

katika meli walizozionea fahari.

1543:15 Isa 42:8; 27:11; 45:11; 41:21Mimi ndimi Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wako,

Muumba wa Israeli, Mfalme wako.”

1643:16 Kut 14:29; Za 77:19; Kut 15:8; Isa 11:15Hili ndilo asemalo Bwana,

yeye aliyefanya njia baharini,

mahali pa kupita kwenye maji mengi,

1743:17 Za 118:12; Kut 14:4-9, 22; Za 76:5-6; Ay 13:25; Yer 51:21; Eze 38:4aliyeyakokota magari ya vita na farasi,

jeshi pamoja na askari wa msaada,

nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe,

wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi:

1843:18 Isa 41:22“Msiyakumbuke mambo yaliyopita,

wala msiyatafakari mambo ya zamani.

1943:19 Hes 20:11; Yer 23:8-9; Ufu 21:5; Isa 40:3; 41:22; Yer 16:14-15; 2Kor 5:17; Isa 35:7Tazama, nitafanya jambo jipya!

Sasa litachipuka, je, hamtalitambua?

Nitafanya njia jangwani

na vijito vya maji katika nchi kame.

2043:20 Hes 20:8; Isa 48:21; 41:17; Za 148:10; Isa 13:22Wanyama wa mwituni wataniheshimu,

mbweha na bundi,

kwa sababu ninawapatia maji jangwani,

na vijito katika nchi kame,

ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua,

2143:21 Za 66:2; 1Pet 2:9; Mwa 2:7; Mal 3:17; Za 102:18watu wale niliowaumba kwa ajili yangu,

ili wapate kutangaza sifa zangu.

22“Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo,

hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli.

2343:23 Zek 7:5-6; Kut 30:35; Yer 7:22; Amo 5:25; Kut 29:41; Mik 6:3; Mal 1:12-13Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa,

wala kuniheshimu kwa dhabihu zako.

Sikukulemea kwa sadaka za nafaka

wala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba.

2443:24 Kut 30:23; Mal 2:17; Isa 7:13; Yer 8:21; Law 3:9; Yer 44:22Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato,

wala hukunipa kwa ukarimu

mafuta ya wanyama wa dhabihu zako.

Lakini umenilemea kwa dhambi zako,

na kunitaabisha kwa makosa yako.

2543:25 2Sam 12:13; Lk 5:21; Eze 20:44; Yer 31:34; Ay 7:21; 2Nya 6:21; Isa 64:9“Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako,

kwa ajili yangu mwenyewe,

wala sizikumbuki dhambi zako tena.

2643:26 Isa 1:18; 41:1; 49:25; 50:8Tafakari mambo yaliyopita,

njoo na tuhojiane,

leta shauri lako uweze kupewa haki yako.

2743:27 Rum 5:12; Isa 28:7; Yer 5:31; Mwa 12:18; Isa 9:15; 24:20Baba yako wa kwanza alitenda dhambi,

wasemaji wako wameasi dhidi yangu.

2843:28 Eze 5:15; Za 39:8; Hes 5:27; Kum 13:15; Isa 42:24; Zek 5:3; Yer 24:9Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako,

nami nitamtoa Yakobo aangamizwe,

na Israeli adhihakiwe.

Nueva Versión Internacional

Isaías 43:1-28

El único Salvador de Israel

1Pero ahora, así dice el Señor,

el que te creó, Jacob,

el que te formó, Israel:

«No temas, que yo te he redimido;

te he llamado por tu nombre; tú eres mío.

2Cuando cruces las aguas,

yo estaré contigo;

cuando cruces los ríos,

no te cubrirán sus aguas;

cuando camines por el fuego,

no te quemarás

ni te abrasarán las llamas.

3Yo soy el Señor tu Dios,

el Santo de Israel, tu Salvador;

yo he entregado a Egipto como precio por tu rescate,

a Cus y a Seba en tu lugar.

4Porque eres precioso a mis ojos

y digno de honra, yo te amo.

A cambio de ti entregaré pueblos;

a cambio de tu vida entregaré naciones.

5No temas, porque yo estoy contigo;

desde el oriente traeré a tu descendencia,

desde el occidente te reuniré.

6Al norte diré: “¡Entrégalos!”.

Y al sur: “¡No los retengas!

Trae a mis hijos desde lejos

y a mis hijas desde los confines de la tierra.

7Trae a todo el que sea llamado por mi nombre,

al que yo he creado para mi gloria,

al que yo hice y formé”».

8Saquen al pueblo ciego, aunque tiene ojos,

al pueblo sordo, aunque tiene oídos.

9Que se reúnan todas las naciones

y se congreguen los pueblos.

¿Quién de sus dioses profetizó estas cosas

y nos anunció lo ocurrido en el pasado?

Que presenten a sus testigos y demuestren tener razón,

para que otros oigan y digan:

«Es verdad».

10«Ustedes son mis testigos», afirma el Señor,

«y mi siervo a quien he escogido,

para que me conozcan y crean en mí,

y entiendan que yo soy.

Antes de mí no hubo ningún otro dios

ni habrá ninguno después de mí.

11Yo, yo soy el Señor,

fuera de mí no hay ningún otro salvador.

12Yo he anunciado, salvado y proclamado;

yo entre ustedes y no un dios extraño.

Ustedes son mis testigos de que yo soy Dios»,

afirma el Señor.

13«Desde los tiempos antiguos, yo soy.

No hay quien pueda librar de mi mano.

Lo que yo hago, nadie puede desbaratarlo».

La misericordia de Dios y la infidelidad de Israel

14Así dice el Señor,

su Redentor, el Santo de Israel:

«Por ustedes enviaré gente a Babilonia;

abatiré a todos como fugitivos.

En los barcos que eran su orgullo,

abatiré a los babilonios.43:14 Lit. caldeos.

15Yo soy el Señor, su Santo;

soy su Rey, el Creador de Israel».

16Así dice el Señor,

el que abrió un camino en el mar,

una senda a través de las aguas caudalosas;

17el que hizo salir carros de combate y caballos,

ejército y guerrero al mismo tiempo,

los cuales quedaron tendidos para nunca más levantarse,

extinguidos como mecha que se apaga:

18«Olviden las cosas de antaño;

ya no vivan en el pasado.

19¡Voy a hacer algo nuevo!

Ya está sucediendo, ¿no se dan cuenta?

Estoy abriendo un camino en el desierto

y ríos en lugares desolados.

20Me honran los animales salvajes,

los chacales y los avestruces;

yo hago brotar agua en el desierto,

ríos en lugares desolados,

para dar de beber a mi pueblo escogido,

21al pueblo que formé para mí mismo,

para que proclame mi alabanza.

22»Pero tú, Jacob, no me has invocado;

tú, Israel, te has cansado de mí.

23No me has traído el cordero de tus holocaustos

ni me has honrado con tus sacrificios.

No te he abrumado exigiendo ofrendas de grano

ni te he agobiado reclamando incienso.

24No me has comprado caña aromática

ni me has saciado con el sebo de tus sacrificios.

¡En cambio, tú me has abrumado con tus pecados

y me has agobiado con tus iniquidades!

25»Soy yo, solo yo, el que por amor a mí mismo

borra tus transgresiones

y no se acuerda más de tus pecados.

26¡Hazme recordar!

Presentémonos a juicio;

plantea el argumento de tu inocencia.

27Tu primer antepasado pecó;

tus voceros se rebelaron contra mí.

28Por eso humillé a las autoridades del templo;

entregué a Jacob a la destrucción total,

entregué a Israel al menosprecio.