Isaya 3 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 3:1-26

Hukumu Juu Ya Yerusalemu Na Yuda.

13:1 Law 26:26; Eze 4:16; Amo 4:6; Yer 37:21; Za 18:18; Isa 5:13; 65:13Tazama sasa, Bwana,

Bwana Mwenye Nguvu Zote,

yu karibu kuwaondolea Yerusalemu na Yuda

upatikanaji wa mahitaji na misaada,

upatikanaji wote wa chakula na tegemeo lote la maji,

23:2 Eze 17:13; Isa 9:14-15; 2Fal 24:14; Kum 18:10shujaa na mtu wa vita,

mwamuzi na nabii,

mwaguzi na mzee,

33:3 Ay 22:8; 2Fal 24:14; Mhu 10:11; Yer 8:17; 2Fal 1:9jemadari wa kikosi cha watu hamsini

na mtu mwenye cheo, mshauri,

fundi stadi na mlozi mjanja.

43:4 Mhu 10:16Nitawafanya wavulana wawe maafisa wao,

watoto ndio watakaowatawala.

53:5 Za 28:3; Yer 9:8; Isa 9:19; Mik 7:2-6Watu wataoneana wao kwa wao:

mtu dhidi ya mtu, na jirani dhidi ya jirani yake.

Kijana atainuka dhidi ya mzee,

mtu mnyonge dhidi ya mtu mwenye heshima.

6Mtu atamkamata mmoja wa ndugu zake

katika nyumba ya baba yake na kusema,

“Unalo joho, sasa uwe kiongozi wetu,

tawala lundo hili la magofu!”

73:7 Yer 30:12; Hos 5:13; Isa 2:11; 24:2; Eze 34:4; Yoe 1:16Lakini siku hiyo atapiga kelele akisema,

“Sina uponyaji.

Sina chakula wala mavazi katika nyumba yangu,

msinifanye niwe kiongozi wa watu.”

83:8 Isa 30:9; 9:15-17; 28:15; 1:7; Ay 1:11; Za 73:9-11; 2Nya 33:6; Isa 65:7Yerusalemu inapepesuka,

Yuda inaanguka;

maneno yao na matendo yao ni kinyume na Bwana,

wakiudharau uwepo wake uliotukuka.

93:9 Mwa 13:13; 2Nya 34:24; Rum 6:23; Hes 32:23; Isa 59:12; Yer 14:7; Mit 8:36; Hos 5:5Nyuso zao zinavyoonekana zinashuhudia dhidi yao,

hujivunia dhambi yao kama Sodoma,

wala hawaifichi.

Ole wao!

Wamejiletea maafa juu yao wenyewe.

103:10 Za 37:17; Yer 22:15; Mwa 15:1; Za 128:2; Kum 12:28; 5:33Waambie wanyofu itakuwa heri kwao,

kwa kuwa watafurahia tunda la matendo yao.

113:11 Kum 28:15-68; Ay 9:13; Isa 57:20; Kum 28:15-68; 2Nya 6:23; Yer 21:14; Mao 5:16; Eze 24:14Ole kwa watu waovu! Maafa yapo juu yao!

Watalipwa kwa ajili ya yale mikono yao iliyotenda.

123:12 Yer 25:16; Mik 3:5; Isa 9:16; 19:14; 28:7; Yer 23:13; 25:16Vijana wanawatesa watu wangu,

wanawake wanawatawala.

Enyi watu wangu, viongozi wenu wanawapotosha,

wanawapoteza njia.

133:13 Ay 10:2; Za 82:1; Isa 2:4Bwana anachukua nafasi yake mahakamani,

anasimama kuhukumu watu.

143:14 1Sam 12:7; Yak 2:6; Ay 22:4; 24:9; Isa 25:4; 11:4Bwana anaingia katika hukumu

dhidi ya wazee na viongozi wa watu wake:

“Ninyi ndio mlioharibu shamba langu la mizabibu,

mali zilizonyangʼanywa maskini zimo nyumbani mwenu.

153:15 Za 94:5; Ay 24:14; Isa 10:6; 26:6; 29:19; 32:6; 5:7Mnamaanisha nini kuwaponda watu wangu

na kuzisaga nyuso za maskini?”

asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote.

163:16 Wim 3:11; Ay 15:25Bwana asema,

“Wanawake wa Sayuni wana kiburi,

wanatembea na shingo ndefu,

wakikonyeza kwa macho yao,

wanatembea kwa hatua za madaha,

wakiwa na mapambo ya njuga kwenye vifundo vya miguu yao.

173:17 Eze 27:31; Amo 8:10Kwa hiyo Bwana ataleta majipu kwenye vichwa vya wanawake wa Sayuni;

Bwana atazifanya ngozi za vichwa vyao kuwa vipara.”

