Isaya 35 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Isaya 35:1-10

Furaha Ya Waliokombolewa

135:1 Isa 27:10; 41:18-19; 51:3; 32:15-16; 27:6Jangwa na nchi kame vitafurahi;

nyika itashangilia na kuchanua maua.

Kama waridi, 235:2 Wim 7:5; Mwa 21:6; Ezr 3:7; Za 105:43; Isa 32:15; 12:6; 25:9; 1Nya 27:29litachanua maua,

litashangilia sana na kupaza sauti kwa furaha.

Litapewa utukufu wa Lebanoni,

fahari ya Karmeli na Sharoni;

wataona utukufu wa Bwana,

fahari ya Mungu wetu.

335:3 Ay 4:3-4; Ebr 12:12Itieni nguvu mikono iliyo dhaifu,

yafanyeni imara magoti yaliyolegea,

435:4 Isa 40:2; 2Nya 32:6; Zek 1:13; Kum 20:3; Isa 21:4; Yos 1:9; Isa 7:4; 1:24; 34:8; 25:9; 40:1; 10:9, 10-11; 51:5; 62:11; Dan 10:19; Ufu 22:12waambieni wale wenye mioyo ya hofu,

“Kuweni hodari, msiogope;

tazama, Mungu wenu atakuja,

pamoja na malipo ya Mungu,

atakuja na kuwaokoa ninyi.”

535:5 Mt 9:27; 11:5; Isa 42:18; 29:18; 2Nya 32:6; Isa 40:2; Zek 1:13; Isa 21:4; Ufu 22:12Ndipo macho ya vipofu yatafumbuliwa

na masikio ya viziwi yatazibuliwa.

635:6 Lk 7:22; Yn 5:8-9; Mk 7:35; Kut 17:6; Yn 7:38; Mdo 3:2; Mt 15:30; Mdo 3:8Ndipo kilema atarukaruka kama kulungu,

nao ulimi wa aliye bubu utapaza sauti kwa shangwe.

Maji yatatiririka kwa kasi katika nyika,

na vijito katika jangwa.

735:7 Za 68:6; Isa 41:17; 44:3; 55:1; 49:10; 58:11; 13:22; Za 107:35; Ay 8:11; 40:21Mchanga wa moto utakuwa bwawa la maji,

ardhi yenye kiu itabubujika chemchemi.

Maskani ya mbweha walikolala hapo awali

patamea majani, matete na mafunjo.

835:8 Yer 31:21; Yoe 3:17; Mt 7:13-14; 1Pet 1:15; Isa 52:1; 33:8Nako kutakuwa na njia kuu,

nayo itaitwa Njia ya Utakatifu.

Wasio safi hawatapita juu yake;

itakuwa ya wale watembeao katika Njia ile;

yeye asafiriye juu yake,

ajapokuwa mjinga, hatapotea.

935:9 Isa 30:9; 11:6-9; Law 25:47-55; Kut 6:6; Isa 13:22; 62:12Huko hakutakuwepo na simba,

wala mnyama mkali hatapita njia hiyo,

wala hawatapatikana humo.

Ila waliokombolewa tu ndio watakaopita huko,

1035:10 Yn 16:22; Isa 51:11; 30:29; Ufu 21:4; Ay 19:25; Za 51:8waliokombolewa na Bwana watarudi.

Wataingia Sayuni wakiimba;

furaha ya milele itakuwa juu ya vichwa vyao.

Watapata furaha na shangwe;

huzuni na majonzi vitakimbia.