183:18 Mwa 41:42; Amu 8:21; Isa 2:11Katika siku ile Bwana atawanyangʼanya uzuri wao: bangili, tepe za kichwani, mikufu yenye alama za mwezi mwandamo, 193:19 Mwa 24:47; Eze 16:11-12vipuli, vikuku, shela, 203:20 Kut 39:28; Eze 44:18; 24:17, 23vilemba, mikufu ya vifundo vya miguu, mshipi, chupa za manukato na hirizi, 213:21 Mwa 24:22; Kut 29:6pete zenye muhuri, pete za puani, 223:22 Rut 3:15majoho mazuri, mitandio, mavazi, kifuko cha kutilia fedha, 233:23 Eze 26:10; 23:26; Kut 29:6; Wim 3:11; Isa 61:3; 62:3vioo, mavazi ya kitani, taji na shali.

243:24 Es 2:12; Mit 31:24; Law 13:40; Yon 3:5-8; Isa 4:4; 20:2; Ay 1:20; 16:15; Mwa 37:34; Yer 4:8; Mao 2:10Badala ya harufu ya manukato kutakuwa na uvundo;

badala ya mishipi, ni kamba;

badala ya nywele zilizotengenezwa vizuri, ni upara;

badala ya mavazi mazuri, ni nguo za magunia;

badala ya uzuri, ni alama ya aibu kwa chuma cha moto.

253:25 Isa 1:20; Yer 15:8Wanaume wako watauawa kwa upanga,

nao mashujaa wako watauawa vitani.

263:26 Yer 14:2; 4:28; Mao 2:10; Ay 2:13; Isa 14:12, 31; 33:9; 24:4, 7; Za 137:1Malango ya Sayuni yataomboleza na kulia,

ataketi mavumbini akiwa fukara.

Japanese Contemporary Bible

イザヤ書 3:1-26

3

エルサレムとユダへのさばき

1天の軍勢の主は、エルサレムとユダ王国の

食糧と水の補給路を断ち、

2指導者たち、軍隊、裁判官、預言者、長老、将校、

3実業家、法律家、魔術師、政治家を取り去ります。

4若者がイスラエルの王になり、

稚拙な政治をします。

5そのため手のつけられない無政府状態となり、

だれもが人を踏みつけ、隣人同士で牙をむき合い、

権威に反抗し、身分の低い者が高貴な人を

あざ笑うようになります。

6そのとき人は、兄弟にすがって哀願します。

「おまえには余分の着物があるではないか。

王になって、この混乱した社会を

何とかしてくれないか。」

7ところが、相手は口をとがらせるばかりです。

「私は何の助けにもならない。

着物も食べ物も余分にはない。

巻き添えにしないでくれ。」

8イスラエルが落ちぶれたのは、

ユダヤ人が主に背を向け、

主を礼拝しようとしなかったからです。

彼らは主の栄光に逆らいました。

9彼らの顔つきが心の内をさらけ出し、

罪があることを物語っています。

おまけに、自分たちの罪はソドムの住民の罪に

匹敵することを誇り、

恥ずかしいなどと少しも思っていません。

なんという絶望的な状況でしょう。

自分で自分の滅亡を決めてしまったのです。

10しかし神を敬う人は、何もかもうまくいきます。

そういう人には、

「すばらしい報いがある」と励ましなさい。

11悪者には、「あなたにもふさわしい報いがある。

あなたは今に恐ろしい刑罰を受けるだろう」

と言いなさい。

12かわいそうな民よ。

支配者がどんなにあなたがたを惑わしているか、

わからないのですか。

女のように弱く、子どものように愚かな者が、

王のまねごとをしているのです。

それで指導者といえるのでしょうか。

彼らはあなたがたを滅びへと

真っさかさまに突き落とす者たちです。

13主は立ち上がります。

検察官として、自分の民の起訴状を読み上げます。

14真っ先に主の怒りに触れるのは、長老や重臣です。

彼らは貧しい人から力ずくで巻き上げ、

力のない小作人から取り上げた穀物で、

倉をいっぱいにしました。

15天の軍勢の主は、

「どうしてわたしの民をこんなに

踏みにじったのか」と、彼らを責めます。

16次に主は、高慢なユダヤの女たちをさばきます。

彼女たちは気取って歩き、鼻をつんと高くし、

くるぶしの飾り輪を鳴らし、

男の気をひこうと人ごみの中で流し目を使います。

17主はその頭をかさぶただらけにし、

裸にして人々のさらし者にします。

18彼女たちはもう二度と、これ見よがしに外を歩けません。美しい化粧や装飾品、 19ネックレス、腕輪、それにストールはみな、はぎ取られるからです。 20スカーフ、くるぶしの飾り輪、ヘア・バンド、イヤリング、香水、 21指輪、宝石、 22夜会服、チュニック・コート、ケープ、彫り物のついたくし、さいふ、 23鏡、美しい肌着、高価なドレス、ベールなどもなくなります。

24彼女たちから香水の香りは消え、

吐き気をもよおす匂いがただよいます。

きれいにセットした髪は抜け落ち、

帯の代わりに荒なわをしめ、

夜会服の代わりに麻袋を着ます。

美貌は失われ、

あるのは恥と屈辱だけです。

25-26夫たちは戦いに倒れ、

何もかも失って、座り込んで泣くのです。